Bishop Hiluka
JF-Expert Member
- Aug 12, 2011
- 7,147
- 14,711
- Thread starter
- #1,161
Taxi - (159)
ILIPOISHIA
Mr. Oduya alihisi kama mwili wake ulikuwa ukicharangwa kwa visu vikali na kubanikwa katika moto mkubwa. Alihisi moto mkali sana ukitambaa kwenye mwili wake na ngozi yake ilikuwa inaungua na kumfanya kuhisi maumivu makali mno. Muda huohuo alihisi hasira kali zikiibuka ndani yake, chumba cha ofisi yake kilionekana kama kilichoshuka nyuzi kumi hivi na kuwa kifupi mno.
Mara simu yake ya mezani ikaanza kuita na kumzindua toka kwenye yale mawazo. Ndipo alipogundua kuwa ile simu ya mkononi ilikuwa bado ipo sikioni ingawa hakuwa akisikia tena kilichoongewa upande wa pili wa simu ile. Hakuweza kukumbuka ilichukua muda gani akiwa ameiweka ile simu sikioni huku mawazo yake yakiwa yamehama toka kwenye maongezi yake na Dk. Masanja hadi muda ule wakati simu ya mezani ilikuwa ikiita.
Hofu ilikuwa imemmeza kabisa, aliitazama ile simu ya mezani kwa wasiwasi huku akianza kuhisi jambo la hatari. Hata hivyo, hakutaka kuendelea kusubiri ile simu iendelee kuita zaidi kwani ilikuwa mbioni kukata baada ya kuita kwa muda mrefu. Hivyo akanyoosha mkono wake kivivuvivu ili kuipokea lakini kabla mkono haujaifikia ile simu ikakatika. Tukio lile likaiongeza hofu yake yake na hivyo akabaki akiikodolea macho ile simu kana kwamba lilikuwa bomu la kutegwa lililokuwa mbioni kulipuka.
Alianza kujiuliza, mpigaji wa simu ile angekuwa nani na angekuwa na shida gani muda ule, au ni yaleyale ya kupewa taarifa mbaya kuhusu Kamishna Omalla? Wakati akijiuliza mara ile simu ya mezani ikaanza kuita tena. Hakutaka iendelee kuita zaidi hivyo haraka akakinyakuwa kiwambo chake na kukiweka sikioni huku akiipa akili yake utulivu wa hali ya juu.
ENDELEA...
Mara tu alipoiweka ile simu sikioni sauti ya upande wa pili wa simu ikamtanabaisha kuwa mpigaji simu alikuwa ni katibu muhtasi wake.
“Bosi, kuna vijana wawili hapa wanadai kuwa lazima wakuone, wanasema ni rafiki zako na kwamba utafurahi sana kukutana nao,” katibu wa Mr. Oduya alisema kwenye simu.
“Sikutaka kuonana na mtu kwa sasa, wamekutajia majina yao na wanakotoka?” Mr. Oduya aliuliza kwa shauku.
“Wanasema wanatokea hapahapa Dar es Salaam. Mmoja anaitwa Tunu na mwingine ni Tom...”
“Kina nani!” sauti ya Mr. Oduya ilinguruma kwenye simu, ikapenya hadi kwenye ngoma ya sikio la katibu muhtasi wake na kutishia kuichana. Mr. Oduya aliogopa sana na hakuweza kusikia katibu wake aliongea au kumjibu nini, hakujua afanye nini na wala hakujua kama alikuwa tayari kuonana na vijana hao.
Alibaki ameduwaa asijue kipi cha kumwambia katibu muhtasi wake, mara akashuhudia mlango wa ofisi yake ukifunguliwa, Tunu na Tom wakaingia na kumkuta akiwa bado katika hali ile ya kuduwaa huku kiwambo cha simu kikiwa sikioni.
“Samahani, mzee, kwa kuingia bila ruhusa yako,” Tunu alisema kwa sauti tulivu ya kirafiki, huku akijikaribisha kwenye kiti pasipo kusubiri kukaribishwa. Tom naye akaketi kitini huku akimtazama Mr. Oduya kwa tabasamu.
