Mkuu Tipau, asante kwa taarifa hii!. Huyu naye?!, eti kama rushwa itazidi?!. Ndani ya CCM, anataka rushwa izidi mara ngapi zaidi ya hii rushwa iliyopo?!. Sumaye anataka ikizidi kufikia kiwango gani?, hapo ilipo ndani ya CCM, rushwa imeisha zidi hadi kufurika kitambo!, sasa huyu anayeulizia kama rushwa ikizidi, anaulizia CCM ipi?!.
Sumaye aseme tuu, baada ya UKAWA kukosa mgombea mmoja wa 2015, wamemuomba yeye agombee and in principle atakuwa kakubali, sasa anatafuta pa kutokea CCM, ili aeleweke na jamii imuelewe!. Tena namshauri afanye hivyo mapema, kabla jamaa zake hawajabadili ile sheria ya viongozi wakuu wastaafu na kuongeza kipengele "kiongozi mkuu mstaafu atalipwa mafao na marupurupu stahiki" only if hatajishughulisha na siasa basada ya kustaafu!" kwani kuendelea kujishughulisha na siasa nayo ni ajira!.
Hajajifunza tuu kwa wenzake!, Mwalimu Nyerere Foundation, Benjamin Mkapa/IOTF, sasa JMK Foundation/WAMA on the making, na yeye aunde NG'0 yake!, hive ile HOPE FOUNDATION imeishia wapi?!.
Thanks.
Pasco.