Suala la Kushusha abiria wote Mbezi Litazamwe upya

Faana

JF-Expert Member
Dec 12, 2011
31,279
32,323
Nawasilisha maoni haya kwa Mamlaka husika, leo asubuhi nimeshuka Magufuli terminal kwa bus na kushushwa kama watawala walivyoamuru, tukiwa wengi tu, tukavuka kwenda upande wa pili kutafuta daladala za kwenda mjini, kiukweli, nimejifunza ule usemi wa "mwenye shibe hamtambui mwenye njaa" una maana kubwa sana, Jiji la Dar bado lina changamoto kubwa sana ya usafiri, kiuhalisia RC wa Dar anatakiwa kujitathimini kama kweli maamuzi aliyotoa yalifanyiwa utafiti wa kina juu ya zuio la mabasi makubwa kutowapa msaada wasafiri wanaoelekea mjini. Narudia kutoa ushauri, ninawaomba watanzania wenzangu tuungane kwa mara nyingine kuisihi serikali kuu kulitazama kipekee jambo hili.
  1. Makamu wa Rais akiwa Kigoma Juzi amewatahadharisha wana Kigoma kuwa makini juu ya Covid 19, hii ikiwa ni pamoja na mikoa mingine 9 yenye takwimu za uwepo wa ugonjwa huo kwa asilimia kadhaa, sidhani Dar inakosekana kwenye orodha hiyo, shidda ya usafiri tuliyokutana nayo Mbezi katika kupanda daladala ni kichocheo kingine cha maambukizi ya ugonjwa huo. Mwenzetu Makala anatumia gari la serikali, hapati machungu wanayopata wananchi wa kipato duni, akina mama na watoto na mizigo. Shida na adha iliyopo ni kubwa, tunaililia serikali kutazama upya maamuzi hayo kandamizi.
  2. Kama sababu kubwa ni kuongeza mapato kwa serikali kupitia hizo biashara alizotaja RC, basi ni bora mara 100 abiria wanaotoka mikoani wakatozwa hiyo nauli ya shilingi 400 kwenye mabasi makubwa ili kupunguza msongamano wa abiria kwenye daladala na hata stand hizo mbili ili kuwanusuru dhidi ya maambukizi mapya yanayoendelea.
  3. RC na timu yake wafanya utafiti wa namna bora ya kuongeza mapato waliyokusudia badala ya huo mpango waliouanzisha, siku zote tunakwama kwenda mbele kwasababu ya kutofanya tafiti kabla kutoa maamuzi sahihi.
  4. Yapo madhara mengi sana yanatokana na maamuzi ya RC, ila wananchi tumekosa mshikamano wa namna bora ya kuyafikisha kwa ngazi za juu zaidi ili kuwanusuru raia wasio na uwezo.
  5. Tegemeo la mwananchi ni kuona kiongozi anatumia ubunifu wake kutatua kero zinazowakabili katika kuondokana na umasikini, lakini alichokifanya RC ni kuongeza umasikini kwa wananchi masikini
Nawasilisha
 
Iringa stendi ya Igumbilo inakwenda mwaka wa pili sasa abiria wanalazimika kushuka stendi na mabadi yanaenda tupu mjini. Maamuzi ya Mkuu wa Mkoa
Serikali imeamua kuwanyanyasa wanyonge ni dhahiri
 
Hivi hawa Wapuuzi wakisema mapato, mbona haiingii akilini? Mapato kwa nani? Maana nikishuka sina ninachonunua! Sasa mapato yanaongezekaje?

Usunbufu wa kitoto tu yaani Njombe unapitishwa hadi Stand then unachukua boda unarudi kwenda kwako unalipia 6000.

Iringa hivyo hivyo, nilikutana na basi la kampuni ya Premier lilikua linatoka Mwanza wanakwenda Mbeya, SAA saba usiku, wakaenda kuwashusha abiria kule porini (stand mpya) hakuna usafiri then urudi usiku huo kwenda mjini ambako ndio umepita. Crazy

Dodoma, ujinga ni ule ule tena! Umetoka Iringa hawaruhusu ushuke kule mwanzo eti hadi nanenane, hawa wapuuzi nadhani huwa wanafanya maamuzi wakiwa uchi! Shenzi
 
Iringa stendi ya Igumbilo inakwenda mwaka wa pili sasa abiria wanalazimika kushuka stendi na mabadi yanaenda tupu mjini. Maamuzi ya Mkuu wa Mkoa
Siyo iringa tu ni mikoa takriban 10, mfano Mwnz, Mby, Tanga, Moro, nk, tatizo ninaloliona ni baadhi ya watz si wasafiri ndiyo maana wanalalamika kwa vitu vya ajabu.
 
wazuie kabusa bus lolote kuingia town, safari iwe mbezi-mikoani-mbezi
 
wazuie kabusa bus lolote kuingia town, safari iwe mbezi-mikoani-mbezi
Nikweli kabisa. Watu wanaropoka tuu malori kuanzia saa 12 asubuh mpaka saa 3 hayaruhusiwi kuvuka mbezi kuingia town nahaya mabasi yasiruhusiwe kabisa ilikuondoa foleni
 
Wafanye kama Morogoro tu!Mfano basi likifika msamvu wale wakushuka watashuka na wale wanaoingia mjini wanabaki ndani ya basi linsingia town kushusha abiria kama daladala inavyoshusha!!!
 
Ujinga kama huo pia nliuona kule Dodoma watu wanashushwa 88 wanahangaika na bajaji magari yakiwashusha yanaenda matupu mjini.

Kwanini magari yasiingie yakalipa huo ushuru wa stendi (Maana ndio wanachokitaka) then likapeleka watu hadi mjini
 
Ujinga kama huo pia nliuona kule Dodoma watu wanashushwa 88 wanahangaika na bajaji magari yakiwashusha yanaenda matupu mjini.

Kwanini magari yasiingie yakalipa huo ushuru wa stendi (Maana ndio wanachokitaka) then likapeleka watu hadi mjini
Daladala wakale wapi? BRT ya kazi sasa?
 
Kwani kabla ya hio stend walikula wapi

Labda kama mgeni Mbezi, daladala za mbezi zinajaza all the time kabla ya kuja hii stand
Ila inabidi pawe na mpangilio, lengo ni kuondoa misongamano ya mabasi hayo makubwa, hata SGR lengo ni ili malorry yasije Dar, yachukulie mizogo bandari kavu huko Morogoro ikiwezekana
 
Nilimsikiliza Makala nikajisemea huyu nae mwehu kaokotwa huko baada ya kudeal na raia vyema anakuja kujaza matatizo. PIGA VITA ABIRIA KUSHUSHWA MBEZI TERMINAL
 
Dodoma pia hivyohivyo, abiria wote wanaotoka mikoani wanashushiwa nanenane regardless gari inaenda mjini ama laah.
 
4 Reactions
Reply
Back
Top Bottom