Story: Ulitenda mema na kulipwa mabaya please share

Story: Ulitenda mema na kulipwa mabaya please share

nakumbuka nilimpa ndugu biashara kwa mtaji wangu na kwa makubaliano ya kugawana 50% ya faida, na kikubwa yeye alikua ameniunganisha na wateja yote nilifanya kwa mapenzi asiwe anakaa bila shughuli yoyote kilichonikuta mwisho alifanya biashara vizuri na hata senti sikupata akaishia kunipiga kiswahili nikamuacha tu kiukweli ndugu ni mtihani sana.
 
Relief Mirzska,
Moja ya kitu ambacho najutia ni kushindwa kutuma maombi in time kwako maana nakumbuka ulitangaza hapa hapa fursa hiyo ya ajira. By the way nahisi was childish thoughts and attitudes in I.

Moja ya maneno nayosikia katika fikra zangu ni "Mkuu you got too much excuses" kila nikiona comments zako. Hii kauli yako imenifunza mengi,..

Hope we'll be together in Jordan (Middle East) who knows 😎
 
Haya majanga tunayo wengi sana,
Nilimfungulia mdogo angu wa tumbo moja biashara mtaji wa ml2, na nilimwambia yeye achague aina ya biashara na frem ilikua tayari, akanunua vitu km redio, tv, deki na vingi vya dizaini hizo, kwa kipindi hicho hiyo biashara ndio ilikua inaenea kwa kasi sana mitaani, tulikua tunauza sana kwa siku tunaenda mjini mara mbili, ndani ya mwaka mtaji ushafika ml10, nktamtafutia msaidizi huku mimi nikiendelea na mishe zangu,
Yaani baada ya mwaka duka limeisha enzi zile za deci washamla ml3 yake akisubiri kuvuna ndio ikafa, nilipata hasira nkalifunga akawa hana kazi mama analalamika namwachaje mdogo angu hivyo, kwa hasira nkampa kiduka kilikua uswazi ila mtaji tu vingine kama friji makreti na vingine aviache, mwisho wa siku na hilo kala kamaliza na ela ya mama laki 7 alimpa aongeze mtaji ikaishia hapo...

Baada ya miaka mi3 karudi kuomba msamaha baada ya kukosa kuuwawa akiwa anapokonywa bodaboda nkamsamehe nkamfungulia tena biashara iliyogharimu ml3.5 baada ya mwaka na nusu nilienda apo nikakuta imefungwa hadi leo sijui iliishia wapi...
Na majanga ya kumlelea watoto wake wa3 kaniachia.

Kipindi hicho nahangaika kutafuta ela mtaji mdogo jamaa yangu tunaishi karibu nkawa namuazima ela, kila laki1 baada ya mwezi nampa laki na kumi, nikichukua laki 3,4, 5 ni hivyohivyo, baada ya mambo yangu kua mazuri yeye ndio akawa ananiazima ela nkawa nampa tena bila riba yoyote baadae 1.6ml ilifia kwake hadi sa hivi hapokei simu yangu.

Kuna watu tumeumbwa kua daraja la wengine kufanikiwa ila hawajitambui hata kidogo mwisho wa siku chenga tupu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wanaume wa siku hizi sijui wakoje mimi kuna lijit humu lilinipiga 25,000 yangu hakyaMungu inaniuma sana yaani halafu linafanya wizara ya mambo ya ndani.
Mie kuna kisa cha kima mmoja nikiandika hapa pilau ntashindwa kulila! Hata kinywaji hakitapanda!kifup usiwe mwema sana!

Erasto kitu ulichonifanyia sitasahau! Na madhila unayoyapata ss hv najua ni kofi!dadeq!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kuna msela mavi alifukuzwa kwa dada yake akaniomba hifadhi gheto akae kwa siku tatu, mimi nilikuwa silali huko gheto kwangu enzi hizo naanza kujitegemea kimaisha.
Baadae jamaa kageuka kama mtoto wangu anakuja kuomba hadi hela ya chakula ofisini kwangu.
Miezi haondoki kama alivyosema, hataki kazi ya kuajiriwa niliyomtafutia. Akaanza kuvaa nguo zangu bila ruhusa.
Mwisho wa siku msela mavi kaniibia kila kitu gheto hadi nguo za ndani na personal note books.
Hilo sengerema ni age mate, classmate, lilitaka nililee miaka kama mtoto wangu.
Liliacha kitanda, godoro na fridge tu, liliiba hadi vifaaa vyangu flani nilivyokuwa nimetunza gheto baada ya kufunga biashara yangu sehemu.

Waswahili maneno mengi wale wanakuambia mfadhili mbuzi utakula nyama au mfadhili mbwa anaweza kukulindia nyumba yako, sio binadamu majanga tu.
 
Wanaume wa siku hizi sijui wakoje mimi kuna lijit humu lilinipiga 25,000 yangu hakyaMungu inaniuma sana yaani halafu linafanya wizara ya mambo ya ndani.


Sent using Jamii Forums mobile app

😅😅😅! Pole sana mm huku hayupo!hahhaa! Mie aliniambia oh nisaidie mmangu ni fukara sana msaidie afuge bloila...mwananke nikaingia mkopo kumpa mazake😅! Alinifanyia mchezo wa ajabu sana!shenz typ
 
Moja ya kitu ambacho najutia ni kushindwa kutuma maombi in time kwako maana nakumbuka ulitangaza hapa hapa fursa hiyo ya ajira. By the way nahisi was childish thoughts and attitudes in I.

Moja ya maneno nayosikia katika fikra zangu ni "Mkuu you got too much excuses" kila nikiona comments zako. Hii kauli yako imenifunza mengi,..

Hope we'll be together in Jordan (Middle East) who knows 😎
Bro!

Pole sana, I will know if you have learnt something or not. You still have my number?? Call me then mkuu!

Umenifanya ni-smile bro hahahahah
 
Back
Top Bottom