Stori ya kusisimua - Taxi

Stori ya kusisimua - Taxi

Riwaya ilikuwa poa ,sema imeisha kirahisi sana lakini pia nimeona uandishi wako ni wa kifilamu zaidi sio ki riwaya ndio maana ulikuwa unaweka details ambazo hazikuwa na umuhimu Sana

Mfano "akakunja barabara fulani akaenda mpk makutano ya barabara fulani,taa zilipo ruhusu akaondoka mpk akafika nyumbani..ni maoni Tu wala sina chuki binafsi
Nakupongeza Kwa muda uliotumia mpk kukamilisha hii riwaya....

Kabla ya kuisoma hii riwaya nilitoka kusoma riwaya inaitwa SIRI ipo kwenye hili hili jukwaa...
Ningependa uipitie na members wengine ni nzuri sababu maudhui hayajatofautiana Sana.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Taxi - (160)

“Usijali, Kamishna. Muda ulikuwa haujafika, maana kila kitu kina wakati wake chini ya jua,” Tunu alisema, kisha yeye na Tom wakaanza kupiga hatua kueleka nje ya ile ofisi. Walitoka wakaelekea kilipo chumba cha lifti ambapo Tom alibonyeza kitufe cha kuteremka, milango ikafunguka na kuwaruhusu kuingia ndani. Wakateremka hadi chini na kuelekea kwenye gari lao.

* * * * *

Saa kumi na robo Tunu na Tom walikuwa wanashuka toka kwenye gari lao katika viunga vya maegesho ya magari ya Hospitali ya Taifa ya Muhimbili na kuelekea kwenye jengo la wodi alimokuwa amehamishiwa Sammy katika jengo la Taasisi ya Tiba ya Mifupa (MOI). Walitembea wakiwa wameshikana mikono kama wanandoa wapya waliotoka kwenye fungate baada ya ndoa yao.

Wakati wakipita kwenye korido ndefu ya jengo lile la Taasisi ya Tiba ya Mifupa walisikia mazungumzo ya watu waliopishana nao wakizungumza kuhusu kifo cha Kamishna Omalla na kukamatwa kwa bilionea Mr. Oduya. Tunu na Tom wakatazamana wakioneshwa kushangazwa sana jinsi habari zile zilivyoweza kusafiri haraka na kufika katika kila pembe ya jiji la Dar es Salaam.

Hawakupata taabu kuifikia wodi alimolazwa Sammy kwani pale nje walimkuta askari mmoja mwenye silaha aliyekuwa akilinda eneo lile aliyewaelekeza. Askari yule alikuwa amepewa taarifa na Naibu Kamishna Mamboleo kuhusu ujio wao.

Waliingia wodini wakamkuta Sammy akiwa amelala kitandani kwenye foronya laini na mto wa kuegemeza kichwa, alikuwa akiongea na Joyce aliyekuwa pembeni yake ameketi kwenye kiti cha magurudumu. Madame Norah, Bi. Pamela, Rafel Jengo na Elli walikuwa wamesimama kando, wote wakimsikiliza Sammy.

Kwa mwonekano wa haraka Sammy alionekana hakuwa katika hatari kama mwanzo na hata chumba alichohamishiwa hakikuwa na mitambo ya kumsaidia kupumua ingawa alikuwa amewekewa kifaa maalumu cha kuchunguza mwenendo wa mapigo ya moyo wake kwenye vidole vya mkono wa kulia.

Tunu na Tom walipoingia wakawafanya watu wote wageuze shingo zao kutazama kwa makini kule mlangoni. Sammy na Elli waliwatambua mara moja. Sammy hakuamini macho yake. Alimtazama Tunu wakati akipiga hatua zake za madaha kuelekea pale kitandani huku mtikisiko wa umbo lake zuri la kike na matata ukizimeza haraka hisia za Sammy pasipo kujali maumivu ya mwili aliyokuwa nayo muda ule.

