Sumaye amgwaya Lowassa!

Sumaye amgwaya Lowassa!

Hana jipya. WanaJF naomba kuuliza ivi ukiwa waziri mkuu mstaafu ina maana ukihama chama unakosa haki zako za uwaziri mkuu mstaafu au katika serikali hii ya Tanganyika inakuwaje. Mi nafikiri waziri mkuu unakuwa kiongozi wa wote bila kujali chama. Na stahiki zako unawezapata hata ukihama chama kama wewe ni waziri mkuu mstaafu. Naomba nielezeni
 
Hebu mtafute Pasco hapo atakuwa navyo hivyo vibahasha, kwenye ghafla kama hizo za vibahasha huwa hakosagi.
Mkuu Mzalendo80, si kweli kuwa hafla za vibahasha mimi huwa sikosi, bali nilipokuwa reporter, hivyo vi bahasha, nimevipokea sana!. Bahasha hizo za waandishi mimi nimezihalalisha rasmi hapa, Waandishi wa Habari na Bahasha: Sio Kila Bahasha ni Rushwa ...na kwa sasa mimi sio reporter tena, ni mwandishi wa kujitegemea, situmwi na mtu, siwajibiki kwa mtu, wala siitegemei media yoyote kutoa habari au program zangu!, ukiniona mahali, ujue mimi ndio nimelipa na sio mimi kulipwa na hizo media, kwenye press conferences zangu, mimi ndio huwa navigawa hivyo vibahasha halali.
P.
 
Mpaka hapa navilaumu vyombo vyetu vya habari, vilipata wapi ujasiri wa kutuandikia zile habari, SUMAYE KUPASUA JIPU, SUMAYE KUSEMA YA MOYONI, SUMAYE ATETA NA CHADEMA, NK......wametuweka matumbo joto kwa kudhani labda Sumaye ataongea lolote jipya juu ya Chama chake, analishwa,anapewa usafiri, anapewa mshahara, anapata ulinzi na mazagazaga mengine leo atapata wapi ujasiri wa kukivua nguo chama chake?
Mzee wa watu alisema ataongea na waandishi wa habari basi, hakusema uzushi magazeti yetu wanaotulisha ili wauze makaratasi yao.
 
Mpaka hapa navilaumu vyombo vyetu vya habari, vilipata wapi ujasiri wa kutuandikia zile habari, SUMAYE KUPASUA JIPU, SUMAYE KUSEMA YA MOYONI, SUMAYE ATETA NA CHADEMA, NK......wametuweka matumbo joto kwa kudhani labda Sumaye ataongea lolote jipya juu ya Chama chake, analishwa,anapewa usafiri, anapewa mshahara, anapata ulinzi na mazagazaga mengine leo atapata wapi ujasiri wa kukivua nguo chama chake?
Mzee wa watu alisema ataongea na waandishi wa habari basi, hakusema uzushi magazeti yetu wanaotulisha ili wauze makaratasi yao.

Hawana jeuri ya kuhama hawa waswahili,si mnakumbuka yule mungine nae aliwahi kuitisha press conference kama hii kule kwake monduli nadhani mwaka huu mwanzoni,tukawekwa matumbo joto mwisho wa siku akaishia kutapatapa tu,mwisho wa siku hakuna mwanachama wa ccm aliye mkubwa kuliko chama,wote wanakiogopa chama.Jamaa wa monduli aliishia kulialia tu kama huyu ndugu yake,alilialia kama ifuatavyo:


Date: Wednesday, 19 October, 2011, 22:28

NDUGU wana habari nimewaita katika mkutano huu leo kwa sababu moja kubwa, kutoa ufafanuzi kuhusu matukio ambayo yamekuwa yakitokea huku yakinihusisha mimi binafsi kwa namna ambayo sasa yanatishia ustawi na mshikamano wa kimaadili, kihistoria na kikazi miongoni mwa viongozi na baina ya wanachama wa Chama Cha Mapinduzi (CCM).

Ndugu wana habari, naamini mmekuwa mkifuatilia kwa karibu habari zinazoripotiwa katika baadhi ya vyombo vya habari zinazolihusisha jina langu na harakati kadha wa kadha chafu ambazo hata mimi mwenyewe ninayehusishwa nazo huwa nazisikia na kuzijua baada ya kuwa zimesharipotiwa katika vyombo hivyo vya habari.

