Stella Manyanya amkaba koo Dr Slaa

Stella Manyanya amkaba koo Dr Slaa

People Record


Vitu viwili kuhusu hii profile ya Stella Manyanya

Kwanza:EMPLOYMENT HISTORY: TANESCO Head of Department 1992 To Date - Stella Manyanya amekuwa mbunge huu ni mwaka wa 6 sasa. Inawezekana bado jina lake liko kwenye payroll system ya TANESCO maana bado anasema anafanya kazi huko? Kanuni za bunge zinaruhusu kuwa mbunge huku bado unaendelea na utumishi kwenye shirika la umma? Kama hafanyi kazi TANESCO kwa nini aandike bado yuko huko 6 years after she joined the Parliament? Kama Stella Manyanya anashindwa hata kutoa taarifa sahihi kuhusu mwajiri wake anawezeje kuwa sahihi kwenye jambo lolote analoongea Bungeni?

La pili: Facial hair - Mwanamke kuwa na facial hair ni 'uchafu' - UNHYGIENIC! Na kama kuna mtu hapa Jamvini mke wake anafuga ndevu au hanyoi nywele miguuni anatakiwa ajue hivyo - UCHAFU. Nimewahi kuona wasichana na wamama wangi wanatembea bila wasiwasi huku miguu imejaa minywele na wengine ndevu kama wanaume! I hope Stella Manyanya wakati anazunguka dunia kuchunguza Richmond alinyoa hizo ndevu maana atakuwa ametoa taswira mbaya kuhusu wanawake wa Tanzania na personal hygiene.


11305.png


 
Shule za kudesa ni hatari sana!!!! Kama bi. Josephine anamuandikia sms kwa nini asimchukulie hatua za kisheria? Anasema hayo mambo bungeni ili iweje? Je hana mambo mengine yanayosumbua wananchi mpaka anachangia mambo ya kipuuzi kiasi hicho? Yes wabunge wengine inapaswa viti vyao ving'olewe bungeni kabisa!!!!!

Anatafuta umaarufu kwa kugombana na DK PHD,Kazi yao kubwa kulala, kupiga meza kuzomea hajui kitu zaidi ya mipasho na kura ya ndiyo hata kama wanatuangamiza
 
Stella hana mume anatafuta mchumba. ukiona mbunge anaongea umbea Bungeni ni mufilisi
 
University of Dar Es Salaam (UDSM) Post Graduate 2005 To Date POSTGRADUATE
Trodheim Technical Collage (NTNU) Norway PGD (Electric Power Distribution System) 1995 1996 POSTGRADUATE
Dar Es Salaam Institute Technology (DIT) Advance Diploma (Electrical Eng.) 1987 1992 ADV DIPLOMA
Dar Es Salaam Institute Technology (DIT) Full Technician Course (FTC) 1980 1983 CERTIFICATE
Songea Girls Secondary School Secondary Education 1976 1979 SECONDARY


Baada ya 'O' level kaenda Certificate badala ya 'A' levels.... that alone ought to classify her into some interesting category academically. Sasa leo kama anongoza Department, huko sijui tutegemee nini, na hata bungeni ukiacha KUCHONGA tu na mikelele isiyo na substance.
Alikuwa failure siku nyingi, na sintashangaa DIVISION IV au sifuri enzi hizo.

Pamoja na kwamba sikubaliani na uropokaji alioufanya bungeni huyu mhandisi manyanya lakini pia labda nikufahamishe tu kwamba hiyo certificate yake-FTC ni tofauti na hizi certificate za miezi mitatu ama sita tunazosoma siku hizi tunapofeli form four.

FTC-Full Technician Certificate ilikuwa ni kozi ya miaka mitatu yenye shule iliyokamilika. Mwanafunzi anaekuwa enrolled kusoma FTC ni lazima awe amemaliza kidato cha nne na kufaulu kwa div. I - div. III tena awe amefaulu masomo ya sayansi PCM. Ingawa sifahamu kiwango cha ufaulu wa manyanya katika masomo yake ya kidato cha nne lakini kwa kuangalia kipindi alichosoma 1980-1983 sina shaka kwamba alifaulu.

Miaka hiyo kulikuwa hakuna suala la uwezeshwaji katika elimu kama siku hizi ambapo wanawake wanaosoma masomo ya sayansi wakifeli wanabebwa kwa mbeleko ya chuma hadi vyuo vikuu na kujipatia degree ambazo sijui huko makazini wanazitumiaje.

