moneytalk
JF-Expert Member
- Jan 23, 2017
- 8,040
- 16,870
mahaba mahabaniMambo unayoyapenda hayo
mahaba mahabaniMambo unayoyapenda hayo
Hahh mzoee tu dear huyo kivurugeAcha tu mdogo wangu
Mmh!😵😵😵 Huyu Shunie huyu si wa mchezo!🙂🙂🙂 kamfanya nini askofu hadi kasalimu amri hivihivi! Ama kweli kila mbabe ana mbabe wake!Taxi (100)
Tunu aliviringika na kutambaa kama nyoka akihama kutoka sofa lile dogo na kwenda kwenye sofa kubwa. Akajilaza kimya akijaribu kusikilizia lakini akahisi chuma kikielekezwa kichwani kwake, moja kwa moja akatambua kuwa ulikuwa ni mtutu wa bastola na aliyeshika bastola hiyo alikuwa hatua moja tu toka alipolala. Mwili wake ukaingiwa na baridi.
Tunu hakutikisika wala kuinua mikono yake iliyoshika bastola. Alijua wazi kuwa alikuwa amepatikana. Hakuwa na ujanja na wala hakutakiwa kufanya lolote lile kwa pupa isipokuwa kuutii kila atakachoambiwa na mtu yule.
“Weka bastola zako chini na uinuke taratibu,” sauti ya ukakamavu ya yule mtu ilimwamrisha Tunu. Taratibu akaziweka chini bastola na kusimama akiwa amenyoosha mikono yake juu.
Alihisi kama ameona mzimu, alijikuta akitazamana na mtutu wa bastola aina ya FNX 45 Tactical yenye kiwambo cha kuzuia sauti. Bastola ile ilikuwa imeshikwa na mwanamume mfupi mwenye umbo lililojengeka kwa misuli kutokana na ratiba nzuri ya mazoezi. Mwanamume yule alikuwa amevaa fulana nyekundu iliyombana na kulionesha vyema umbo lake lililojengeka kwa misuli, suruali ya bluu ya jeans na miguuni alivaa raba nyeusi.
Tunu alimtazama kwa wasiwasi. Macho ya yule mwanamume yalikuwa na dalili zote za ukatili, uwendawazimu na unyama uliokubuhu.
“Uledi!” Tunu alimaka kwa mshangao. Alikuwa akimfahamu vyema Uledi Mkama tangu alipokutana naye katika ofisi ya Mr. Oduya wakati huo yeye Tunu akifanya kazi hapo. Alifahamu kuwa Uledi alikuwa mmoja wa vijana wawili waliokuwa wakitumwa kufanya kazi maalumu na za siri za Mr. Oduya, yeye na Dulla Mcomoro. Alikumbuka kuwa ni hawa wawili wakishirikiana na Spoiler waliohusika kwenye mauaji ya Jaji Lutego.
“Uledi!” Tunu aliita katika namna ya kutaka kumzubaisha lakini Uledi hakutaka maongezi yoyote na Tunu, yeye alidhamiria kuua na kupeleka kichwa kama alivyoagizwa na Mr. Oduya.
Alianza kuvuta ndimi ya bastola, Tunu akafumba macho kwani alijua kile ambacho kingetokea na hakutaka kuona. Mara ukasikika mlio mkubwa wa risasi kutoka kwenye bastola isiyo na kiwambo cha kuzuia sauti, damu zikamrukia Tunu ambaye alianguka sakafuni huku akihisi moyo wake ulikuwa umepoteza mapigo yake, kisha akatulia kama mfu akiwa hajui iwapo alikuwa amekufa au alikuwa ndotoni.
“Sister! Sister!” Tunu akasikia sauti ya mwanamume ambayo haikuwa ngeni masikioni mwake, alihisi kuitambua vyema. Akajiuliza ameisikia wapi?
“Sister... ni mimi dereva wako. Inuka tuondoke haraka kuna wenzao wataingia hapa dakika yoyote kuanzia sasa,” ile sauti ilisema tena kwa wasiwasi. Sasa aliikumba vyema. Ni kweli ilikuwa ni sauti ya yule dereva wa teksi aliyoikodi. Hata hivyo hakujitokeza kwa kuogopa kuwa huenda ulikuwa ni mtego.
Tunu aliinua uso wake kwa wasiwasi na kumwona yule dereva akiwa ameshika bastola akiangalia kule kwenye mlango mkubwa wa kuingilia sebuleni kwa wasiwasi na kuanza kutoka haraka. Tunu hakutaka kuwa mbishi, akainuka na kuokota haraka bastola yake na mkoba wake, akautupia jicho mwili wa Uledi na kuona jinsi kichwa chake kilivyokuwa kimefumuliwa kwa risasi, hakutaka kuzubaa akatoka kuanza kumfuata nyuma yule dereva.
Walielekea nyuma ya ile nyumba na wakati huo huo ukasikika muungurumo wa gari lililokuwa linaikaribia ile nyumba na kukomea mbele ya geti kubwa la nyumba ile. Hawakusubiri, wakarukia matawi ya mti yaliyokuwa yameinamia mle ndani na kupanda haraka kisha wakajirusha na kuangukia nje ya ukuta wa ile nyumba. Yule dereva akaanza kutimua mbio kuelekea bondeni. Tunu akamfuata. Baada ya mwendo mfupi wakaanza kuambaa na ule Mto Msimbazi kabla hawajaanza tena kupandisha kama wanarudi juu lakini wakiwa mbali na eneo la ile nyumba waliyotoka.
“Tunu, are you okay?” yule dereva alimuuliza Tunu wakati wakikimbia. Tunu akashtuka sana kusikia yule dereva akimwita kwa jina lake, muda huo walikuwa wanapita katika vichochoro vya nyumba za eneo lile.
“I’m okay!” Tunu akamjibu yule dereva kwa ufupi huku akiwa katika tahadhari kubwa. Bastola amezishika mkononi tayari kwa lolote.
“Endelea kunifuata, gari nilikwenda kulificha sehemu huko mbele ili wasinishtukie.” yule dereva alisema huku akiendelea kukimbia.
Pamoja na kuendelea kumfuata yule dereva lakini Tunu bado alikuwa katika mawazo kumuhusu yule dereva. Alikuwa anajiuliza yule nin nani hasa? Kwa nini amemwokoa toka kwa wale watu wakati inasemekana yeye pia ni mmoja wao? Je, katumwa na nani aje amwokoe? Au yeye pia ni undercover? Tunu alijiambia kuwa alikwisha hisi tangu mwanzo kuwa yule dereva hakuwa wa kawaida kama walivyo madereva wengine, alionekana mwelewa sana wa mambo na mwepesi wa kushika maelekezo.
Waliendelea kukimbia kwa kasi, yule dereva akiwa mbele na Tunu akiwa nyuma ingawa kwa upande fulani alianza kumwogopa sana. Jasho jingi lilikuwa linamtoka kwa kukimbia. Baada ya dakika kadhaa za kukimbia wakatokea kwenye kichochoro kimoja na kuikuta ile taxi ikiwa imeegeshwa hapo. Yule dereva akageuka kumtazama Tunu kwa macho makali.
“Pole sana, huo ndiyo uzalendo kwa nchi yako,” yule dereva alisema lakini Tunu hakumjibu. Alimtazama usoni kwa makini.
Mchezo unazidi kunoga, wamejitokeza wengi na sasa kuna huyu dereva wa taxi! Kuna nini ndani ya Taxi? Endelea kufuatilia hadi mwisho...