“Nilipata salamu zako kuwa umekuwa ukinitafuta sana, umetumia rasilimali kubwa kuhakikisha unanipata, hivyo nimeona leo nije mwenyewe ili usipate taabu ya kuendelea kunitafuta. Sijui unasemaje, mzee?” Tunu alisema huku uso wake ukiwa umepambwa na tabasamu bashasha.
Hakuna jibu lililotoka kinywani mwa Mr. Oduya bali aliendelea kuduwaa huku akiwatazama Tunu na Tom kwa mshangao.
“Mr. Oduya, wewe ni mtu mbaya sana usiye na shukrani hata chembe,” Tunu aliendelea kuongea kwa sauti tulivu huku akiyatuliza macho yake kwenye uso wa Mr. Oduya. “Nafasi na heshima uliyo nayo kwenye jamii ya Watanzania ni kubwa sana lakini hujaridhika. Mamilioni ya Watanzania wamekuamini sana kiasi kwa kudhani ungefaa kuwa Rais ajaye lakini kumbe ni mbwa mwitu ndani ya ngozi ya kondoo! Unadiriki kushiriki katika mipango michafu ili kutimiza lengo lako. Aibu ilioje...”
Mr. Oduya akaonekana kurudiwa na fahamu, aliinuka huku akiwakazia macho Tunu na Tom. Muda wote Tom alikuwa kimya kabisa akimtazama Mr. Oduya kwa makini kama aliyekuwa akiyasoma mawazo yake.
“Get out of my office now!” Mr. Oduya alifoka huku sauti na mwili wake ukitetemeka kwa ghadhabu.
Tunu na Tom waliendelea kuketi kwenye viti vyao wakiwa hawana wasiwasi wowote, walikuwa wakimtazama kwa makini huku nyuso zao zikipambwa na tabasamu.
“Mzee, nilidhani ungefurahi kutuona hapa kwani ulikuwa unatusaka kwa udi na uvumba. Umesababisha vifo vya watu wako na hata rafiki’angu Victor yupo hospitali akipigania uhai wake, yote ni sababu ya kuhakikisha unatupata, sasa...”
“Toka nje! Tokeni kabla sijawafanyia kitu kibaya...” Mr. Oduya limkatisha Tunu huku akifoka kwa ghadhabu. Povu la hasira lilianza kumtoka mdomoni.
“...usijali, nikimaliza kukueleza niliyokusudia tutatoka,” Tunu alisema pasipo kujali vitisho vya Mr. Oduya. “Kumbuka taifa hili siyo kampuni ambayo yeyote anaweza kuimiliki, uliweza kuwanunua watu wengi akiwemo Kamishna Omalla na Victor lakini ukasahau kuwa wapo wenye moyo wa kizalendo kama Faustine Thomas Ndejembi, ambaye wewe unamfahamu kwa jina la Tom...”
“Toka!” Mr. Oduya alifoka huku akivuta mtoto wa meza na kutoa bastola aina ya FNX 45 Tactical. Akaishika vyema mkononi na kuielekeza kwa Tunu na Tom, alikuwa ameghadhabika mno na povu lilizidi kumtoka mdomoni. “Tokeni ofisi kwangu, vinginevyo sitasita kuwaua,” alifoka.
Tunu na Tom waliangaliana, wakaachia tabasamu wakionekana kutokuwa na hofu yoyote. Kitendo kile kikamshangaza sana Mr. Oduya. Kabla hajafanya chochote mlango wa ofisi yake ukapigwa kumbo, Naibu Kamishna Mamboleo na vijana wake sita waliokuwa wamebebelea bunduki na vifua vyao vikiwa vimekingwa na mavazi maalumu yanayozuia risasi wakaingia na kutawanyika ndani ya ile ofisi. Wale askari wote walikuwa na sura ya kazi.
Mr. Oduya akapigwa na butwaa, alimtazama Naibu Kamishna Mamboleo kwa macho yenye mchanganyiko wa aibu na hasira, kisha akayahamisha macho yake kuwataza wale askari kwa zamu kabla hajayarudisha kwa Tunu na Tom, ambao sura zao zilikuwa bado zimepambwa na tabasamu.
