Stori ya kusisimua - Taxi

Stori ya kusisimua - Taxi

Wakuu, mkiona kimya msihofu, wiki hii nimebanwa kidogo na majukumu fulani ya kikazi✍✍✍. Nadhani kuanzia keshokutwa, Mungu akipenda, tunaweza kuendelea na mtiririko wetu wa hadithi kama kawaida...😜😜😜 wacha niingie tena chimbo...🏃‍♂️🏃‍♂️🏃‍♂️
Wewe jamaa mjanja sana,🤣🤣 umemwepushia songombingo Shunie kiaina, naona leo kijiwe kimepoa kabisa. Sisikii tena watu wakimtafuta Shunie😜😜
 
Mkuu bishop hiluka umesahau kuniTag.Mimi pia ni mdau wa riwaya!
 
bishop hivi keshokutwa si ndo leo maneno haya ulisema juzii ety 🙄 🙄 🙄 🙄 🙄 njoo utumwagie vtu wenzio ety
 
Mkuu bishop hiluka umesahau kuniTag.Mimi pia ni mdau wa riwaya!

Mkuu, karibu tujumuike kwenye safari hii...


Taxi - (113)

ILIPOISHIA

Tunu alimwangalia kwa makini huku akiendelea kutabasamu na kusema, “Ndiyo, tafadhali unaweza kuniruhusu kuingia ndani?” Tunu alisema kwa sauti tulivu.

Kidogo Lucy akaonekana kusita, hakumwamini mgeni wake. “Unaweza kuniambia hitaji lako?”

“Naomba uniruhusu niinge ndani, ninahitaji kuonana na Winifrida, nimeelekezwa hapa na kaka’ake anayeitwa Sammy,” Tunu alisema na kugeuza shingo yake, akatazama kushoto na kulia kwake kuhakikisha kuna hali ya usalama kisha halafu akamtazama tena Lucy.

Lucy akashusha pumzi. Kimya kifupi kikapita huku Lucy akionekana kutafakari kisha akauma magego na kufanya mataya yake kuchezacheza kama aliyekuwa anatafuna kitu kigumu. Mara ikasikika sauti ya Victoria, “Dada, kwani unaongea na nani?”

Lucy aligeuza shingo yake na kumwona Victoria akiwa amesimama kwenye baraza kubwa ya ile nyumba. “Anasema amekuja kumwona Winifrida, ameelekezwa hapa na Sammy,” Lucy alisema.

SASA ENDELEA...

Victoria alielekea kule getini na alipofika alichungulia nje, akamwona Tunu akiwa bado amesimama pale pale huku tabasamu usoni kwake likiwa halijaenda likizo. Victoria alimtazama kwa makini. “Habari yako, dada?” Victoria alimsalimia.

“Nzuri, anti... naitwa Tunu na...” Tunu aliitikia na kuanza kujitambulisha.

“Ooh, Tunu! Karibu ndani,” Victoria alisema na kuachia tabasamu pana kisha akamgeukia Lucy. “Mfungulie geti aingize gari lake.”

Lucy alishusha pumzi na kulifungua lile geti kubwa akimruhusu Tunu kuingia. Tunu aliingiza gari lake ndani ya uzio wa ile nyumba, akaliegesha kwenye eneo la wazi jirani na banda maalumu la wazi la maegesho ya magari. Ndani ya banda lile kulikuwa na magari mawili, moja lilikuwa Toyota Hilux double cabin la rangi nyeupe na jingine ni aina ya Landcruiser GX V8 rangi nyeusi.

Alitulia kidogo ndani ya gari akiliacha liungurume kwa dakika chache kisha akazima injini na kushuka. Victoria alimwongoza kuelekea ndani ambako walimkuta Pendo akiwa ameketi juu ya sofa, peke yake, akionekana mwenye huzuni. Winifrida hakuwepo.

Wakati Tunu anaingia Pendo alimwangalia pasipo kuonesha tashwishwi yoyote usoni kwake, akili yake ya kitoto ilikuwa inawaza mbali sana. Alikuwa akimwaza mama yake.

“Shemeji Sammy alinipigia simu kunijulisha kuhusu ujio wako, nilipoona muda unazidi kwenda nikajua labda umeahirisha. Karibu sana, Tunu,” Victoria alisema wakati wanaketi juu ya masofa pale sebuleni.

“Ahsante. Kuna mambo fulani yaliingiliana, ikanibidi kwanza niyaweke sawa ndipo nije huku,” Tunu alisema huku akishusha pumzi kisha akaendelea. “Na kwa kuwa nimechelewa kidogo ningeomba twende moja kwa moja kwenye suala lililonileta hapa... shida yangu ni kuongea na Winifrida, sijui yupo?”

“Alikuwapo hapa sasa hivi, nadhani kaingia chumbani maana tangu tukio la jana hawajihisi tena kama wapo salama,” Victoria alisema na kugeuza shingo yake kumwangalia Pendo. “Huyu ni mtoto wa Sammy.”

Okay!” Tunu alisema huku akimtupia jicho Pendo, “Hujambo, mtoto mzuri?”

“Sijambo, shikamoo anti!” Pendo alisalimia, hakuonesha ule uchangamfu ambao amekuwa nao siku zote.

“Marhaba!” Tunu alisema huku akiachia tabasamu pana.

“Pendo nenda kamwite anti Winnie,” Victoria alimwambia Pendo. Pendo akatoka na kuelekea chumbani huku akiita kwa sauti. “Anti Winnie!”

“Nawahurumia sana hawa watoto, hawako sawa kisaikolojia,” Victoria alisema kwa huzuni.

“Mnapaswa kuhakikisha wanaonana na mwanasaikolojia wa watoto ili ajaribu kuwaweka sawa,” Tunu alishauri.

“Ndiyo maana wapo hapa kwani hiyo ndiyo taaluma yangu. Nimeomba ruhusa ya siku saba kazini ili kushughulikia suala hili,” Victoria alisema na kushusha pumzi za ndani kwa ndani.

“Umefanya vyema. Hili ni suala tata zito sana na watoto hawa hawawezi kulibeba,” Tunu alisema huku akishusha pumzi. “Pia, awali ya kila jambo tunatakiwa kumshukuru Mungu.”

“Kabisa!” Victoria aliafiki na wakati huo huo Winifrida na Pendo wakaingia sebuleni. Winifrida alimtazama Tunu kwa wasiwasi mkubwa, akashusha pumzi na kumsalimia kisha akaketi juu ya sofa.