Uamuzi wangu wa kukutana nanyi leo hauna makusudi ya kuzozana na vyombo vya habari wala kwenda kinyume na utamaduni wa kimaadili wa ndani ya chama changu unaotutaka viongozi kujadili masuala yanayokihusu chama chetu ndani ya vikao vyetu rasmi vya kimaamuzi bali kutoa ufafanuzi na angalizo kwa pande zote hizo mbili ambazo zinaguswa na matukio yanayoendelea kutokea leo hii.

Moja ya mambo ambayo yameligusa jina langu kwa namna hiyo ni lile linalonihusisha eti na kundi moja la wanasiasa ambao wamekuwa na mikakati ya kumhujumu mwenyekiti wetu wa chama, Mheshimiwa Rais Jakaya Kikwete. Hakuna shaka ni madai ya kipuuzi, kizushi na yenye malengo machafu.

Hawakuishia hapo sasa wamefikia hatua ya kuvitumia vyombo hivyo hivyo vya habari na kufikia hatua ya kudai kwamba nimeanza kuandaa orodha ya kile wanachokiita madhambi ya Rais Kikwete ambayo wanadai nimepanga kuyasoma wakati wa kikao kijacho cha Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM (CCM).


Ninaamini kwa dhati kabisa kwamba, waandishi wa habari wanaofuatilia kwa karibu na kwa umakini mwenendo wa masuala ya kisiasa nchini wanatambua kwamba, watu wanaopenyeza taarifa hizi katika vyombo vya habari wanafanya hivyo kwa malengo ya kufikirika ya kujisafishia njia kisiasa.

Ni jambo lisiloingia akilini kunihusisha na kile kinachoitwa mikakati ya kumhujumu rais au chama ambacho mimi ni kada wake wa muda mrefu, mbunge anayetokana na chama hicho hicho na mtu ninayeiongoza Kamati nyeti ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama na zaidi ya yote kiongozi wa ngazi mbalimbali za kisiasa na kiserikali nilizowahi kushikilia.

Kuhusu hili napenda kusema kwa uwazi kwamba, mbali ya ukweli kuwa sijapata kufikiria hata mara moja kuhusu hicho wanachokiiita mabaya au madhambi ya rais, sina na wala siijui hiyo wanayoitaja kuwa ni orodha ya mabaya ya namna yoyote dhidi ya Rais Kikwete.

Mbali ya ukweli kwamba huo ni uongo wa wazi, silika yangu kama mwanasiasa na mtu mwenye dhamana kubwa kwa watu wa Monduli na kwa taifa langu haiwezi kamwe kunituma nianze kupanga mikakati ya kumhujumu kiongozi wetu mkuu au chama ambacho kimenilea na mimi mwenyewe nikakitumikia kwa uadilifu na kwa juhudi kubwa pengine kuliko ilivyo kwa hao wazushi.

Ndugu wana habari, nitakuwa ni mtu wa mwisho kufikiria au kupanga kumhujumu mwenyekiti wetu wa chama na rais ambaye nimemuunga mkono kwa dhati kwa muda mrefu na kushirikiana naye katika harakati nyingi za kifikra na za kiuongozi katika ngazi mbalimbali na kwa miaka mingi. Nilipata kulisema hili na leo nalirudia tena. Mimi na na Rais Kikwete hatukukutana barabarani.

Tangu serikali ya Awamu ya Nne iingie madarakani kuna kundi la watu limekuwa likifanya juhudi kubwa kunigombanisha na Rais wakitumia kila aina ya hoja za kupikwa.


Kundi hilo ambalo sasa limekuja na uzushi mpya, ndilo ambalo mwaka juzi lilipenyeza ndani ya chama chetu na katika jamii hoja kwamba nilikuwa nimejipanga kugombea urais kwa tiketi ya chama chetu katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka jana, likidai kwamba nilikuwa na malengo ya kumpinga Rais Kikwete ambaye wakati huo alikuwa ndiyo kwanza anaelekea kukamilisha ngwe yake ya kwanza madarakani.

Katika kuthibitisha kwamba watu hao walikuwa na hila, nilipohojiwa na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam miezi kadhaa kabla ya Uchaguzi Mkuu nilijibu kwa kifupi nikisema, hatutukutana na Rais Kikwete barabarani.

