Stella Manyanya amkaba koo Dr Slaa

Stella Manyanya amkaba koo Dr Slaa

duh hiyo ya sms ni kali ya wik, mama spika alisemaje alipoona ishu ambazo ni personal tena kwa mtu ambaye sio mbunge kuzumziwa bungeni! plz nipeni updates plz

nadhani alibaki kukenua meno yake yule spika..........ingefaa akamuuliza ilisemaje..,au angemkatisha asiongelee mabo ya sms..
 
Jukwaa gani tena wakati unajua josephine si mwanasiasa wa majukwaani? afterall njia aliyoitumia kumfikishia ujumbe ni muafaka kabisa, mwenye matatizo ni manyanya alkiyeamua kulipuka, tena bungeni ambapo anajua kwamba josephine hayupo na hawezi kumjibu.Punguza speculation mkuu, "conflict of interest" ipi tena wakati josephine alikuwa amefika kijijini kwao na kukuta hali ngumu ya maisha ya wanakijiji ndo akaona bora amkumbushe manyanya kuwawakilisha vizuri wanakijiji wenzake badala ya kuwa vuvuzela!!??
Mtani wangu Mwita........Nijuavyo mimi Josephine ni mwanasiasa hasa,tena wa jukwaani,mara nyingi wakati wa kampeni alikuwa akihutubia kwenye majukwaa na hata wakati wa maandamano ya Arusha ni mmojawapo wa walioshiriki na kupigwa na polisi na baadaye kukamatwa na mpaka sasa ni mmojawapo wa washtakiwa wa ile kesi iliyopo mahakamani......Na hata huko kijijini kwa Manyanya alienda kisiasa,wakati wa ziara ya operesheni Sangara......................Kuhusu speculation....nadhani hukunielewa vizuri mkuu wangu,soma posts za mwanzoni za thread hii utaona nini namaanisha,kuna watu wamedai kwamba Josephine na Stella wanamgombea Wilbroad Slaa,PHD kimapenzi(sasa sio speculations hizi)?......Wengine wanadai Stella alitaka mahusiano na Dk.Slaa Josephine akastuka..........Angalia pos za mwanzo utaona..........Otherwise,cheers.
 
Mtani wangu Mwita........Nijuavyo mimi Josephine ni mwanasiasa hasa,tena wa jukwaani,mara nyingi wakati wa kampeni alikuwa akihutubia kwenye majukwaa na hata wakati wa maandamano ya Arusha ni mmojawapo wa walioshiriki na kupigwa na polisi na baadaye kukamatwa na mpaka sasa ni mmojawapo wa washtakiwa wa ile kesi iliyopo mahakamani......Na hata huko kijijini kwa Manyanya alienda kisiasa,wakati wa ziara ya operesheni Sangara......................Kuhusu speculation....nadhani hukunielewa vizuri mkuu wangu,soma posts za mwanzoni za thread hii utaona nini namaanisha,kuna watu wamedai kwamba Josephine na Stella wanamgombea Wilbroad Slaa,PHD kimapenzi(sasa sio speculations hizi)?......Wengine wanadai Stella alitaka mahusiano na Dk.Slaa Josephine akastuka..........Angalia pos za mwanzo utaona..........Otherwise,cheers.
.........bala is always here!!
 
Haijalishi wala haihalalishi Kama wewe si mstaarabu kuwa na mwengine awe si mstaarabu pia.

Kama alikuwa na nia njema angechagua maneno mazuri ya kumwambia, besides Manyanya ni mbunge Wa viti maalum na ni msaidizi tu wa jimbo
.

mwalimu nakuelewa sana lakini unajua kwa namna yule manyanya alivyoongea bungeni kwa mtu ambeye amesikia na kuona wakati anaongea ....kuna watu wanadhani ni bonge la issue......kumbe alikuwa anaambiwa ukweli....hata kama yeye si muwakilishi wa jimbo alipaswa aongee kwa maslahi ya wananchi na sio kupaka rangi upepo.....sasa hivi ccm wengi wanachoongea ni personal attack kwa watu wengine.....maaana huwa hawasomi tafiti zozote ili kujua kweli......
 
ni jambo la kwaida kabisa katika kusema ukweli kuwa huo ni unafiki maana hawakilishi ipasavyo wananchi wake.......hata mimi nilishawahi andika kwa jk tena nafuu ya hii josephine ..labda atanijibu kupitia hotuba ya mwisho wa mwezi ..

viongozi wa kibongo bongo hawapendi kuambiwa ukweli, wanataka kusifiwa tu hata kama wanafanya mambo ya kijinga, ndo maana na sisi wananchi tumekumbwa na dhoruba hiyo hiyo. Ukisema ukweli unaambiwa wewe si mstaaarabu, mara unatafuta umaarufu wa kisiasa na maneno mengine mengi kama hayo.
 
