Stori ya kusisimua - Taxi

Stori ya kusisimua - Taxi

Dear Bishop nimemiss kusoma maandishi yako kwenye utunzi wa simulizi tafadhali ikukupendeza fanya lolote jambo. wako mtiifu..
 
Habari mambo naitwa Mr Equator Nimeandika ujumbe huu kuku omba swala moja tu!
Mimi nimetengeza website ya ku share story ambayo ni http://www.equatorstory.com/
Je umekuwa ukipata tabu kupost story zako hapa?
Hili ndo suluhisho lako.
Mimi nataka nkupe nafasi ya kuwa mmoja wapo wa kwanza kutumia hii website
unda account yako na uweze kupost story yako mpya.
 
Mr. Bishop Hiluka ww ni zaidi ya mtunzi. I salute you for a good job. Asante saan kwa simulizi hii nzuri na umenijenga kwa mengi sana
 
Taxi - (64)

Mwanadada yule aliitwa Cynthia West, alikuwa na umri wa miaka 25, sura yake ilikuwa ndefu kiasi na pua ndogo ndefu. Alivaa sketi fupi iliyoishia sentimita chache juu ya magoti yake, ilikuwa nyeusi yenye miraba myeupe, blauzi nyeupe ya mikono mirefu na viatu vyeusi vyenye vikanyagio virefu vya mchuchumio

Alikuwa chotara wa kizungu mwenye shingo ndefu kiasi iliyobeba mabega ya kike na shingoni alivaa kidani cha dhahabu kilichoning’inia kifuani kwake na kuzama katikati ya uchochoro wa matiti yake ya ukubwa wa wastani.

Elli na Sammy waliwasalimia kwa Kiswahili wale watu waliowakuta mle ndani. Ni wale Waafrika pekee walioitikia ile salamu kwa pamoja, kasoro wale wazungu na yule mwanadada aliyeko kwenye kompyuta.

Kisha Sammy na Elli waliwasalimia wale wazungu kwa Kiingereza huku wakipunga mikono yao ya kulia na kuwafanya wale wazungu waitikie kwa bashasha zote.

Muda huo yule mwanadada aliyeko kwenye kompyuta aliinua uso wake mara moja na kuwaangalia Sammy na Elli. Macho yake yakagongana na yale ya Elli na Sammy. Yule mwanadada akaachia tabasamu pana na kurudisha macho yake kwenye kompyuta.

“Cynthia, hujambo dada’angu?” Elli alimsalimia yule binti kwa bashasha.

“Sijambo, kaka Elli, shikamoo,” Cynthia alisema huku akiacha kuchapa huku akiendelea kutabasamu.

“Marahaba. Pole na kazi,” Elli aliitikia huku akimsogelea.

“Asante, karibuni sana,” Cynthia aliitikia kisha akageuza shingo yake kumtazama Sammy huku akiendelea kutabasamu.

“Shikamoo,” alimsalimia Sammy kwa hesima zate.

“Marhaba, za kazi?” Sammy aliitikia huku naye akitabasamu.

“Nzuri,” Cynthia alisema huku akiyarudisha macho yake kwenye kompyuta mara moja na kuyarudisha tena macho yake kuwaangalia wageni wake huku akionekana ni mtu mwenye furaha muda wote.

Kabla Elli hajamuuliza Cynthia chochote mlango wa ofisi ile ulifunguliwa na mwanamume mmoja mnene na mrefu aliyefuga rasta aliingia. Alikuwa pia chotara wa kizungu na aliitwa McDonald West. Alipowaona Elli na Sammy aliwasogelea haraka huku akimtazama Elli kwa mshangao kama vile hakuwa ametegemea kumwona pale muda ule.

“Umepaa?” McDonald alimdaka Elli juu kwa juu bila hata ya salamu.

“Wala sijapaa, barabara tuliyojia haikuwa na foleni kabisa, askari wa usalama barabarani walikuwa wakiziita gari, nadhani kuna mkubwa fulani alikuwa anaandaliwa kupita,” Elli alisema huku akinyoosha mkono wake kumsalimia McDonald. Wakasalimiana kwa furaha kisha McDonald aliwakaribisha ofisini kwake.