Nayasema haya na kurejea baadhi ya mambo huku nikiwa na imani ya dhati kabisa kwamba, viongozi wenzangu ndani ya CCM na wale walio na nia njema na chama chetu na taifa hili, akiwapo Mwenyekiti wetu wa Taifa, Mheshimiwa Rais Jakaya Kikwete hawawezi kamwe kuamini au kushawishiwa na propaganda chafu zinazoendeshwa na kikundi kidogo cha wanasiasa hao kwa zaidi ya miaka mitatu sasa ambao malengo yao ya kisiasa yako wazi na yanayojulikana.

Kama hiyo haitoshi, wanasiasa hao hao baada ya kulitumia jina langu kama ajenda yao ya uzushi wa kila namna, sasa wameanza kunihusisha hata na matukio ya kisiasa kama yale yaliyotokea majuzi tu hapa Arusha.

Ndugu wana habari baada ya kukaa kimya kwa muda mrefu sasa, nimeamua kuanza kuchukua hatua mbalimbali za kisiasa na kisheria ambazo naamini zitatoa majibu sahihi dhidi ya wale wote walio nyuma ya ajenda hizi chafu kwa lengo la kuweka kumbukumbu sawia ndani ya chama changu na kwa jamii nzima ya Watanzania ambao kwa muda mrefu wamelishwa mambo mengi ya kizushi na wakati mwingine ya hatari dhidi yangu.

Tayari nimepanga kuanza kuwasiliana na kuwasilisha malalamiko yangu kwa mamlaka husika zinazosimamia mienendo ya kimaadili na weledi wa kitaaluma wa vyombo vya habari kama vile Msajili wa Magazeti na Baraza la Habari Tanzania.


Kama hiyo haitoshi, baada ya kukaa kimya kwa muda mrefu nimeshaanza kufikiria na kujipanga kuanza kuchukua hatua za kisheria dhidi ya waandishi wa habari na wahariri ambao kwa makusudi wameamua kutumia vibaya uhuru wa habari ambao serikali imeutoa. Naamini sote tunakubaliana kuwa; ‘UHURU USIO NA NIDHAMU NI FUJO.'

Ndugu zangu wana habari napenda kutumia fursa hii kutoa wito kwa viongozi wa chama na wale wa serikali kumsaidia rais na chama chetu kwa kutimiza ipasavyo wajibu wao badala ya baadhi yao tena wakiwamo wale wenye dhamana nyeti kuwa vinara wa kutunga mambo ya kufikirika kama haya wanayofanya leo.

Viongozi wenye mawazo ya namna hiyo wanapaswa kutambua kwamba, muda adhimu wanaoutumia kubuni na kuzusha uongo kila kukicha mbali ya kuwavunjia heshima wao wenyewe unavidhalilisha vyombo vya dola ambavyo vinafanya kazi kubwa kuhakikisha hujuma za namna yoyote dhidi ya viongozi na taifa zinadhibitiwa.

Nikiwa Mwenyekiti wa Kamati ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama ya Bunge na mtu aliyepata kuwa Waziri Mkuu ninatambua na kuiheshimu kwa dhati kazi hiyo kubwa inayofanywa kwa weledi mkubwa na taasisi mbalimbali za dola zenye wajibu wa kuhakikisha ulinzi na usalama wa viongozi wetu na taifa kwa ujumla.

Ndugu wanahabari nazungumza nanyi baada ya kurejea nikitokea katika nchi za Nigeria, Malaysia, Singapore, India, Uingereza, Ufaransa na Ujerumani ambako nilipata fursa ya kujifunza mambo mengi lakini moja muhimu likiwa ni namna vyombo vya habari (kwa maana ya waandishi wa habari) na wanasiasa wanavyotumia muda wao mwingi kujadili masuala yanayogusa maisha na maendeleo ya watu wao.



Tofauti na kile wanachofanya wenzetu hapa nyumbani, ninyi wanahabari na sisi wanasiasa tumekuwa tukitumia muda wetu mwingi kujadili watu na propaganda za kisiasa zisizo na tija wakati tukitambua kwamba, taifa linakabiliwa na changamoto nyingi kama zile za kuhamasisha uwekezaji wa ndani na nje ya nchi, kuimarisha mifumo ya utawala bora, kuporomoka kwa thamani ya shilingi kila kukicha, mdororo wa uchumi, tatizo kubwa la ajira kwa vijana, kushuka kwa kiwango cha elimu na ugumu wa maisha kwa ujumla. TUNAPASWA KUJISAHIHISHA.

