Sumaye amgwaya Lowassa!

Sumaye amgwaya Lowassa!

Kachemka vibaya hakuwa na sababu ya kuita waandishi wa habari zaidi angetuma tu taarifa waandishi na ujumbe ungekuwa umefika
 
mie nilitegemea habar hot za kutawala anga za siasa za nchi hii kwa wiki kadhaa kumbe kilio cha mzee mwoga akihofia penshen yake
 
Waandishi bana, hivi hawajui kama Sumaye ni Waziri mkuu mstaafu na bado anakula pension na kutunzwa na serikali ya CCM. Sasa walikua wanategemea alipue bomu gani tena, ni vile tu ni uroho wa madaraka ingekuwa mimi ni waziri mkuu mstaafu ningetulia zangu nyumbani nasubiri tu kuitwa kwenye makongamano ambayo hata risala naandaliwa.Mtu anapata kwa mwezi 80% ya mshahara wake wakati anamaliza uwaziri mkuu sasa angewaponda wanaompatia mshara huo. Waandishi wa Bongo bwana kusoma hawajui hata picha imewashinda
 
Aliwahi kuwa wm ametengeneza njia ya ufisadi sasa alalama nini? WANAOTAKA MAMBO YAO YAENDE VIZURI WAENDE CCM. sasa nini wakait mambo yao yameenda vizuri
 
Ondoa boliti yako kwanza kwenye jicho lako,then ndo uone ya mwenzako! Ha ha ha ha ha ha ha ha ha ha ha!
 
vipi amezungumzia chochote juu ya ile kauli yake aliyoitoa ktk Uwanja wa Namfua Singida kuwa
"ukitaka mambo yako yakunyookee njoo CCM" ? sasa hapo alimaanisha nini kama sio rushwa na kupendeleana.
leo rushwa hiyo hiyo kwa kuwa imemnyima uongozi analalamika ? mkuki kwa nguruwe?
akamuulize mwenzie aliesema akirudi CCM basi amzini mama yake, amerud basi hadi leo akili yake haijakaa sawa, labda hadi amzini kweli.
 
  • Thanks
Reactions: Ame
Kama ameshindwa kwa kuwa rushwa ilitumika kumwangusha na yeye hatakata rufaa kwa ajili ya hilo, kwangu mimi inamaanisha kuwa anakmubaliana na matokeo hayo yaliyotokana na matumizi ya rushwa. Kwa maneno mengine, anbakubaliana na rushwa ndani ya chama chake.... bado tuna safari ndefu


Msiwe so emotional bila sababu.....Inamaana ametoa taarifa kuwa kuna rushwa ya wazi na hata kama atakata rufaa hakuna wa kumsikiliza maana ndani ya chama chao wale wanaotoa rushwa hawatoi bila kuwa na kinga so he cant waste his time for nothing....If he is to fight back there are so many ways and there is no need ya kuwaambia ata fight vipi ila matokeo ndiyo yataamua kama yeye ni mjinga kiasi hicho ama vipi...Let us join hands with who ever fight against corruption leo hii fight insingekuwa na mafanikio kama people like him ambao wapo ndani hawakuamua kufight against maana hata wao sometimes kama walifanya hivyo wamejifunza they at the end fall a victim....

The fight for curruption is for all of us kama yeye ni corrupt basi mwache atusaidie then siku hiyo tukisha rudisha nchi mikononi mwa raia na kuiondoa mikononi mwa mafisadi hata yeye atatuambia for whose name aliibia nchi na kutufanya sisi wote wajinga...
 
Mr. Zero hana jipya la kuoffer. Alikuwa mmoja wa waasisi wa mfumo unaommaliza. Kama hakuwahi kuwajali watanzania katika uongozi wake, anaomba huruma ya watanzania leo? To hell with him!!!
 
kwaakili za kawaida tuu! Sumae hawezi kuondoka CCM kipindi hiki, anazijua athari zake.Hata kama anania ya dhati ya kuamia CDM.
 
Sumaye:
Hanang'kulikuwa na matumizi makubwa ye fedha, uharamia wa kuhamisha watu... Sitokata rufaa wala sitolalamika chamani maana kila jambo lilikuwa hadharani na media ilitoa taarifa.

Siko CCM kwa ajili ya vyeo... Nchi nyingi zimeingia katika vurugu na kuhatarisha amani ktk uchaguzi,,, Tanzania tusichafue kwa kusababisha matatizo kwa kutimia vibaya umasikini wa Watanzania.

Najua si matamu kwa masikio ya wengine na tusiwanyamazishe wanaozungumzie kwa uwazi.

Mungu ibariki Tanzania

Si mara moja wala mara mbili Mzee Sumaye analalamikia mambo haya ndani ya Chama chake. Mfano, baada ya kutendwa kwenye kusaka nafasi ya kugombea urais mwaka 2005 aliibuka hivihivi. Aache kulalamika sasa kwani amezoea na amekulia humo.