Victoria na Tunu wakaangaliana kwa muda kisha Victoria akakohoa kidogo ili kusafisha sauti yake. “Winnie, huyu dada anaitwa Tunu, ameelekezwa hapa na kaka’ako, anataka kuongea na wewe,” Victoria alisema na kuinuka, akamshika mkono Pendo.

“Sasa, da’ Tunu, ngoja tuwaache wenyewe muongee kwa uhuru zaidi,” Victoria alisema huku akianza kuondoka.

“Haina shida, dada. Tukimalizana nitakwambia,” Tunu alisema huku akijiweka sawa pale kwenye sofa. Kikatokea kitambo kifupi cha ukimya, kila mmoja alionekana kutafakari. Winifrida alikuwa anamwangalia Tunu kwa jicho la kuibia, uso wake ulionesha wasiwasi fulani.

“Winnie, kwanza nikupe pole kwa yote yaliyotokea jana usiku... Najua hivi sasa unapitia mengi tu na huoni mtu wa kumweleza. Labda si kosa lako. Na sijui ni kwa nini umeshindwa kumweleza hata kaka’ako, au unaogopa?” Tunu alimuuliza Winifrida huku akiwa ameyatuliza macho yake kwenye uso wake.

Winifrida hakujibu, alibaki kimya akiangalia viganja vyake alivyoviweka juu ya mapaja yake. Tunu aliiona hali ya Winifrida kwa jinsi alivyokuwa na hofu, akatabasamu na kutafuta namna ya kuyaelekeza mazungumzo.

“Niko hapa mimi na wewe, wawili tu...” Tunu alisema na kusita, akashusha pumzi za ndani kwa ndani huku akionekana kama aliyekuwa akitafakari nini cha kusema. “Labda nikutoe wasiwasi, mimi nafanya kazi usalama wa taifa na chochote utakachoniambia, kama hupendi kaka’ako ajue kitabaki kuwa siri kati yetu. Nikutoe hofu kuwa wote waliofanya tukio hilo la kinyama watapatikana tu kama utakuwa muwazi...” Tunu alinyamaza kidogo ili maneno yale yamwingie Winifrida.

“Kwa sasa polisi wapo kazini wanawatafuta, mimi pia nimejitolea kusaidia ili kuhakikisha wote wanakamatwa... labda tu nikudokeze kuwa wapo watu ninaowahisi kufanya tukio hilo na ninazo picha zao, kwa hiyo huna sababu ya kunificha chochote unachokijua.” Tunu aliweka kituo, akaminya midomo yake yenye maki na kuficha vishimo vidogo vijitokeze kwenye mashavu yake.

“Sijui umenielewa?” Tunu alimuuliza Winifrida huku akimwangalia kwa makini.

“Nimekuelewa, dada,” Winifrida alisema, akavuta pumzi ndefu na kuzishusha taratibu huku akifanya kifua chake kipande na kushuka. Matiti yake madogo yaliyochongoka yalimiliki vyema eneo la kifua.

Tunu alitoa simu yake ya mkononi, ilikuwa simu nzuri na mpya kabisa aina ya iPhone 11 Pro Max, akaanza kupekuapekua kwenye ile simu kisha akamwonesha Winifrida picha ya Spoiler. “Ulimwona mtu mwenye sura kama hii?” alimuuliza huku akimtazama katika hali ya kumkagua.

Inaendelea

CC the_legend Norshad bobefu zoefu Pablo PAKAYA Ibney blackstarline Bryece Tater Bigjahman moneytalk marybaby nipo2 ram kisukari Smart911 Madame S carbamazepine Astelia culture gal Prisoner of hope Mine eyes kuku mweus Thad hearly Shunie Tumosa Mine eyes Kudo swahiba92 ludist Toyota escudo Clkey macson3 boga la kiangazi LEGE Smart911 Richard irakunda skfull popie Krizy Beat hearly nipo2 MWINDAJI HARAMU kakhulu Katavi Norami mbududa iron2012 popie Bughy Harry Mlenge Kacheda mjasiliamali Laki Si Pesa cocochanel kinusikwetu big jambo mludego Shupavu Kacheda mjasiliamali Mweweso Songa Heri esiankiki mnadhimu mkuu wa jf red apple the-sniper MR KUO dan oseko Jackal

NB: Litro 👩
 
Tumvumilie kidogo Bishop jamani yupo busy
Asante kwa kunielewa mama...

Hii story unaweza ilia chai bila vitafunwa
🤣🤣🤣...

Dah, wallahi leo Bishop katutoa mrisi!😱😱 Wapi Shunie?😉😉
bishop hivi keshokutwa si ndo leo maneno haya ulisema juzii ety 🙄 🙄 🙄 🙄 🙄 njoo utumwagie vtu wenzio ety
Shunie Boss. Leo Tunaomba useme naye. Twasubiri. Mana Hakuna mkate mgumu mbele ya chai yenye hiriki.

Leo nimekuja kamili kamili, tayari nimeshaanza kutupia...

NB: Litro 👩
 
karibu mkuu tuwe wote

Taxi - (113)

ILIPOISHIA

Tunu alimwangalia kwa makini huku akiendelea kutabasamu na kusema, “Ndiyo, tafadhali unaweza kuniruhusu kuingia ndani?” Tunu alisema kwa sauti tulivu.

Kidogo Lucy akaonekana kusita, hakumwamini mgeni wake. “Unaweza kuniambia hitaji lako?”

“Naomba uniruhusu niinge ndani, ninahitaji kuonana na Winifrida, nimeelekezwa hapa na kaka’ake anayeitwa Sammy,” Tunu alisema na kugeuza shingo yake, akatazama kushoto na kulia kwake kuhakikisha kuna hali ya usalama kisha halafu akamtazama tena Lucy.

Lucy akashusha pumzi. Kimya kifupi kikapita huku Lucy akionekana kutafakari kisha akauma magego na kufanya mataya yake kuchezacheza kama aliyekuwa anatafuna kitu kigumu. Mara ikasikika sauti ya Victoria, “Dada, kwani unaongea na nani?”

Lucy aligeuza shingo yake na kumwona Victoria akiwa amesimama kwenye baraza kubwa ya ile nyumba. “Anasema amekuja kumwona Winifrida, ameelekezwa hapa na Sammy,” Lucy alisema.

SASA ENDELEA...

Victoria alielekea kule getini na alipofika alichungulia nje, akamwona Tunu akiwa bado amesimama pale pale huku tabasamu usoni kwake likiwa halijaenda likizo. Victoria alimtazama kwa makini. “Habari yako, dada?” Victoria alimsalimia.

“Nzuri, anti... naitwa Tunu na...” Tunu aliitikia na kuanza kujitambulisha.