AHSANTENI KWA KUNISIKILIZA
 
kachanganyikiwa kushindwa na mwanamke, kama rusha ilitawala kwenye uchaguzi,utaratibu wa nini kifanyike anaujua. yaani kwa hii press aliyoitisha ameonesha udhaifu wake na kumpaisha juu mshindani wake
 
  • Thanks
Reactions: Ame
Sumaye has been P our PM for 10 ten fuc king yrs! Anatutaka nini? Alianzisha takrima Leo analia lia nini like a hIgh school girl on the first day out?

Kaka punguza ukali wa maneno...otherwise utakula ban mda si mrefu.
 
Msiwe so emotional bila sababu.....Inamaana ametoa taarifa kuwa kuna rushwa ya wazi na hata kama atakata rufaa hakuna wa kumsikiliza maana ndani ya chama chao wale wanaotoa rushwa hawatoi bila kuwa na kinga so he cant waste his time for nothing....If he is to fight back there are so many ways and there is no need ya kuwaambia ata fight vipi ila matokeo ndiyo yataamua kama yeye ni mjinga kiasi hicho ama vipi...Let us join hands with who ever fight against corruption leo hii fight insingekuwa na mafanikio kama people like him ambao wapo ndani hawakuamua kufight against maana hata wao sometimes kama walifanya hivyo wamejifunza they at the end fall a victim....

The fight for curruption is for all of us kama yeye ni corrupt basi mwache atusaidie then siku hiyo tukisha rudisha nchi mikononi mwa raia na kuiondoa mikononi mwa mafisadi hata yeye atatuambia for whose name aliibia nchi na kutufanya sisi wote wajinga...
Thanks for not being emotional. Kweli tunawahitaji viongozi shupavu na mahiri kama Sumaye am,baye anachukia rushwa na kuipiga vita kwa maneno
 
  • Thanks
Reactions: Ame
Hawana jeuri ya kuhama hawa waswahili,si mnakumbuka yule mungine nae aliwahi kuitisha press conference kama hii kule kwake monduli nadhani mwaka huu mwanzoni,tukawekwa matumbo joto mwisho wa siku akaishia kutapatapa tu,mwisho wa siku hakuna mwanachama wa ccm aliye mkubwa kuliko chama,wote wanakiogopa chama.Jamaa wa monduli aliishia kulialia tu kama huyu ndugu yake,alilialia kama ifuatavyo:

Na hawa waandishi wetu vp huwa hawaulizi maaswali maana kuna mengi ya kumuuliza, kama alivyosema mchangiaji mmoja kwamba ikiwa hakati rufaa it means amekubaliana na rushwa ndani ya chama chake, hakika sijaona lolote la maana aliloongea zaidi ya MUNGU IBARIKI TANZANIA.
 
  • Thanks
Reactions: Ame
Kakutuma huku kuja kuwatoa watu kwenye mada?nimeonamlolongo wa mahoteli tuuu,hakuna chochote cha maana,kwenda zako gamba wewe.
mie sijamuelewa alieweka hiyo link,
1. hizo hoteli ni za sumaye
2. za mpinzani wake/ magamba mwenzie?
3. ndo huwa anafikia(sumaye)
4................
vinginevyo jamaa mpumbavu au atupe korilesheni ya uzi huu na hizo hoteli
 
Rushwa alifanya yeye 2005 kuwania Urais kwa kuwapa wajumbe wa NEC kupitia Mkuu wa Mkoa wa Mtwara. enzi hizo (Mpare) wajumbe hao walikunja buku 300 kila mmoja South corridor na Hyanda a juu walimpa Mwandosya.

Hiyo Mikoa ya Lindi & Mtwara Mama wa Mgombea aliwaonya hizo hela kuleni na kura mpeni Shemeji yenu ndio maana 3 bora NEC hawakumpitisha licha ya kutoa rushwa ndani ya CCM.

