Stori ya kusisimua - Taxi

Stori ya kusisimua - Taxi

Taxi - (159)

ILIPOISHIA

Mr. Oduya alihisi kama mwili wake ulikuwa ukicharangwa kwa visu vikali na kubanikwa katika moto mkubwa. Alihisi moto mkali sana ukitambaa kwenye mwili wake na ngozi yake ilikuwa inaungua na kumfanya kuhisi maumivu makali mno. Muda huohuo alihisi hasira kali zikiibuka ndani yake, chumba cha ofisi yake kilionekana kama kilichoshuka nyuzi kumi hivi na kuwa kifupi mno.

Mara simu yake ya mezani ikaanza kuita na kumzindua toka kwenye yale mawazo. Ndipo alipogundua kuwa ile simu ya mkononi ilikuwa bado ipo sikioni ingawa hakuwa akisikia tena kilichoongewa upande wa pili wa simu ile. Hakuweza kukumbuka ilichukua muda gani akiwa ameiweka ile simu sikioni huku mawazo yake yakiwa yamehama toka kwenye maongezi yake na Dk. Masanja hadi muda ule wakati simu ya mezani ilikuwa ikiita.

Hofu ilikuwa imemmeza kabisa, aliitazama ile simu ya mezani kwa wasiwasi huku akianza kuhisi jambo la hatari. Hata hivyo, hakutaka kuendelea kusubiri ile simu iendelee kuita zaidi kwani ilikuwa mbioni kukata baada ya kuita kwa muda mrefu. Hivyo akanyoosha mkono wake kivivuvivu ili kuipokea lakini kabla mkono haujaifikia ile simu ikakatika. Tukio lile likaiongeza hofu yake yake na hivyo akabaki akiikodolea macho ile simu kana kwamba lilikuwa bomu la kutegwa lililokuwa mbioni kulipuka.

Alianza kujiuliza, mpigaji wa simu ile angekuwa nani na angekuwa na shida gani muda ule, au ni yaleyale ya kupewa taarifa mbaya kuhusu Kamishna Omalla? Wakati akijiuliza mara ile simu ya mezani ikaanza kuita tena. Hakutaka iendelee kuita zaidi hivyo haraka akakinyakuwa kiwambo chake na kukiweka sikioni huku akiipa akili yake utulivu wa hali ya juu.

ENDELEA...

Mara tu alipoiweka ile simu sikioni sauti ya upande wa pili wa simu ikamtanabaisha kuwa mpigaji simu alikuwa ni katibu muhtasi wake.

“Bosi, kuna vijana wawili hapa wanadai kuwa lazima wakuone, wanasema ni rafiki zako na kwamba utafurahi sana kukutana nao,” katibu wa Mr. Oduya alisema kwenye simu.

“Sikutaka kuonana na mtu kwa sasa, wamekutajia majina yao na wanakotoka?” Mr. Oduya aliuliza kwa shauku.

“Wanasema wanatokea hapahapa Dar es Salaam. Mmoja anaitwa Tunu na mwingine ni Tom...”

“Kina nani!” sauti ya Mr. Oduya ilinguruma kwenye simu, ikapenya hadi kwenye ngoma ya sikio la katibu muhtasi wake na kutishia kuichana. Mr. Oduya aliogopa sana na hakuweza kusikia katibu wake aliongea au kumjibu nini, hakujua afanye nini na wala hakujua kama alikuwa tayari kuonana na vijana hao.

Alibaki ameduwaa asijue kipi cha kumwambia katibu muhtasi wake, mara akashuhudia mlango wa ofisi yake ukifunguliwa, Tunu na Tom wakaingia na kumkuta akiwa bado katika hali ile ya kuduwaa huku kiwambo cha simu kikiwa sikioni.

“Samahani, mzee, kwa kuingia bila ruhusa yako,” Tunu alisema kwa sauti tulivu ya kirafiki, huku akijikaribisha kwenye kiti pasipo kusubiri kukaribishwa. Tom naye akaketi kitini huku akimtazama Mr. Oduya kwa tabasamu.

“Nilipata salamu zako kuwa umekuwa ukinitafuta sana, umetumia rasilimali kubwa kuhakikisha unanipata, hivyo nimeona leo nije mwenyewe ili usipate taabu ya kuendelea kunitafuta. Sijui unasemaje, mzee?” Tunu alisema huku uso wake ukiwa umepambwa na tabasamu bashasha.