Namshauri akae kimya akubaliane na mfumo huo au ajitoe haraka iwezekanavyo kwenye uchafu anaodai umezagaa nchi nzima ndani ya CCM. Kama ni msafi kwa nini miaka yote hiyo aishi na uchafu? Vinginevyo akae kimya milele.Maana najiuliza angeshinda nafasi hiyo ya NEC pamoja na yeye kuwa na taarifa za vitendo vya rushwa katika chaguzi hizo za CCM angelalamika hivyo? Jibu ni hapana. It is like a very clean maggot that live and feed on farces
 
Sumaye alikuwa na nia ya kutiririka tatizo amevujisha siri mapema. Kama kawaida magamba wakampa angalizo na baada ya kuchekecha akapotezea.Tunao magamba tunaowakubali lakini ninachojua "TIME WILL TELL NOT SO LONG"

Tatizo ndiyo hilo na kama ameonekana ataleta damage basi anaambiwa bw mkubwa tutamshughulikia huyo mtu wako kiakili we kwa sasa tulia na kwakuanzia waka mwangusha chaguzi iliyofuata...Poor TZ hakuna anaye maanisha kupigana kulinda nchi wengi mawazo binafsi kwanza the waTZ wanafuata baadaye...

It truly ameingia mkenge kwakupewa chambo then the ushauri wangu kwake ni kuwa ategemee kuanguka zaidi na zaidi kama ilivyotokea kwa mR. Six.. These people never learn through experience if at all they are not able to discern the invisibles!
 
vipi amezungumzia chochote juu ya ile kauli yake aliyoitoa ktk Uwanja wa Namfua Singida kuwa
"ukitaka mambo yako yakunyookee njoo CCM" ? sasa hapo alimaanisha nini kama sio rushwa na kupendeleana.
leo rushwa hiyo hiyo kwa kuwa imemnyima uongozi analalamika ? mkuki kwa nguruwe?
akamuulize mwenzie aliesema akirudi CCM basi amzini mama yake, amerud basi hadi leo akili yake haijakaa sawa, labda hadi amzini kweli.

Mkuu hapo kwenye RED pasua jibu, weka wazi. Usiwe kama Sumaye na wewe. Teh teh teh
 
hata afanyaje alishawahi kuwepo kwenye system kandamizi sasa analia lia nini sasa, mzee wa white paper mnamkumbuka?
 
Alipokuwa wairi mkuu wa ccm alisema mtu akitaka biashara yake isipate bughudha awe mwanachama wa ccm.
 
n00b, samahani namba kuuliza Alikuwa anaongea mbele ya Camera na mikes au ilikuwa ni mbele ya mtutu?
 
Last edited by a moderator:
Kuhusu Fredrick Sumaye, jana hata kabla ya press co yake nilisema hivi
Sumaye yeye sio mtaji lolote, sio mtaji chochote, na akihama CCM, atajihamia yeye kama yeye, hana wafuasi wowote wa kutishia usalama wa CCM!. Angetishia kuhama yule Mzee wa ....ndio CCM ingetingishika!.

Hata hivyo, sifa za kugombea urais kupitia CCM sio ujumbe wa NEC bali ni kwa mwana CCM yoyote mwenye sifa!, hivyo hata kama Sumaye amebwagwa ujumbe wa NEC na ki..da wake, kisa ki..da huyo pia katembea na Muzeiye, hiyo sio sababu ya yeye kuihama CCM!.

Kwa vile Sumaye hata kitu chochote cha maana zaidi tule tujumba alitotujenga kwa mikopo ya kifisadi ya NSSF, then hana jeuri yoyote ya kuihama CCM wakati tegemeo lake ni mafao ya kustaafu ambayo ni 80% ya current PM!. Japo hata akihama pensheni yake iko pale pale, bali masimango yatammaliza bure!.

Wapiganaji wa kweli ni wale ambao wako tayari to take risk kwa kusimama mbali na uvundo kuwathibitishia watanzania kuwa huku tuliko chama kimetekwa na mafisadi.

Wale kina Sumaye type, wanaopigania nafsi zao, mtawatambua kwa kutokubali kuriski nafasi zao ndani ya CCM ambako mafisadi wana upper hand. Kwa vile CCM ina wenyewe, na baadhi ya wenyewe hao ndio hao hao mafisadi na wengine wao ndio hao kina Sumaye, hapa ni mwendo wa mwenye kisu kikali ndie anayekula nyama, maadamu wenye nguvu ni mafisadi, mwenye nguvu mpishe, hao kina Sumaye type watajikuta kuliko kuriski loosing, wakijua hawawezi kuwashinda, watatumia formular ya 'if you can't beat them, join them' watajiunga nao na wote wakuwa kwenye tenga moja la samaki, na wote watakuwa ndio wale wale!.
P.
Nidhani ni press conference ya kutangaza nia!. Kumbe ni press co ya blah blah!.
P.
 
Katika uchaguzi wa demokrasia, mtu huchaguliwa kwa uwezo na kwa ajili yao kuwatumikia, katika demokrasia ya rushwa, fedha huwachagulia watu mwakilishi kwa ajili ya waliotoa fedha, kama nimetoa fedha kwa ajili yako, na wapiga kura wanakua wapiga mihuri.

Sasa imetoka mtu kuhonga achaguliwe, na sasa mtu anatoa rushwa kununua watu ili apate kujenga mtandao wake na sasa ni rushwa ya kimtandao ambayo ni hatari sana...


Hapa nimeishajua anamzungumzia nani.
 
posho ya UPM mstaafu haitoshi?
Ni busara ukawa kando wanaokuambia urudi kwa siasa wanakudanganya!
Utajajishushia hadhi yako badala ya kuipandisha
 
Kama hicho alichoongea Sumaye ndiyo alichowaitia waandishi wa habari, basi ameanza kuzeeka vibaya.
 
Back
Top Bottom