“Tunu!” Sammy alijikuta akitamka jina hilo kwa mshangao mkubwa uliochanganyika na furaha huku akitamani kuinuka kutoka pale kitandani ili amkumbatie. Lakini akajionya asifanye hivyo na kumtupia jicho mkewe.

“Sammy!” Tunu naye aliita kwa mshangao huku akiharakisha kwenda pale kitandani, alipofika alinyoosha mkono wake na kumgusa paji lake la uso kwa furaha huku akitokwa machozi ya furaha. Kisha alinyoosha mikono yake juu kumshukuru Mungu. “Vipi unajisikiaje kwa sasa?” Tunu alimuuliza Sammy huku akigeuza shingo yake kuwatazama watu wengine.

“Najisikia nafuu sasa, hasa baada ya kupata taarifa njema kuhusu kukamatwa kwa Mr. Oduya,” Sammy aliongea kwa furaha, kisha kama aliyegutuka akageuza shingo yake kumtazama Joyce. “By the way, huyu ni Joyce mke wangu...” alimtambulisha Joyce kwa Tunu.

Tunu alinyoosha mkono wake kumsalimia Joyce. “Nafurahi kukufahamu, maana juzi asubuhi nilikuja hospitali lakini sikuruhusiwa kukuona. Natumai unaendelea vyema,” alisema huku akiachia tabasamu.

“Naendelea vizuri, namshukuru Mungu kwa kunilinda, maana ni vigumu sana kuamini kuwa hadi sasa nipo hai,” Joyce alisema huku akinyoosha mkono wake kumsalimia Tunu. Waliangaliana kwa muda, kila mmoja alionekana kumhusudu mwenziwe.
Kisha Sammy aliwatambulisha Madame Norah, Bi. Pamela na Rafel Jengo kwa Tunu na Tom kisha akawaeleza kwa kifupi kuhusu Tunu. Wote walibaki mdomo wazi wakimshangaa Tunu, msichana mrembo lakini hatari kuliko hata hatari yenyewe. Ni Elli peke yake ambaye hakushangaa, kwani alimfahamu vyema Tunu.

Kisha kitambo kifupi cha ukimya kikapita mle ndani huku kila mmoja akionekana kuzama kwenye tafakuri juu ya mambo yote yaliyotokea. Simu ya Tunu ikaanza kuita, Tunu aliitazama kwa makini na kuliona jina la Dk. Mgaya Kingoba, Mkurugenzi Mkuu wa Idara ya Usalama wa Taifa (TISS). Akamtupia jicho Tom na kuwaomba radhi watu wengine kisha akajitenga nao na kuipokea ile simu.

“Hallo!” Tunu alisema kwa sauti tulivu baada ya kuiweka sikioni.

“Nimepata taarifa zenu, kwanza hongereni sana kwa kazi nzuri,” Dk. Kingoba alisema kwa sauti tulivu.

“Ahsante, mkuu,” Tunu alisema na kushusha pumzi za ndani kwa ndani.

“Katika oparesheni hii ulikuwa nani?”

“Mimi na Faustine Ndejembi, yule wa Ofisi ya Waziri Mkuu. Na watu wengine wawili ambao ni wapelelezi wa kujitegemea.”

“Ndejembi yupo wapi sasa hivi?”

“Ninaye hapa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili. Vipi mkuu?”

“Rais anahitaji kuonana nanyi leo usiku, hivyo ninaomba mfike ofisini kwangu kabla ya saa kumi na mbili,” Dk. Kingoba alisema na kukata simu.

Tunu alikenua meno kwa furaha na kurudi pale kitandani. “Sahamani, tunawaacha tumeitwa makao makuu haraka,” Tunu alimwambia Sammy kisha akawataka radhi watu wengine. Yeye na Tom wakatoka kuelekea kwenye gari lao wakiwaacha watu wote wakiwasindikiza kwa macho yaliyowahusudu sana.