Kilikuwa ni chumba cha ofisi cha ukubwa wa kawaida chenye samani chache muhimu za kiofisi. Kulikuwa na zulia lenye rangi za bendera ya taifa la Tanzania sakafuni, meza kubwa ya kiofisi ambayo juu yake kulikuwa na kompyuta aina ya Acer i5 na kioo cha flat, kiti kirefu cha ngozi halisi cha kiofisi chenye magurudumu madogo yaliyokiwezesha kusogea, na kilikuwa kinazunguka.

Mbele ya ile meza kulikuwa na viti viwili pamoja na kochi moja la sofa kwa ajili ya wageni, meza ya kioo ya pembe nne na chini ya meza ile kulikuwa na magazeti na majarida kadhaa yaliyoandikwa “Dar Guides”. Juu ya meza ile kulikuwa na vitabu, nakala chache za magazeti ya siku ile na nakala kadhaa za ramani kubwa ya Tanzania ikionesha maeneo ya vivutio vya utalii.

Kwa pembeni kulikuwa na rafu iliyopangwa vitabu na majarida chungu nzima ya utalii na ukutani kulikuwa na ramani kubwa ya Tanzania, yenye kuonesha maeneo mbalimbali yenye vivutio. Elli na Sammy waliketi kwenye viti vilivyokuwa mbele ya meza ya McDonald.

“Uliponipigia simu nilikuwa maeneo ya Muhimbili nikadhani huenda ningekuwahi, enhe nipe habari?” McDonald alisema baada ya Elli na Sammy kuketi kitako.

“Ni kama nilivyokueleza, huyu ni ndugu yangu, anaitwa Sammy…” Elli alianza kuelezea huku akimwoneshea Sammy kwa McDonald.

“Sasa, ngoja kwanza niwatoe hawa jamaa hapo mapokezi, wametokea Uswisi jana na walipaswa kuwa safarini kuelekea Iringa leo hii…” McDonald alisema na kuinuka, akatoka nje ya ofisi yake akiwaacha Sammy na Elli.

Muda huo huo simu ya Sammy ilianza kuita, alipoiangalia kwa makini akagundua kuwa ilikuwa simu kutoka kwa Dk. Masanja. Sammy alisita kidogo kisha akaamua kuipokea.

“Hello!” alisema mara tu alipoiweka kwenye sikio. Akasikia mwangwi wa sauti yake ukimrudia, akashtuka. Hii ilimaanisha kuwa simu ilikuwa imewekwa sauti ya juu ‘Loud speaker’ ili kumwezesha mtu au watu wa upande wa pili kusikia yanayoongelewa upande wa pili wa simu pasipo kuiweka sikioni.

“Hujambo, kijana wangu?” ilikuwa sauti ya Dk. Masanja aliyeongea kwa sauti tulivu.

“Sijambo, shikamoo.”

“Marhaba, vipi unaweza kuwa na nafasi ufike hapa ofisini kwangu leo?” Dk. Masanja alisema kwa sauti tulivu.

“Leo! Sidhani kama nitaweza kufika, nipo mbali kidogo, labda kesho kama itawezekana,” Sammy alisema huku akionesha kusita. Akasikia sauti ya Mr. Oduya ikiongea upande wa pili wa simu kumtaka Dk. Masanja amuulize alipo ili wamfuate. Sammy alishtuka kidogo, hata hivyo hakutaka kumwonesha Elli kuwa alishtuka.

“Kwani upo wapi, naweza hata kukufuata huko huko uliko!” Dk. Masanja alimuuliza Sammy.

Sammy alibaki kimya kwa muda akifikiria nini aongee, kwani alianza kuhisi kuwa kulikuwa na jambo lisilo la kawaida likiendelea. Alikumbuka jinsi alivyogombana na Mr. Oduya walipokutana ofisini kwa Dk. Masanja pale alipomtaka awe mshirika wake. Akajiuliza, huyo mzee alikuwa anamtakia nini!

Sammy, are you there?” Dk. Masanja aliuliza kwa wasiwasi baada ya kuona kimya.

“Mmh… kwani ulikuwa unasemaje mzee, wangu? Labda naweza kukujibu hata humu kwenye simu.”