Miradi ya Kilimo ya IFAD ilijaa rushwa na ukabila Shinyanga Dodoma na Manyara ktk Mashamba ya Manyata na Basuto huingii hata kwa Rushwa leo kasahau.

Nimefurahi alivyosema atatulia huo ndio uungwana kuliko kuhama CCM.

Huyo aliyemzidi kete hataupata Urais kwani rushwa ipo juu tu huku chini kwa mpiga kura haipo
 
tatizo la ccm ni kuwahi kuzibana midomo, tena kwa vitisho. Alianza lowassa kipindi kile akiwaita waandishi hadi monduli. Akabwabwaja pumba. Akaja mwakyembe akasema ataanika kila kitu. Mara kimya, mara yuko kanisani. Akaja ulimboka. Mara kimya. Sasa huyu sumaye, mara naye anabwabwaja.
 
Sumaye hata angeenda CDM, aende CUF, aanzishe chama chake hakuna legacy aliyoiacha itakayokuwa mvuto kwa uzalendo. Ni mmoj kati ya waziri mkuu aliyeboronga kabisa. Walitoka madarakani na sifa mbaya sana yeye na mkuu wake Ben. Nakuambia hata Pinda akistaafu atakuwa na heshima kuliko huyu mla rushwa anayelialia kuzidiwa kete na wala rushwa wenzake. To hell Sumaye. To hell Lowasa. To hell Sitta. To hell Mwakyembe. To hell Benard Membe. To hell Asha R Migiro. To hell all CCM Hyenas.
 
  • Thanks
Reactions: Ame
Pamoja nimechelewa kuuona uzi huu ila nimeishia page ya kwanza tu kuusoma, sina muda wakuwasikiliza wapuuzi, Sumaye is Dead snake. That's it.
 
Takrima si ilianza kwa Sumaye!! S yeye aliua agenda ya Uzawa! Si yeye alidhoofisha kabisa upinzani nchini akiwa na boss wake BM. Hili ni fundisho kuwa "kiongozi lazima uwe visionary" na ukiona "manyoya, ujue kaliwa". Habari ndio hiyo!!
 
hili jamaa punga sasa kapoteza muda wa nini kwa waandishi? na waandishi wetu hovyo kabisa kesho utaona wanaandika huu upuuzi
 
• Akana kuwa na uhasama naye, adai hamwogopi mtu

na Edson Kamukara

WAZIRI Mkuu mstaafu, Fredrick Sumaye, ametoa dukuduku lake la moyoni akisema hana uhasama na Waziri Mkuu aliyejiuzulu Edward Lowassa na kubainisha kuwa rushwa ya kimtandao iliyokighubika Chama cha Mapinduzi (CCM), ndiyo iliyomwangusha wilayani Hanang'.

Sumaye ambaye amepigwa mweleka kwenye uchaguzi wa ujumbe wa Halmashauri Kuu (NEC) Taifa kupitia wilayani Hanang' na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Uwekezaji na Uwezeshaji), Mary Nagu, alikutana na wanahabari kuelezea mwendo mzima wa uchaguzi huo na hatima ya CCM.

Akizungumza kwa kujiamini huku akinukuu kauli zake za nyuma kuhusu mwenendo wa rushwa ndani ya chama chake, alisema uchaguzi wa Hanang' ulighubikwa na matumizi makubwa ya rushwa, vitisho vingi, uharamia wa kuhamisha wapiga kura usiku na maovu mengineyo mengi.

"La msingi ni kuwa mimi sijakata na wala sitakata rufaa ya kupinga matokeo wala kupeleka malalamiko katika chama changu kwa sababu yaliyokuwa yakitendeka yalikuwa yanafahamika," alisema.

Katika kile kinachoweza kutafsiriwa kama kuondoa uvumi uliokuwepo kuwa Sumaye na Lowassa wana ugomvi wa kisiasa hasa wakati huu wa kujipanga kuelekea mbio za urais 2015, kiongozi huyo alisema hajazungumza na mtu kuhusiana na mambo hayo.

Sumaye alisema taarifa hizo zimekuwa zikisambazwa na kunukuliwa kuwa zimetoka kwenye chanzo kilicho karibu naye, lakini akafafanua kuwa hawezi kupambana na Lowassa kwa sababu hana uhasama naye.

"Nikiamua kugombea urais sitagombea kwa sababu ya mtu fulani bali nitagombea kwa sababu ya nchi na wananchi wa Tanzania," alisema.