“Ooh, Tunu! Karibu ndani,” Victoria alisema na kuachia tabasamu pana kisha akamgeukia Lucy. “Mfungulie geti aingize gari lake.”

Lucy alishusha pumzi na kulifungua lile geti kubwa akimruhusu Tunu kuingia. Tunu aliingiza gari lake ndani ya uzio wa ile nyumba, akaliegesha kwenye eneo la wazi jirani na banda maalumu la wazi la maegesho ya magari. Ndani ya banda lile kulikuwa na magari mawili, moja lilikuwa Toyota Hilux double cabin la rangi nyeupe na jingine ni aina ya Landcruiser GX V8 rangi nyeusi.

Alitulia kidogo ndani ya gari akiliacha liungurume kwa dakika chache kisha akazima injini na kushuka. Victoria alimwongoza kuelekea ndani ambako walimkuta Pendo akiwa ameketi juu ya sofa, peke yake, akionekana mwenye huzuni. Winifrida hakuwepo.

Wakati Tunu anaingia Pendo alimwangalia pasipo kuonesha tashwishwi yoyote usoni kwake, akili yake ya kitoto ilikuwa inawaza mbali sana. Alikuwa akimwaza mama yake.

“Shemeji Sammy alinipigia simu kunijulisha kuhusu ujio wako, nilipoona muda unazidi kwenda nikajua labda umeahirisha. Karibu sana, Tunu,” Victoria alisema wakati wanaketi juu ya masofa pale sebuleni.

“Ahsante. Kuna mambo fulani yaliingiliana, ikanibidi kwanza niyaweke sawa ndipo nije huku,” Tunu alisema huku akishusha pumzi kisha akaendelea. “Na kwa kuwa nimechelewa kidogo ningeomba twende moja kwa moja kwenye suala lililonileta hapa... shida yangu ni kuongea na Winifrida, sijui yupo?”

“Alikuwapo hapa sasa hivi, nadhani kaingia chumbani maana tangu tukio la jana hawajihisi tena kama wapo salama,” Victoria alisema na kugeuza shingo yake kumwangalia Pendo. “Huyu ni mtoto wa Sammy.”

Okay!” Tunu alisema huku akimtupia jicho Pendo, “Hujambo, mtoto mzuri?”

“Sijambo, shikamoo anti!” Pendo alisalimia, hakuonesha ule uchangamfu ambao amekuwa nao siku zote.

“Marhaba!” Tunu alisema huku akiachia tabasamu pana.

“Pendo nenda kamwite anti Winnie,” Victoria alimwambia Pendo. Pendo akatoka na kuelekea chumbani huku akiita kwa sauti. “Anti Winnie!”

“Nawahurumia sana hawa watoto, hawako sawa kisaikolojia,” Victoria alisema kwa huzuni.

“Mnapaswa kuhakikisha wanaonana na mwanasaikolojia wa watoto ili ajaribu kuwaweka sawa,” Tunu alishauri.

“Ndiyo maana wapo hapa kwani hiyo ndiyo taaluma yangu. Nimeomba ruhusa ya siku saba kazini ili kushughulikia suala hili,” Victoria alisema na kushusha pumzi za ndani kwa ndani.

“Umefanya vyema. Hili ni suala tata zito sana na watoto hawa hawawezi kulibeba,” Tunu alisema huku akishusha pumzi. “Pia, awali ya kila jambo tunatakiwa kumshukuru Mungu.”

“Kabisa!” Victoria aliafiki na wakati huo huo Winifrida na Pendo wakaingia sebuleni. Winifrida alimtazama Tunu kwa wasiwasi mkubwa, akashusha pumzi na kumsalimia kisha akaketi juu ya sofa.

Victoria na Tunu wakaangaliana kwa muda kisha Victoria akakohoa kidogo ili kusafisha sauti yake. “Winnie, huyu dada anaitwa Tunu, ameelekezwa hapa na kaka’ako, anataka kuongea na wewe,” Victoria alisema na kuinuka, akamshika mkono Pendo.

“Sasa, da’ Tunu, ngoja tuwaache wenyewe muongee kwa uhuru zaidi,” Victoria alisema huku akianza kuondoka.

“Haina shida, dada. Tukimalizana nitakwambia,” Tunu alisema huku akijiweka sawa pale kwenye sofa. Kikatokea kitambo kifupi cha ukimya, kila mmoja alionekana kutafakari. Winifrida alikuwa anamwangalia Tunu kwa jicho la kuibia, uso wake ulionesha wasiwasi fulani.

“Winnie, kwanza nikupe pole kwa yote yaliyotokea jana usiku... Najua hivi sasa unapitia mengi tu na huoni mtu wa kumweleza. Labda si kosa lako. Na sijui ni kwa nini umeshindwa kumweleza hata kaka’ako, au unaogopa?” Tunu alimuuliza Winifrida huku akiwa ameyatuliza macho yake kwenye uso wake.

Winifrida hakujibu, alibaki kimya akiangalia viganja vyake alivyoviweka juu ya mapaja yake. Tunu aliiona hali ya Winifrida kwa jinsi alivyokuwa na hofu, akatabasamu na kutafuta namna ya kuyaelekeza mazungumzo.

“Niko hapa mimi na wewe, wawili tu...” Tunu alisema na kusita, akashusha pumzi za ndani kwa ndani huku akionekana kama aliyekuwa akitafakari nini cha kusema. “Labda nikutoe wasiwasi, mimi nafanya kazi usalama wa taifa na chochote utakachoniambia, kama hupendi kaka’ako ajue kitabaki kuwa siri kati yetu. Nikutoe hofu kuwa wote waliofanya tukio hilo la kinyama watapatikana tu kama utakuwa muwazi...” Tunu alinyamaza kidogo ili maneno yale yamwingie Winifrida.

“Kwa sasa polisi wapo kazini wanawatafuta, mimi pia nimejitolea kusaidia ili kuhakikisha wote wanakamatwa... labda tu nikudokeze kuwa wapo watu ninaowahisi kufanya tukio hilo na ninazo picha zao, kwa hiyo huna sababu ya kunificha chochote unachokijua.” Tunu aliweka kituo, akaminya midomo yake yenye maki na kuficha vishimo vidogo vijitokeze kwenye mashavu yake.

“Sijui umenielewa?” Tunu alimuuliza Winifrida huku akimwangalia kwa makini.

“Nimekuelewa, dada,” Winifrida alisema, akavuta pumzi ndefu na kuzishusha taratibu huku akifanya kifua chake kipande na kushuka. Matiti yake madogo yaliyochongoka yalimiliki vyema eneo la kifua.

Tunu alitoa simu yake ya mkononi, ilikuwa simu nzuri na mpya kabisa aina ya iPhone 11 Pro Max, akaanza kupekuapekua kwenye ile simu kisha akamwonesha Winifrida picha ya Spoiler. “Ulimwona mtu mwenye sura kama hii?” alimuuliza huku akimtazama katika hali ya kumkagua.

Inaendelea

CC the_legend Norshad bobefu zoefu Pablo PAKAYA Ibney blackstarline Bryece Tater Bigjahman moneytalk marybaby nipo2 ram kisukari Smart911 Madame S carbamazepine Astelia culture gal Prisoner of hope Mine eyes kuku mweus Thad hearly Shunie Tumosa Mine eyes Kudo swahiba92 ludist Toyota escudo Clkey macson3 boga la kiangazi LEGE Smart911 Richard irakunda skfull popie Krizy Beat hearly nipo2 MWINDAJI HARAMU kakhulu Katavi Norami mbududa iron2012 popie Bughy Harry Mlenge Kacheda mjasiliamali Laki Si Pesa cocochanel kinusikwetu big jambo mludego Shupavu Kacheda mjasiliamali Mweweso Songa Heri esiankiki mnadhimu mkuu wa jf red apple the-sniper MR KUO dan oseko Jackal

NB: Litro 👩
woyoooooo bshop kashusha mzigo huku kujen msomeee wapendwa 😁 😁 💃💃💃
 
Taxi - (114)

Winifrida aliiangalia ile picha kwa makini, akaonekana kutafakari kwa sekunde chache kisha akatingisha kichwa chake kushoto na kulia taratibu akionekana kutokuwa na uhakika. Tunu akashusha pumzi na kupekua tena, akapata picha ya Uledi na kumwonesha Winifrida.

Winifrida aliitazama ile picha na kuonekana kukumbuka jambo fulani, akakunja uso wake huku akishindwa kuficha hofu aliyokuwa nao. Tunu aliiona hali ya Winifrida kwa jinsi alivyoingiwa na hofu, akatabasamu na kutafuta picha nyingine. Ilikuwa ni picha ya Dulla Mcomoro, akamwonesha tena Winifrida.

Winifrida aliitazama ile picha mara moja tu na kuonesha mshituko mkubwa huku akionekana kuumia sana moyoni. Machozi yalianza kumlenga lenga machoni kwa namna alivyoumia. Tunu alimsogelea, akamkumbatia katika hali ya kumfariji huku akimpigapiga mgongoni.

* * * * *

Ndani ya ofisi za Mr. Oduya zilizo kwenye ghorofa ya sita ya jengo la ghorofa kumi na mbili katika barabara ya Bagamoyo, jijini Dar es Salaam, Mr. Oduya alikuwa amesimama karibu ya dirisha akiangalia nje. Macho yake yaliangalia barabarani kulikokuwa kunapita magari. Kisha yakahama na kuangalia chini ya lile jengo la ofisi zake kwenye viunga vya maegesho ya magari, kulikuwa na machache yaliyoegeshwa katika sehemu hiyo.

Kwa dakika kadhaa Mr. Oduya alitulia pale dirishani akitazama barabara ya Bagamoyo kana kwamba alikuwa anaiona kwa mara ya kwanza katika maisha yake. Aliendelea kutazama eneo lile kwa makini na asijue alikuwa akiangalia nini. Uso wake haukuweza kuficha hali ya wasiwasi aliyokuwa nayo moyoni kwa wakati huo.

Macho yake yalikuwa mekundu na uso wake ulikuwa umesawajika mno akionekana kuwa hoi na mchovu, ni kama vile mtu ambaye hakuwa amepata usingizi kwa juma zima.

Alichukua pakti ya sigara aina ya Parliament toka katika mfuko wa koti lake na kutoa sigara mbili, moja akaipachika kwenye pembe ya mdomo wake na kuchukua kiberiti cha gesi, akaiwasha ile sigara na kuvuta mkupuo mmoja mkubwa wa pafu la moshi kisha akatoa moshi mwingi nje kupitia mdomo na tundu za pua. Muda wote alionekana kutatizwa sana na jambo.

Ndani ya ile ofisi walikuwa wawili tu, yeye na Mr. Mafuru aliyekuwa ameketi kwa utulivu kwenye kiti kimojawapo ya viti vilivyopo mle ndani. Muda wote Mr. Mafuru alikuwa akimtazama Mr. Oduya kwa wasiwasi. Uso wake pia ulikuwa umesawajika mno na moyo wake haukuwa kwenye mapigo ya kawaida.

Baada ya kupiga mikupuo mitatu mikubwa na kisha kuutoa moshi wa sigara, Mr. Oduya aligeuza shingo yake kumtazama Mr. Mafuru. Wakaangaliana kwa kitambo kirefu pasipo kusema chochote, kila mmoja aliendelea kuwa kimya. Mr. Oduya alikohoa kidogo kusafisha koo lake.

“Mafuru, usimchukulie kirahisi kabisa Madame Norah, muone hivyo hivyo tu, ni mtu wa hatari sana pale unapogusa maslahi yake au mtu anayemhusu...” Mr. Mafuru alisema kisha akavuta tena pafu kubwa la moshi wa sigara na kuutoa ule moshi taratibu huku akiutazama kwa makini.

“Hapaswi kabisa, kwa namna yoyote ile, kufahamu kuwa ni watu wetu ndio waliofanya kitendo hicho kwa mwanawe, na endapo akifahamu basi tutakuwa tumeharibu kila kitu,” Mr. Oduya alisema na kuanza kupiga hatua taratibu kurudi kwenye kiti chake.

“Na vipi kuhusu Tunu, is there any information about her?” Mr. Mafuru aliuliza baada ya kutafakari kidogo kisha akashusha pumzi ndefu.

“Huyo ndiyo hapaswi kabisa kuwa hai. Ni bora hata Madame Norah ambaye unaweza kumweleza akakuelewa kuliko Tunu,” Mr. Oduya alisema na kuketi kwenye kiti chake kikubwa cha magurudumu yanayokiwezesha kutembea, kisha akapiga mkupuo mwingine mkubwa wa moshi wa sigara na kukiminya kipande cha sigara ndani ya kisahani kidogo cha kuwekea majivu.

“Mwenyewe unakumbuka kuwa Tunu alikuwa mtu wetu, anayajua mengi n ahata tulipomshtukia tukajaribu kumtia mikononi mwetu mara tatu lakini mara zote ameweza kutoweka. Tukishindwa kumpata safari hii itakuwa ngumu sana kumpata tena… na kama tukifanikiwa kutakuwa na gharama yake! Tena gharama kubwa sana!” Mr. Oduya alisema na kuwasha ile sigara nyingine, akaendelea kuvuta taratibu.

