OKW BOBAN SUNZU
Platinum Member
- Aug 24, 2011
- 49,243
- 103,925
Aida Olomi akibebwa kama mzoga na askari wa jeshi la Polisi, February 16, baada ya kupigwa risasi mguuni (jeraha la risasi limezungushiwa alama). Polisi walimuokota akiwa hawezi kutembea na kumuongezea kipigo cha marungu kabla ya kumbeba na kumtupa kwenye gari. Aida na wenzie walipelekwa mahabusu kituo cha polisi Oysterbay, ambapo inadaiwa hajapatiwa matibabu yoyote na kidonda chake kimeanza kuoza. Taarifa zinaeleza kuwa Aida amegoma kula tangu jana ili kushinikiza haki yake ya matibabu.
Kamanda wa Polisi mkoa wa Kinondoni ACP Muliro Jumanne amekiri kuwa ni kweli jeshi hilo linawashikilia watu watatu wenye majeraha ya risasi, akiwemo Aida lakini wameshapatiwa matibabu. Hata hivyo Muliro hakutaja hospitali zilizowapa matibabu watu hao, zaidi ya kusema ni hospitali za serikali.
KeshoAida na wenzake watatimiza siku 10 mahabusu tangu wakamatwe, bila kupandishwa kizimbani. Polisi wamekataa kuwapeleka mahakamani kwa maelezo kwamba upelelezi haujakamilika, jambo ambalo ni kinyume na sheria. Polisi pia wamezuia haki ya mahabusu hao kutembelewa na ndugu na jamaa zao.!
Updates
[HASHTAG]#Justice4Aida[/HASHTAG]Mkt wa BAWACHA Segerea bi. Agnesta Lambert anashikiliwa na Jeshi la Polisi Oysterbay na amenyimwa dhamana. Kosa analotuhumiwa ni kupiga picha.
Kiongozi huyo alikwenda kwa lengo la kumtembelea bi. Aida majeruhi wa risasi ambaye yuko mikononi mwa polisi siku ya 11 sasa.
------
Hongera Jeshi la Polisi kwa kusimamia maadili.