“Ah, kuna mambo haipendezi kuyaongea kwenye simu, ndiyo maana nilitaka kujua upo wapi!”

“Kuna tatizo lolote?” Sammy aliuliza huku akikunja sura yake na kuminya midomo.

“Hakuna, kuna mambo fulani nataka nikushirikishe,” Dk. Masanja alisema na kushusha pumzi.

“Unishirikishe?” Sammy aliuliza huku akiwa bado amekuja sura yake.

“Ndiyo, kwani kuna ubaya kukushirikisha? Au mimi na wewe tumeshakuwa na uadui siku hizi?”

“Hakuna ubaya, lakini kwa leo haitawezekana. Nipo nje ya mji na ninatarajia kurudi kesho.”

“Kesho saa ngapi nikutegemee?”

“Ngoja nione halafu nitakujulisha,” Sammy alisema na kukata simu, akashusha pumzi za ndani kwa ndani. Elli alimtazama kwa makini.

Itaendelea...
Tamu sana
 
Taxi - (132)

Hakujua uelekeo ule ungemfikisha wapi ila alichokuwa amepanga ni kutoweka haraka eneo lile. Wakati akiharakisha kutoweka eneo lile kichwa chake kilikuwa kimetawaliwa na mchanganyiko wa mawazo. Moyo wake ulikuwa ukienda mbio sana. Alizidi kujichanganya na watu wengine na mbele kidogo akakutana na mtaa mwingine wa Morogoro uliokatisha mbele yake.

Kabla ya kujua afuate uelekeo wa upande gani; kulia au kushoto akakumbuka kutazama nyuma yake na hapo moyo wake ukapiga kite kwa nguvu. Alimwona mtu mmoja tu, mwanamume aliyekuwa amevaa suti nyeusi, kofia kubwa nyeusi ya pama na miwani myeusi ya jua akimfuatilia kwa nyuma.

Japokuwa kulikuwa na msongamano mkubwa wa watu katika eneo lile la soko lakini uzoefu wa mbinu za kijasusi ulimsaidia Tunu kugundua kuwa yule mtu alikuwa akimfuatilia yeye. Hata hivyo, kuna kitu kilianza kumchanganya, alijiuliza yule mtu alitokea wapi kwani hakuwa mmoja wa wale wawili waliokuwa wakimfuatilia tangu mwanzo.

Tunu aliamua kushika uelekeo wa upande wa kulia akiufuata mtaa wa Morogoro huku mkono wake ukiwa tayari umezama mafichoni kuipapasa bastola yake ya kijasusi. Kwa kweli alikuwa ameanza kuchoshwa sana na hali ya kufuatiliwa, hivyo alipanga kufanya shambulizi la kujihami na la kushtukiza kwa kugeuka na kumshindilia risasi za kutosha mtu yule bila kujali macho ya watu waliokuwa eneo lile kisha angepotea haraka toka eneo lile.

Aligeuka tena nyuma kumtazama yule mtu aliyekuwa akimfuatilia huku akiwa tayari amekwisha jiandaa kumfanyia shambulizi la kushtukiza lakini hakumwona! Akashangaa kidogo lakini mara akawaona tena wale wanaume wawili waliokuwa wakimfuata tangu mwanzo toka kule hospitali. Sasa walikuwa wakitimua mbio kumfuata. Tunu hakutaka kuanza kutimua mbio kwani kwa kufanya hivyo angeweza kuyavuta macho ya watu waliokuwa eneo lile, hivyo aliongeza mwendo huku akipanga namna ya kuwafanyia shambulizi la kushtukiza.

Aliufikia mtaa wa Pangani na kabla hajajua afanye nini au aelekee upande upi alimwona mwendesha bodaboda mmoja aliyekuwa anapita pale akitokea katika msikiti wa Irshaad Salafy na kuelekea upande wa Kariakoo. Tunu alikimbia kisha akarukia juu ya ile bodaboda huku akimtaka yule mwendesha bodaboda amkimbize haraka Machinga Complex, Kariakoo. Lilikuwa ni tukio la ghafla sana na wale watu waliokuwa wakimfukuza Tunu hawakuwa wamelitarajia kabisa.

Yule mwendesha bodaboda hakuwa amemtilia shaka yoyote Tunu ingawa alishangazwa na kitendo chake cha kurukia juu ya pikipiki wakati ikiwa katika mwendo. Pikipiki iliongeza mwendo na kwenda kasi kama alivyotaka Tunu, wakaufuata mtaa ule wa Pangani hadi walipoufikia mtaa wa Tabora, wakaingia upande wa kulia na safari ikaendelea. Wakati wakiingia katika mtaa wa Tabora Tunu aligeuza shingo yake kutazama nyuma, hakuwaona tena wale watu waliokuwa wakimfukuza nyuma yake.

Walipofika eneo la Machinga Complex Tunu alimlipa yule mtu wa bodaboda fedha aliyoitaja, akateremka na kujichanganya na watu wengine, kisha akachukua bodaboda nyingine akimtaka dereva wake ampeleke haraka mtaa wa Kongo. Vivyo hivyo alipofika mtaa wa Kongo na kushuka alichukua bodaboda nyingine hadi Mnazi Mmoja.

Aliendelea na mchezo huo wa kubadilisha pikipiki toka eneo moja hadi jingine na baadaye alichukua taxi katika eneo la Gerezani iliyompeleka Temeke kisha akachukua taxi nyingine, na akiwa ndani ya taxi simu yake ya mkononi ikaanza kuita. Tunu aliitazama na kuliona jina la Tom, hata hivyo aliikata na kumtumia ujumbe kuwa angempigia baadaye kwani hakuwa sehemu nzuri. Tom alimsisitiza kutoacha kumpigia kwani ilikuwa muhimu.

Saa yake ya mkononi ilimwonesha kuwa ilikuwa ikielekea kutimia saa kumi na nusu wakati alipokuwa anasimama mbele ya geti kubwa jeusi la nyumba ya kifahari ya Elli katika eneo la Kurasini, huku akiiacha ile taxi ikitoweka nyuma yake. Kwa kiasi fulani alikuwa amechanganyikiwa kutokana na kuona kuwa harakati zake za upelelezi ziliingia dosari baada ya lile shambulizi la bomu nyumbani kwa Sammy.

Alibonyeza kitufe cha kengele kilichokuwa kando ya lile geti na kushangaa kuona kulikuwa na ulinzi tofauti na alivyokuwa ameacha alipokuja mwanzoni. Geti dogo kando ya lile geti kubwa jeusi likafunguliwa, mlinzi mmoja aliyekuwa wamevaa sare maalumu za kampuni binafsi ya ulinzi na mkononi akiwa ameshika bunduki akachungulia nje na kumuona Tunu.

Alimtazama kwa makini kwa kumkazia macho. Tunu alimsalimia kisha akajieleza kuwa yeye ni rafiki wa familia ya Elli na alifika hapo kuonana na Victoria. Baada ya maswali mawili matatu hatimaye Victoria aliulizwa na kuwataka wale walinzi wamruhusu Tunu aingie.

Tunu aliruhusiwa kuingia ndani ya ule uzio alikowakuta walinzi wengine wawili. Akapokelelwa na Victoria aliyemshangaa baada ya kuona akiwa hana gari. Tunu alimwabia kuwa alilazimika kuliacha kule kwenye mgahawa wa Elli’s kwa sababu za kiusalama, wakaongozana na kuingia sebuleni alikomkuta Winifrida akiwa amejikuyata kwa huzuni huku akilia kilio cha kwikwi. Winifrida alipomwona Tunu akaanza kulia kwa uchungu uchungu mkubwa na kwa sauti ya juu, mwili wote ulikuwa unamtetemeka.

“Winnie!” Tunu aliita huku akimshika Winifrida mikono, akamwinua na kumkumbatia lakini miguu ya Tunu haikuwa na nguvu hata za kusimama. Tunu akamketisha kwenye sofa huku akiketi kando yake na kuanza kumpetipeti mgongoni katika hali ya kumfariji. Tunu alikuwa amepata taarifa za shambulizi lililomlaza kitandani kaka yake Sammy.

Shughuli bado pevu na mambo ni . Je, nini kitaendelea? Usikose kufuatilia simulizi hii ya kusisimua...

NB: Litro
Narud
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom