SUGU mahakamani leo tar.11/9/2013 DODOMA

SUGU mahakamani leo tar.11/9/2013 DODOMA

Status
Not open for further replies.
Sasa mzifuate hizo sheria za nchi mkivunja sheria lazima mpigwe tu hakuna jinsi

wema_1, sheria ni kwa ajili ya watu wote, mimi wewe na wengine hivyo inabidi tuzifuate sote, au wewe uko juu ya sheria nini? maana yake unaongea kama mh. Pinda au mwanae nini?
 
Sasa mzifuate hizo sheria za nchi mkivunja sheria lazima mpigwe tu hakuna jinsi

wema_1, usitake niamini kwamba tz wa kwanza kuvunja sheria ni mtawala; sasa mtu unapoagiza watu wapigwe! sheria ipi inaruhusu kiongozi aagize watu wapigwe?&sheria ipi inaruhusu polisi kutoa hukumu ya kupiga watu?tuwe makini sana. Gadafi aliwaita raia wake rats, cockroaches...; kilichomkuta Mungu ndio anajua, alijiona yuko juu ya sheria! Kile usichopenda kufanyiwa, usimfanyie mwingine, tukizingatia hayo amani itadumu.
 
walipewa ruhusa na boss wao "mimi nasema wapigeni tuu ........." - Pinda

hii kauli ya '... wapigeni tu...' ni hatari sana, isijefika muda watu waheshimiwa wakaanza kumtia vichwa kiongozi wao!
 
Sugu na wewe fungua kesi ya kupingwa kwani na wao polisi hawana Haki ya kukupiga ili unbalance yaani kesi juu ya kesi shitaki nikushitaki hapo ni mwendo wa kushitakiana kwani Hakuna mwenye Haki ya kumpiga mwenzake
Hebu jiulize kama askari anakatwaza kisheria kupiga ni kwanini anapewa vitendea kazi kama rungu, bunduki n.k? sheria sio sawa na hadithi za shigongo. Think twice.
 
Tunaongelea bunge sio ubalozi hapa au umeshakunywa viroba?

wewe ndo umekunywa viroba na kanguleni - ungemsikia jembe TL akidadavua kuhusu kinga ya Mbunge inaishia wapi leo 11/09/2013 saa mbili usiku karibu tv zote.
 
Ni miezi miwili sasa tangia Waziri mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,mh Mizengo Kayanza Peter Pinda alipotoa kauli ya kuwaagiza askari polisi kuwapiga watu au mtu yeyote yule anaekaidi amri ya polisi!

Akijibu swali kutoka kwa mbunge mmoja wa Cuf alietaka kujua nini kauli ya serikali kuhusu polisi wanaua raia!?mh Pinda alisema kwamba kama unaambiwa usifanye hivi na unafanya basi hakuna njia ni lazima tu upigwe na mimi nasema wapigeni maana sasa tumechoka!!

Baada ya kauli hiyo au ruhusa hiyo kwa polisi ndipo sasa unyanyasaji wa raia ikiwa ni pamoja na vipigo vikazidi. Wiki iliyopita wakati wa kikao cha bunge kulitokea mabishano na kutoelewana kati ya kiongozi wa bunge Naibu Spika Ndugai na wabunge wa Upinzani wakiongozwa na Kiongozi wa Upinzani Bungeni mh Freeman Mbowe hali iliyopelekea vuta nikuvute na Naibu Spika aliamuru Polisi kumtoa nje KUB!!

Baada ya sintofahamu hiyo ndipo Mbunge wa Mbeya mjini mh Joseph Mbilinyi na wabunge wengine wa CUF,NCCR na CHADEMA wakaingilia kati kuzuia kiongozi wao kutolewa na polisi nje,ndipo mh Sugu alishambuliwa na Polisi hao na kumdhalilisha kwa kumburuza km mwizi na kumtoa nje,baadae Sugu alidai kuwa kuna polisi mmoja alimpiga teke wakati wakimbeba na akaamua kulipiza kwa kumrushia Konde huyo polisi.

Pamoja na haki na kinga ya kibunge aliyonayo SUGU chakushangaza polisi wamemfungulia Mashtaka sijui ya kumpiga askari au ya nini!? Je polisi waliompiga Sugu wao watashtakiwa kwa nani? Na kama polisi walipewa ruhusa ya kupiga je mwananchi akiamua kujitetea ni kosa? Na je kati ya Sugu na Polisi nani aliekiuka utaratibu kwa kumdhalilisha mwenzake? Je kwa udhalilishaji aliofanyiwa Sugu hakuwa na haki ya kujitetea na hata ikibidi kwa kulipiza!?

Mbona polisi wanakimbilia mahakamani wakati wao ndio walioamua kutii amri za kipumbavu kwa kuamrishwa na Nduagai bila kujiuliza kuwa je ni sahihi kutii kila amri hata pasipostahili?
 
Kwa kauli hiyo ya Tindu Lissu, kama ilivyokuwa kauli ya Mabere Marando kuhusu tuhuma za ugaidi zilizokuwa zinawakabili Lwakatare na Ludovick, serikali kama kweli ni 'sikivu' waachane na hiyo kesi, vinginevyo wajiandae kuumbuka tena mahakamani!

