MchunguZI
JF-Expert Member
- Jun 14, 2008
- 4,009
- 2,173
Wana JF, Katika kuhangaikia wanetu wanaorudishwa vyuo Vikuu kwa taratibu ngumu, nilimpa kampani kijana wangu kuelekea SUA. Nimefika kwa mara ya kwanza na kujionea ambayo yamekuwa yakiandikwa magazetini.
SUA imekaa kama Sekondari ya kata iliyopata mfadhiri. Ikiashiria uhaba wa kifedha. La kushangaza ni aina ya magari yaliyojipanga mbele ya jengo la utawala. Kuna la mkuu wa Chuo, Msaidizi 1 na Msaidizi 2. Yote matatu hakuna la bei chini ya milioni 100! Hizi ni ada za wanetu.
Kibaya zaidi wanafunzi
Hawana hosteli,
Hawana internet,
Hawana madarasa ya chuo kikuu,
Hawana viti madarasani vya chuo kikuu
Hawana mabarabara,
Maabara pia hakuna!
Nasikia usiku ni kama kijiji maana hawana taa za nje,
Je, Ni kweli serikali inakubali kuwa na viongozi kama hawa ambao wanakusanya ada sawa na vyuo vingine, lakini matumizi yao ni ya binafsi tu? Au tusubiri baada ya muda wao ndo tuwapeleke mahakamani kwamba ni mafisadi kama Mramba?
Lazima hawa walipewa uongozi kwa kufahamiana na kiongozi fulani.
Mulioko SUA tuambieni Hao viongozi muliwapataje?
SUA imekaa kama Sekondari ya kata iliyopata mfadhiri. Ikiashiria uhaba wa kifedha. La kushangaza ni aina ya magari yaliyojipanga mbele ya jengo la utawala. Kuna la mkuu wa Chuo, Msaidizi 1 na Msaidizi 2. Yote matatu hakuna la bei chini ya milioni 100! Hizi ni ada za wanetu.
Kibaya zaidi wanafunzi
Hawana hosteli,
Hawana internet,
Hawana madarasa ya chuo kikuu,
Hawana viti madarasani vya chuo kikuu
Hawana mabarabara,
Maabara pia hakuna!
Nasikia usiku ni kama kijiji maana hawana taa za nje,
Je, Ni kweli serikali inakubali kuwa na viongozi kama hawa ambao wanakusanya ada sawa na vyuo vingine, lakini matumizi yao ni ya binafsi tu? Au tusubiri baada ya muda wao ndo tuwapeleke mahakamani kwamba ni mafisadi kama Mramba?
Lazima hawa walipewa uongozi kwa kufahamiana na kiongozi fulani.
Mulioko SUA tuambieni Hao viongozi muliwapataje?