Huyo anatafuta namna ya kuhamishwa tu,,hizo ni MBWINU wanatumiaga baadhi ya watumishi hasa walimu wakichoka kukaa vijijini wakati wapo chuo ndoto zao zilikuwa kuliga kazi town,,,Mwaka 2015 Masasi kuna mwalimu nae alileta mchezo kama huo akakutwa kalala chini ya daraja,,Mkurugenzi akastukia kuwa ni janja janja ila yule jamaa alikaza kabisa hataki kubaki kule bora aache kazi,,na wazazi wa kile kijiji nao waligoma kabisa yule jamaa abaki pale wakisema amewachafulia sana hali na ustaarabu wao,toka pazaliwe hicho kijiji na toka shule ianze miaka hiyo ya ukoloni ikiitwa Middle school hapajawahi tokea tukio kama hilo mkurugenzi akaamua kumuhamishia akampeleka shule ipo maeneo ya kati ya Masasi mjini na ndanda ila akiunda tume yake ya uchunguzi,,mwisho wa picha ikaja gundulika jamaa alifake sababu hakuwa ameyapenda yale mazingira basi akapigwa onyo kalii na kulipwa nusu mshahara kwa miezi mitatu ila ikawa ndo ashahama zake