Bishop Hiluka
JF-Expert Member
- Aug 12, 2011
- 7,147
- 14,711
- Thread starter
- #821
Taxi - (122)
“Afande, mwenye nyumba iliyopata tatizo ni ndugu yangu, nataka kujua kama kuna mtu yeyote ameokolewa hai kutoka katika nyumba hiyo,” Elli alisema huku akishuka na kumkabili yule askari. Mwili wake ulikuwa unatetemeka kwa hofu na alikuwa akiomba Mungu jambo lile liwe ni ndoto tu.
“Sijui kama atakuwa ni mmoja wa waliookolewa, hadi sasa tumepata watu wawili waliojeruhiwa, wote wanaume na tayari wamekimbizwa hospitali ya Amana, unaweza kwenda huko kuangalia kama yumo huyo ndugu yako. Mambo mengine ni kama unavyoyaona. Bado tunaendelea na zoezi la uokoaji kuona kama kuna chochote tunaweza kuokoa,” yule askari mwenye silaha alimwambia Elli kisha akaondoka eneo lile kwenda kuwazuia vibaka waliotaka kujipenyeza kwenda kuiba.
Ilimchukua Elli takriban dakika kumi na tano akiwa bado amepigwa na butwaa, alikuwa amesimama pale pembeni ya barabara akiiangalia nyumba ya Sammy ilivyobomoka na kubaki kama gofu, gari lake lilikuwa halitamaniki kwani kilichoonekana pale ni chuma chakavu tu. Michirizi ya machozi ilionekana kwenye macho ya Elli na mikono yake ilikuwa kichwani.
Baada ya dakika kumi na tano Elli alionekana kuzinduka, akatoa mikono yake kichwani na kufuta michirizi ya machozi, kisha akaliendea gari lake na kuingia, akatia moto na kuondoka eneo lile kwa mwendo wa kasi kama aliyepandwa na wazimu.
* * * * *
“Unawaza nini, Tunu?” Tom alimuuliza Tunu baada ya kumwona akiwa kimya kabisa amejiegemeza kwenye gari lake aina ya BMW X6 xDrive 50i huku akionekana kuzama kwenye lindi la mawazo.
Tunu alionekana kuzinduka na kushusha pumzi ndefu, akamtazama Tom na kuachia tabasamu, hata hivyo tabasamu lake halikuwa la furaha kwani macho yake yalionesha wasiwasi fulani. “Kuna kitu bado kinanitatiza kidogo hapa,” Tunu alisema akiwa anatazama kifikra.
“Najua, Tunu...” Tom alisema huku akiachia tabasamu kisha akaongeza. “Ni kuhusu hawa jamaa zetu, siyo?” alisema kwa sauti ya kunong’ona huku akigeuza shingo yake kutazama kule walikoingia wale wanaume waliokuwa wakikagua gari la Tunu.
Tunu alibetua kichwa chake kukubali. “Kwa vyovyote watu wa Mr. Oduya watafuatilia hapa kujua kilichotokea, naogopa hawa jamaa wasije wakabanwa halafu wakaropoka kila kitu,” Tunu alisema huku usoni kwake akionesha shaka fulani.
“Wala huna haja ya kuhofu kuhusu hawa jamaa. Ni watu wetu, tena watu wa kazi kwelikweli! Huwa tunawatumia pale idarani kama informers wetu katika oparesheni za hatari zinazohusisha uhalifu mkubwa,” Tom alisema.
“Vipi kuhusu wenye jengo hili, hawawezi kubanwa wakasema?” Tunu aliuliza tena huku akiyatuliza macho yake kwenye uso wa Tom.
“Hata wakija hapa hawawezi kukuta mtu, hili jengo halikaliwi na mtu. Ni mali ya Idara ya Usalama wa Taifa na ni maalumu kwa kazi maalumu...” Tom alisema na kushusha pumzi, kisha akaendelea, “Uliponipigia simu kunieleza kuhusu wasiwasi wako nami nikawapigia hawa jamaa na ndani ya dakika kumi tu wakafika hapa. Hivi sasa kwa kuwa wamemaliza kazi yao, wanasepa wala huwezi kujua wamepitia wapi.”
