Sports Extra ya Clouds Fm

Sports Extra ya Clouds Fm

Hiki kipindi ni cha ajabu sana. Shafii Dauda anachapia mno kila anapojaribu kuongea kingereza na vile vile kipindi wanakifanya kama vile wako maskani wanapiga story tuu. Hivi kweli wanakosa hata muda wa kupanga nini wakiongelee ndanin ya kipindi? yani wana ruka toka hapa kwenda kule.

Si unge tune station ingine mkuu!!!
 
Sidhani kama kuna kipindi bora cha sports km sports extra sbb wanachambua hbr kiundani za bongo na duniani,no comment
 
Hyo ya BATHELONA NDO DUH!
aiseee....kumbe tuko wengi!
Binafsi kipindi nakipenda sana ila mbwembwe za Watangazaji ndio zinakera hasa pale wanapotamka Barcelona(batherona), Zaragoza(tharaghotha). Hata kama wanajitahidi kuongea kiispania, mbona SuperSport wanasema Barcelona(baselona) Zaragoza(zaragoza).

Shafii yuko poa japo kidhungu kina mkaba bora aachane nacho.

Kuna huyo Maestro kwa kweli angetafuta kipindi kingine au aache kutangaza, jamaa anabore sana na anapotangaza mbwembwe za kijinga hadi anasahau kutamka mambo muhimu anaweza sema timu flan imeshinda akaweka mbwembwe akasahau kutaja magoli.

Lwambano yuko poa na makini kwa kazi yake.

Mbwiga wa Mbwiguke ndio hovyoooo kabisa!
 
Unaweza kuichukia na kuiponda CLOUDS FM pamoja na vipindi na watangazaji wake upendavyo Lakini huwezi kuondoa ukweli kuwa CLOUDS FM ndio redio bora zaidi ya radio stations zote hapa Bongo, Wala huwezi kuondoa ukweli kuwa CLOUDS FM ndio radio station inayoongoza kwa kusikilizwa na watu wengi zaidi hapa DSM na kwingineko Pia huwezi kuondoa ukweli kuwa CLOUDS FM ndio radio yenye ushawishi mkubwa zaidi hivyo kupokea matangazo yanye kuingiza mkwanja wa nguvu zaidi...........nk nk nk
 
creativity...tatizo wabongo mnapenda mambo yawe kama yalivyokua miaka 40 iliyopita..sikiliza redio za nje uone jinsi watu wanavyotangaza..clouds ni redio ya burudani..hivyo watangazaji inabidi hatakama wanatoa mada yenye umuhimu..waipresent katika mfumo unaovutia na si utaomboa msikilizaji..mnataka mtu atangaze kipindi cha michezo kama matangazo ya vifo bwana?? inawezekana kukawa na upungufu wa hapa na pale..hilo sipingani nalo..linakubalika ..lakini upungufu huo usizidi na kufikia kuondoa mantiki na ubora wa kipindi jambao ambalo naona halijafikia kwa clouds.. binafsi kuna huyu jamaa anaesemaga valenthia anapotaja valencia..au pale wanapotudangaya kua uwanja wa inter milan unaitwa guessepe "de" meazza badala ya guessepe meazza..panabiboa..kipindi kizuri sana ila kinahitajika maboresho kadri siku zinavyokwenda...na jambo lingine linalonikera HAPA BONGO KWENYE MEDIA!!!! NI kwa taarifa za habari almost TV zote isipokuwa chanel 10 kuwa saa mbili usiku..hii naboa..mtu unakosa kupata habari mbalimbali maana uwasilishwaji wa habari unatofautiana baina ya media na media..vile vile..kupiga muziki siku nzima badala ya kutoa vipindi vyenye mafundisho hapo tu nakereka..
 
Mimi binafsi sina shaka na jinsi Clouds wanavyoendesha vipindi vyao; na ni moja ya shabiki wao; kama binadamu wengine watangazaji wa clouds nao wana kasoro zao na sio kila siku wanakua hovyo ndivyo ilivyo kwa binadamu wengi tulivyo; ndo maana kuna redio nyingi pia nadhani hata wao kuna wakati huchemka vile vile; Kuhusu kiingishi hii lugha ya wenyewe hii hakuna mtz halisi alozaliwa nayo hapa kwetu; kwa kuvunja yai viza na lililo fresh ndio namna ya kuimaster, huo ndio msingi tunaosonga nao"
Mtazamo wangu
 
Kwa nini mnaumiza akiri zenu hivi harufu mbaya unaweza kuendelea kuinusa? radio ziko nyingi acheni kabisa kusikiliza hiyo clouds sikilizeni zingine wala hamtakeleka sana. Tabia ya watanzania kulalamika itaisha lini? Kibonde hii radio siyo yake na pia kituo kinaendeshwa kisheria kama ulikuwa hujui ni kwamba kama kuna kitu chochote kimekuudhi katika radio na una ushahidi unaweza kwenda kwanza kwa mkurugenzi wa kituo akikuzingua nenda TCRA hawa ndio mabosi wao.
 
creativity...tatizo wabongo mnapenda mambo yawe kama yalivyokua miaka 40 iliyopita..sikiliza redio za nje uone jinsi watu wanavyotangaza..clouds ni redio ya burudani..hivyo watangazaji inabidi hatakama wanatoa mada yenye umuhimu..waipresent katika mfumo unaovutia na si utaomboa msikilizaji..mnataka mtu atangaze kipindi cha michezo kama matangazo ya vifo bwana?? inawezekana kukawa na upungufu wa hapa na pale..hilo sipingani nalo..linakubalika ..lakini upungufu huo usizidi na kufikia kuondoa mantiki na ubora wa kipindi jambao ambalo naona halijafikia kwa clouds.. binafsi kuna huyu jamaa anaesemaga valenthia anapotaja valencia..au pale wanapotudangaya kua uwanja wa inter milan unaitwa guessepe "de" meazza badala ya guessepe meazza..panabiboa..kipindi kizuri sana ila kinahitajika maboresho kadri siku zinavyokwenda...na jambo lingine linalonikera HAPA BONGO KWENYE MEDIA!!!! NI kwa taarifa za habari almost TV zote isipokuwa chanel 10 kuwa saa mbili usiku..hii naboa..mtu unakosa kupata habari mbalimbali maana uwasilishwaji wa habari unatofautiana baina ya media na media..vile vile..kupiga muziki siku nzima badala ya kutoa vipindi vyenye mafundisho hapo tu nakereka..

We kijana unaakili sana,wengine wanaponda kw kuwa m2 fulani kaponda.swali umenza kukereka lini? Ni baadaya mleta tread au kabla na kama ni kabla mbona ulete tread yako.tusipende kuendea sokoni kwa kichwa mwenzako ni uvivu wa kufikiri. Clouds kwa ujumla inatimiza wajibu wke kwa wasikilizaji wake achia mbali mapungufu kidogo yanayojitokeza.
 
Unaweza kuichukia na kuiponda CLOUDS FM pamoja na vipindi na watangazaji wake upendavyo Lakini huwezi kuondoa ukweli kuwa CLOUDS FM ndio redio bora zaidi ya radio stations zote hapa Bongo, Wala huwezi kuondoa ukweli kuwa CLOUDS FM ndio radio station inayoongoza kwa kusikilizwa na watu wengi zaidi hapa DSM na kwingineko Pia huwezi kuondoa ukweli kuwa CLOUDS FM ndio radio yenye ushawishi mkubwa zaidi hivyo kupokea matangazo yanye kuingiza mkwanja wa nguvu zaidi...........nk nk nk

hao hawajui kitu kabisa...clouds ni bomba sanaa.....kwani clouds wanafundisha english course..?,km unataka kujifunza kiingereza kuna vijiwe vingi sana mtaani...
tena mbwiga anatuburudisha sanaa....hao mi naona sports so fani yaoo..na hawana jipya kabisaa....
 
Sikilizeni Saturday Sport ya EA fm @1600HRS ndio utajua Sports Extra ya Clouds fm ****!
 
heni ujinga kwani hamuwezi kusikiliza michezo kupitia kituo kingine......
 
Sidhani kama kuna kipindi bora cha sports km sports extra sbb wanachambua hbr kiundani za bongo na duniani,no comment
nakuunga mkono mkuu, kwa tz iwe tv ama radio kwa upande wa michezo clouds wapo juu, bila kujali eti english... kwani
wanafanya interview? ile ni michezo...napenda wanavyogusa kila kona ndo mana kipindi chao ni lisaa lizima. kwa tbc nilikuwa napenda alipokuwa anatangaza pendael omary, cjui kapotelea wapi yule chalii.
 
Sikilizeni Saturday Sport ya EA fm @1600HRS ndio utajua Sports Extra ya Clouds fm ****!
 
Back
Top Bottom