“Mr. Oduya, tafadhali weka bastola yako chini na ujisalimishe. Kama ni mipango imeshaharibika. Umemwaga damu zisizo na hatia, umethubutu kununua watu hadi walinzi wa Amani kwa sababu ya kutaka kutimiza mipango yako michafu ili uwe kiongozi wa nchi hii. Jisalimishe ili sheria ichukue mkondo wake,” Naibu Kamishna Mamboleo alimwamuru Mr. Oduya.
Mr. Oduya alimtazama Naibu Kamishna Mamboleo kwa hasira, alionekana kuchanganyikiwa. Aliyasaga meno yake kwa hasira. “Siwezi kukubali kukamatwa na kupelekwa mahakamani, nitaitazama vipi jamii? Nitamtazama vipi Rais?” Mr. Oduya aliwaza na kuielekeza bastola yake kichwani kwake.
Kumbe Tunu na Tom walikuwa wakiyasoma mawazo yake, kwa kasi ya ajabu Tunu alichupa, akaruka juu na kutua mbele ya Mr. Oduya na wakati huohuo Tom aliserereka juu ya meza na kumdaka Mr. Oduya. Tunu aliupiga teke mkono wa Mr. Oduya ulioshika bastola na wakati huohuo ukasikika mlipuko wa bastola.
Naibu Kamishna Mamboleo na vijana wake walipotazama kwa makini wakamwona Mr. Oduya akiwa amedhibitiwa. Tom alikuwa amemkandamiza kwa nguvu huku amembana mikono yake kwa nyuma na Tunu alitoa pingu na kumfunga, kisha wakamwinua na kumkabidhi kwa Naibu Kamishna Mamboleo.
“Kamishna, nasikitika muda hautoshi kuzungumza mengi, kwani kuna mahali tunatakiwa kuwahi,” Tunu alimwambia Naibu Kamishna Mamboleo baada ya kuitazama saa yake ya mkononi.
“Nadhani kesho utapata faili lenye taarifa zote kuhusu mtandao wa uhalifu. Ila huko Kinyerezi kuna nyumba moja ambayo ndani yake tumewafungia wahalifu wanne waliotumwa na huyu mzee kutuua mimi na Tom. Hapo chini kuna wenzetu wawili, Bob na Dumba, watawapeleka kwenye nyumba hiyo,” Tunu alisema huku akimshika mkono Tom tayari kwa kuondoka.
“Pia katika Hospitali ya St. Agatha iliyopo Mikocheni inayomilikiwa ya rafiki wa Mr. Oduya, kuna mtu anaitwa Victor, Ofisa Usalama wa Taifa anayeshughulikia Kanda ya Kinondoni, amelazwa akitibiwa kwa siri baada ya kuvunjwa mbavu alipopambana nami, alitumwa na huyu mzee kuja kuniua,” Tunu alisema huku akipiga hatua kuondoka.
“Kwa nini, vijana?” Naibu Kamishna Mamboleo alifoka. “Kwa nini hamkuyaweka mambo haya wazi mapema hadi damu nyingi imemwagika? Mnajua huyu mtu alikaribia kunifanya nijiuzulu kazi yangu!” Naibu Kamishna Mamboleo alisema kwa huzuni.
Inaendelea...
CC the_legend Norshad bobefu zoefu Pablo PAKAYA Ibney blackstarline Bryece Tater Bigjahman moneytalk marybaby nipo2 ram kisukari Smart911 Madame S carbamazepine Astelia culture gal Prisoner of hope Mine eyes kuku mweus Thad hearly Shunie Tumosa Mine eyes Kudo swahiba92 ludist Toyota escudo Clkey macson3 boga la kiangazi LEGE Smart911 Richard irakunda skfull popie Krizy Beat hearly nipo2 MWINDAJI HARAMU kakhulu Katavi Norami mbududa iron2012 popie Bughy Harry Mlenge Kacheda mjasiliamali Laki Si Pesa cocochanel kinusikwetu big jambo mludego Shupavu Kacheda mjasiliamali Mweweso Songa Heri esiankiki mnadhimu mkuu wa jf red apple the-sniper MR KUO dan oseko Jackal kuku mweus mtugani wa wapi huyo chiqutitta ndukulusudicho ADK aggyd BAHARI J
NB: Litro 👩
ILIPOISHIA
Mr. Oduya alihisi kama mwili wake ulikuwa ukicharangwa kwa visu vikali na kubanikwa katika moto mkubwa. Alihisi moto mkali sana ukitambaa kwenye mwili wake na ngozi yake ilikuwa inaungua na kumfanya kuhisi maumivu makali mno. Muda huohuo alihisi hasira kali zikiibuka ndani yake, chumba cha ofisi yake kilionekana kama kilichoshuka nyuzi kumi hivi na kuwa kifupi mno.