“Lakini naamini safari hii hana ujanja ni heri kama angeendelea kujificha, maana kazi haitakuwa ngumu sana kama ilivyokuwa hapo mwanzoni,” Mr. Mafuru alijaribu kumtoa hofu Mr. Oduya.

Mr. Oduya alitingisha kichwa chake taratibu na kucheka, “Mafuru, you are serious at all, sijui kama unajua unachoongea. Kutakuwa na gharama, tena kubwa sana kumtia Tunu mkononi!”

Mr. Mafuru alitaka kusema lakini Mr. Oduya akamtatisha. “Muda mfupi tu uliopita Silas na Job walikuwa wanamfuatilia, tena kwa tahadhari kubwa bila yeye kujua lakini unajua kilichotokea?” Mr. Oduya alimuuliza Mafuru kisha akajijibu mwenye. “Kawapiga chenga ya akili na mwili wasijue alikoelekea. Na taarifa nilizozipata alitua Dar es Salaam jana asubuhi, anaonekana anazo taarifa nyeti kutuhusu ambazo zinaweza kutuharibia kila kitu,” Mr. Oduya alisema kwa wasiwasi.

“Nadhani sasa unaweza kuelewa nini naongelea,” Mr. Oduya alimwambia Mafuru kisha akavuta pumzi ndefu na kuzishusha taratibu huku akiegemeza mkono mmoja kwenye kiti na kuvuta sigara yake kwa pupa kama hana akili nzuri.

“Sasa tunafanyeje, boss, ili tuwe salama? Ina maana hauna mpango kabisa?” Mr. Mafuru aliuliza huku hofu ikijionesha waziwazi usoni kwake.

Inaendelea...

NB: Litro 👩
 
Taxi - (114)

Winifrida aliiangalia ile picha kwa makini, akaonekana kutafakari kwa sekunde chache kisha akatingisha kichwa chake kushoto na kulia taratibu akionekana kutokuwa na uhakika. Tunu akashusha pumzi na kupekua tena, akapata picha ya Uledi na kumwonesha Winifrida.

Winifrida aliitazama ile picha na kuonekana kukumbuka jambo fulani, akakunja uso wake huku akishindwa kuficha hofu aliyokuwa nao. Tunu aliiona hali ya Winifrida kwa jinsi alivyoingiwa na hofu, akatabasamu na kutafuta picha nyingine. Ilikuwa ni picha ya Dulla Mcomoro, akamwonesha tena Winifrida.

Winifrida aliitazama ile picha mara moja tu na kuonesha mshituko mkubwa huku akionekana kuumia sana moyoni. Machozi yalianza kumlenga lenga machoni kwa namna alivyoumia. Tunu alimsogelea, akamkumbatia katika hali ya kumfariji huku akimpigapiga mgongoni.

* * * * *

Ndani ya ofisi za Mr. Oduya zilizo kwenye ghorofa ya sita ya jengo la ghorofa kumi na mbili katika barabara ya Bagamoyo, jijini Dar es Salaam, Mr. Oduya alikuwa amesimama karibu ya dirisha akiangalia nje. Macho yake yaliangalia barabarani kulikokuwa kunapita magari. Kisha yakahama na kuangalia chini ya lile jengo la ofisi zake kwenye viunga vya maegesho ya magari, kulikuwa na machache yaliyoegeshwa katika sehemu hiyo.

Kwa dakika kadhaa Mr. Oduya alitulia pale dirishani akitazama barabara ya Bagamoyo kana kwamba alikuwa anaiona kwa mara ya kwanza katika maisha yake. Aliendelea kutazama eneo lile kwa makini na asijue alikuwa akiangalia nini. Uso wake haukuweza kuficha hali ya wasiwasi aliyokuwa nayo moyoni kwa wakati huo.

Macho yake yalikuwa mekundu na uso wake ulikuwa umesawajika mno akionekana kuwa hoi na mchovu, ni kama vile mtu ambaye hakuwa amepata usingizi kwa juma zima.

Alichukua pakti ya sigara aina ya Parliament toka katika mfuko wa koti lake na kutoa sigara mbili, moja akaipachika kwenye pembe ya mdomo wake na kuchukua kiberiti cha gesi, akaiwasha ile sigara na kuvuta mkupuo mmoja mkubwa wa pafu la moshi kisha akatoa moshi mwingi nje kupitia mdomo na tundu za pua. Muda wote alionekana kutatizwa sana na jambo.

Ndani ya ile ofisi walikuwa wawili tu, yeye na Mr. Mafuru aliyekuwa ameketi kwa utulivu kwenye kiti kimojawapo ya viti vilivyopo mle ndani. Muda wote Mr. Mafuru alikuwa akimtazama Mr. Oduya kwa wasiwasi. Uso wake pia ulikuwa umesawajika mno na moyo wake haukuwa kwenye mapigo ya kawaida.

Baada ya kupiga mikupuo mitatu mikubwa na kisha kuutoa moshi wa sigara, Mr. Oduya aligeuza shingo yake kumtazama Mr. Mafuru. Wakaangaliana kwa kitambo kirefu pasipo kusema chochote, kila mmoja aliendelea kuwa kimya. Mr. Oduya alikohoa kidogo kusafisha koo lake.

“Mafuru, usimchukulie kirahisi kabisa Madame Norah, muone hivyo hivyo tu, ni mtu wa hatari sana pale unapogusa maslahi yake au mtu anayemhusu...” Mr. Mafuru alisema kisha akavuta tena pafu kubwa la moshi wa sigara na kuutoa ule moshi taratibu huku akiutazama kwa makini.

“Hapaswi kabisa, kwa namna yoyote ile, kufahamu kuwa ni watu wetu ndio waliofanya kitendo hicho kwa mwanawe, na endapo akifahamu basi tutakuwa tumeharibu kila kitu,” Mr. Oduya alisema na kuanza kupiga hatua taratibu kurudi kwenye kiti chake.

“Na vipi kuhusu Tunu, is there any information about her?” Mr. Mafuru aliuliza baada ya kutafakari kidogo kisha akashusha pumzi ndefu.

“Huyo ndiyo hapaswi kabisa kuwa hai. Ni bora hata Madame Norah ambaye unaweza kumweleza akakuelewa kuliko Tunu,” Mr. Oduya alisema na kuketi kwenye kiti chake kikubwa cha magurudumu yanayokiwezesha kutembea, kisha akapiga mkupuo mwingine mkubwa wa moshi wa sigara na kukiminya kipande cha sigara ndani ya kisahani kidogo cha kuwekea majivu.

