Sumaye: Rushwa ikizidi CCM nitajiondoa

Sumaye: Rushwa ikizidi CCM nitajiondoa

mzee boya kweli hivi nani kamwambia kuwa anafaa kuwa Rais hii nchi inawazee wengine wa ajabu kweli.
Kwa nini washauri wake hawamkumbushi kuwa wakati akiwa waziri mkuu, Rais Mkapa hakumwamini kabisa hadi wizara ya TAMISEMI ilihamishiwa ofisi ya rais!

Tafadhali mfahamisheni kuwa hafai kabisa kuwa rais wa nchi hii!! Ni vema akatulia aendelee kula pensheni yake pole pole!!!
 
Mkuu Tipau, asante kwa taarifa hii!. Huyu naye?!, eti kama rushwa itazidi?!. Ndani ya CCM, anataka rushwa izidi mara ngapi zaidi ya hii rushwa iliyopo?!. Sumaye anataka ikizidi kufikia kiwango gani?, hapo ilipo ndani ya CCM, rushwa imeisha zidi hadi kufurika kitambo!, sasa huyu anayeulizia kama rushwa ikizidi, anaulizia CCM ipi?!.

Sumaye aseme tuu, baada ya UKAWA kukosa mgombea mmoja wa 2015, wamemuomba yeye agombee and in principle atakuwa kakubali, sasa anatafuta pa kutokea CCM, ili aeleweke na jamii imuelewe!. Tena namshauri afanye hivyo mapema, kabla jamaa zake hawajabadili ile sheria ya viongozi wakuu wastaafu na kuongeza kipengele "kiongozi mkuu mstaafu atalipwa mafao na marupurupu stahiki" only if hatajishughulisha na siasa basada ya kustaafu!" kwani kuendelea kujishughulisha na siasa nayo ni ajira!.

Hajajifunza tuu kwa wenzake!, Mwalimu Nyerere Foundation, Benjamin Mkapa/IOTF, sasa JMK Foundation/WAMA on the making, na yeye aunde NG'0 yake!, hive ile HOPE FOUNDATION imeishia wapi?!.

Thanks.
Pasco.
UKAWA kamwe hawawezi kumwomba Sumaye awe mgombea wao urais!
 
Kwa kuwa chadema ni chama makini akitaka kujiunga najua watamkubali lakini akileta mambo ya uccm watamfanya kama walivyomfanya Shibuda
 
Waziri Mkuu mstaafu, Fredrick Sumaye amesema kwamba ikiwa rushwa itazidi ndani ya chama chake chama cha CCM, atajiondoa kutoka chama hicho. Haikuweza kufahamika mara moja kama atahamia chama gani lakini kuna tetesi kwamba huenda akahamia CHADEMA.

Chanzo: Mwananchi

Na isipozidi ila ikaendelea mdogomdogo kama anavyoona yeye hatajiondoa!
Tatizo anataka uraisi wala syo mzalendo wa kweli. Dhambi ni dhambi tu hata kama rushwa ni ya ccm itaendelea kuitwa takrima na wali wa wageni waliotoka mbali kuja kusikiliza kampeni.

Huwezi kuish sehem moja na mtu kama hamna nia moja. CCM WOTE HOVYO TUU MAANA WAMEWEKWA WOTE KWA MFUMO MOJA WA RUSHWA.
 
Kama mpaka sasa hivi haoni kuwa rushwa imezidi ndani ya CCM na Serikali yake basi hafai kabisa. Pia alikuwa na muda wa miaka 10 kuonyesha utendaji wake lakini hatuna cha kumkumbuka ambacho ni cha pekee.

Hatutaki watu ambao walikuwa na nafasi ya kubadilisha nchi hii ambao hawakuitumia. Huyu hana jipya atakalolifanya ambalo hakuweza kulifanya akiwa Waziri Mkuu.

We need new faces.
 
Iliwashangaza wananchi wengi Mkapa alipomteua kwa kipindi cha pili kuwa PM as hakuwa na lolote katka utendaji. Nafikiri alipewa uPM kwa ushauri wa Nyerere akifikiri kuwa pengine angeweweza kuwa mkali kama Sokoine kwa sababu ya eneo analotoka ingawa si mmasai.
 
Nadhani ana mpango wa kujiunga na ACT. Mwambieni kabisa, CDM au UKAWA hakuna nafasi ya uongozi wa watu waliofeli kisiasa ka yeye.
Tuna uongozi wa kutosha, watu walio amua kupoteza ili waongoze si waliokwisha shindwa uongozi waje kujitutumua huku. Angojee musiki mnene 2015.
 
Waziri Mkuu mstaafu, Fredrick Sumaye amesema kwamba ikiwa rushwa itazidi ndani ya chama chake chama cha CCM, atajiondoa kutoka chama hicho. Haikuweza kufahamika mara moja kama atahamia chama gani lakini kuna tetesi kwamba huenda akahamia CHADEMA.

Chanzo: Mwananchi

kwani ukiwa ccm lazima upate uongozi? wewe ni mmojawapo uliua mashamba ya ngano hanang'a
 
Sumaye aseme tuu, baada ya UKAWA kukosa mgombea mmoja wa 2015, wamemuomba yeye agombee and in principle atakuwa kakubali, sasa anatafuta pa kutokea CCM, ili aeleweke na jamii imuelewe!. Tena namshauri afanye hivyo mapema, kabla jamaa zake hawajabadili ile sheria ya viongozi wakuu wastaafu na kuongeza kipengele "kiongozi mkuu mstaafu atalipwa mafao na marupurupu stahiki" only if hatajishughulisha na siasa basada ya kustaafu!" kwani kuendelea kujishughulisha na siasa nayo ni ajira!.

Mbona sheria kama hiyo ikipitishwa akina Benjamin Mkapa, Ally Hassan Mwinyi & Co. watakufa kwa njaa!

Au siasa kwa CCM ni pale unapojihusisha na upinzani?!
 
Huyu nae hajielewi, unapimaje hicho kiwango cha rushwa ili ujue kimezidi? yaani hata kwa rushwa inayoendelea si tu ndani ya ccm lakini hata katika serikali ya ccm, yeye bado anaona haijazdi, hii inadhihirisha nae ni mla rushwa

Bado hajaona kama imezidi. Watu wanamiliki pauni bilion 1 za wizi wanaziita VIJISENTI na wengine wanahongwa bilioni 2 wanaziita HELA ZA UGORO, sijui Sumaye anataka watu wafanye ufisadi wa shilingi ngapi ndio ajue kwamba ndani ya CCM kuna RUSHWA na UFISADI!!!!!
 
Yaaani habari hii kwako umuhimu ni atakakoenda badala ya uzito wa hiyo "rushwa"?????!!!!

Nchi rahisi sana kuwa kiongozi hii

Eti namshaangaa huu jama
Badala ya kufikiria hoja ya jamaa kuhusu rushwa yeye ana maanisha nin .maana mikataba mingi ya rushwa kama IPTL ,RADA na MADIN imengiwa yeye akiwa ndo MKUU wa shughuli zote za serikali na namshaangaa anopojifanya yeye ni msafi , bora akae tu kimya . Rusha ilikithiri mno kipindi chake sema uhuru haukuwepo kama sasa hivi tunavotumia jf kueleza uozo wa serikali .
 
Kama bado huyu mwizi hajagundua kwamba ndani ya CCM kuna rushwa, basi hafai hata kuwa mwenyekiti wa kitongoji. Kwanza arudishe zile hekta 80,000 alizojimilikisha kule Mvomero huku wananchi wakikosa mashamba ya kulima.
View attachment 185597
 
Back
Top Bottom