Baada ya hapo walipanga ratiba ya shughuli zao, wakakubaliana kuongeza nguvu kwa kuwajumuisha wale jamaa waliokagua gari la Tunu, pamoja na kina Bob ili kupambana na watu wa Mr. Oduya. Kisha Tunu akaaga kuwa alikuwa anaelekea Hospitali ya Amana kuonana na Sammy.
Tunu alijipakia kwenye gari lake, akawasha injini ya kulitoa nje, kisha akaliegesha kando ya barabara ya mtaa na kuonekana akiangaza macho yake kila pembe kuhakikisha usalama wake. Alitazama vioo vya pembeni vya kuangalia vitu vilivyo nyuma yake ili kuhakikisha usalama, punde akaliona gari moja aina ya Toyota Cresta gx100 jeupe likijiegesha nyuma kwa mbali kidogo.
Alilitazama kwa makini lakini hakuona kama alipaswa kuwa na shaka, kwani mtaa ule wa Sonega na eneo lote la Shaurimoyo, Ilala lilikuwa ni eneo la pilika pilika na magari mengi yalifika hapo kutokana na uwepo wa maduka mengi ya kuuza vipuri vya magari. Tunu alishusha pumzi za ndani kwa ndani, akaendelea kuangazaangaza macho yake na kuridhika na hali ya pale nje.
Akaandika ujumbe kwenye simu yake na kumtumia Tom, “Baadaye, hapa nje hali ni shwari!” alipomaliza akaondoa gari lake na kuingia barabara ya Shaurimoyo, akakunja kushoto na kujichanganya na msururu wa magari mengine.
“Tumfuate!” mwanamume mmoja aliyekuwa ndani ya lile gari aina ya Toyota Cresta gx100 jeupe alisema baada ya Tunu kuondoka. Ndani ya lile gari kulikuwa na watu wawili, kumbe walikuwa wanamfuatilia Tunu.
“Hakuna haja ya kumfuata, ngoja tuone nani mwingine atatoka humo ndani,” mwanamume mwingine aliyekuwa kwenye usukani alisema. “Tunachotakiwa kujua ni nani anashirikiana naye, basi!”
Yule aliyekuwa ameketi kwenye usukani alikuwa ni Victor na alikuwa ameshika kamera ndogo akipiga picha eneo lile kwa tahadhari. Mara wakamwona Tom akitoka ndani ya lile jengo na kupiga hatua zake haraka haraka huku akitazama chini, kisha akazama kwenye gari moja na kuondoka zake.
Wale watu waliokuwemo kwenye gari walimtazama kwa makini wakaonekana kumtambua, wakajikuta wakitabasamu.
“Dah! Nilihisi kitu kama hiki kutokea, hatimaye tumepata jibu. Sasa ni Tom na Tunu!” Victor alisema kisha akaangua kicheko hafifu kilichokuwa kimebeba uchungu na hasira huku akimtazama mwenzake aliyekuwa amekaa kando. “Nadhani sasa umenielewa, siyo?”
“Ulikuwa sahihi, Victor!” yule mwingine alisema huku akishusha pumzi ndefu.
“Nilikwambia tuliza kimuhemuhe kila kitu kitajulikana...” Victor alisema na kuwasha gari lake, wakaondoka.
* * * * *
Jitihada za madaktari na wauguzi hatimaye zilikuwa zimezaa matunda, Joyce alikuwa amezinduka na alishangaa sana kuona akiwa katika chumba chenye mitambo mingi pamoja na computer, yeye akiwa amelala kitandani amevishwa mitambo maalumu ya kumsaidia kupumua. Alizungusha macho yake huku na kule na kuwaona wauguzi wawili wakiwa bize kuchunguza hiki na kile ndani ya chumba kile.
Usichoke, safari bado inasonga, kama ni gari basi limekata breki kwenye mteremko mkali wa Mlima Kitonga. Endelea kufuatilia stori hii ya kusisimua ili kuujua mwisho wake...