* * * * *

Tom aliendesha gari lake katika barabara ile ya Umoja wa Mataifa akielekea Makao Makuu ya Idara ya Usalama wa Taifa, eneo la Oysterbay. Macho alikuwa ameyakaza barabarani lakini mawazo yake yalikuwa kwa Tunu, mwanadada jamali na aliyeumbika vyema. Kila nukta iliyopita Tom alijikuta akishindwa kuvumilia. Alihisi pumzi zikimpaa, akajiambia kimoyomoyo kuwa katika maisha yake hakupata kukutana na kiumbe wa shani kama Tunu!

Ingawa aliwahi kuwa na uhusiano na wasichana wengi wasio na idadi, lakini hakuwahi kuhisi hali kama aliyoihisi wakati huo akiwa ameketi pembeni ya mrembo wa shani anayeweza kumsahaulisha yeyote machungu yote ya dunia. Kwa Tom, Tunu alikuwa ua waridi machoni mwake, miski puani mwake na pepo masikioni mwake. Hata hivyo, alihisi donge la wivu likimkaba kooni baada ya kukumbuka kuwa Tunu alikuwa bado anampenda Sammy.

“Inaonesha bado unampenda sana Sammy! Kwa nini usimsahau na kuufungua moyo wako kwa mwanamume mwingine?” Tom alijikuta akimuuliza Tunu.

“Kwa sasa Sammy ninampenda kama rafiki na si kimapenzi, ninaiheshimu ndoa yake,” Tunu alisema na kuachia tabasamu lililoficha uchungu. “Endapo nitampata mwanamume mwenye mapenzi ya kweli na mimi nikampenda basi nitaufungua moyo wangu kwake.”

I wish I could be that man!” Tom alisema kwa sauti ya chini ambayo iliweza kumfikia Tunu.

“Umesemaje, Tom? Tunu aliuliza huku akimtazama kwa makini.

Oh! Forget what I said. Kuna nyakati ulimi unatamka jambo bila kuwasiliana kwanza na ubongo,” Tom alisema huku akiachia kicheko hafifu.

“Tafadhali rudia kile ulichokisema, nimesikia ukisema jambo ila sijakupata vyema,” Tunu alisisitiza huku akiyatuliza macho yake kwenye uso wa Tom.

“Nilisema I wish I could be that man!” Tom alisema huku akimtazama Tunu kwa tabasamu.

“Kwa nini utamani, kwani ukitaka iwe hivyo haitakuwa?” Tunu aliuliza huku akiwa bado ameyatuliza macho yake kwa Tom.

“Tunu, wewe ni msichana mrembo uliyejaaliwa sifa zote zimfaazo mke, ni mwanamke wa kipekee kabisa ambaye nimewahi kukutana naye katika maisha yangu. Unastahili kuwa na mume bora. Naamini mwanamume atakayekupata atakuwa na bahati sana. Ninatamani kuwa mwanamume huyo lakini sijui kama ninazo sifa za kuwa na wewe,” Tom alisema kwa huzuni na kushusha pumzi za ndani kwa ndani.

Kikapita kimya kizito ndani ya lile gari kilichomfanya Tom kushtuka, akageuza shingo yake kumtazama Tunu na kumwona akiwa ameinamisha kichwa chake akionekana kuwa mbali sana kimawazo.

“Tunu... usichukie. Nimeyasema haya kwa sababu sitaki kuendelea kuumia, huu ndiyo ukweli ulio ndani ya moyo wangu… nimenyoosha mikono yangu kuomba zawadi unayodhani itanifaa na sistahili kuona utakachonipa, ni hiari yako kuniwekea mikononi kile unachodhani kinanifaa zaidi hata kama ni kaa la moto...”

“Wala usijali, Tom. Ninaelewa kilichomo moyoni mwako kupitia macho yako. Siwezi kuzuia maana kila kitu hupangwa na Mungu. Ninadiriki kusema kuwa nadhani nimezaliwa kwa ajili yako…” Tunu alisema maneno yaliyoufanya mkondo wa umeme kupitishwa ghafla katika mwili wa Tom. Vita vilikuwa vimekwisha na yeye akiwa kasalimu amri!