“Mwenyewe unakumbuka kuwa Tunu alikuwa mtu wetu, anayajua mengi n ahata tulipomshtukia tukajaribu kumtia mikononi mwetu mara tatu lakini mara zote ameweza kutoweka. Tukishindwa kumpata safari hii itakuwa ngumu sana kumpata tena… na kama tukifanikiwa kutakuwa na gharama yake! Tena gharama kubwa sana!” Mr. Oduya alisema na kuwasha ile sigara nyingine, akaendelea kuvuta taratibu.

“Lakini naamini safari hii hana ujanja ni heri kama angeendelea kujificha, maana kazi haitakuwa ngumu sana kama ilivyokuwa hapo mwanzoni,” Mr. Mafuru alijaribu kumtoa hofu Mr. Oduya.

Mr. Oduya alitingisha kichwa chake taratibu na kucheka, “Mafuru, you are serious at all, sijui kama unajua unachoongea. Kutakuwa na gharama, tena kubwa sana kumtia Tunu mkononi!”

Mr. Mafuru alitaka kusema lakini Mr. Oduya akamtatisha. “Muda mfupi tu uliopita Silas na Job walikuwa wanamfuatilia, tena kwa tahadhari kubwa bila yeye kujua lakini unajua kilichotokea?” Mr. Oduya alimuuliza Mafuru kisha akajijibu mwenye. “Kawapiga chenga ya akili na mwili wasijue alikoelekea. Na taarifa nilizozipata alitua Dar es Salaam jana asubuhi, anaonekana anazo taarifa nyeti kutuhusu ambazo zinaweza kutuharibia kila kitu,” Mr. Oduya alisema kwa wasiwasi.

“Nadhani sasa unaweza kuelewa nini naongelea,” Mr. Oduya alimwambia Mafuru kisha akavuta pumzi ndefu na kuzishusha taratibu huku akiegemeza mkono mmoja kwenye kiti na kuvuta sigara yake kwa pupa kama hana akili nzuri.

“Sasa tunafanyeje, boss, ili tuwe salama? Ina maana hauna mpango kabisa?” Mr. Mafuru aliuliza huku hofu ikijionesha waziwazi usoni kwake.

Inaendelea...

NB: Litro 👩
 
Taxi - (115)

“Siwezi kukosa mpango... ninao watu wengi kwenye vyombo vya dola wenye kila aina ya mbinu walio kwenye payroll yangu,” Mr. Oduya alisema huku akiutazama kwa makini ule moshi wa sigara wakati akiutoa. “Nimeshampa kazi Victor, yule shushushu wa Ofisi ya Waziri Mkuu, anamfahamu vyema Tunu kwa kuwa ni rafiki’ake mkubwa, yeye ndiye aliyempokea jana wakati anatua kiwanja cha ndege. Kwa kumtumia yeye itakuwa ni kete yetu muhimu ya kumpata. Tukishindwa kuitumia nafasi hii then we are fucked up!”

* * * * *

Baada ya maongezi yake kwenye simu na Mr. Mafuru, Madame Norah aliwageukia watu wengine na kuwatazama kwa muda kama aliyekuwa anatafuta namna ya kuanza kujieleza. Aliwatazama kwa zamu akianza na Sammy, kisha akamtazama Jengo na baadaye macho yake yakaishia kwa Bi. Pamela.

Wakati akiwatazama kwa zamu Madame Norah alikuwa ameuona mshangao kwenye macho ya Sammy, hali ya kusawajika kwenye macho ya Jengo na chuki ya waziwazi kwenye macho ya Bi. Pamela. Alidhani kuwa pengine Bi. Pamela hakuwa amefurahishwa kabisa na ujio wake katika maisha yao.

Ni kweli. Bi. Pamela alihisi donge la wivu likimkaba kooni, ulikuwa ni wivu wa hofu ya kunyang’anywa vyote; mumewe Jengo na Joyce aliyekuwa amuaminisha kuwa yeye ndiye mama yake.

Hata hivyo, Madame Norah alikuwa na ya kwake moyoni, yeye hakumfikiria kabisa Jengo bali mwanawe Joyce. Hadi muda ule hakuyaamini macho yake wala masikio yake. Alijitahidi kuishirikisha akili yake kikamilifu katika kumletea taarifa za kuaminika. Ni kweli alikuwa amempata mwanawe aliyempoteza miaka therathini na mbili iliyopita!

Mwanawe alikuwa hai ingawa muda huo alikuwa akiyapigania maisha yake kitandani, jambo hilo lilimhuzunisha sana Madame Norah, lakini ingalau alijua kuwa Joyce ndiye mwanawe! Kuna muda alihisi labda yupo ndotoni. Hata hivyo, hakutaka kabisa ile iwe ndoto. Kila alipomtazama Jengo na mkewe aliwaona wakiyaepuka macho yake. Ni Sammy peke yake ambaye, mbali na kuwa na majonzi, alikuwa katika hali ya kawaida japo mshangao ulikuwa haujamtoka.

Eneo lile lilianza kutawaliwa na hali ya ukimya ulioanza kumtisha kila mtu. Madame Norah hakuwa ametegemea kama ingemtokea katika Maisha yake, siku kama hiyo, siku ambayo ilimtaka kusimama kidete ili kuhakikisha anairudisha tena furaha iliyomponyoka kwa miaka zaidi ya therathini. Kuna wakati alitamani mambo hayo yaoze na kuteketea kabisa katika roho yake, bahati mbaya hakuwa na namna ya kuyasahau.

“Yaelekea leo ni siku ya ajabu,” Madame Norah aliwaza. “Hakika leo Mungu kaamua kutenda jambo,” alijikuta akisema kwa sauti na kuwafanya watu wote wamtazame kwa mshangao.

Alipogundua kuwa watu wote walikuwa wanamtazama kwa mshangao, Madame Norah alishauri jambo, “Nadhani ninyi wanaume mnaweza kwenda kupumzika mkatuachia kazi hii sisi wanawake, mimi na bibie,” Madame Norah alisema huku akimwangalia Bi. Pamela. “Mwanamke mwenzangu, naomba tuwe na mazungumzo kidogo, kama wanawake.”

Jengo alimtazama Madame Norah kwa mshangao, alionesha kusita sana. Hata Bi. Pamela pia alionesha kusita. Alijiuliza mwanamke yule alitaka kuzungumza naye kuhusu nini lakini hakuweza kubaini. Iliwachukua takriban dakika kumi na tano kufikia mwafaka wa kuzika tofauti zao ili kuangalia namna ya kumsaidia Joyce aweze kupona na kurudi katika Maisha yake ya kawaida.