NB: Litro 👩🦱
“Afande, mwenye nyumba iliyopata tatizo ni ndugu yangu, nataka kujua kama kuna mtu yeyote ameokolewa hai kutoka katika nyumba hiyo,” Elli alisema huku akishuka na kumkabili yule askari. Mwili wake ulikuwa unatetemeka kwa hofu na alikuwa akiomba Mungu jambo lile liwe ni ndoto tu.
“Sijui kama atakuwa ni mmoja wa waliookolewa, hadi sasa tumepata watu wawili waliojeruhiwa, wote wanaume na tayari wamekimbizwa hospitali ya Amana, unaweza kwenda huko kuangalia kama yumo huyo ndugu yako. Mambo mengine ni kama unavyoyaona. Bado tunaendelea na zoezi la uokoaji kuona kama kuna chochote tunaweza kuokoa,” yule askari mwenye silaha alimwambia Elli kisha akaondoka eneo lile kwenda kuwazuia vibaka waliotaka kujipenyeza kwenda kuiba.
Ilimchukua Elli takriban dakika kumi na tano akiwa bado amepigwa na butwaa, alikuwa amesimama pale pembeni ya barabara akiiangalia nyumba ya Sammy ilivyobomoka na kubaki kama gofu, gari lake lilikuwa halitamaniki kwani kilichoonekana pale ni chuma chakavu tu. Michirizi ya machozi ilionekana kwenye macho ya Elli na mikono yake ilikuwa kichwani.
Baada ya dakika kumi na tano Elli alionekana kuzinduka, akatoa mikono yake kichwani na kufuta michirizi ya machozi, kisha akaliendea gari lake na kuingia, akatia moto na kuondoka eneo lile kwa mwendo wa kasi kama aliyepandwa na wazimu.
* * * * *
“Unawaza nini, Tunu?” Tom alimuuliza Tunu baada ya kumwona akiwa kimya kabisa amejiegemeza kwenye gari lake aina ya BMW X6 xDrive 50i huku akionekana kuzama kwenye lindi la mawazo.
Tunu alionekana kuzinduka na kushusha pumzi ndefu, akamtazama Tom na kuachia tabasamu, hata hivyo tabasamu lake halikuwa la furaha kwani macho yake yalionesha wasiwasi fulani. “Kuna kitu bado kinanitatiza kidogo hapa,” Tunu alisema akiwa anatazama kifikra.
“Najua, Tunu...” Tom alisema huku akiachia tabasamu kisha akaongeza. “Ni kuhusu hawa jamaa zetu, siyo?” alisema kwa sauti ya kunong’ona huku akigeuza shingo yake kutazama kule walikoingia wale wanaume waliokuwa wakikagua gari la Tunu.
Tunu alibetua kichwa chake kukubali. “Kwa vyovyote watu wa Mr. Oduya watafuatilia hapa kujua kilichotokea, naogopa hawa jamaa wasije wakabanwa halafu wakaropoka kila kitu,” Tunu alisema huku usoni kwake akionesha shaka fulani.
“Wala huna haja ya kuhofu kuhusu hawa jamaa. Ni watu wetu, tena watu wa kazi kwelikweli! Huwa tunawatumia pale idarani kama informers wetu katika oparesheni za hatari zinazohusisha uhalifu mkubwa,” Tom alisema.
“Vipi kuhusu wenye jengo hili, hawawezi kubanwa wakasema?” Tunu aliuliza tena huku akiyatuliza macho yake kwenye uso wa Tom.
“Hata wakija hapa hawawezi kukuta mtu, hili jengo halikaliwi na mtu. Ni mali ya Idara ya Usalama wa Taifa na ni maalumu kwa kazi maalumu...” Tom alisema na kushusha pumzi, kisha akaendelea, “Uliponipigia simu kunieleza kuhusu wasiwasi wako nami nikawapigia hawa jamaa na ndani ya dakika kumi tu wakafika hapa. Hivi sasa kwa kuwa wamemaliza kazi yao, wanasepa wala huwezi kujua wamepitia wapi.”
