kSumaye:
Baadhi ya taarifa katika magazeti na taarifa za habari.... Kuna gazeti limeandika "Sumaye kupasua jipu Dar es Salaam...." Sina jipu wala jipu wala bomu la kupasua.
Kuna lililonishangaza kwamba 'Sumaye amtangazia jipu Lowassa, ikiwa ataingia Lowassa basi atamkabili kwa namna yoyote....'
Hakuna aliyezungumza na mimi kwamba nitapambana na Lowassa, siamini kama kuna source ya karibu na mimi. Basi sikifahamu na kama chanzo kipo sikifahamu, sijaongea na mtu na wala nisingeweza kuyasema, sina uhasama na Lowassa, na niliamua kugombea sitogombea kwa sababu ya mtu, bali kwa sababu ya maslahi ya nchi na si ya mtu.
Kwa kweli Chadema wanatakiwa kumsimisha Sumaye kuwa mgombea wao wa urais.
ndio amemaliza kirahisi namna hiyo? kweli siasa ni mchezzo mchafu!
Nakumbuka kipindi akiwa PM watu walikuwa wanamwita zero sasa ndio anafanya justification ya Hilo jina
Sumaye:
Mambo ya Hanang, yalitokea nchi nzima... Na yalitokea kwa staili tofauti
Tatizo ni kubwa sana, maana nchi nzima matumizi makubwa ya fedha... Tatizo ni kubwa na limeota mizizi
Nimewahi kuzungumzia mara kadhaa...
Nilisema nikiwa Same "Rushwa ni tatizo Barani na Tanzania pia... Kwetu sisi huwezi kushinda bila kutoa fedha"
Nilisema haya 2010:
"Kiongozi anayetoa rushwa anapata wapi kama si mwizi na mla rushwa... Hawezi kuwatendea haki maana wananchi ni kama bidhaa na hatawatumikia bali atatfuta za kihonga baadae"
Nasikia wewe Ritz na bibi kiroboto ndio mmeachiwa nchi na JK kuiongoza wakati yeye anakula bata Canada pole Rais kivuli
kama hao waandishi walipewa bahasha basi itakuwa ni baada ya hiki kituko, other wise wangeondoka waka muacha peke yake kabla ya kumaliza. unaweza kudhani unaota
Nimeshastuka hakuna jipya hapa. Yale yale ya EL kusema sikukutana na JK barabarani. Aseme ameita mkutano kusema nini hasa