Hakuna jibu lililotoka kinywani mwa Mr. Oduya bali aliendelea kuduwaa huku akiwatazama Tunu na Tom kwa mshangao.
“Mr. Oduya, wewe ni mtu mbaya sana usiye na shukrani hata chembe,” Tunu aliendelea kuongea kwa sauti tulivu huku akiyatuliza macho yake kwenye uso wa Mr. Oduya. “Nafasi na heshima uliyo nayo kwenye jamii ya Watanzania ni kubwa sana lakini hujaridhika. Mamilioni ya Watanzania wamekuamini sana kiasi kwa kudhani ungefaa kuwa Rais ajaye lakini kumbe ni mbwa mwitu ndani ya ngozi ya kondoo! Unadiriki kushiriki katika mipango michafu ili kutimiza lengo lako. Aibu ilioje...”

Mr. Oduya akaonekana kurudiwa na fahamu, aliinuka huku akiwakazia macho Tunu na Tom. Muda wote Tom alikuwa kimya kabisa akimtazama Mr. Oduya kwa makini kama aliyekuwa akiyasoma mawazo yake.

Get out of my office now!” Mr. Oduya alifoka huku sauti na mwili wake ukitetemeka kwa ghadhabu.

Tunu na Tom waliendelea kuketi kwenye viti vyao wakiwa hawana wasiwasi wowote, walikuwa wakimtazama kwa makini huku nyuso zao zikipambwa na tabasamu.

“Mzee, nilidhani ungefurahi kutuona hapa kwani ulikuwa unatusaka kwa udi na uvumba. Umesababisha vifo vya watu wako na hata rafiki’angu Victor yupo hospitali akipigania uhai wake, yote ni sababu ya kuhakikisha unatupata, sasa...”

“Toka nje! Tokeni kabla sijawafanyia kitu kibaya...” Mr. Oduya limkatisha Tunu huku akifoka kwa ghadhabu. Povu la hasira lilianza kumtoka mdomoni.

“...usijali, nikimaliza kukueleza niliyokusudia tutatoka,” Tunu alisema pasipo kujali vitisho vya Mr. Oduya. “Kumbuka taifa hili siyo kampuni ambayo yeyote anaweza kuimiliki, uliweza kuwanunua watu wengi akiwemo Kamishna Omalla na Victor lakini ukasahau kuwa wapo wenye moyo wa kizalendo kama Faustine Thomas Ndejembi, ambaye wewe unamfahamu kwa jina la Tom...”

“Toka!” Mr. Oduya alifoka huku akivuta mtoto wa meza na kutoa bastola aina ya FNX 45 Tactical. Akaishika vyema mkononi na kuielekeza kwa Tunu na Tom, alikuwa ameghadhabika mno na povu lilizidi kumtoka mdomoni. “Tokeni ofisi kwangu, vinginevyo sitasita kuwaua,” alifoka.

Tunu na Tom waliangaliana, wakaachia tabasamu wakionekana kutokuwa na hofu yoyote. Kitendo kile kikamshangaza sana Mr. Oduya. Kabla hajafanya chochote mlango wa ofisi yake ukapigwa kumbo, Naibu Kamishna Mamboleo na vijana wake sita waliokuwa wamebebelea bunduki na vifua vyao vikiwa vimekingwa na mavazi maalumu yanayozuia risasi wakaingia na kutawanyika ndani ya ile ofisi. Wale askari wote walikuwa na sura ya kazi.

Mr. Oduya akapigwa na butwaa, alimtazama Naibu Kamishna Mamboleo kwa macho yenye mchanganyiko wa aibu na hasira, kisha akayahamisha macho yake kuwataza wale askari kwa zamu kabla hajayarudisha kwa Tunu na Tom, ambao sura zao zilikuwa bado zimepambwa na tabasamu.

“Mr. Oduya, tafadhali weka bastola yako chini na ujisalimishe. Kama ni mipango imeshaharibika. Umemwaga damu zisizo na hatia, umethubutu kununua watu hadi walinzi wa Amani kwa sababu ya kutaka kutimiza mipango yako michafu ili uwe kiongozi wa nchi hii. Jisalimishe ili sheria ichukue mkondo wake,” Naibu Kamishna Mamboleo alimwamuru Mr. Oduya.

Mr. Oduya alimtazama Naibu Kamishna Mamboleo kwa hasira, alionekana kuchanganyikiwa. Aliyasaga meno yake kwa hasira. “Siwezi kukubali kukamatwa na kupelekwa mahakamani, nitaitazama vipi jamii? Nitamtazama vipi Rais?” Mr. Oduya aliwaza na kuielekeza bastola yake kichwani kwake.

Kumbe Tunu na Tom walikuwa wakiyasoma mawazo yake, kwa kasi ya ajabu Tunu alichupa, akaruka juu na kutua mbele ya Mr. Oduya na wakati huohuo Tom aliserereka juu ya meza na kumdaka Mr. Oduya. Tunu aliupiga teke mkono wa Mr. Oduya ulioshika bastola na wakati huohuo ukasikika mlipuko wa bastola.