Baada ya hapo walipanga ratiba ya shughuli zao, wakakubaliana kuongeza nguvu kwa kuwajumuisha wale jamaa waliokagua gari la Tunu, pamoja na kina Bob ili kupambana na watu wa Mr. Oduya. Kisha Tunu akaaga kuwa alikuwa anaelekea Hospitali ya Amana kuonana na Sammy.
Tunu alijipakia kwenye gari lake, akawasha injini ya kulitoa nje, kisha akaliegesha kando ya barabara ya mtaa na kuonekana akiangaza macho yake kila pembe kuhakikisha usalama wake. Alitazama vioo vya pembeni vya kuangalia vitu vilivyo nyuma yake ili kuhakikisha usalama, punde akaliona gari moja aina ya Toyota Cresta gx100 jeupe likijiegesha nyuma kwa mbali kidogo.
Alilitazama kwa makini lakini hakuona kama alipaswa kuwa na shaka, kwani mtaa ule wa Sonega na eneo lote la Shaurimoyo, Ilala lilikuwa ni eneo la pilika pilika na magari mengi yalifika hapo kutokana na uwepo wa maduka mengi ya kuuza vipuri vya magari. Tunu alishusha pumzi za ndani kwa ndani, akaendelea kuangazaangaza macho yake na kuridhika na hali ya pale nje.
Akaandika ujumbe kwenye simu yake na kumtumia Tom, “Baadaye, hapa nje hali ni shwari!” alipomaliza akaondoa gari lake na kuingia barabara ya Shaurimoyo, akakunja kushoto na kujichanganya na msururu wa magari mengine.
“Tumfuate!” mwanamume mmoja aliyekuwa ndani ya lile gari aina ya Toyota Cresta gx100 jeupe alisema baada ya Tunu kuondoka. Ndani ya lile gari kulikuwa na watu wawili, kumbe walikuwa wanamfuatilia Tunu.
“Hakuna haja ya kumfuata, ngoja tuone nani mwingine atatoka humo ndani,” mwanamume mwingine aliyekuwa kwenye usukani alisema. “Tunachotakiwa kujua ni nani anashirikiana naye, basi!”
Yule aliyekuwa ameketi kwenye usukani alikuwa ni Victor na alikuwa ameshika kamera ndogo akipiga picha eneo lile kwa tahadhari. Mara wakamwona Tom akitoka ndani ya lile jengo na kupiga hatua zake haraka haraka huku akitazama chini, kisha akazama kwenye gari moja na kuondoka zake.
Wale watu waliokuwemo kwenye gari walimtazama kwa makini wakaonekana kumtambua, wakajikuta wakitabasamu.
“Dah! Nilihisi kitu kama hiki kutokea, hatimaye tumepata jibu. Sasa ni Tom na Tunu!” Victor alisema kisha akaangua kicheko hafifu kilichokuwa kimebeba uchungu na hasira huku akimtazama mwenzake aliyekuwa amekaa kando. “Nadhani sasa umenielewa, siyo?”
“Ulikuwa sahihi, Victor!” yule mwingine alisema huku akishusha pumzi ndefu.
“Nilikwambia tuliza kimuhemuhe kila kitu kitajulikana...” Victor alisema na kuwasha gari lake, wakaondoka.
* * * * *
Jitihada za madaktari na wauguzi hatimaye zilikuwa zimezaa matunda, Joyce alikuwa amezinduka na alishangaa sana kuona akiwa katika chumba chenye mitambo mingi pamoja na computer, yeye akiwa amelala kitandani amevishwa mitambo maalumu ya kumsaidia kupumua. Alizungusha macho yake huku na kule na kuwaona wauguzi wawili wakiwa bize kuchunguza hiki na kile ndani ya chumba kile.
Usichoke, safari bado inasonga, kama ni gari basi limekata breki kwenye mteremko mkali wa Mlima Kitonga. Endelea kufuatilia stori hii ya kusisimua ili kuujua mwisho wake...
NB: Litro 👩🦱
🦱