C.T.U
JF-Expert Member
- Jun 1, 2011
- 5,070
- 3,718
Muigizaji wa Filamu hapa Bongo, Jacqueline Pentezel ‘Jack wa Chuzi' ametoa kali ya mwaka baada ya kuamua kuanika idadi ya wanaume aliowahi kula nao urojo tangu awe supastaa.Msanii huyo alifikia hatua hiyo alipokuwa katika mahojiano maalum na mwandishi wa GLOBAL PUBLISHER na kutakiwa kutoa ufafanuzi wa juu ya taarifa zilizozaga kuwa, kuna mwanaume kajitokeza anataka kumchukua jumla jumla.Katika kutoa ufafanuzi wake, Jack alikiri kuwepo kwa mpango wa kutaka kuingia katika maisha ya ndoa na mwanaume aliyemtaja kwa jina moja la Jojoz na kuweka wazi kuwa,huyo ni mwanaume wake wa kumi katika maisha yake ya kimapenzi.