Na baada ya kumaliza masomo ya FTC ulikuwa unagonga mtihani wa uhakika ulioandaliwa na NECTA na ukifaulu unasonga chuo kikuu na kukutana na wale waliopitia njia fupi(kwa mujibu wa MTM). Kwahiyo utaona kwamba waliopita FTC walikuwa ni watu wako vizuri upstairs. Tatizo lililopo kwa sasa ni kwamba either umepita njia ndefu ama fupi, ukishaingia ccm uwezo wako wa kuchambua mambo unapungua, na ndio hoja iliyotufikisha hapa tunamshangaa mhandisi huyu alivyoishia kutema pumba bungeni badala ya kuonyesha thamani ya mhandisi.
 
Ni kweli nilimtumia msg.nilimwambia hivi.Apunguze ushabiki na unafiki anapokuwa anazungumzia hoja bungeni kwani hata katika kijiji chake watu ni masikini sana badala yake aongee uhalisia na si nadharia.Anadhalilisha fani yake.Hii ni baada ya mimi kwenda kijijini kwake.she can prove me wrong.
Well done mama
 
Anavyoitwa Engineer, mbona sioni alipograduate?
Mimi navyoelewa ili uwe Eng. inabidi uwe na bachelor of engeering; vilevile ili uwe Dr (professional) inabidi uwe na bachelor ya Medicine au Veterinary.
Huyu sasa yupo kundi gani la engineers?

Mkuu kwa taarifa yako sio lazima uwe na bachelor ili uwe engineer, hata walio na advanced diploma ni maengineer kama alivyo manyanya ingawa yeye amekwenda mbele kidogo ana post graduate.
 
hana akili huyu stella. yaani anatumia muda wa buynge kudiscuss upupu?
 
Kwa nini usingemsema kwa kupitia jukwaa?...Nadhani ujumbe ungemfikia kwa urahisi zaidi......Btw......Kuna watu wameshaanza kutafsiri mengine hapa kwamba huenda kuna 'conflict of interest' kati yako na mhe. mbunge ndiyo maana wewe ukamtumia ujumbe.....
Mheshimiwa mbunge ali "over react" asingetumia kikao cha bunge kujibu sms, ndio maana inaleta tafsili mbaya kwake mwenyewe na mtuma sms.
 
Mkuu,
ni lazima uwe na bachelor ili uweze kuwa na title ya engineer..
ni lazima uwe na bachelor ili uitwe medical doctor au veterinary doctor..
ni lazima uwe na bachelor ya sheria ili uwe lawyer..etecetera
Labda uniambie siku hizi Tanzania ina vigezo vyake vipya tofauti na ulimwengu uliounda na kutengeneza hizo taaluma..
Mkuu, hapa wala usigusie masuala ya postgraduate kabisaa!! inawezekana yasiwe na uhusiano wa moja kwa moja na bachelor degree.

Mkuu kwa taarifa yako sio lazima uwe na bachelor ili uwe engineer, hata walio na advanced diploma ni maengineer kama alivyo manyanya ingawa yeye amekwenda mbele kidogo ana post graduate.
 
huyu si ndiyo yule engineer mwanasiasa - au njaa ndiyo zinawapeleka huko? yaani unaitupa carrier yako ya ufundi unaingia kupiga majungu.
kama dr slaa alivyoacha upadre kukimbilia wachumba na siasa
 
naangalia Bunge kuna baadhi ya wabunge wa ccm wanaongea point kama mbunge wa Temeke (ccm) lakini hawa stella heli kingesimamishwa kivuli
 
Mkuu,
ni lazima uwe na bachelor ili uweze kuwa na title ya engineer..
ni lazima uwe na bachelor ili uitwe medical doctor au veterinary doctor..
ni lazima uwe na bachelor ya sheria ili uwe lawyer..etecetera
Labda uniambie siku hizi Tanzania ina vigezo vyake vipya tofauti na ulimwengu uliounda na kutengeneza hizo taaluma..
Mkuu, hapa wala usigusie masuala ya postgraduate kabisaa!! inawezekana yasiwe na uhusiano wa moja kwa moja na bachelor degree.

Mkuu haina maana yoyote kubisha kitu usichokifahamu, nadhani nikushauri tu ujitahidi kwenda ERB-Engineers registration board watakusaidia zaidi.

Mfumo wetu wa elimu ndani ya nchii hii ni watu wengi hawaufahamu jinsi unavyooperate, unachokizungumza ni watu wengi wanaamini hivyo, ingawa sivyo ilivyo.

Labda nikuulize tu swali jepesi, Dr. Aisha Kigoda ana elimu gani?? Je unafahamu ni kwa nini Stella Manyanya anaitwa Engineer?? nadhani anzia hapo ili upate kujua kinachoendelea.
 