“Unasema kweli au unanitania?” Tom aliuliza kwa sauti iliyoonesha wazi kuwa hakuamini alichokisikia. Ni kweli hakutegemea kujibiwa kirahisi namna ile. Aliduwaa kwa muda akiwa hajimudu huku akiajabia sauti iliyovunjika, na macho yaliyolegea. Vyote pamoja vilitoa haiba ya kike ndani mwa Tunu na kumwaia.

“Sina sababu ya kukutania,” Tunu alisema huku akiachia tabasamu pana. Jibu lile likamfanya Tom aachie usukani na kumkumbatia Tunu huku akimporomoshea mabusu, akajisahau kama alikuwa barabarani akiendesha gari. Gari likaanza kupoteza mwelekeo na kuserereka likielekea mtoni kwenye daraja la Selander. Kidogo wapate ajali, kama isingekuwa Tunu kumshtua!

Tom alikanyaga breki, gari likasimama. Kisha wote wawili waliangaliana na kujikuta wakicheka kwa sauti kubwa. Kilikuwa ni kicheko cha furaha isiyopimika!

TAMATI
Maoni, ushauri na ujumbe: 0685 666964 (WhatsApp)

NB: Litro

Hongera sana. Mkuu. Mi Ni msoma novel mzuri sana kitambo na Sasa nadeal na David Baldacci Tom Clancy etc. Umenipa raha sana kwa muda wote. Kwanza lugha yetu ya Kiswahili, lakini zaidi flow ya Story. Big up. Kesho Ni siku nyingine. Usiku mwema. Sisi saa tano Sasa. Na huko itakuwa saba.
 
Riwaya ilikuwa poa ,sema imeisha kirahisi sana lakini pia nimeona uandishi wako ni wa kifilamu zaidi sio ki riwaya ndio maana ulikuwa unaweka details ambazo hazikuwa na umuhimu Sana

Mfano "akakunja barabara fulani akaenda mpk makutano ya barabara fulani,taa zilipo ruhusu akaondoka mpk akafika nyumbani..ni maoni Tu wala sina chuki binafsi
Nakupongeza Kwa muda uliotumia mpk kukamilisha hii riwaya....

Kabla ya kuisoma hii riwaya nilitoka kusoma riwaya inaitwa SIRI ipo kwenye hili hili jukwaa...
Ningependa uipitie na members wengine ni nzuri sababu maudhui hayajatofautiana Sana.

Sent using Jamii Forums mobile app
Kwanini usingemfuata huko PM na kutoa ushauri badala ya kuja hapa?
 
Riwaya ilikuwa poa ,sema imeisha kirahisi sana lakini pia nimeona uandishi wako ni wa kifilamu zaidi sio ki riwaya ndio maana ulikuwa unaweka details ambazo hazikuwa na umuhimu Sana

Mfano "akakunja barabara fulani akaenda mpk makutano ya barabara fulani,taa zilipo ruhusu akaondoka mpk akafika nyumbani..ni maoni Tu wala sina chuki binafsi
Nakupongeza Kwa muda uliotumia mpk kukamilisha hii riwaya....

Kabla ya kuisoma hii riwaya nilitoka kusoma riwaya inaitwa SIRI ipo kwenye hili hili jukwaa...
Ningependa uipitie na members wengine ni nzuri sababu maudhui hayajatofautiana Sana.

Sent using Jamii Forums mobile app
Ni mtazamo wako wala siwezi kukupinga, lakini elewa kuwa hakuna kanuni moja ya kufuatwa katika uandishi wa riwaya labda kama uwezo wako wa kufikiri umeishia hapo...
 
Daah! Kwa kipindi kirefu sikuingia JF, leo ndio nimeingia na kuimaliza simulizi hii. Kwa kweli ni stori nzuri sana, hongera sana Bishop kwa mpangilio wa matukio.
 
Taxi - (160)

“Usijali, Kamishna. Muda ulikuwa haujafika, maana kila kitu kina wakati wake chini ya jua,” Tunu alisema, kisha yeye na Tom wakaanza kupiga hatua kueleka nje ya ile ofisi. Walitoka wakaelekea kilipo chumba cha lifti ambapo Tom alibonyeza kitufe cha kuteremka, milango ikafunguka na kuwaruhusu kuingia ndani. Wakateremka hadi chini na kuelekea kwenye gari lao.

