Startimes local channel sasa kulipiwa 6,000/=

Startimes local channel sasa kulipiwa 6,000/=

Hapa sijizungumzii mimi ninawazungumzia watanzania walio wengi. Mfano pato la mtanzania kwa mwaka ni Tshs 3,000,000/= ÷ 12 = 250,000/= ÷ 31 = 806 Pato la Mtanzania kwa siku. Sasa chukua 6,000/= ÷ 800 = 7.5 ~ Mlo wa siku 8. Inamaanisha ili kulipia King'amuzi Mtanzania anahitaji kutumia mlo wa siku 8.

Nadhani umenielewa.
Watanzania hawajai kulalamika kuhusu hiyo bei usiwasemee. Ni hela ndogo sana hiyo kwa kupata taarifa.
 
Unalalamika sh elfu 6 tu mwanaume mzima?



Waonee huruma wale waioweza kupata hata 2600/= ya sukari kule kijijini. waonee huruma wale wanaoitafuta 1,200 ya kununua chumvi kwa mwezi mzima kule kijijini,
furaha yao ni kuwepo kwa uememe ingawa nao hawezi kulipia LUKU hata kama ingekuwa Tsh 2000 kwa mwezi.

Je kingamuzi cha kulipia 6,000, itawezekana vipi ikiwa tu mahitaji muhimu kwao ni ndoto kama siyo kusubiri wakati wa kampeni watunukiwe zawadi za sukari na chumvi.

Fikiri mara mbili mkuu!
 
Serikali ipo kimya kabisa.. wakati mkuu anadai yeye ni Rais wa masikini... Sijajua ni masikini wa nchi ipi..
 

Waonee huruma wale waioweza kupata hata 2600/= ya sukari kule kijijini. waonee huruma wale wanaoitafuta 1,200 ya kununua chumvi kwa mwezi mzima kule kijijini,
furaha yao ni kuwepo kwa uememe ingawa nao hawezi kulipia LUKU hata kama ingekuwa Tsh 2000 kwa mwezi.

Je kingamuzi cha kulipia 6,000, itawezekana vipi ikiwa tu mahitaji muhimu kwao ni ndoto kama siyo kusubiri wakati wa kampeni watunukiwe zawadi za sukari na chumvi.

Fikiri mara mbili mkuu!
Mtu mwenye TV na decoder awezi kukosa elfu 6 ya kulipia. Msipende kuleta siasa kwenye kila kitu... Ombeni basi ata magazeti na simu ziwe bure.
 
Wengine wanavyo kwa kurithi si lazima wawe wamenunua.
Umenisaidia mkuu,

Watanzania wengi wamekulia mjini na hawaendi kwao (vijiji) hata kwa kusalimia tu. Hili linafanya wajione kama malaika wenye kila kitu. Kuna Kijiji nilienda nikatoa 10,000/= yaani chenchi ilikuwa ni issue.
 
Niliwapigia cm wiki iliyopita wakanijibu itakuwa inaonyesha TBC pekee isipokuwa channel on test pekee!!
 
Ngoja tuisome namba vizuri. Ndio akili zije. Mpaka 2025 tutakuwa km mashetani
sipati picha wale wanaosubiria ajira za serikalini, wanaishi km mashetani.
 
hapa nadhani serikali inatakiwa ijitathimini kwa kina sana.

Maana kama Baba inahitaji Ujionyeshe Mbele ya Watoto kwamba wewe ni Mkakamavu, ili watoto wasije wakakudharau.

Kwa hili nasema kabisa Serikali iwaombe Radhi wananchi wake kwa kushindwa kuonyesha kuwatetea kwa Mabwanyenye hawa wenye makampuni Haya.

Nampongeza sana Mzalendo Mzee Mengi na kingamuzi chake cha DigTek Amekuwa Mzalendo Hatozi Fedha Yeyote ni Free kabisa.

Nawashauri watanzania waamie DigTek. Wapate Raha Duniani.
 
Hapa sijizungumzii mimi ninawazungumzia watanzania walio wengi. Mfano pato la mtanzania kwa mwaka ni Tshs 3,000,000/= ÷ 12 = 250,000/= ÷ 31 = 806 Pato la Mtanzania kwa siku. Sasa chukua 6,000/= ÷ 800 = 7.5 ~ Mlo wa siku 8. Inamaanisha ili kulipia King'amuzi Mtanzania anahitaji kutumia mlo wa siku 8.

Nadhani umenielewa.
....we jamaa laki mbili Na nusu ukigawanya kwa 30 unapata 806 kweli au umekosea tu
 
Niliwapigia cm wiki iliyopita wakanijibu itakuwa inaonyesha TBC pekee isipokuwa channel on test pekee!!
TV 1 wameiacha kwa muda ili watu wakizoea mpira nayo wafanye ya kulipia.
 
....we jamaa laki mbili Na nusu ukigawanya kwa 30 unapata 806 kweli au umekosea tu
Mimi nimechukua 250,000/= ÷ 31

Wewe umechukua 250,000/= ÷ 30

MAJIBU YOTE UKIKARIBISHA UNAPATA 800/= Tshs kwa siku.
 
Yaani bei inapanda kila leo. Wakijisikia tu wanapandisha. Namuona Mh. Nape kwa mbaali na yeye anaanza kuwa Waziri Mzigo.
Wakubwa wamewekeza kwenye baadhi ya haya mashirika, nadhani ndio maana yana jeuri namna hii.
 
Back
Top Bottom