Thisi is for you Shunie
🤣🤣🤣Huachwi hadi utueleze umempa nini askofu!Niacheeee
Mfyuuu ukivuruge wangu ni niniHahh mzoee tu dear huyo kivuruge




ukielezwa aliyopewa utapasuka ngoma za masikio,ila jua huyo ni mama mchungaji
Huachwi hadi utueleze umempa nini askofu!
huyo kijana askari ni mnoko mnoko anaonekana...View attachment 1216986
Na Bishop Hiluka
(Mwandishi wa stori za kusisimua zilizowahi kuchapishwa hapa JF za Kizungumkuti!; Laiti Ningejua!; Hekaheka!; Hadi Lini! na nyinginezo)
0685 666964 au bjhiluka@yahoo.com
SAA 1:35 asubuhi, Samuel Kambona alishuka kutoka ndani ya gari aina ya Toyota Alphard la rangi ya bluu katika viunga vya maegesho ya magari vya majengo ya hoteli ya Udzungwa Beach Resort, iliyopo katika ufukwe wa Oystebay, jijini Dar es Salaam.
Gari lile lilikuwa na nembo ubavuni iliyokuwa na maandishi ya Udzungwa Beach Resort.
Samuel maarufu kama Sammy, alikuwa kijana mtanashati mwenye umri wa miaka 35 na msomi wa Shahada ya Umahili ya Biashara za Kimataifa na Lugha (M.A in International Business with Languages), aliyoipata kutoka Chuo Kikuu cha Warwick nchini Uingereza,
Alikuwa mrefu na mweupe mithili ya chotara wa kizungu, mwenye sura ya tabasamu muda wote. Urefu, mwili wake wa kimazoezi, utanashati na asili ya ngozi yake nyeupe ni vitu vilivyowavutia wasichana wengi aliokutana nao.
Ukiongezea na ndevu nyingi alizopenda kuzinyoa katika mtindo wa circle beard au kama wengi walivyozoea kuita “O”, vilimfanya azidi kuwa mvuto mkubwa kwa walimbende pindi walipomtia machoni.
Siku ile ilikuwa Ijumaa, kama kawaida yake, Sammy alikuwa katika mwonekano maridadi kabisa, akiwa amevalia shati zuri la rangi ya samawati la kitambaa brandi ya Barba ndani ya suti nyeusi ya aina ya Dunhill, tai ya rangi ya bluu shingoni na viatu ghali vya ngozi halisi kutoka nchini Switzerland.
Pia alikuwa amevaa saa ya mkononi aina ya Cartier iliyokuwa na nakshi ya madini ya dhahabu na kujipulizia manukato ghali aina ya Dolce & Gabbana. Mkononi alikuwa amebeba mkoba wake mdogo wa kiofisi aina ya Pad & Quill wa rangi ya hudhurungi.
Wakati akishuka kutoka kwenye gari manyunyu mepesi ya mvua yalikuwa yakianguka ardhini, lakini bado hayakumzuia Sammy kutembea taratibu akikatisha kwenye viunga vya maegesho ya magari na kuelekea mbele ya jengo la mbele la ile hoteli ya kitalii yenye hadhi ya nyota tano.
Wakati akitembea macho yake yaliangaza huku na kule kana kwamba alikuwa akitafuta kitu. Alipishana na askari mmoja wa ulinzi kutoka kampuni ya ulinzi ya Spark K7 aliyekuwa akilinda eneo lile la viunga vya maegesho ya magari.
Eneo lile lilikuwa pana likiwa na uwezo wa kuruhusu magari madogo hadi 100 kuegeshwa kwa wakati mmoja, na lilikuwa limepandwa miti mirefu ya kivuli aina ya ‘Quercus virginiana’ na ‘Arecaceae’ iliyojulikana pia kama ‘coconut palms’.
Pia eneo lile lilipandwa nyasi nzuri laini aina ya ‘Citronella’ na kulikuwa na bustani ya maua ya kupendeza yaliyotoa hewa safi ya upepo wa asili baina ya sehemu moja ya maegesho ya magari na sehemu nyingine, ndani ya uzio wa yale majengo ya hoteli.
Kwa yeyote aliyefika Udzungwa Beach Resort angeweza kubaini mara moja kuwa majengo ya hoteli hiyo yalijengwa kwa ufanisi wa hali ya juu.
Kulikuwa na majengo makuu mawili, moja lilikuwa mbele na la pili lilikuwa nyuma na kila moja lilikuwa na ghorofa saba za juu na mbili za chini, zilizotumika kwa ajili ya kumbi za burudani, kumbi za mikutano na migahawa ya kisasa ya chakula cha kitanzania na cha kimataifa. Pia kulikuwa na maduka na ofisi za utawala kwenye orofa ya chini nay a kwanza ya jengo la mbele.
Katika eneo lile kulikuwa na duka kubwa la bidhaa mbalimbali maarufu kama “supermarket”, duka kubwa la vipodozi na nguo za kisasa (boutique), na duka la kubadilishia fedha za kigeni maarufu kama “Bureau de Change” na vyumba viwili vidogo vyenye Mashine za ATM
Pia kulikuwa na jengo maalumu la klabu iliyojulikana kama Paradise Club, ambayo ilikuwa kwenye jengo la nyuma iliyowakutanisha mabilionea na baadhi ya vigogo serikalini na ilikuwa na ulinzi mkubwa sana, nje na ndani ya klabu.
Walioruhusiwa kuingia ndani ya klabu hiyo ni wanachama tu waliokidhi vigezo na kusajiliwa, ambao walilipa kiasi kikubwa cha ada ya uanachama kila mwaka.
Ndani ya majengo yote ya hoteli hiyo kulikuwa na kamera za usalama (CCTV) kila kona, viyoyozi vilivyosambaa kila mahali, na kutoka ghorofa moja kwenda nyingine kulikuwa na ngazi za kawaida na vyumba maalumu vya lifti za kisasa. Pia kulikuwa na ngazi iliyoendeshwa kwa umeme.
Yale majengo yalijengwa katika eneo tulivu mno lisilo na bughudha la ufukwe wa Oysterbay, jirani kabisa na ofisi za kibalozi na makazi ya watu wenye ukwasi, takriban kilomita tatu tu kutoka katikati ya jiji la Dar es Salaam.
Kwa watu wengi wenye ukwasi, Udzungwa Beach Resort ilikuwa ndiyo sehemu nzuri na tulivu zaidi ya kwenda kujipumzisha na kufurahia maisha, kwani ilikuwa imezungushiwa uzio madhubuti wenye ulinzi na kamera za usalama ulioifanya kuwa mahali patulivu zaidi na pa usalama wa uhakika.
Asubuhi ile kulikuwa na magari machache madogo na mabasi mawili ya wanafunzi wa vyuo vikuu vya Cape Town cha nchini Afrika Kusini na Chinhoyi cha nchini Zimbabwe yaliyokuwa yameegeshwa katika viunga vya maegesho ya magari.
Pia kulikuwa na malori mawili makubwa ya kubebea watalii wa masafa marefu aina ya Mercedes Benz, yaliyokuwa yameegeshwa mwisho kabisa wa yale majengo.
Mbele ya ile hoteli katika jengo la mbele Sammy aliipita milingoti saba iliyokuwa na bendera za Afrika Mashariki, Marekani, Uingereza, India, China, Afrika Kusini na bendera yenye nembo ya Udzungwa Beach Resort, zilizokuwa zinapepea taratibu.
Kulikuwa na mlango mkubwa wa vioo mbele ya jengo na varanda pana yenye ngazi iliyofunikwa kwa kofia nzuri ya zege ikiwa na sakafu nzuri yenye marumaru iliyonakshiwa kwa maandishi ya “Udzungwa Beach Resort”.
Kijana mmoja askari wa kampuni ya ulinzi ya Spark K7 alikuwa amesimama kikakamavu kwenye ile varanda pana akiwa kando ya ule mlango mkubwa wa vioo wa kuingilia ndani. Yule askari wa ulinzi aliyeitwa Fred Luvanda alimuona Sammy na kumpokea kwa tabasamu la kirafiki lililokuwa na bashasha zote kwenye uso wake.
Endelea kufuatilia...
Ni mahaba tuHuachwi hadi utueleze umempa nini askofu!

Nimelipenda jibu hili, short n clear!Ni mahaba tu![]()