Vitu viwili kuhusu hii profile ya Stella Manyanya

Kwanza:EMPLOYMENT HISTORY: TANESCO Head of Department 1992 To Date - Stella Manyanya amekuwa mbunge huu ni mwaka wa 6 sasa. Inawezekana bado jina lake liko kwenye payroll system ya TANESCO maana bado anasema anafanya kazi huko? Kanuni za bunge zinaruhusu kuwa mbunge huku bado unaendelea na utumishi kwenye shirika la umma? Kama hafanyi kazi TANESCO kwa nini aandike bado yuko huko 6 years after she joined the Parliament? Kama Stella Manyanya anashindwa hata kutoa taarifa sahihi kuhusu mwajiri wake anawezeje kuwa sahihi kwenye jambo lolote analoongea Bungeni?

La pili: Facial hair - Mwanamke kuwa na facial hair ni 'uchafu' - UNHYGIENIC! Na kama kuna mtu hapa Jamvini mke wake anafuga ndevu au hanyoi nywele miguuni anatakiwa ajue hivyo - UCHAFU. Nimewahi kuona wasichana na wamama wangi wanatembea bila wasiwasi huku miguu imejaa minywele na wengine ndevu kama wanaume! I hope Stella Manyanya wakati anazunguka dunia kuchunguza Richmond alinyoa hizo ndevu maana atakuwa ametoa taswira mbaya kuhusu wanawake wa Tanzania na personal hygiene.


11305.png



Stella Manyanya bado anahesabika ni mtumishi wa TANESCO ingawa ni mbunge,yuko kwenye likizo ya bila malipo......

Si yeye tu,ni wabunge wengi ambao wako kwenye likizo ya namna hii,wakishapata ubunge wanaruhusiwa ama kuacha kazi ama kuomba likizo ya bila malipo mpaka watakapoacha ubunge wao....

Baada ya kuacha ubunge wanayo hiari ya kuendelea na ajira zao ama kuendelea na ustaarabu mwingine wa kuwa wastaafu....


Angalia waraka huu namba 1 wa mwaka 2000,pia kuna marekebisho ambayo yamefanywa katika waraka namba 2 na namba 3 kama sikosei...

Waraka Namba 1 wa Mwaka 2000​
KUHUSU WAGOMBEA UDIWANI, WAGOMBEA UBUNGE WA VITI MAALUM, UBUNGE WA KUTEULIWA NA RAIS KATIKA BUNGE LA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA NA WAGOMBEA UBUNGE KATIKA BUNGE LA JUMUIYA YA AFRIKA MASHARIKI​
1.0 Waraka wa Mkuu wa Utumishi wa Umma Na.1 wa Mwaka 2000 uliwekwa Masharti yanayowaongoza Watumishi wa Umma kushiriki katika shughuli za Kisiasa nchini.
2.0 Baada ya Masharti hayo kutumika kwa muda wa takriban mwaka mmoja na nusu, Serikali imeamua kufanya marekebisho katika Waraka huo kwa lengo la kuboresha Masharti hayo kwa Watumishi wa Umma watakaoamua kugombea au watakaoteuliwa katika nafasi zilizotajwa hapo juu kama ifuatavyo:
2.1 Watumishi wa Umma wanaoamua kugombea Udiwani
Watumishi wa Umma watakaoamua kugombea Udiwani wanaruhusiwa kufanya hivyo na endapo watabahatika kushinda wataendelea na ajira zao kwani Udiwani sio ajira.
Hata hivyo Watumishi wa Umma ambao ni waajiriwa katika Halmashauri (Council) hawaruhusiwi kugombea Udiwani katika Halmashauri wanazofanya kazi.
2.2 Watumishi wa Umma Wanaoamua Kugombea Ubunge Kupitia Viti Maalum
Watumishi wa Umma watakaoamua kugombea Ubunge kupitia Viti Maalulm wanaruhusiwa kufanya hivyo na endapo watashindwa wana hiari ya ama kuacha kazi na kulipwa mafao yao au kuchukua likizo bila malipo kwa kipindi chote cha uhai wa Bunge tangu Tume ya Uchaguzi itakapowatangaza kuwa Wabunge.
2.3 Watumishi wa Umma Wanaoteuliwa na Rais wa Kuwa Wabunge kwa Mujibu wa Ibara ya 66(1)(e) ya Katiba ya Jamhuri wa Muungano wa Tanzania ya Mwaka 1977 (Toleo la Mwaka 2000)
Watumishi wa Umma watakaoteuliwa na Rais kuwa Wabunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa mujibu wa Ibara ya 66(1)(e) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977 (Toleo la Mwaka 2000) wana hiari ya ama kuacha kazi na kulipwa mafao yao au kuchukua likizo bila malipo kwa kipindi chote cha uhai wa Bunge kuanzia siku watakayoteuliwa.
2.4 Watumishi wa Umma Watakaogombea Ubunge Katika Bunge la Jumuiya ya Afrika Mashariki
Watumishi wa Umma watakaochaguliwa kuwa Wabunge katika Bunge la Jumuiya ya Afrika Mashariki wanaweza kuendelea na kazi katika Utumishi wa Umma au kuchukua likizo bila malipo. Aidha, wakati wa kuhudhuria Vikao vya Bunge la Jumuiya ya Afrika Mashariki watalazimika kutoa taarifa kwa Waajiri wao na watapewa ruhusa maalumu ya kuhudhuria Vikao hiyvo.
3.0 MWISHO
Masharti mengine yanabaki kama yalivyo. Aidha, marekebisho haya yatatumika kuanzia tarehe ya Waraka huu; Isipokuwa kwa Wabunge wa Bunge la Jamhuri ya Afrika Mashariki marekebisho haya yatatumika kuanzia tarehe 15 Juni, 2001.
 