Kisha Sammy na Jengo wakaondoka wakiwaacha wanawake wawili ambao waliamua kwenda kuketi katika mgahawa uliomo ndani ya Hospitali ya Rufaa ya Amana kwa maongezi kama wazazi wa Joyce, mmoja akiwa mama mzazi na mwingine mama mlezi.

* * * * *

Saa saba kasorobo mchana ilimkuta Tunu akiwa katika eneo la Magomeni Mikumi, alikuwa ametulia ndani ya gari aina ya Toyota Prado alilolichukua kutoka kwa Victor, alikuwa akimsubiri Victor waliyekubaliana kukutana hapo.

Kwa kiasi fulani alikuwa amefarijika moyoni mwake baada ya kuanza kupata mwanga wa kile kilichomsumbua kushindwa kukikamilisha kwa miaka mitatu. Katika mazungumzo yake na Winifrida aliweza kupata picha kamili ya nani waliomshambulia Joyce. Jambo lililomtatiza kwa nini walikuwa wanatumia nguvu kubwa kupambana na Sammy?

Jambo moja alilolijua ni kwamba gari la Sammy aina ya Cadillac DeVille lilikuwa likimilikiwa na Omari Oduya, mtoto wa kwanza wa Mr. Oduya ambaye alikimbilia nchini Marekani baada ya kufanya mauaji akimuua aliyekuwa mpenzi wake, Layla Adil.

Wakati huo Tunu alikuwa amerudi toka Israel na alipopata taarifa za mauaji ya Layla, aliumia sana kwa kuwa alimfahamu vyema Layla kwani walisoma darasa moja katika Shule ya Jangwani. Layla alikuwa chotara wa Kiarabu na mwonekano wake mzuri uliwafanya watu wengi kudhani alikusudiwa kuumbwa malaika badala ya binadamu!

Tunu aliamua kufuatilia sakata hilo ili haki itendeke baada ya kuhisi polisi hawakujishughulisha na kesi hiyo kwa kuwa aliyefanya hivyo alikuwa mtoto wa mtu mzito. Kwa kuwa alikuwa na taaluma iliyohitajika sana ya Computer System Analysis alifanikiwa kujipenyeza na kupata kazi kwenye kampuni ya Mr. Oduya ya The Splendid Ltd.

Alipofuatilia aligundua kuwa mapenzi kati ya Omari na Layla yalijaa ukatili na unyanyasaji ambao Layla alishindwa kuvumilia na kuamua kuachana na Omari. Chanzo cha haya yote ni Omari kutokukubali kuachwa.

Omari alikuwa akimnyanyasa sana Layla kingono n ahata kwa vipigo na vitisho vya bastola kuwa angemuua. Miezi miwili kabla ya kifo chake Omari alimchukua kinguvu Layla na kumfungia ndani ya nyumba akimpa vipigo na akiwa hawezi kutoka nje. Tukio hilo liliwafanya ndugu wa Layla kuomba msaada kwa jeshi la polisi ili kumtoa ndugu yao ndani ya nyumba hiyo.

Baada ya kufanikiwa kumtoa walipanga kumwondoa nchini na kumpeleka Kenya ili kusitisha uhusiano huo. Ni katika kipindi hicho Omari alimbembeleza sana Layla amrudie lakini Layla alimshauri atafute kwanza msaada wa kisaikolojia kama alitaka warudiane, kwa kuwa alimwona ni mtu wa hasira kila wakati, vipigo visivyoisha na mbaya zaidi akimtishia kumuua mara kwa mara, kitu ambacho siyo cha kawaida.

Aliendelea kumtaka kuwa akishapata msaada wa kisaikolojia ndiyo angekuwa tayari kuwa naye tena ila kwa muda huo alitaka aachwe kwanza. Omari hakukubali, aliamua kuwatumia watu wa baba’ake; Dulla na Uledi kumteka Layla na hatimaye akatekeleza mauaji hayo. Kisha kwa msaada wa baba yake alitorokea nje ya nchi bila kutiwa nguvuni...

Je, nini kitaendelea katika sakata hili lililoibuliwa na Taxi 🚖? Endelea kuwemo kwani safari bado inaendelea 🚴‍♀️ 🚴‍♂️ 🚴‍♂️ hadi kieleweke 🔚...

NB: Litro 👩
 
Taxi - (115)

“Siwezi kukosa mpango... ninao watu wengi kwenye vyombo vya dola wenye kila aina ya mbinu walio kwenye payroll yangu,” Mr. Oduya alisema huku akiutazama kwa makini ule moshi wa sigara wakati akiutoa. “Nimeshampa kazi Victor, yule shushushu wa Ofisi ya Waziri Mkuu, anamfahamu vyema Tunu kwa kuwa ni rafiki’ake mkubwa, yeye ndiye aliyempokea jana wakati anatua kiwanja cha ndege. Kwa kumtumia yeye itakuwa ni kete yetu muhimu ya kumpata. Tukishindwa kuitumia nafasi hii then we are fucked up!”

* * * * *

Baada ya maongezi yake kwenye simu na Mr. Mafuru, Madame Norah aliwageukia watu wengine na kuwatazama kwa muda kama aliyekuwa anatafuta namna ya kuanza kujieleza. Aliwatazama kwa zamu akianza na Sammy, kisha akamtazama Jengo na baadaye macho yake yakaishia kwa Bi. Pamela.

Wakati akiwatazama kwa zamu Madame Norah alikuwa ameuona mshangao kwenye macho ya Sammy, hali ya kusawajika kwenye macho ya Jengo na chuki ya waziwazi kwenye macho ya Bi. Pamela. Alidhani kuwa pengine Bi. Pamela hakuwa amefurahishwa kabisa na ujio wake katika maisha yao.

Ni kweli. Bi. Pamela alihisi donge la wivu likimkaba kooni, ulikuwa ni wivu wa hofu ya kunyang’anywa vyote; mumewe Jengo na Joyce aliyekuwa amuaminisha kuwa yeye ndiye mama yake.

Hata hivyo, Madame Norah alikuwa na ya kwake moyoni, yeye hakumfikiria kabisa Jengo bali mwanawe Joyce. Hadi muda ule hakuyaamini macho yake wala masikio yake. Alijitahidi kuishirikisha akili yake kikamilifu katika kumletea taarifa za kuaminika. Ni kweli alikuwa amempata mwanawe aliyempoteza miaka therathini na mbili iliyopita!