* * * * *

Saa kumi na robo Tunu na Tom walikuwa wanashuka toka kwenye gari lao katika viunga vya maegesho ya magari ya Hospitali ya Taifa ya Muhimbili na kuelekea kwenye jengo la wodi alimokuwa amehamishiwa Sammy katika jengo la Taasisi ya Tiba ya Mifupa (MOI). Walitembea wakiwa wameshikana mikono kama wanandoa wapya waliotoka kwenye fungate baada ya ndoa yao.

Wakati wakipita kwenye korido ndefu ya jengo lile la Taasisi ya Tiba ya Mifupa walisikia mazungumzo ya watu waliopishana nao wakizungumza kuhusu kifo cha Kamishna Omalla na kukamatwa kwa bilionea Mr. Oduya. Tunu na Tom wakatazamana wakioneshwa kushangazwa sana jinsi habari zile zilivyoweza kusafiri haraka na kufika katika kila pembe ya jiji la Dar es Salaam.

Hawakupata taabu kuifikia wodi alimolazwa Sammy kwani pale nje walimkuta askari mmoja mwenye silaha aliyekuwa akilinda eneo lile aliyewaelekeza. Askari yule alikuwa amepewa taarifa na Naibu Kamishna Mamboleo kuhusu ujio wao.

Waliingia wodini wakamkuta Sammy akiwa amelala kitandani kwenye foronya laini na mto wa kuegemeza kichwa, alikuwa akiongea na Joyce aliyekuwa pembeni yake ameketi kwenye kiti cha magurudumu. Madame Norah, Bi. Pamela, Rafel Jengo na Elli walikuwa wamesimama kando, wote wakimsikiliza Sammy.

Kwa mwonekano wa haraka Sammy alionekana hakuwa katika hatari kama mwanzo na hata chumba alichohamishiwa hakikuwa na mitambo ya kumsaidia kupumua ingawa alikuwa amewekewa kifaa maalumu cha kuchunguza mwenendo wa mapigo ya moyo wake kwenye vidole vya mkono wa kulia.

Tunu na Tom walipoingia wakawafanya watu wote wageuze shingo zao kutazama kwa makini kule mlangoni. Sammy na Elli waliwatambua mara moja. Sammy hakuamini macho yake. Alimtazama Tunu wakati akipiga hatua zake za madaha kuelekea pale kitandani huku mtikisiko wa umbo lake zuri la kike na matata ukizimeza haraka hisia za Sammy pasipo kujali maumivu ya mwili aliyokuwa nayo muda ule.

“Tunu!” Sammy alijikuta akitamka jina hilo kwa mshangao mkubwa uliochanganyika na furaha huku akitamani kuinuka kutoka pale kitandani ili amkumbatie. Lakini akajionya asifanye hivyo na kumtupia jicho mkewe.

“Sammy!” Tunu naye aliita kwa mshangao huku akiharakisha kwenda pale kitandani, alipofika alinyoosha mkono wake na kumgusa paji lake la uso kwa furaha huku akitokwa machozi ya furaha. Kisha alinyoosha mikono yake juu kumshukuru Mungu. “Vipi unajisikiaje kwa sasa?” Tunu alimuuliza Sammy huku akigeuza shingo yake kuwatazama watu wengine.

“Najisikia nafuu sasa, hasa baada ya kupata taarifa njema kuhusu kukamatwa kwa Mr. Oduya,” Sammy aliongea kwa furaha, kisha kama aliyegutuka akageuza shingo yake kumtazama Joyce. “By the way, huyu ni Joyce mke wangu...” alimtambulisha Joyce kwa Tunu.

Tunu alinyoosha mkono wake kumsalimia Joyce. “Nafurahi kukufahamu, maana juzi asubuhi nilikuja hospitali lakini sikuruhusiwa kukuona. Natumai unaendelea vyema,” alisema huku akiachia tabasamu.