Naibu Kamishna Mamboleo na vijana wake walipotazama kwa makini wakamwona Mr. Oduya akiwa amedhibitiwa. Tom alikuwa amemkandamiza kwa nguvu huku amembana mikono yake kwa nyuma na Tunu alitoa pingu na kumfunga, kisha wakamwinua na kumkabidhi kwa Naibu Kamishna Mamboleo.

“Kamishna, nasikitika muda hautoshi kuzungumza mengi, kwani kuna mahali tunatakiwa kuwahi,” Tunu alimwambia Naibu Kamishna Mamboleo baada ya kuitazama saa yake ya mkononi.

“Nadhani kesho utapata faili lenye taarifa zote kuhusu mtandao wa uhalifu. Ila huko Kinyerezi kuna nyumba moja ambayo ndani yake tumewafungia wahalifu wanne waliotumwa na huyu mzee kutuua mimi na Tom. Hapo chini kuna wenzetu wawili, Bob na Dumba, watawapeleka kwenye nyumba hiyo,” Tunu alisema huku akimshika mkono Tom tayari kwa kuondoka.

“Pia katika Hospitali ya St. Agatha iliyopo Mikocheni inayomilikiwa ya rafiki wa Mr. Oduya, kuna mtu anaitwa Victor, Ofisa Usalama wa Taifa anayeshughulikia Kanda ya Kinondoni, amelazwa akitibiwa kwa siri baada ya kuvunjwa mbavu alipopambana nami, alitumwa na huyu mzee kuja kuniua,” Tunu alisema huku akipiga hatua kuondoka.

“Kwa nini, vijana?” Naibu Kamishna Mamboleo alifoka. “Kwa nini hamkuyaweka mambo haya wazi mapema hadi damu nyingi imemwagika? Mnajua huyu mtu alikaribia kunifanya nijiuzulu kazi yangu!” Naibu Kamishna Mamboleo alisema kwa huzuni.

Inaendelea...

CC the_legend Norshad bobefu zoefu Pablo PAKAYA Ibney blackstarline Bryece Tater Bigjahman moneytalk marybaby nipo2 ram kisukari Smart911 Madame S carbamazepine Astelia culture gal Prisoner of hope Mine eyes kuku mweus Thad hearly Shunie Tumosa Mine eyes Kudo swahiba92 ludist Toyota escudo Clkey macson3 boga la kiangazi LEGE Smart911 Richard irakunda skfull popie Krizy Beat hearly nipo2 MWINDAJI HARAMU kakhulu Katavi Norami mbududa iron2012 popie Bughy Harry Mlenge Kacheda mjasiliamali Laki Si Pesa cocochanel kinusikwetu big jambo mludego Shupavu Kacheda mjasiliamali Mweweso Songa Heri esiankiki mnadhimu mkuu wa jf red apple the-sniper MR KUO dan oseko Jackal kuku mweus mtugani wa wapi huyo chiqutitta ndukulusudicho ADK aggyd BAHARI J

NB: Litro 👩
 
Taxi - (160)

“Usijali, Kamishna. Muda ulikuwa haujafika, maana kila kitu kina wakati wake chini ya jua,” Tunu alisema, kisha yeye na Tom wakaanza kupiga hatua kueleka nje ya ile ofisi. Walitoka wakaelekea kilipo chumba cha lifti ambapo Tom alibonyeza kitufe cha kuteremka, milango ikafunguka na kuwaruhusu kuingia ndani. Wakateremka hadi chini na kuelekea kwenye gari lao.

* * * * *

Saa kumi na robo Tunu na Tom walikuwa wanashuka toka kwenye gari lao katika viunga vya maegesho ya magari ya Hospitali ya Taifa ya Muhimbili na kuelekea kwenye jengo la wodi alimokuwa amehamishiwa Sammy katika jengo la Taasisi ya Tiba ya Mifupa (MOI). Walitembea wakiwa wameshikana mikono kama wanandoa wapya waliotoka kwenye fungate baada ya ndoa yao.

Wakati wakipita kwenye korido ndefu ya jengo lile la Taasisi ya Tiba ya Mifupa walisikia mazungumzo ya watu waliopishana nao wakizungumza kuhusu kifo cha Kamishna Omalla na kukamatwa kwa bilionea Mr. Oduya. Tunu na Tom wakatazamana wakioneshwa kushangazwa sana jinsi habari zile zilivyoweza kusafiri haraka na kufika katika kila pembe ya jiji la Dar es Salaam.

Hawakupata taabu kuifikia wodi alimolazwa Sammy kwani pale nje walimkuta askari mmoja mwenye silaha aliyekuwa akilinda eneo lile aliyewaelekeza. Askari yule alikuwa amepewa taarifa na Naibu Kamishna Mamboleo kuhusu ujio wao.

Waliingia wodini wakamkuta Sammy akiwa amelala kitandani kwenye foronya laini na mto wa kuegemeza kichwa, alikuwa akiongea na Joyce aliyekuwa pembeni yake ameketi kwenye kiti cha magurudumu. Madame Norah, Bi. Pamela, Rafel Jengo na Elli walikuwa wamesimama kando, wote wakimsikiliza Sammy.

Kwa mwonekano wa haraka Sammy alionekana hakuwa katika hatari kama mwanzo na hata chumba alichohamishiwa hakikuwa na mitambo ya kumsaidia kupumua ingawa alikuwa amewekewa kifaa maalumu cha kuchunguza mwenendo wa mapigo ya moyo wake kwenye vidole vya mkono wa kulia.

Tunu na Tom walipoingia wakawafanya watu wote wageuze shingo zao kutazama kwa makini kule mlangoni. Sammy na Elli waliwatambua mara moja. Sammy hakuamini macho yake. Alimtazama Tunu wakati akipiga hatua zake za madaha kuelekea pale kitandani huku mtikisiko wa umbo lake zuri la kike na matata ukizimeza haraka hisia za Sammy pasipo kujali maumivu ya mwili aliyokuwa nayo muda ule.

“Tunu!” Sammy alijikuta akitamka jina hilo kwa mshangao mkubwa uliochanganyika na furaha huku akitamani kuinuka kutoka pale kitandani ili amkumbatie. Lakini akajionya asifanye hivyo na kumtupia jicho mkewe.

“Sammy!” Tunu naye aliita kwa mshangao huku akiharakisha kwenda pale kitandani, alipofika alinyoosha mkono wake na kumgusa paji lake la uso kwa furaha huku akitokwa machozi ya furaha. Kisha alinyoosha mikono yake juu kumshukuru Mungu. “Vipi unajisikiaje kwa sasa?” Tunu alimuuliza Sammy huku akigeuza shingo yake kuwatazama watu wengine.

“Najisikia nafuu sasa, hasa baada ya kupata taarifa njema kuhusu kukamatwa kwa Mr. Oduya,” Sammy aliongea kwa furaha, kisha kama aliyegutuka akageuza shingo yake kumtazama Joyce. “By the way, huyu ni Joyce mke wangu...” alimtambulisha Joyce kwa Tunu.

Tunu alinyoosha mkono wake kumsalimia Joyce. “Nafurahi kukufahamu, maana juzi asubuhi nilikuja hospitali lakini sikuruhusiwa kukuona. Natumai unaendelea vyema,” alisema huku akiachia tabasamu.

“Naendelea vizuri, namshukuru Mungu kwa kunilinda, maana ni vigumu sana kuamini kuwa hadi sasa nipo hai,” Joyce alisema huku akinyoosha mkono wake kumsalimia Tunu. Waliangaliana kwa muda, kila mmoja alionekana kumhusudu mwenziwe.
Kisha Sammy aliwatambulisha Madame Norah, Bi. Pamela na Rafel Jengo kwa Tunu na Tom kisha akawaeleza kwa kifupi kuhusu Tunu. Wote walibaki mdomo wazi wakimshangaa Tunu, msichana mrembo lakini hatari kuliko hata hatari yenyewe. Ni Elli peke yake ambaye hakushangaa, kwani alimfahamu vyema Tunu.

Kisha kitambo kifupi cha ukimya kikapita mle ndani huku kila mmoja akionekana kuzama kwenye tafakuri juu ya mambo yote yaliyotokea. Simu ya Tunu ikaanza kuita, Tunu aliitazama kwa makini na kuliona jina la Dk. Mgaya Kingoba, Mkurugenzi Mkuu wa Idara ya Usalama wa Taifa (TISS). Akamtupia jicho Tom na kuwaomba radhi watu wengine kisha akajitenga nao na kuipokea ile simu.

“Hallo!” Tunu alisema kwa sauti tulivu baada ya kuiweka sikioni.

“Nimepata taarifa zenu, kwanza hongereni sana kwa kazi nzuri,” Dk. Kingoba alisema kwa sauti tulivu.

“Ahsante, mkuu,” Tunu alisema na kushusha pumzi za ndani kwa ndani.

“Katika oparesheni hii ulikuwa nani?”

“Mimi na Faustine Ndejembi, yule wa Ofisi ya Waziri Mkuu. Na watu wengine wawili ambao ni wapelelezi wa kujitegemea.”

“Ndejembi yupo wapi sasa hivi?”

“Ninaye hapa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili. Vipi mkuu?”

“Rais anahitaji kuonana nanyi leo usiku, hivyo ninaomba mfike ofisini kwangu kabla ya saa kumi na mbili,” Dk. Kingoba alisema na kukata simu.

Tunu alikenua meno kwa furaha na kurudi pale kitandani. “Sahamani, tunawaacha tumeitwa makao makuu haraka,” Tunu alimwambia Sammy kisha akawataka radhi watu wengine. Yeye na Tom wakatoka kuelekea kwenye gari lao wakiwaacha watu wote wakiwasindikiza kwa macho yaliyowahusudu sana.

* * * * *

Tom aliendesha gari lake katika barabara ile ya Umoja wa Mataifa akielekea Makao Makuu ya Idara ya Usalama wa Taifa, eneo la Oysterbay. Macho alikuwa ameyakaza barabarani lakini mawazo yake yalikuwa kwa Tunu, mwanadada jamali na aliyeumbika vyema. Kila nukta iliyopita Tom alijikuta akishindwa kuvumilia. Alihisi pumzi zikimpaa, akajiambia kimoyomoyo kuwa katika maisha yake hakupata kukutana na kiumbe wa shani kama Tunu!

Ingawa aliwahi kuwa na uhusiano na wasichana wengi wasio na idadi, lakini hakuwahi kuhisi hali kama aliyoihisi wakati huo akiwa ameketi pembeni ya mrembo wa shani anayeweza kumsahaulisha yeyote machungu yote ya dunia. Kwa Tom, Tunu alikuwa ua waridi machoni mwake, miski puani mwake na pepo masikioni mwake. Hata hivyo, alihisi donge la wivu likimkaba kooni baada ya kukumbuka kuwa Tunu alikuwa bado anampenda Sammy.

“Inaonesha bado unampenda sana Sammy! Kwa nini usimsahau na kuufungua moyo wako kwa mwanamume mwingine?” Tom alijikuta akimuuliza Tunu.

“Kwa sasa Sammy ninampenda kama rafiki na si kimapenzi, ninaiheshimu ndoa yake,” Tunu alisema na kuachia tabasamu lililoficha uchungu. “Endapo nitampata mwanamume mwenye mapenzi ya kweli na mimi nikampenda basi nitaufungua moyo wangu kwake.”

I wish I could be that man!” Tom alisema kwa sauti ya chini ambayo iliweza kumfikia Tunu.

“Umesemaje, Tom? Tunu aliuliza huku akimtazama kwa makini.

Oh! Forget what I said. Kuna nyakati ulimi unatamka jambo bila kuwasiliana kwanza na ubongo,” Tom alisema huku akiachia kicheko hafifu.

“Tafadhali rudia kile ulichokisema, nimesikia ukisema jambo ila sijakupata vyema,” Tunu alisisitiza huku akiyatuliza macho yake kwenye uso wa Tom.

“Nilisema I wish I could be that man!” Tom alisema huku akimtazama Tunu kwa tabasamu.

“Kwa nini utamani, kwani ukitaka iwe hivyo haitakuwa?” Tunu aliuliza huku akiwa bado ameyatuliza macho yake kwa Tom.

“Tunu, wewe ni msichana mrembo uliyejaaliwa sifa zote zimfaazo mke, ni mwanamke wa kipekee kabisa ambaye nimewahi kukutana naye katika maisha yangu. Unastahili kuwa na mume bora. Naamini mwanamume atakayekupata atakuwa na bahati sana. Ninatamani kuwa mwanamume huyo lakini sijui kama ninazo sifa za kuwa na wewe,” Tom alisema kwa huzuni na kushusha pumzi za ndani kwa ndani.

Kikapita kimya kizito ndani ya lile gari kilichomfanya Tom kushtuka, akageuza shingo yake kumtazama Tunu na kumwona akiwa ameinamisha kichwa chake akionekana kuwa mbali sana kimawazo.

“Tunu... usichukie. Nimeyasema haya kwa sababu sitaki kuendelea kuumia, huu ndiyo ukweli ulio ndani ya moyo wangu… nimenyoosha mikono yangu kuomba zawadi unayodhani itanifaa na sistahili kuona utakachonipa, ni hiari yako kuniwekea mikononi kile unachodhani kinanifaa zaidi hata kama ni kaa la moto...”

“Wala usijali, Tom. Ninaelewa kilichomo moyoni mwako kupitia macho yako. Siwezi kuzuia maana kila kitu hupangwa na Mungu. Ninadiriki kusema kuwa nadhani nimezaliwa kwa ajili yako…” Tunu alisema maneno yaliyoufanya mkondo wa umeme kupitishwa ghafla katika mwili wa Tom. Vita vilikuwa vimekwisha na yeye akiwa kasalimu amri!

“Unasema kweli au unanitania?” Tom aliuliza kwa sauti iliyoonesha wazi kuwa hakuamini alichokisikia. Ni kweli hakutegemea kujibiwa kirahisi namna ile. Aliduwaa kwa muda akiwa hajimudu huku akiajabia sauti iliyovunjika, na macho yaliyolegea. Vyote pamoja vilitoa haiba ya kike ndani mwa Tunu na kumwaia.

“Sina sababu ya kukutania,” Tunu alisema huku akiachia tabasamu pana. Jibu lile likamfanya Tom aachie usukani na kumkumbatia Tunu huku akimporomoshea mabusu, akajisahau kama alikuwa barabarani akiendesha gari. Gari likaanza kupoteza mwelekeo na kuserereka likielekea mtoni kwenye daraja la Selander. Kidogo wapate ajali, kama isingekuwa Tunu kumshtua!

Tom alikanyaga breki, gari likasimama. Kisha wote wawili waliangaliana na kujikuta wakicheka kwa sauti kubwa. Kilikuwa ni kicheko cha furaha isiyopimika!

TAMATI
Maoni, ushauri na ujumbe: 0685 666964 (WhatsApp)

NB: Litro 👩
 
Wow!! Hii ni next level, hongera sana mkuu, na ahsante kwa simulizi hii ya kusisimua. Nimepanga kuirudia tena during Christmas holiday!
 
Daaaaah jamani Tunu na Thom kama walikuwepo mawazon mwang nlitaman sana waoane
Ahsante Bishop kwa muda wako kutupa chakula ya ubungo
Tumefurah na kuhuzunika pia
Na tumejifunza meng vile vile
Mungu azidi kuimarisha kipawa chako
Be blessed rfk yetu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Taxi - (160)

“Usijali, Kamishna. Muda ulikuwa haujafika, maana kila kitu kina wakati wake chini ya jua,” Tunu alisema, kisha yeye na Tom wakaanza kupiga hatua kueleka nje ya ile ofisi. Walitoka wakaelekea kilipo chumba cha lifti ambapo Tom alibonyeza kitufe cha kuteremka, milango ikafunguka na kuwaruhusu kuingia ndani. Wakateremka hadi chini na kuelekea kwenye gari lao.

* * * * *

Saa kumi na robo Tunu na Tom walikuwa wanashuka toka kwenye gari lao katika viunga vya maegesho ya magari ya Hospitali ya Taifa ya Muhimbili na kuelekea kwenye jengo la wodi alimokuwa amehamishiwa Sammy katika jengo la Taasisi ya Tiba ya Mifupa (MOI). Walitembea wakiwa wameshikana mikono kama wanandoa wapya waliotoka kwenye fungate baada ya ndoa yao.

Wakati wakipita kwenye korido ndefu ya jengo lile la Taasisi ya Tiba ya Mifupa walisikia mazungumzo ya watu waliopishana nao wakizungumza kuhusu kifo cha Kamishna Omalla na kukamatwa kwa bilionea Mr. Oduya. Tunu na Tom wakatazamana wakioneshwa kushangazwa sana jinsi habari zile zilivyoweza kusafiri haraka na kufika katika kila pembe ya jiji la Dar es Salaam.

Hawakupata taabu kuifikia wodi alimolazwa Sammy kwani pale nje walimkuta askari mmoja mwenye silaha aliyekuwa akilinda eneo lile aliyewaelekeza. Askari yule alikuwa amepewa taarifa na Naibu Kamishna Mamboleo kuhusu ujio wao.

Waliingia wodini wakamkuta Sammy akiwa amelala kitandani kwenye foronya laini na mto wa kuegemeza kichwa, alikuwa akiongea na Joyce aliyekuwa pembeni yake ameketi kwenye kiti cha magurudumu. Madame Norah, Bi. Pamela, Rafel Jengo na Elli walikuwa wamesimama kando, wote wakimsikiliza Sammy.

Kwa mwonekano wa haraka Sammy alionekana hakuwa katika hatari kama mwanzo na hata chumba alichohamishiwa hakikuwa na mitambo ya kumsaidia kupumua ingawa alikuwa amewekewa kifaa maalumu cha kuchunguza mwenendo wa mapigo ya moyo wake kwenye vidole vya mkono wa kulia.

Tunu na Tom walipoingia wakawafanya watu wote wageuze shingo zao kutazama kwa makini kule mlangoni. Sammy na Elli waliwatambua mara moja. Sammy hakuamini macho yake. Alimtazama Tunu wakati akipiga hatua zake za madaha kuelekea pale kitandani huku mtikisiko wa umbo lake zuri la kike na matata ukizimeza haraka hisia za Sammy pasipo kujali maumivu ya mwili aliyokuwa nayo muda ule.

“Tunu!” Sammy alijikuta akitamka jina hilo kwa mshangao mkubwa uliochanganyika na furaha huku akitamani kuinuka kutoka pale kitandani ili amkumbatie. Lakini akajionya asifanye hivyo na kumtupia jicho mkewe.

“Sammy!” Tunu naye aliita kwa mshangao huku akiharakisha kwenda pale kitandani, alipofika alinyoosha mkono wake na kumgusa paji lake la uso kwa furaha huku akitokwa machozi ya furaha. Kisha alinyoosha mikono yake juu kumshukuru Mungu. “Vipi unajisikiaje kwa sasa?” Tunu alimuuliza Sammy huku akigeuza shingo yake kuwatazama watu wengine.

“Najisikia nafuu sasa, hasa baada ya kupata taarifa njema kuhusu kukamatwa kwa Mr. Oduya,” Sammy aliongea kwa furaha, kisha kama aliyegutuka akageuza shingo yake kumtazama Joyce. “By the way, huyu ni Joyce mke wangu...” alimtambulisha Joyce kwa Tunu.

Tunu alinyoosha mkono wake kumsalimia Joyce. “Nafurahi kukufahamu, maana juzi asubuhi nilikuja hospitali lakini sikuruhusiwa kukuona. Natumai unaendelea vyema,” alisema huku akiachia tabasamu.

“Naendelea vizuri, namshukuru Mungu kwa kunilinda, maana ni vigumu sana kuamini kuwa hadi sasa nipo hai,” Joyce alisema huku akinyoosha mkono wake kumsalimia Tunu. Waliangaliana kwa muda, kila mmoja alionekana kumhusudu mwenziwe.
Kisha Sammy aliwatambulisha Madame Norah, Bi. Pamela na Rafel Jengo kwa Tunu na Tom kisha akawaeleza kwa kifupi kuhusu Tunu. Wote walibaki mdomo wazi wakimshangaa Tunu, msichana mrembo lakini hatari kuliko hata hatari yenyewe. Ni Elli peke yake ambaye hakushangaa, kwani alimfahamu vyema Tunu.

Kisha kitambo kifupi cha ukimya kikapita mle ndani huku kila mmoja akionekana kuzama kwenye tafakuri juu ya mambo yote yaliyotokea. Simu ya Tunu ikaanza kuita, Tunu aliitazama kwa makini na kuliona jina la Dk. Mgaya Kingoba, Mkurugenzi Mkuu wa Idara ya Usalama wa Taifa (TISS). Akamtupia jicho Tom na kuwaomba radhi watu wengine kisha akajitenga nao na kuipokea ile simu.

“Hallo!” Tunu alisema kwa sauti tulivu baada ya kuiweka sikioni.

“Nimepata taarifa zenu, kwanza hongereni sana kwa kazi nzuri,” Dk. Kingoba alisema kwa sauti tulivu.

“Ahsante, mkuu,” Tunu alisema na kushusha pumzi za ndani kwa ndani.

“Katika oparesheni hii ulikuwa nani?”

“Mimi na Faustine Ndejembi, yule wa Ofisi ya Waziri Mkuu. Na watu wengine wawili ambao ni wapelelezi wa kujitegemea.”

“Ndejembi yupo wapi sasa hivi?”

“Ninaye hapa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili. Vipi mkuu?”

“Rais anahitaji kuonana nanyi leo usiku, hivyo ninaomba mfike ofisini kwangu kabla ya saa kumi na mbili,” Dk. Kingoba alisema na kukata simu.

Tunu alikenua meno kwa furaha na kurudi pale kitandani. “Sahamani, tunawaacha tumeitwa makao makuu haraka,” Tunu alimwambia Sammy kisha akawataka radhi watu wengine. Yeye na Tom wakatoka kuelekea kwenye gari lao wakiwaacha watu wote wakiwasindikiza kwa macho yaliyowahusudu sana.

* * * * *

Tom aliendesha gari lake katika barabara ile ya Umoja wa Mataifa akielekea Makao Makuu ya Idara ya Usalama wa Taifa, eneo la Oysterbay. Macho alikuwa ameyakaza barabarani lakini mawazo yake yalikuwa kwa Tunu, mwanadada jamali na aliyeumbika vyema. Kila nukta iliyopita Tom alijikuta akishindwa kuvumilia. Alihisi pumzi zikimpaa, akajiambia kimoyomoyo kuwa katika maisha yake hakupata kukutana na kiumbe wa shani kama Tunu!

Ingawa aliwahi kuwa na uhusiano na wasichana wengi wasio na idadi, lakini hakuwahi kuhisi hali kama aliyoihisi wakati huo akiwa ameketi pembeni ya mrembo wa shani anayeweza kumsahaulisha yeyote machungu yote ya dunia. Kwa Tom, Tunu alikuwa ua waridi machoni mwake, miski puani mwake na pepo masikioni mwake. Hata hivyo, alihisi donge la wivu likimkaba kooni baada ya kukumbuka kuwa Tunu alikuwa bado anampenda Sammy.

“Inaonesha bado unampenda sana Sammy! Kwa nini usimsahau na kuufungua moyo wako kwa mwanamume mwingine?” Tom alijikuta akimuuliza Tunu.

“Kwa sasa Sammy ninampenda kama rafiki na si kimapenzi, ninaiheshimu ndoa yake,” Tunu alisema na kuachia tabasamu lililoficha uchungu. “Endapo nitampata mwanamume mwenye mapenzi ya kweli na mimi nikampenda basi nitaufungua moyo wangu kwake.”

I wish I could be that man!” Tom alisema kwa sauti ya chini ambayo iliweza kumfikia Tunu.

“Umesemaje, Tom? Tunu aliuliza huku akimtazama kwa makini.

Oh! Forget what I said. Kuna nyakati ulimi unatamka jambo bila kuwasiliana kwanza na ubongo,” Tom alisema huku akiachia kicheko hafifu.

“Tafadhali rudia kile ulichokisema, nimesikia ukisema jambo ila sijakupata vyema,” Tunu alisisitiza huku akiyatuliza macho yake kwenye uso wa Tom.

“Nilisema I wish I could be that man!” Tom alisema huku akimtazama Tunu kwa tabasamu.

“Kwa nini utamani, kwani ukitaka iwe hivyo haitakuwa?” Tunu aliuliza huku akiwa bado ameyatuliza macho yake kwa Tom.

“Tunu, wewe ni msichana mrembo uliyejaaliwa sifa zote zimfaazo mke, ni mwanamke wa kipekee kabisa ambaye nimewahi kukutana naye katika maisha yangu. Unastahili kuwa na mume bora. Naamini mwanamume atakayekupata atakuwa na bahati sana. Ninatamani kuwa mwanamume huyo lakini sijui kama ninazo sifa za kuwa na wewe,” Tom alisema kwa huzuni na kushusha pumzi za ndani kwa ndani.

Kikapita kimya kizito ndani ya lile gari kilichomfanya Tom kushtuka, akageuza shingo yake kumtazama Tunu na kumwona akiwa ameinamisha kichwa chake akionekana kuwa mbali sana kimawazo.

“Tunu... usichukie. Nimeyasema haya kwa sababu sitaki kuendelea kuumia, huu ndiyo ukweli ulio ndani ya moyo wangu… nimenyoosha mikono yangu kuomba zawadi unayodhani itanifaa na sistahili kuona utakachonipa, ni hiari yako kuniwekea mikononi kile unachodhani kinanifaa zaidi hata kama ni kaa la moto...”

“Wala usijali, Tom. Ninaelewa kilichomo moyoni mwako kupitia macho yako. Siwezi kuzuia maana kila kitu hupangwa na Mungu. Ninadiriki kusema kuwa nadhani nimezaliwa kwa ajili yako…” Tunu alisema maneno yaliyoufanya mkondo wa umeme kupitishwa ghafla katika mwili wa Tom. Vita vilikuwa vimekwisha na yeye akiwa kasalimu amri!

“Unasema kweli au unanitania?” Tom aliuliza kwa sauti iliyoonesha wazi kuwa hakuamini alichokisikia. Ni kweli hakutegemea kujibiwa kirahisi namna ile. Aliduwaa kwa muda akiwa hajimudu huku akiajabia sauti iliyovunjika, na macho yaliyolegea. Vyote pamoja vilitoa haiba ya kike ndani mwa Tunu na kumwaia.

“Sina sababu ya kukutania,” Tunu alisema huku akiachia tabasamu pana. Jibu lile likamfanya Tom aachie usukani na kumkumbatia Tunu huku akimporomoshea mabusu, akajisahau kama alikuwa barabarani akiendesha gari. Gari likaanza kupoteza mwelekeo na kuserereka likielekea mtoni kwenye daraja la Selander. Kidogo wapate ajali, kama isingekuwa Tunu kumshtua!

Tom alikanyaga breki, gari likasimama. Kisha wote wawili waliangaliana na kujikuta wakicheka kwa sauti kubwa. Kilikuwa ni kicheko cha furaha isiyopimika!

TAMATI
Maoni, ushauri na ujumbe: 0685 666964 (WhatsApp)

NB: Litro 👩

Safi sana... Story nzuri sana...


Chapter Closed...



Cc: mahondaw
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom