Sukari: Dr. Ackson Tulia (Naibu Spika), upongezwe?

Sukari: Dr. Ackson Tulia (Naibu Spika), upongezwe?

Hoja ya vibali haina uhusiano na majadiliano, kwa nini walizuia uagizaji hali wakijua viwanda vya ndani havikizi, serekali ya jpm ijitafsiri iache kukurupuka


havikizi>>>>>>>>>>>>>>>>>havikidhi

serekali>>>>>>>>>>>>>>>>>serikali

ijitafsiri>>>>>>>>>>>>>>>>>ijitathmini
 
haya ni maoni ya mke wangu name baba wa familia naungana nayo kuwa ni kweli DR TULIA hakuwa sawa kuzima hoja hiyo ukilinganisha kuwa yeye mwenyewe haoni tatizo hili kwakuwa yeye haigizi sukari alipaswa kutumia ubinadamu tu. kuna wakati mwingine hii kauli ya hapa kazi tu inawaponza wawakilishi wetu hasa wa upande wa chama changu
 
ongezeko la bei ya sukari zaidi tshs1000/= kwa kilo moja bado kuna baadhi ya watanzania wanaona hoja ya kuzungumzia swala hilo haina mashiko? hakika huu ushabiki wa kisiasa unatupeleka kusiko
 
Zitto alifurahia Rais alipozuwia leo anajisikiaje?
 
Walimchagua mwenyewe waache waisoma namba wazee wa kujitoa ufahamu wamekutana hapo
 
Hoja ya vibali haina uhusiano na majadiliano, kwa nini walizuia uagizaji hali wakijua viwanda vya ndani havikizi, serekali ya jpm ijitafsiri iache kukurupuka
Hivi kuna mtanzania yeyote anaye jua wapi JPM ana ipeleka nchi hii, au ni ushabiki tu. Sababu mpaka sasa tunacho sikia ni kutumbua majipu tu, sija sikia akisema ndani ya miaka mitano hii tuta itoa nchi hapa na kuifikisha hapa au ndani ya miaka kumi ijayo. Hata kama utakusanya kodi vipi lakini kama huna vision na mission hufiki kokote, itabaki kutoa fedha kasma hii kupeleka kule, na kutoa kule kupeleka kule kutokana na matukio ya hapa kwa hapa mwisho muda unaisha ukiwa unapambana na dharula.
 
Huyo aliwekwa hapo na mkuu wa kaya unafikir hata mpige kelele yeye hana chakupoteza zaid nikulinda yote ya aliyemuweka hapo
 
Leo asubuhi,Mbunge wa Nzega Mjini, Hussein Bashe ( CCM) alitoa hoja ya haja ya dharura kulitaka Bunge kujadili uhaba wa sukari nchini. Bashe alitoa mfano wa bei ya sukari kwasasa,kuthibitisha uhaba uliopo kwa sasa,kuwa kilo moja inauzwa kati ya 3000 na 4000.

Pamoja na kupata uungwaji mkono utakiwayo,kwa Wabunge wenzake kusimama,Kiti cha Spika chini ya Dr. Tulia kiliizima hoja hiyo ya Bashe. Naibu Spika Dr. Tulia alisema kuwa hakuna haja kuwepo mjadala wa uhaba wa sukari nchini kwa kuwa Waziri Mkuu Majaliwa alishatoa taarifa ya serikali.

Waziri Mkuu Majaliwa alisema kuwa Serikali ina nia ya kutoa vibali vya kuagiza sukari. Naibu Spika yuko sawa kuizima hoja ya Bashe?

Mzee Tupatupa wa Lumumba (kwasasa Dodoma)
Hako kama mama kapo pale sijui kwa maslahi ya nani?
 
Huyo wamvue tu hicho cheo maana inaonekana yuko hapo kwa kazi maalumu na wabunge wa CCM walifanya kosa kuchagua mtu ambae alikuwa chaguo la watu fulani.
Hao wabunge wa ccm hakuna wajuwalo zaidi ya kupiga makofi tu
 
Huyu naibu spika Dk Ackison Tulia nadhani aliteuliwa na Mh Rais kwa kazi maalum na sasa kazi hiyo anaifanya vizuri kweli.. Kamzima mpaka Mh Ndugai yeye sasa ndio top.. Sukari itafika mpaka 4000 na Watanzania tulivyo tunaenda kulalamikia dukani bila kujua muuzaji naye kanunua bei ghali
Tuliyasema hapa vijana wa lumumba wakataka kututoa roho kwa matusi sasa wote ndio tunaisoma namba bila kujali kama huyu ni ccm au ni chama cha upinzani
 
Nampongeza sana dk tulia, kuna mambo mengi sana yakujadiliwa, istoshe waziri mkuu keshalitolea ufafanuzi, chicho kiti kakitendea haki kweli kweli
Utakuwa haupo Tanzania,sukari kununuliwa 3000/4000 unachulia poa!
 
Leo asubuhi,Mbunge wa Nzega Mjini, Hussein Bashe ( CCM) alitoa hoja ya haja ya dharura kulitaka Bunge kujadili uhaba wa sukari nchini. Bashe alitoa mfano wa bei ya sukari kwasasa,kuthibitisha uhaba uliopo kwa sasa,kuwa kilo moja inauzwa kati ya 3000 na 4000.

Pamoja na kupata uungwaji mkono utakiwayo,kwa Wabunge wenzake kusimama,Kiti cha Spika chini ya Dr. Tulia kiliizima hoja hiyo ya Bashe. Naibu Spika Dr. Tulia alisema kuwa hakuna haja kuwepo mjadala wa uhaba wa sukari nchini kwa kuwa Waziri Mkuu Majaliwa alishatoa taarifa ya serikali.

Waziri Mkuu Majaliwa alisema kuwa Serikali ina nia ya kutoa vibali vya kuagiza sukari. Naibu Spika yuko sawa kuizima hoja ya Bashe?

Mzee Tupatupa wa Lumumba (kwasasa Dodoma)
Kimsingi yuko sahihi. Hakuna Baja ya kujadili jambo dogo kama hilo. Itakuwa ni kupoteza muda. Suala hapa ni sukari kupatikana. Na kupatikana ya kutosha ni kuagiza nje tu, jambo dogo tu lisilohitaji mjadala wa Bunge. Serikali itoe vibali watu walete sukari. Mh. Rais angepiga marufuku uingizaji mitumba nchini ningepiga makofi kumpongeza. Tunashindwa kufikiri namna ya kuzalisha nguo kwa sababu ya hii mitumba.
 
Tuliyasema hapa vijana wa lumumba wakataka kututoa roho kwa matusi sasa wote ndio tunaisoma namba bila kujali kama huyu ni ccm au ni chama cha upinzani
Cha msingi walalahoi tujioganize tuandamane kupinga ongezeko la hiyo bei
 
Wakati wa mkwamo wa uchumi wa ulaya miaka ya 1930s,ujerumani nayo haikuachwa na mtikisiko huo, alipochukua madaraka Adolf Hitler alionekana kama mkombozi wa hali mbaya ya uchumi inayowakabili. Msimamo wake aliouchukua wa chuki dhidi ya wayahudi akiwalaumu ndiyo sababu ya matatizo yote yaliwavutia watu wengi wakawa wanaimba sifa zake. Kilichotokea baadae dunia hadi leo wanakumbukia, walitengengeneza mmoja wa madikteta aliyesababisha maafa katika historia ya dunia hii.

Dikteta anapenda kusifiwa, hapendi kukosolewa (rejea kesi ya kijana aliyeita bwege), na asiyetaka kukosolewa ataminya uhuru wa vyombo vya habari (kuzuia matangazo live ya bunge) , atataka kuhodhi madaraka yote(bunge, mahakama mifano tunaiona) , ataweza puppets wake ili wawe answerable kwake (tunamuona na mfano ndiyo huyo mama hapo bungeni), wabunge wa CCM nawaomba waendelee kusema tu ndiiiiyooooo! Nawaapia wakija kushtuka na uzwazwa wao it will be too late, haijachukua hata miezi sita tunaanza kuisoma namba, na bado tuna miaka minne na miezi sita TITAKOMA!!!
 
Wakati wa mkwamo wa uchumi wa ulaya miaka ya 1930s,ujerumani nayo haikuachwa na mtikisiko huo, alipochukua madaraka Adolf Hitler alionekana kama mkombozi wa hali mbaya ya uchumi inayowakabili. Msimamo wake aliouchukua wa chuki dhidi ya wayahudi akiwalaumu ndiyo sababu ya matatizo yote yaliwavutia watu wengi wakawa wanaimba sifa zake. Kilichotokea baadae dunia hadi leo wanakumbukia, walitengengeneza mmoja wa madikteta aliyesababisha maafa katika historia ya dunia hii.

Dikteta anapenda kusifiwa, hapendi kukosolewa (rejea kesi ya kijana aliyeita bwege), na asiyetaka kukosolewa ataminya uhuru wa vyombo vya habari (kuzuia matangazo live ya bunge) , atataka kuhodhi madaraka yote(bunge, mahakama mifano tunaiona) , ataweza puppets wake ili wawe answerable kwake (tunamuona na mfano ndiyo huyo mama hapo bungeni), wabunge wa CCM nawaomba waendelee kusema tu ndiiiiyooooo! Nawaapia wakija kushtuka na uzwazwa wao it will be too late, haijachukua hata miezi sita tunaanza kuisoma namba, na bado tuna miaka minne na miezi sita TITAKOMA!!!

MKUU, pamoja na mapungufu ya Adolf Hitler lakini utawala wake wa mkono wa chuma aliweza kufufua uchumi wa Ujerumani, kuiendeleza kisayansi na kiteknolojia hakuna Taifa lolote Duniani lilikuwa linaizidi Ujerumani kata nyanja mbili tajwa hapo juu.

Kosa kubwa alilofanya ni kuanzisha vita hasa hasa operation Barbarosa ilimtia hasara kubwa na kuvuruga kabisa Uchumi wa Ujerumani na miundombinu yake yote, askali na raia wengi kupoteza maisha, kama Hitler hasingeanzisha vita Ujerumani ingekuwa mbali sana kimaendeleo, sayansi na teknolojia kuliko Marekani.
 
Back
Top Bottom