Mwanawe alikuwa hai ingawa muda huo alikuwa akiyapigania maisha yake kitandani, jambo hilo lilimhuzunisha sana Madame Norah, lakini ingalau alijua kuwa Joyce ndiye mwanawe! Kuna muda alihisi labda yupo ndotoni. Hata hivyo, hakutaka kabisa ile iwe ndoto. Kila alipomtazama Jengo na mkewe aliwaona wakiyaepuka macho yake. Ni Sammy peke yake ambaye, mbali na kuwa na majonzi, alikuwa katika hali ya kawaida japo mshangao ulikuwa haujamtoka.

Eneo lile lilianza kutawaliwa na hali ya ukimya ulioanza kumtisha kila mtu. Madame Norah hakuwa ametegemea kama ingemtokea katika Maisha yake, siku kama hiyo, siku ambayo ilimtaka kusimama kidete ili kuhakikisha anairudisha tena furaha iliyomponyoka kwa miaka zaidi ya therathini. Kuna wakati alitamani mambo hayo yaoze na kuteketea kabisa katika roho yake, bahati mbaya hakuwa na namna ya kuyasahau.

“Yaelekea leo ni siku ya ajabu,” Madame Norah aliwaza. “Hakika leo Mungu kaamua kutenda jambo,” alijikuta akisema kwa sauti na kuwafanya watu wote wamtazame kwa mshangao.

Alipogundua kuwa watu wote walikuwa wanamtazama kwa mshangao, Madame Norah alishauri jambo, “Nadhani ninyi wanaume mnaweza kwenda kupumzika mkatuachia kazi hii sisi wanawake, mimi na bibie,” Madame Norah alisema huku akimwangalia Bi. Pamela. “Mwanamke mwenzangu, naomba tuwe na mazungumzo kidogo, kama wanawake.”

Jengo alimtazama Madame Norah kwa mshangao, alionesha kusita sana. Hata Bi. Pamela pia alionesha kusita. Alijiuliza mwanamke yule alitaka kuzungumza naye kuhusu nini lakini hakuweza kubaini. Iliwachukua takriban dakika kumi na tano kufikia mwafaka wa kuzika tofauti zao ili kuangalia namna ya kumsaidia Joyce aweze kupona na kurudi katika Maisha yake ya kawaida.

Kisha Sammy na Jengo wakaondoka wakiwaacha wanawake wawili ambao waliamua kwenda kuketi katika mgahawa uliomo ndani ya Hospitali ya Rufaa ya Amana kwa maongezi kama wazazi wa Joyce, mmoja akiwa mama mzazi na mwingine mama mlezi.

* * * * *

Saa saba kasorobo mchana ilimkuta Tunu akiwa katika eneo la Magomeni Mikumi, alikuwa ametulia ndani ya gari aina ya Toyota Prado alilolichukua kutoka kwa Victor, alikuwa akimsubiri Victor waliyekubaliana kukutana hapo.

Kwa kiasi fulani alikuwa amefarijika moyoni mwake baada ya kuanza kupata mwanga wa kile kilichomsumbua kushindwa kukikamilisha kwa miaka mitatu. Katika mazungumzo yake na Winifrida aliweza kupata picha kamili ya nani waliomshambulia Joyce. Jambo lililomtatiza kwa nini walikuwa wanatumia nguvu kubwa kupambana na Sammy?

Jambo moja alilolijua ni kwamba gari la Sammy aina ya Cadillac DeVille lilikuwa likimilikiwa na Omari Oduya, mtoto wa kwanza wa Mr. Oduya ambaye alikimbilia nchini Marekani baada ya kufanya mauaji akimuua aliyekuwa mpenzi wake, Layla Adil.

Wakati huo Tunu alikuwa amerudi toka Israel na alipopata taarifa za mauaji ya Layla, aliumia sana kwa kuwa alimfahamu vyema Layla kwani walisoma darasa moja katika Shule ya Jangwani. Layla alikuwa chotara wa Kiarabu na mwonekano wake mzuri uliwafanya watu wengi kudhani alikusudiwa kuumbwa malaika badala ya binadamu!

Tunu aliamua kufuatilia sakata hilo ili haki itendeke baada ya kuhisi polisi hawakujishughulisha na kesi hiyo kwa kuwa aliyefanya hivyo alikuwa mtoto wa mtu mzito. Kwa kuwa alikuwa na taaluma iliyohitajika sana ya Computer System Analysis alifanikiwa kujipenyeza na kupata kazi kwenye kampuni ya Mr. Oduya ya The Splendid Ltd.

Alipofuatilia aligundua kuwa mapenzi kati ya Omari na Layla yalijaa ukatili na unyanyasaji ambao Layla alishindwa kuvumilia na kuamua kuachana na Omari. Chanzo cha haya yote ni Omari kutokukubali kuachwa.

Omari alikuwa akimnyanyasa sana Layla kingono n ahata kwa vipigo na vitisho vya bastola kuwa angemuua. Miezi miwili kabla ya kifo chake Omari alimchukua kinguvu Layla na kumfungia ndani ya nyumba akimpa vipigo na akiwa hawezi kutoka nje. Tukio hilo liliwafanya ndugu wa Layla kuomba msaada kwa jeshi la polisi ili kumtoa ndugu yao ndani ya nyumba hiyo.

Baada ya kufanikiwa kumtoa walipanga kumwondoa nchini na kumpeleka Kenya ili kusitisha uhusiano huo. Ni katika kipindi hicho Omari alimbembeleza sana Layla amrudie lakini Layla alimshauri atafute kwanza msaada wa kisaikolojia kama alitaka warudiane, kwa kuwa alimwona ni mtu wa hasira kila wakati, vipigo visivyoisha na mbaya zaidi akimtishia kumuua mara kwa mara, kitu ambacho siyo cha kawaida.

Aliendelea kumtaka kuwa akishapata msaada wa kisaikolojia ndiyo angekuwa tayari kuwa naye tena ila kwa muda huo alitaka aachwe kwanza. Omari hakukubali, aliamua kuwatumia watu wa baba’ake; Dulla na Uledi kumteka Layla na hatimaye akatekeleza mauaji hayo. Kisha kwa msaada wa baba yake alitorokea nje ya nchi bila kutiwa nguvuni...

Je, nini kitaendelea katika sakata hili lililoibuliwa na Taxi 🚖? Endelea kuwemo kwani safari bado inaendelea 🚴‍♀️ 🚴‍♂️ 🚴‍♂️ hadi kieleweke 🔚...

NB: Litro 👩
yaaan mim leo npo sambamba na wewe sitaki kabsa kupitwa na huu uhondooooo🤤🤤🤤
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom