Kwahiyo Chadema ndio kokoro la oil chafu?
rushwa izidi hapo ilipofika ndio aachie ngazi! muongo huyuWaziri mkuu mstaafu, Fredrick Sumaye amesema iwapo misingi ya uchaguzi ndani ya CCM italalia kwenye rushwa, Hataendelea kuwa mwanachama na kuonya kuwa tatizo hilo limefikia pabaya na litakiangusha chama hicho.
Source: Mwananchi
Daah! Ina maana ameridhika kabisa na rushwa iliyopo?
Sometimes ni bora kunyamaza kimya tu!
Waziri mkuu mstaafu, Fredrick Sumaye amesema iwapo misingi ya uchaguzi ndani ya CCM italalia kwenye rushwa, Hataendelea kuwa mwanachama na kuonya kuwa tatizo hilo limefikia pabaya na litakiangusha chama hicho.
Source: Mwananchi
Nimecheka sana !rushwa izidi hapo ilipofika ndio aachie ngazi! muongo huyu
Sumaye vipi Tena, CCM na rushwa si tayari ni mapacha, au Ana maanisha rushwa ikipitisha mgombea wa CCM urais mwakani?
Sent from my iPhone using JamiiForums
Kulingana na habari hii,rushwa anayoiogopa Sumaye ni ya kwenye uteuzi wa mgombea wa urais CCM 2015.Kwamba ana wasiwasi jina lake halitapitishwa kwenye vikao vya chama vya mchujo,kwa vile washindani wake watamzidi katika kuhonga wajumbe.Na hili likitokea basi atajiondoa CCM na kutafuta chama kingine kitakachompa tiketi ya kugombea urais
Vinginevyo rushwa na ufisadi wote uliotamalaki katika nchi hii kwake si muhimu kabisa.Rushwa inayomkera yeye ni ile tu inayogusa maslahi yake,yaani inayokwamisha mipango na harakati zake za kuwa rais wa Tanzania