Sukari: Dr. Ackson Tulia (Naibu Spika), upongezwe?

Sukari: Dr. Ackson Tulia (Naibu Spika), upongezwe?

VUTA-NKUVUTE

JF-Expert Member
Joined
Nov 25, 2010
Posts
6,140
Reaction score
18,006
Leo asubuhi,Mbunge wa Nzega Mjini, Hussein Bashe ( CCM) alitoa hoja ya haja ya dharura kulitaka Bunge kujadili uhaba wa sukari nchini. Bashe alitoa mfano wa bei ya sukari kwasasa,kuthibitisha uhaba uliopo kwa sasa,kuwa kilo moja inauzwa kati ya 3000 na 4000.

Pamoja na kupata uungwaji mkono utakiwayo,kwa Wabunge wenzake kusimama,Kiti cha Spika chini ya Dr. Tulia kiliizima hoja hiyo ya Bashe. Naibu Spika Dr. Tulia alisema kuwa hakuna haja kuwepo mjadala wa uhaba wa sukari nchini kwa kuwa Waziri Mkuu Majaliwa alishatoa taarifa ya serikali.

Waziri Mkuu Majaliwa alisema kuwa Serikali ina nia ya kutoa vibali vya kuagiza sukari. Naibu Spika yuko sawa kuizima hoja ya Bashe?

Mzee Tupatupa wa Lumumba (kwasasa Dodoma)
 
Hoja ya vibali haina uhusiano na majadiliano, kwa nini walizuia uagizaji hali wakijua viwanda vya ndani havikizi, serekali ya jpm ijitafsiri iache kukurupuka
 
Leo asubuhi,Mbunge wa Nzega Mjini, Hussein Bashe ( CCM) alitoa hoja ya haja ya dharura kulitaka Bunge kujadili uhaba wa sukari nchini. Bashe alitoa mfano wa bei ya sukari kwasasa,kuthibitisha uhaba uliopo kwa sasa,kuwa kilo moja inauzwa kati ya 3000 na 4000.

Pamoja na kupata uungwaji mkono utakiwayo,kwa Wabunge wenzake kusimama,Kiti cha Spika chini ya Dr. Tulia kiliizima hoja hiyo ya Bashe. Naibu Spika Dr. Tulia alisema kuwa hakuna haja kuwepo mjadala wa uhaba wa sukari nchini kwakuwa Waziri Mkuu Majaliwa alishatoa taarifa ya serikali.

Waziri Mkuu Majaliwa alisema kuwa Serikali ina nia ya kutoa vibali vya kuagiza sukari. Naibu Spika yuko sawa kuizima hoja ya Bashe?

Mzee Tupatupa wa Lumumba (kwasasa Dodoma)
Waziri mkuu ana majukumu mengi yatupasa kumkumbusha huku mtaani hali mbaya sukari imekuwa anasa
 
Huyu naibu spika Dk Ackison Tulia nadhani aliteuliwa na Mh Rais kwa kazi maalum na sasa kazi hiyo anaifanya vizuri kweli.. Kamzima mpaka Mh Ndugai yeye sasa ndio top.. Sukari itafika mpaka 4000 na Watanzania tulivyo tunaenda kulalamikia dukani bila kujua muuzaji naye kanunua bei ghali
 
Nampongeza sana dk tulia, kuna mambo mengi sana yakujadiliwa, istoshe waziri mkuu keshalitolea ufafanuzi, chicho kiti kakitendea haki kweli kweli
 
Kulikuwa hakuna haja ya kuizima hiyo hoja.

Serikali lazima ikubali kusikiliza mawazo ya wananchi kupitia wawakilishi wao, kama serikali inakuja na mipango yake na bado inapwaya kukabili tatizo kwanini isisikilize mawazo ya wengine??
 
nani aukosoe serikali wakati tuli.a yupo kuikingia kifua
 
Nampongeza sana dk tulia, kuna mambo mengi sana yakujadiliwa, istoshe waziri mkuu keshalitolea ufafanuzi, chicho kiti kakitendea haki kweli kweli
Ushabiki mwingine hauna maana kabisa, sasa 'chicho' ndo nini?
 
Kwani hamkujua kazi maalum iliyomuweka hapo?Ndio hiyo anaifanya!Wapinzani walipohoji muhimili wa bunge kuingiliwa na serikali katika kuwapata viongozi wake mliwaponda,sasa wananchi ndio tunaisoma namba!
 
Wabunge wa ccm ndio wanatusababishia haya mateso wanashindwa kusimamia serikali yao an kama naibu spika anawaburuza wapige kura ya kutokuwa na imani nae waache kulilia mtaani maisha magumu sana tunatumbuliwa sisi badara ya majipu
 
Nampongeza sana dk tulia, kuna mambo mengi sana yakujadiliwa, istoshe waziri mkuu keshalitolea ufafanuzi, chicho kiti kakitendea haki kweli kweli
Kama umebahatika kupita kwenye mfumo wa Elimu unaotumika hapa nchini na niliotumia na mm mpaka naandika hiki ninacho kiandika naujutia sana mfumu huu wa Elimu ulio kufanya uandike ujinga huu hapa maana wewe ni hamnazo kabisa
 
Huyu Tulia ndani miaka 5 nae ataisoma namba! Ataomba poo mwenyewe arudi alikotoka!
 
Nampongeza sana dk tulia, kuna mambo mengi sana yakujadiliwa, istoshe waziri mkuu keshalitolea ufafanuzi, chicho kiti kakitendea haki kweli kweli
Hakuna pongezi ktk swala kama hilo wakat ukweli walikurupuka kuzuia sukari ya nje huku iliyopo haikidhi mahitaji so ametumia ubabe tu viongoz hawa hatukuwachagua aina ya dr tulia zaid atateuliwa kla mwaka wa election
 
Back
Top Bottom