Akifafanua kuhusu vitendo vya rushwa ndani ya CCM, alisema kuwa nchi nyingi hasa zenye demokrasia changa kama Tanzania zimeingia katika vurugu na kuhatarisha amani na utulivu nyakati za uchaguzi.

Sumaye alisema madaraka yatakuja tu kama wananchi wapiga kura wanaona wewe ndiye utayewafaa na wala wasirubuniwe kwa fedha au jambo lolote kwa kutumia vibaya nafasi ya umaskini wao.

"Hivi leo tunavyoongea hali ya rushwa wakati wa uchaguzi imekuwa mbaya zaidi. Katika uchaguzi wa kidemokrasia wapiga kura humchagua mwakilishi wanayemtaka kwa sababu ya uwezo wake yaani humchagua mwakilishi wao kwa ajili yao.

"Katika demokrasia iliyopondeka kwa rushwa, fedha huwachagulia watu mwakilishi kwa ajili ya waliotoa fedha. Wapiga kura ni wapiga mihuri tu," alisema.

Sumaye bila kutaja majina ya wahusika, alisema hali imetoka kwenye kuhonga ili achaguliwe katika eneo lake na badala yake kuna rushwa za kimtandao ambapo mtu hutoa fedha katika maeneo mbalimbali nchini ili watakaochaguliwa wawe wafuasi wake mbele ya safari atakapowahitaji.

"Uchaguzi huu umeghubikwa sana na matumizi makubwa ya fedha za rushwa. Suala la rushwa katika nchi yetu na katika CCM siyo mgeni lakini sasa tatizo hilo limeota mizizi na linazidi kuwa kubwa," alisema.

Kuhusu kwenda CHADEMA
Sumaye alikanusha vikali akisema hajawahi kukutana na kiongozi yeyote wa CHADEMA wala chama chochote cha upinzani.
Lakini akabainisha kuwa hawapaswi kufikia kudai kuwa vyama vya upinzani au viongozi wake ni maadui wa CCM.

"Mimi ningekuwa nimekutana nao ningesema tu mbona hata hao wengine wanaoutafuta urais kwa udi na uvumba huwa wanakutana nao? Alihoji.

Alisema yeye ni mwanachama mwaminifu wa CCM na kwamba alishawahi kusema kuwa hayuko kwa ajili ya cheo na wala kukosa ujumbe wa NEC na hasa kwa njia iliyotumika hakumnyimi usingizi wala hahuzuniki kugombea urais kwa tiketi ya CCM endapo ataamua kufanya hivyo.

Sumaye alisema kama ni matatizo, vyama vyote vina kasoro zake, hivyo haoni kama kuhama chama ni suluhu na kutamba kuwa kushindwa kwake kumempa nguvu zaidi na hivyo akiamua kugombea urais lazima apitie CCM.

Kuhusu TAKUKURU
Alipoulizwa kuhusu utendaji wa Taaasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) kama imetimiza wajibu wake kushughulikia tuhuma za rushwa kwenye uchaguzi wilayani Hanang', Sumaye alitafakari kidogo kisha akajibu kwa kutumia mfano.

"Hivi kama nyie wanahabari mmekuja hapa mkanisikiliza haya ninayowaeleza, halafu kesho watu wanasoma kwenye magazeti yenu hawakuti kitu au kwenye televisheni hawaoni, wanaweza kusema mmetimiza jukumu lenu? Alihoji Sumaye.

Kada huyo aliwaachia wanahabari watafsiri wenyewe kama kweli TAKUKURU inatimiza wajibu wake katika kushughulikia madai ya rushwa kwenye chaguzi.

"Napenda nitambue kuwa haya ninayoyasema si matamu masikioni mwa baadhi yetu lakini ni vema tukayasikiliza kwa makini na kuchukua hatua chanya ili yasilete madhara zaidi katika jamii na wala tusidiriki kuwanyamazisha wanaoyazungumzia
 
Sumaye hana ubavu wa kupambana na Lowasa hata kwa dakika moja tu,ila ni kweli chaguzi za ccm zimetekwa na wanamtandao,kumbuka uchaguzi 2010 Selelii,mh sitta (uspika) na wengine wengi.
 
Back
Top Bottom