viongozi wa kibongo bongo hawapendi kuambiwa ukweli, wanataka kusifiwa tu hata kama wanafanya mambo ya kijinga, ndo maana na sisi wananchi tumekumbwa na dhoruba hiyo hiyo. Ukisema ukweli unaambiwa wewe si mstaaarabu, mara unatafuta umaarufu wa kisiasa na maneno mengine mengi kama hayo.

ni kweli mura....tena siku hizi wana hicho ki msamiati...''umaarufu wa kisiasa'' lakini kweli hakuna lolote wanalofanya...tatizo kubwa ni kuwa hawasomi na kujifunza ili kujua matatizo ya wananchi...ndio maana wanapona cdm wako juu katika kusema ukweli tena kwa data...basi wana haha na njia pekee wanayobaki nayo ni kuchangia kwa kumshambulia mtu...........
 
Sera ya Magwanda (CDM) ni kuwapa wananchi vitu vya bure, sasa siwezi kushangazwa na Slaa kusema hivyo kwani huyu jamaaa hapendi watu wafanye kazi anapenda awape watu vitu vya bure bure

wewe na yule mbunge wa kilindi ni ndugu?
 
Stella Manyanya atema cheche Bungeni akimtuhumu Dr Slaa kwa kuwafundisha wananchi wasifanye kazi wakati yeye amewahamasisha wananchi wa kijiji chake (hakukitaja) wajitolee kufanya kazi za maendeleo, anasema ameudhiwa sana na kauli ya Dr Slaa kuwaambia wananchi wakisikia harufu ya chakula kizuri basi kinakuwa kimepikwa kwa mbunge. Pia amemuonya anayeitwa Mchumba wa Dr Slaa kwa kumuandikia SMS za kumtukana, anasema eti alifuatilia hizo SMS akakuta zimetoka kwa Josephine Emmanuel.Najiuliza hivi wabunge wa CCM hawana mambo ya kuchangia zaidi yakuingiza personalities?
Hivi Dkt Slaa anaweza kuwaambia wananchi wasifanye kazi kweli?,hawa wabunge wa ccm vipi!?hebu jaribuni kuwa makini maana ni ngumu sana kwa mtu mwenye akili timamu kuwanyima watu wasifanye kazi sasa watakula wapi!!?
 
Angejua namna Dr Slaa anavyonitia mimi hamasa ya kufanya kazi hadi saa mbili usiku huku nikiwa na matumaini Dr Slaa akiwa rais matunda ya utendaji wangu yatawanufaisha wananchi wote tofauti na sasa wananufaika mafisadi tu. Kweli ubunge wa viti maalum ni mzigo, kama ni kweli hiyo ishu wangewasiliana waimalize kwani imekaa kibinafsi na sio kutumia muda wa watanzania na posho ya leo ya 70,000 kujiaibisha.
 
Mtani wangu Mwita........Nijuavyo mimi Josephine ni mwanasiasa hasa,tena wa jukwaani,mara nyingi wakati wa kampeni alikuwa akihutubia kwenye majukwaa na hata wakati wa maandamano ya Arusha ni mmojawapo wa walioshiriki na kupigwa na polisi na baadaye kukamatwa na mpaka sasa ni mmojawapo wa washtakiwa wa ile kesi iliyopo mahakamani......Na hata huko kijijini kwa Manyanya alienda kisiasa,wakati wa ziara ya operesheni Sangara......................Kuhusu speculation....nadhani hukunielewa vizuri mkuu wangu,soma posts za mwanzoni za thread hii utaona nini namaanisha,kuna watu wamedai kwamba Josephine na Stella wanamgombea Wilbroad Slaa,PHD kimapenzi(sasa sio speculations hizi)?......Wengine wanadai Stella alitaka mahusiano na Dk.Slaa Josephine akastuka..........Angalia pos za mwanzo utaona..........Otherwise,cheers.

Mkuu Balantanda nakubaliana nawe, lakini utakumbuka kwamba si kila mtu anayeandamana anakuwa ni mwanasiasa wa majukwaani, kwakuwa naamini kila binadamu ni mwanasiasa kwa nafasi yake kwakuwa siasa ndio maisha. Kwahiyom josephine kuandamana arusha hadi kupigwa sio hoja ya kujustfy uansiasa wake kwa mtazamo wa sms aliyomtumia manyanya. Na hata hivyo utakumbuka kwamba wakati wa kampeni alikuwa akitambulishwa kama mchumba wa Slaa na kupewa nafasi ya kusalimia, mi namuona kama ni mwanasiasa in the making.

Pamoja na yote bado sioni mantiki ya manyanya kwenda kumlalamikia josephine bungeni, kimsingin hapa alikuwa anamlenga Slaa kutokana na pressure anayowapa. Kwani alishindwa nini manyanya kumjibu kwa sms kama alivyoandikiwa?? nadhani kwa hili nitakopa msemo wao kwamba anatafuta umaarufu wa kisiasa!!
 
Kwa hiyo....?

Gaijin acha ubishi, hata mimi ukunizingua nakuchana live, iwe kwa maneno, sms au mail maadam ujumbe wangu uupate kwa wakati ninaouona mimi sahihi. Sasa kama Mama aliona hali hovyo huko kijijini wakati huohuo 'injinia' anaongea utumbo bungeni angemkawiza?
 
ni jambo la kwaida kabisa katika kusema ukweli kuwa huo ni unafiki maana hawakilishi ipasavyo wananchi wake.......hata mimi nilishawahi andika kwa jk tena nafuu ya hii josephine ..labda atanijibu kupitia hotuba ya mwisho wa mwezi ..
Kama wanajuana its okay lakini sometimes kwenye hili Game la Siasa sio vema kuwapa wenzako makombora ambayo wanaweza kuyabadilisha au kuyatumia kwenye Propaganda
 
Mkuu Balantanda nakubaliana nawe, lakini utakumbuka kwamba si kila mtu anayeandamana anakuwa ni mwanasiasa wa majukwaani, kwakuwa naamini kila binadamu ni mwanasiasa kwa nafasi yake kwakuwa siasa ndio maisha. Kwahiyom josephine kuandamana arusha hadi kupigwa sio hoja ya kujustfy uansiasa wake kwa mtazamo wa sms aliyomtumia manyanya. Na hata hivyo utakumbuka kwamba wakati wa kampeni alikuwa akitambulishwa kama mchumba wa Slaa na kupewa nafasi ya kusalimia, mi namuona kama ni mwanasiasa in the making.

Pamoja na yote bado sioni mantiki ya manyanya kwenda kumlalamikia josephine bungeni, kimsingin hapa alikuwa anamlenga Slaa kutokana na pressure anayowapa. Kwani alishindwa nini manyanya kumjibu kwa sms kama alivyoandikiwa?? nadhani kwa hili nitakopa msemo wao kwamba anatafuta umaarufu wa kisiasa!!


mtani hapo kwenye red umesema kweli.....mana hata ukiwangaliwa sms aliyotumiwa ilikuwa ni ya kumfanya awajibike ipasavyo...haikuwa matusi kama alivyodai....bali ni ukweli mtupu....huyu mama manyanya sijui vipi
 
Haijalishi wala haihalalishi Kama wewe si mstaarabu kuwa na mwengine awe si mstaarabu pia.

Kama alikuwa na nia njema angechagua maneno mazuri ya kumwambia, besides Manyanya ni mbunge Wa viti maalum na ni msaidizi tu wa jimbo

Hivi kumbe neno unafiki ni baya eeh!! nilikuwa sijui. Mwishowe tutaanza kuikana lugha yetu!!

Sasa kama mtu nim mnafiki tumuiteje mwalimu? labda utusaidie nenoi mbadala.
 
Eeeeh! Na sisi bana,These are just trivial and absolutely solvable issues...no wonder hii thread imefika huku na inaendelea tu!

As for the so called Engineeer whoever.....It seems Chadema unleashed emotional laceration and you were thrown into a state of utter catalepsy.You had inured yourself in the aqua of self abnegation and immolation just to give credible representation to the down-trodden(Poor Tanzanians)..Huoni aibu kuongelea issue kama hizi bungeni? Some people are funny,shah!
 
Simple minds talk about people and their personality while strong minds discuss issues and visualize the future Mwenye cv na academic competence ya huyu mama aijaze hapa
Hahahaaa!Yani huo ndo mchango wake wa budget?Too cheap! Aibu!Watu wanakata nondo za issues za maendeleo na allocation ya resources.Yeye amesahau kama hapo ni bungeni na sio saluni!
 
Gaijin acha ubishi, hata mimi ukunizingua nakuchana live, iwe kwa maneno, sms au mail maadam ujumbe wangu uupate kwa wakati ninaouona mimi sahihi. Sasa kama Mama aliona hali hovyo huko kijijini wakati huohuo 'injinia' anaongea utumbo bungeni angemkawiza?

Haijalishi, utakuwa ni mkosefu wa ustaarabu vile vile. Huwezi kumwambia mtu "acha unafiki" kisha ukasema hakuwa akitafuta shari.

Manyanya si mstaarabu kwa kuwa haikuwa na mantiki ya kutangaza bungeni, lakini na Josephine nae ustaarabu haujui vile vile
 
Back
Top Bottom