kweli nimeamin CCM inachakachua AKILI za watu, sms ni personal isue, bungeni imefikaje? Ni stella huyu nnaemjua mimi au? Kweli ccm inakufa vibya..
tukae mkao kusikiliza kesho atatuletea mambo ya chumbani alivyofanyiwa na Jogoo lake,siku hizi ndio hoja zao hizo kuanika mambo yao binafsi bungeni,yananikera sana haya majitu.
 
Mkuu,
ni lazima uwe na bachelor ili uweze kuwa na title ya engineer..
ni lazima uwe na bachelor ili uitwe medical doctor au veterinary doctor..
ni lazima uwe na bachelor ya sheria ili uwe lawyer..etecetera
Labda uniambie siku hizi Tanzania ina vigezo vyake vipya tofauti na ulimwengu uliounda na kutengeneza hizo taaluma..
Mkuu, hapa wala usigusie masuala ya postgraduate kabisaa!! inawezekana yasiwe na uhusiano wa moja kwa moja na bachelor degree.

Ni vizuri ukatofautisha Daktari/Mganga,mwanasheria na mhandisi.....

Si lazima mtu asome shahada ya uhandisi ndiyo aitwe mhandisi.....

Hivi unajua FTC(ya miaka ile,nadhani mpaka sasa ni hivyo hivyo) ilikuwa ni miaka mitatu.....Stella ni mhandisi,hii haina shaka yoyote.....Kapiga FTC na Adv.Dip pia ana PGD ya Norway na sasa anasoma PGD UDSM........Hebu soma hapa chini uangalie mhandisi ni nani...
Engineer - Wikipedia, the free encyclopedia
 
Ninavyofahamu mie ni kuwa DIT ambayo zamani ilikuwa Dar Technical College, kwa sasa wanatoa Diploma na wanaomaliza wanaitwa Wahandisi.

Kuwa Dr si lazima usome uganga au mifugo. Unaweza kupewa huo U-Dr au ukasoma masomo mengine hadi degree ya tatu (ukiacha waganga) na ukimaliza basi unapata kitu inaitwa PhD yaani Doctor of Philosopy. Hawa nao huitwa Dr.

Mama anaweza kuwa na tatizo kama alilonalo Dr. Billal ambalo wengi waliosoma UDSM kwenye uhandisi, wanakumbuka ukali wa huyu mzee ila inapokuja kwenye siasa, si mkali kihivyo. Unaweza kukuta kiungozi, anapitwa mbali sana na Mbowe ambaye ukiwalinganisha na Billal au Prof. Lipumba/Kapuya unaona kuwa Mbowe kiuongozi anawaacha mbali sana.

Mnafanya makosa sana kuchanganya Siasa na akili za darasani/kazini.
 
Mkuu,
hao uliyowataja hakuna hata mmoja anayestahili hizo title..unless walifanya miujiza ndiyo wakapewa katika mazingira maalum..
Nikupe mfano: Bill Gates ambae hakuwahi ku-graduate lakini amefanya mengi katika ulimwengu wa science and technology..huyu wakimtunuku u-engineer wa heshima hakuna tatizo kabisa.
Lakini huyo Bi. Kagoda na Bi. Manyanya uliyowanukuu wamefanya yapi makubwa na ya ajabu hapa Tanzania ili tuwatunuku na kuwaenzi kwa hizo title?

Mkuu haina maana yoyote kubisha kitu usichokifahamu, nadhani nikushauri tu ujitahidi kwenda ERB-Engineers registration board watakusaidia zaidi.

Mfumo wetu wa elimu ndani ya nchii hii ni watu wengi hawaufahamu jinsi unavyooperate, unachokizungumza ni watu wengi wanaamini hivyo, ingawa sivyo ilivyo.

Labda nikuulize tu swali jepesi, Dr. Aisha Kigoda ana elimu gani?? Je unafahamu ni kwa nini Stella Manyanya anaitwa Engineer?? nadhani anzia hapo ili upate kujua kinachoendelea.
 
Back
Top Bottom