Mkuu wa kiti Hawa jamaa Kama wanachanganyikwa! Unajua unapokaribia ngome yao yani wanazidi kuvurunda na kuwa wakali! Tutegemee Hawa Mafisiemu kuvurunda sana!
 
Kwa kauli hiyo ya Tindu Lissu, kama ilivyokuwa kauli ya Mabere Marando kuhusu tuhuma za ugaidi zilizokuwa zinawakabili Lwakatare na Ludovick, serikali kama kweli ni 'sikivu' waachane na hiyo kesi, vinginevyo wajiandae kuumbuka tena mahakamani!

Mkuu wa kiti Hawa jamaa Kama wanachanganyikwa! Unajua unapokaribia ngome yao yani wanazidi kuvurunda na kuwa wakali! Tutegemee Hawa Mafisiemu kuvurunda sana!
 
kama kweli lissu anajua kwamba kupeleka kesi hii mahakamani ni umbumbumbu wa kisheria na pia atakuwa anavunja ama kukiuka katiba iliyopo, basi ni dhahiri kwamba tendo lile lilifanyika kwa makusudi kwa kujua kwamba mbunge ana hiyo kinga.

kama ukiaangalia footage ile, mh. sugu hakuonekana kumtishia askari kwa kuaka kumpiga akiwa ndani ya bunge, ingawa alitolewa nje kwa njia ya kushusha heshima kidogo. ila muendelezo wa footage inaonesha nje ya ukumbu sugu anamvamia askari.. naamini kama kweli wabunge wa upinzani walitoka nje wote ni naweza kuamini kwa njia moja ama nyingine kwamba sugu alishawishiwa kufanya aliyofanya kwa sababu tu kuna kunga ya mbunge ama ndani ya bunge ama kwenye viwanja vya bunge.
kwa upande mwingine, nadhani kamati ya nidham na maadili ya wabunge kama ipo na kufanya kazi basi ni vema ikachukua hatua yake. hatuwezi, binafsi siwezi kukaa na kuona utovu wa nidhamu unaoletwa na baadhi ya wabunge ambao naweza kusema wana upeo mdogo sana kwenye siasa na nyanja zake zote. kutoka kwenye jukwaa lakuimba matusi na kushabikiwa na watu ndo unataka kuleta bungeni

kama ni kweli mh sugu anataka kutetea wanyonge ama kupigania haki kama navyosema, basi ni dhahiri ajenge hoja sio kutumia nguvu kulaimisha umaarufu. aige mfano kwa kina mnyika, slaa, mbowe na hata zitto na lissu pia..
 
kama kweli lissu anajua kwamba kupeleka kesi hii mahakamani ni umbumbumbu wa kisheria na pia atakuwa anavunja ama kukiuka katiba iliyopo, basi ni dhahiri kwamba tendo lile lilifanyika kwa makusudi kwa kujua kwamba mbunge ana hiyo kinga.

kama ukiaangalia footage ile, mh. sugu hakuonekana kumtishia askari kwa kuaka kumpiga akiwa ndani ya bunge, ingawa alitolewa nje kwa njia ya kushusha heshima kidogo. ila muendelezo wa footage inaonesha nje ya ukumbu sugu anamvamia askari.. naamini kama kweli wabunge wa upinzani walitoka nje wote ni naweza kuamini kwa njia moja ama nyingine kwamba sugu alishawishiwa kufanya aliyofanya kwa sababu tu kuna kunga ya mbunge ama ndani ya bunge ama kwenye viwanja vya bunge.
kwa upande mwingine, nadhani kamati ya nidham na maadili ya wabunge kama ipo na kufanya kazi basi ni vema ikachukua hatua yake. hatuwezi, binafsi siwezi kukaa na kuona utovu wa nidhamu unaoletwa na baadhi ya wabunge ambao naweza kusema wana upeo mdogo sana kwenye siasa na nyanja zake zote. kutoka kwenye jukwaa lakuimba matusi na kushabikiwa na watu ndo unataka kuleta bungeni

kama ni kweli mh sugu anataka kutetea wanyonge ama kupigania haki kama navyosema, basi ni dhahiri ajenge hoja sio kutumia nguvu kulaimisha umaarufu. aige mfano kwa kina mnyika, slaa, mbowe na hata zitto na lissu pia..
 
Wema-1 unafurahisha sana! Wanaokujibu post zako wamekuheshimu sana! Tena wanakubembeleza! Ila bahati ya Leo usifikiri Na siku ingine itakua Kama Leo! Kikubwa unatakiwa ufahamu kua hauna hoja yoyote wewe juu ya huo ufisiemu!
 
Kinachosikitisha sijui kama Spika/Naibu Spika na wenyeviti ,hivi wabunge waCCM wanapowatukana wapinzani wao wanahaki kamili kutoka kwenye kiti lakini pale wapinzani wanapokuwa provocked na hali ya kutothaminiwa basi wapinzani wanakuwa wamekosa sana kama vile wameua mtu.Hivi Lusinde,Juma Nkamia,Kigwangala walivyotukna bungeni viongozi wa bunge hawakusikia au kuona? Kwa nini wabunge waupinzani wamekuwa kama second citizens?Je ni njia ya kuua upinzani?Mbona kwa sasa watanzania wengi wamekuwa waelewa sana?Kama umaarufu viongozi wabunge ndiyo wanawapa na mwisho wa siku viongozi hawa wanajikuta wanajidhalilisha wenyewe.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom