Stiegler’s Gorge kuanza kujengwa rasmi

Sasahivi unapikia kuni kama mnyonge likiisha utapikia umeme usijali
Haya ni matumaini kwa marehem anayekaribia kufa kwa ugonjwa wa kansa!!!Ingekua umem ndio mwarobaini wa shida za watu basi ethiopia wanaozalisha zaid ya matumiz yao watu wasingekua wanakimbia nchi
 
Haya ni matumaini kwa marehem anayekaribia kufa kwa ugonjwa wa kansa!!!Ingekua umem ndio mwarobaini wa shida za watu basi ethiopia wanaozalisha zaid ya matumiz yao watu wasingekua wanakimbia nchi

Ww hujui lolote kuhusu uwepo wa umeme. Umeme ni source ya kila kitu
Ukiwa na umeme utapata yafuatayo
1. Maji utayapata kwa urahisi mno hivyo kurahisisha maisha ya maskini kutumia muda mwingi kutafuta maji ilia afanye shughuli nyingine za kiuchumi, kama kulima, ujasiria mali n.k
2. Maji yanafanya kilimo kisiwe cha kubahatisha tukipata umeme twaweza kuvuta maji kutoka ziwa victoria au Tnganyika na kuyafikisha mpaka moro, singida tukalima sisi maskin

3. Treni itaendeshwa kwa umeme na itasafirisha mazao yataenda bandari au kwenye viwanda vinavyotegemea umeme na vitabangua hayo mazao kwa bei rahisi zaidi kwa sababu umeme upo kwa wingi.

Na mengine mengi tu
 
Kuna watu humu walisema JPM hawawezi kujenga hili bwawa ni porojo tu anapiga, kaeni kitaalam sababu hatupoi leo wala kesho.
 
Hizi ndio huwa lugha zenu alafu mwisho wa siku hadithi hubadilika.

Ndio walivyosema kwenye mradi wa gesi, kwamba tutauza gesi na umeme wa gesi mpaka Rwanda, Burundi, Bukenya, Bumalawi...

Halafu ukaja mkongo wa internet ukazinduliwa na Jk tukaambiwa tutapata mtandao wa 4G kwa kwenda mbele mpaka tutauza kwenye landlocked countries ambazo mkongo wa baharini haupiti....

Tukaishia na pasua kichwa cha Halotel Chuo!
 
Umezoea kukariri ndio maana hamna hija ya msingi, sema kama umeme hauna faida, una hasara gani? Sio kuongea kama Sokwe ambaye hafikiriii
Hakuna asiyejua umuhim wa umem hata hivy huwezi kupeleka rasilimali karibu zote kwenye umem wakat kuna matatizo lukuki, nimekupa mfano ethiopia ambao wanazalisha zaid ya wanavyohitaj unaonaje ustawi wao wa maisha???Kwa kuwa mivuvuzera hamuhitaji matumizi ya akili ni kushangilia kama mizombie vile.Hilo tren la umem lipo ethiopia fifteen years back,issue hapa ni ufupi wa kufikiri wa kushindwa kujua kipi kinatakiwa kianze,eti ooh mkulima atasafirisha kwa uraisi,nani kakwambia matatizo ya wakulima ni usafir,kwenda wapi?Hivi korosho kwa sasa inahitaji treni ya umem kupeleka wapi?Hivi kipi kinaanza kiwanda au malighafi, hivi unaweza kujenga kiwanda alafu unaanza mipango ya malighafi?
Tatizo kubwa la awamu hii ni matumizi kidogo ya akili katika kufanya maamuzi ya kutengeneza kipaumbele,mambo yanafanyika kienyeji tu, na bahati mbaya sana wanaomsaidia malaika ni wanafiki,washangiliaji na wapiga vigeregere tu hakuna matumizi ya akili zaidi kukubali lolote linaloamuliwa na malaika,ni jambo la ajabu sana!!!
 
Back
Top Bottom