Mara simu yake ya mezani ikaanza kuita na kumzindua toka kwenye yale mawazo. Ndipo alipogundua kuwa ile simu ya mkononi ilikuwa bado ipo sikioni ingawa hakuwa akisikia tena kilichoongewa upande wa pili wa simu ile. Hakuweza kukumbuka ilichukua muda gani akiwa ameiweka ile simu sikioni huku mawazo yake yakiwa yamehama toka kwenye maongezi yake na Dk. Masanja hadi muda ule wakati simu ya mezani ilikuwa ikiita.
Hofu ilikuwa imemmeza kabisa, aliitazama ile simu ya mezani kwa wasiwasi huku akianza kuhisi jambo la hatari. Hata hivyo, hakutaka kuendelea kusubiri ile simu iendelee kuita zaidi kwani ilikuwa mbioni kukata baada ya kuita kwa muda mrefu. Hivyo akanyoosha mkono wake kivivuvivu ili kuipokea lakini kabla mkono haujaifikia ile simu ikakatika. Tukio lile likaiongeza hofu yake yake na hivyo akabaki akiikodolea macho ile simu kana kwamba lilikuwa bomu la kutegwa lililokuwa mbioni kulipuka.
Alianza kujiuliza, mpigaji wa simu ile angekuwa nani na angekuwa na shida gani muda ule, au ni yaleyale ya kupewa taarifa mbaya kuhusu Kamishna Omalla? Wakati akijiuliza mara ile simu ya mezani ikaanza kuita tena. Hakutaka iendelee kuita zaidi hivyo haraka akakinyakuwa kiwambo chake na kukiweka sikioni huku akiipa akili yake utulivu wa hali ya juu.
ENDELEA...
Mara tu alipoiweka ile simu sikioni sauti ya upande wa pili wa simu ikamtanabaisha kuwa mpigaji simu alikuwa ni katibu muhtasi wake.
“Bosi, kuna vijana wawili hapa wanadai kuwa lazima wakuone, wanasema ni rafiki zako na kwamba utafurahi sana kukutana nao,” katibu wa Mr. Oduya alisema kwenye simu.
“Sikutaka kuonana na mtu kwa sasa, wamekutajia majina yao na wanakotoka?” Mr. Oduya aliuliza kwa shauku.
“Wanasema wanatokea hapahapa Dar es Salaam. Mmoja anaitwa Tunu na mwingine ni Tom...”
“Kina nani!” sauti ya Mr. Oduya ilinguruma kwenye simu, ikapenya hadi kwenye ngoma ya sikio la katibu muhtasi wake na kutishia kuichana. Mr. Oduya aliogopa sana na hakuweza kusikia katibu wake aliongea au kumjibu nini, hakujua afanye nini na wala hakujua kama alikuwa tayari kuonana na vijana hao.
Alibaki ameduwaa asijue kipi cha kumwambia katibu muhtasi wake, mara akashuhudia mlango wa ofisi yake ukifunguliwa, Tunu na Tom wakaingia na kumkuta akiwa bado katika hali ile ya kuduwaa huku kiwambo cha simu kikiwa sikioni.
“Samahani, mzee, kwa kuingia bila ruhusa yako,” Tunu alisema kwa sauti tulivu ya kirafiki, huku akijikaribisha kwenye kiti pasipo kusubiri kukaribishwa. Tom naye akaketi kitini huku akimtazama Mr. Oduya kwa tabasamu.
“Nilipata salamu zako kuwa umekuwa ukinitafuta sana, umetumia rasilimali kubwa kuhakikisha unanipata, hivyo nimeona leo nije mwenyewe ili usipate taabu ya kuendelea kunitafuta. Sijui unasemaje, mzee?” Tunu alisema huku uso wake ukiwa umepambwa na tabasamu bashasha.
Hakuna jibu lililotoka kinywani mwa Mr. Oduya bali aliendelea kuduwaa huku akiwatazama Tunu na Tom kwa mshangao.
“Mr. Oduya, wewe ni mtu mbaya sana usiye na shukrani hata chembe,” Tunu aliendelea kuongea kwa sauti tulivu huku akiyatuliza macho yake kwenye uso wa Mr. Oduya. “Nafasi na heshima uliyo nayo kwenye jamii ya Watanzania ni kubwa sana lakini hujaridhika. Mamilioni ya Watanzania wamekuamini sana kiasi kwa kudhani ungefaa kuwa Rais ajaye lakini kumbe ni mbwa mwitu ndani ya ngozi ya kondoo! Unadiriki kushiriki katika mipango michafu ili kutimiza lengo lako. Aibu ilioje...”
Mr. Oduya akaonekana kurudiwa na fahamu, aliinuka huku akiwakazia macho Tunu na Tom. Muda wote Tom alikuwa kimya kabisa akimtazama Mr. Oduya kwa makini kama aliyekuwa akiyasoma mawazo yake.
“Get out of my office now!” Mr. Oduya alifoka huku sauti na mwili wake ukitetemeka kwa ghadhabu.
Tunu na Tom waliendelea kuketi kwenye viti vyao wakiwa hawana wasiwasi wowote, walikuwa wakimtazama kwa makini huku nyuso zao zikipambwa na tabasamu.
“Mzee, nilidhani ungefurahi kutuona hapa kwani ulikuwa unatusaka kwa udi na uvumba. Umesababisha vifo vya watu wako na hata rafiki’angu Victor yupo hospitali akipigania uhai wake, yote ni sababu ya kuhakikisha unatupata, sasa...”
“Toka nje! Tokeni kabla sijawafanyia kitu kibaya...” Mr. Oduya limkatisha Tunu huku akifoka kwa ghadhabu. Povu la hasira lilianza kumtoka mdomoni.
“...usijali, nikimaliza kukueleza niliyokusudia tutatoka,” Tunu alisema pasipo kujali vitisho vya Mr. Oduya. “Kumbuka taifa hili siyo kampuni ambayo yeyote anaweza kuimiliki, uliweza kuwanunua watu wengi akiwemo Kamishna Omalla na Victor lakini ukasahau kuwa wapo wenye moyo wa kizalendo kama Faustine Thomas Ndejembi, ambaye wewe unamfahamu kwa jina la Tom...”
“Toka!” Mr. Oduya alifoka huku akivuta mtoto wa meza na kutoa bastola aina ya FNX 45 Tactical. Akaishika vyema mkononi na kuielekeza kwa Tunu na Tom, alikuwa ameghadhabika mno na povu lilizidi kumtoka mdomoni. “Tokeni ofisi kwangu, vinginevyo sitasita kuwaua,” alifoka.
Tunu na Tom waliangaliana, wakaachia tabasamu wakionekana kutokuwa na hofu yoyote. Kitendo kile kikamshangaza sana Mr. Oduya. Kabla hajafanya chochote mlango wa ofisi yake ukapigwa kumbo, Naibu Kamishna Mamboleo na vijana wake sita waliokuwa wamebebelea bunduki na vifua vyao vikiwa vimekingwa na mavazi maalumu yanayozuia risasi wakaingia na kutawanyika ndani ya ile ofisi. Wale askari wote walikuwa na sura ya kazi.
Mr. Oduya akapigwa na butwaa, alimtazama Naibu Kamishna Mamboleo kwa macho yenye mchanganyiko wa aibu na hasira, kisha akayahamisha macho yake kuwataza wale askari kwa zamu kabla hajayarudisha kwa Tunu na Tom, ambao sura zao zilikuwa bado zimepambwa na tabasamu.
“Mr. Oduya, tafadhali weka bastola yako chini na ujisalimishe. Kama ni mipango imeshaharibika. Umemwaga damu zisizo na hatia, umethubutu kununua watu hadi walinzi wa Amani kwa sababu ya kutaka kutimiza mipango yako michafu ili uwe kiongozi wa nchi hii. Jisalimishe ili sheria ichukue mkondo wake,” Naibu Kamishna Mamboleo alimwamuru Mr. Oduya.
Mr. Oduya alimtazama Naibu Kamishna Mamboleo kwa hasira, alionekana kuchanganyikiwa. Aliyasaga meno yake kwa hasira. “Siwezi kukubali kukamatwa na kupelekwa mahakamani, nitaitazama vipi jamii? Nitamtazama vipi Rais?” Mr. Oduya aliwaza na kuielekeza bastola yake kichwani kwake.
Kumbe Tunu na Tom walikuwa wakiyasoma mawazo yake, kwa kasi ya ajabu Tunu alichupa, akaruka juu na kutua mbele ya Mr. Oduya na wakati huohuo Tom aliserereka juu ya meza na kumdaka Mr. Oduya. Tunu aliupiga teke mkono wa Mr. Oduya ulioshika bastola na wakati huohuo ukasikika mlipuko wa bastola.
Naibu Kamishna Mamboleo na vijana wake walipotazama kwa makini wakamwona Mr. Oduya akiwa amedhibitiwa. Tom alikuwa amemkandamiza kwa nguvu huku amembana mikono yake kwa nyuma na Tunu alitoa pingu na kumfunga, kisha wakamwinua na kumkabidhi kwa Naibu Kamishna Mamboleo.
“Kamishna, nasikitika muda hautoshi kuzungumza mengi, kwani kuna mahali tunatakiwa kuwahi,” Tunu alimwambia Naibu Kamishna Mamboleo baada ya kuitazama saa yake ya mkononi.
“Nadhani kesho utapata faili lenye taarifa zote kuhusu mtandao wa uhalifu. Ila huko Kinyerezi kuna nyumba moja ambayo ndani yake tumewafungia wahalifu wanne waliotumwa na huyu mzee kutuua mimi na Tom. Hapo chini kuna wenzetu wawili, Bob na Dumba, watawapeleka kwenye nyumba hiyo,” Tunu alisema huku akimshika mkono Tom tayari kwa kuondoka.
“Pia katika Hospitali ya St. Agatha iliyopo Mikocheni inayomilikiwa ya rafiki wa Mr. Oduya, kuna mtu anaitwa Victor, Ofisa Usalama wa Taifa anayeshughulikia Kanda ya Kinondoni, amelazwa akitibiwa kwa siri baada ya kuvunjwa mbavu alipopambana nami, alitumwa na huyu mzee kuja kuniua,” Tunu alisema huku akipiga hatua kuondoka.
“Kwa nini, vijana?” Naibu Kamishna Mamboleo alifoka. “Kwa nini hamkuyaweka mambo haya wazi mapema hadi damu nyingi imemwagika? Mnajua huyu mtu alikaribia kunifanya nijiuzulu kazi yangu!” Naibu Kamishna Mamboleo alisema kwa huzuni.
Inaendelea...
CC the_legend Norshad bobefu zoefu Pablo PAKAYA Ibney blackstarline Bryece Tater Bigjahman moneytalk marybaby nipo2 ram kisukari Smart911 Madame S carbamazepine Astelia culture gal Prisoner of hope Mine eyes kuku mweus Thad hearly Shunie Tumosa Mine eyes Kudo swahiba92 ludist Toyota escudo Clkey macson3 boga la kiangazi LEGE Smart911 Richard irakunda skfull popie Krizy Beat hearly nipo2 MWINDAJI HARAMU kakhulu Katavi Norami mbududa iron2012 popie Bughy Harry Mlenge Kacheda mjasiliamali Laki Si Pesa cocochanel kinusikwetu big jambo mludego Shupavu Kacheda mjasiliamali Mweweso Songa Heri esiankiki mnadhimu mkuu wa jf red apple the-sniper MR KUO dan oseko Jackal kuku mweus mtugani wa wapi huyo chiqutitta ndukulusudicho ADK aggyd BAHARI J
NB: Litro 👩
Natamani aje awatolee povu lake na vile hawezagi kuvumilia