“Naendelea vizuri, namshukuru Mungu kwa kunilinda, maana ni vigumu sana kuamini kuwa hadi sasa nipo hai,” Joyce alisema huku akinyoosha mkono wake kumsalimia Tunu. Waliangaliana kwa muda, kila mmoja alionekana kumhusudu mwenziwe.
Kisha Sammy aliwatambulisha Madame Norah, Bi. Pamela na Rafel Jengo kwa Tunu na Tom kisha akawaeleza kwa kifupi kuhusu Tunu. Wote walibaki mdomo wazi wakimshangaa Tunu, msichana mrembo lakini hatari kuliko hata hatari yenyewe. Ni Elli peke yake ambaye hakushangaa, kwani alimfahamu vyema Tunu.

Kisha kitambo kifupi cha ukimya kikapita mle ndani huku kila mmoja akionekana kuzama kwenye tafakuri juu ya mambo yote yaliyotokea. Simu ya Tunu ikaanza kuita, Tunu aliitazama kwa makini na kuliona jina la Dk. Mgaya Kingoba, Mkurugenzi Mkuu wa Idara ya Usalama wa Taifa (TISS). Akamtupia jicho Tom na kuwaomba radhi watu wengine kisha akajitenga nao na kuipokea ile simu.

“Hallo!” Tunu alisema kwa sauti tulivu baada ya kuiweka sikioni.

“Nimepata taarifa zenu, kwanza hongereni sana kwa kazi nzuri,” Dk. Kingoba alisema kwa sauti tulivu.

“Ahsante, mkuu,” Tunu alisema na kushusha pumzi za ndani kwa ndani.

“Katika oparesheni hii ulikuwa nani?”

“Mimi na Faustine Ndejembi, yule wa Ofisi ya Waziri Mkuu. Na watu wengine wawili ambao ni wapelelezi wa kujitegemea.”

“Ndejembi yupo wapi sasa hivi?”

“Ninaye hapa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili. Vipi mkuu?”

“Rais anahitaji kuonana nanyi leo usiku, hivyo ninaomba mfike ofisini kwangu kabla ya saa kumi na mbili,” Dk. Kingoba alisema na kukata simu.

Tunu alikenua meno kwa furaha na kurudi pale kitandani. “Sahamani, tunawaacha tumeitwa makao makuu haraka,” Tunu alimwambia Sammy kisha akawataka radhi watu wengine. Yeye na Tom wakatoka kuelekea kwenye gari lao wakiwaacha watu wote wakiwasindikiza kwa macho yaliyowahusudu sana.

* * * * *

Tom aliendesha gari lake katika barabara ile ya Umoja wa Mataifa akielekea Makao Makuu ya Idara ya Usalama wa Taifa, eneo la Oysterbay. Macho alikuwa ameyakaza barabarani lakini mawazo yake yalikuwa kwa Tunu, mwanadada jamali na aliyeumbika vyema. Kila nukta iliyopita Tom alijikuta akishindwa kuvumilia. Alihisi pumzi zikimpaa, akajiambia kimoyomoyo kuwa katika maisha yake hakupata kukutana na kiumbe wa shani kama Tunu!

Ingawa aliwahi kuwa na uhusiano na wasichana wengi wasio na idadi, lakini hakuwahi kuhisi hali kama aliyoihisi wakati huo akiwa ameketi pembeni ya mrembo wa shani anayeweza kumsahaulisha yeyote machungu yote ya dunia. Kwa Tom, Tunu alikuwa ua waridi machoni mwake, miski puani mwake na pepo masikioni mwake. Hata hivyo, alihisi donge la wivu likimkaba kooni baada ya kukumbuka kuwa Tunu alikuwa bado anampenda Sammy.

“Inaonesha bado unampenda sana Sammy! Kwa nini usimsahau na kuufungua moyo wako kwa mwanamume mwingine?” Tom alijikuta akimuuliza Tunu.

“Kwa sasa Sammy ninampenda kama rafiki na si kimapenzi, ninaiheshimu ndoa yake,” Tunu alisema na kuachia tabasamu lililoficha uchungu. “Endapo nitampata mwanamume mwenye mapenzi ya kweli na mimi nikampenda basi nitaufungua moyo wangu kwake.”

I wish I could be that man!” Tom alisema kwa sauti ya chini ambayo iliweza kumfikia Tunu.

“Umesemaje, Tom? Tunu aliuliza huku akimtazama kwa makini.

Oh! Forget what I said. Kuna nyakati ulimi unatamka jambo bila kuwasiliana kwanza na ubongo,” Tom alisema huku akiachia kicheko hafifu.

“Tafadhali rudia kile ulichokisema, nimesikia ukisema jambo ila sijakupata vyema,” Tunu alisisitiza huku akiyatuliza macho yake kwenye uso wa Tom.

“Nilisema I wish I could be that man!” Tom alisema huku akimtazama Tunu kwa tabasamu.

“Kwa nini utamani, kwani ukitaka iwe hivyo haitakuwa?” Tunu aliuliza huku akiwa bado ameyatuliza macho yake kwa Tom.

“Tunu, wewe ni msichana mrembo uliyejaaliwa sifa zote zimfaazo mke, ni mwanamke wa kipekee kabisa ambaye nimewahi kukutana naye katika maisha yangu. Unastahili kuwa na mume bora. Naamini mwanamume atakayekupata atakuwa na bahati sana. Ninatamani kuwa mwanamume huyo lakini sijui kama ninazo sifa za kuwa na wewe,” Tom alisema kwa huzuni na kushusha pumzi za ndani kwa ndani.

Kikapita kimya kizito ndani ya lile gari kilichomfanya Tom kushtuka, akageuza shingo yake kumtazama Tunu na kumwona akiwa ameinamisha kichwa chake akionekana kuwa mbali sana kimawazo.

“Tunu... usichukie. Nimeyasema haya kwa sababu sitaki kuendelea kuumia, huu ndiyo ukweli ulio ndani ya moyo wangu… nimenyoosha mikono yangu kuomba zawadi unayodhani itanifaa na sistahili kuona utakachonipa, ni hiari yako kuniwekea mikononi kile unachodhani kinanifaa zaidi hata kama ni kaa la moto...”

“Wala usijali, Tom. Ninaelewa kilichomo moyoni mwako kupitia macho yako. Siwezi kuzuia maana kila kitu hupangwa na Mungu. Ninadiriki kusema kuwa nadhani nimezaliwa kwa ajili yako…” Tunu alisema maneno yaliyoufanya mkondo wa umeme kupitishwa ghafla katika mwili wa Tom. Vita vilikuwa vimekwisha na yeye akiwa kasalimu amri!

“Unasema kweli au unanitania?” Tom aliuliza kwa sauti iliyoonesha wazi kuwa hakuamini alichokisikia. Ni kweli hakutegemea kujibiwa kirahisi namna ile. Aliduwaa kwa muda akiwa hajimudu huku akiajabia sauti iliyovunjika, na macho yaliyolegea. Vyote pamoja vilitoa haiba ya kike ndani mwa Tunu na kumwaia.

“Sina sababu ya kukutania,” Tunu alisema huku akiachia tabasamu pana. Jibu lile likamfanya Tom aachie usukani na kumkumbatia Tunu huku akimporomoshea mabusu, akajisahau kama alikuwa barabarani akiendesha gari. Gari likaanza kupoteza mwelekeo na kuserereka likielekea mtoni kwenye daraja la Selander. Kidogo wapate ajali, kama isingekuwa Tunu kumshtua!

Tom alikanyaga breki, gari likasimama. Kisha wote wawili waliangaliana na kujikuta wakicheka kwa sauti kubwa. Kilikuwa ni kicheko cha furaha isiyopimika!

TAMATI
Maoni, ushauri na ujumbe: 0685 666964 (WhatsApp)

NB: Litro 👩
Eeh kumbe imeisha nillkuwa naangalia chini km inaendelea sikuona neno TAMATI
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom