Spika Ndugai: Vijana wa Tanzania hawaaminiki, wakiachiwa biashara bila kuiba wanajiona wajinga

Replica

JF-Expert Member
Aug 28, 2017
1,446
7,817
Wakati Waziri Mkuu akiahirisha Bunge baada ya hotuba ya Waziri Mkuu, Spika Ndugai ameongelea suala la uaminifu wa watanzania hasa kwa vijana na kudai wawekezaji wengi wamekuwa wakilalamika. Ndugai amesema mtu anaeanzisha mradi atajikuta tu amefilisika asipokuwa makini.

'' Mtu akianzisha labda tuseme 'super market' nisikilizie kama bado utamkuta barabarani miaka mitatu ijayo. Ataibiwa pale si kawaida, hata wewe wekeza halafu njoo bungeni hapa umewaachia miezi sita hujawatembelea, subiri siku utakayoenda upige mahesabu, utakuta umepigwa'' Alisema spika Ndugai.



Aliendelea '' Mswahili humuachii shughuli mkakubaliana usipigwe kwa sababu ya uaminifu, sijui namna gani tutafanyia kazi?''

''Kijana akiwa na fursa kama hiyo akaachiwa asimamie biashara asikuibie, wenzake mtaani wanasema mjinga sana yule, alipewa goli liko wazi kaliacha, mjinga kweli! Jamaa mwaka mzima yuko bungeni kule, yeye kakaa tu lakini uaminifu unalipa sana katika maisha'' Alimalizia Spika Ndugai.
 
Ndugai kama kiongozi wa mhimili "unaojitegemea" ameshindwa kutoa solution ameamua kulalamika tu, kwa hiyo yale madudu yaliyosomwa kwenye ripoti ya CAG yaachwe tu kwasababu ndio tabia za waswahili "kufunga" goli likiachwa wazi.

Kumbe ndio maana mwisho wa siku wale wezi huwa hawawajibishwi maisha yanaendelea tu, tutakuwa taifa pekee duniani linaloongozwa na viongozi waliofikia mwisho wa uwezo wao wa kufikiri.
 
Mheshimiwa Speaker sheria mbovu ulizopitisha ndio chanzo.

Mfano Makati ya mikopo kwa wanafunzi wa chuo kikuu, mtu anafanya kazi mishahara haikutani sababu ya makato
Rekebisha Sheria, za Makati ya mikopo, fao la kujitoa, etc Mambo yatakuwa Kama zamani
 
Spika wa bunge Tanzania analalamika namna tatizo la wizi limekidhiri Tanzania mpaka yule asiyeiba anaonwa mjinga, ukiwekeza supermaket wanakufilisi ndani ya miaka mitatu, ni tatizo sugu na limekosa utatuzi.
Ameongea kwa huruma sana kama aliyekata tamaa kwa namna wote wamekua majizi.

 
Spika wa bunge Tanzania analalamika namna tatizo la wizi limekidhiri Tanzania mpaka yule asiyeiba anaonwa mjinga, ukiwekeza supermaket wanakufilisi ndani ya miaka mitatu, ni tatizo sugu na limekosa utatuzi.


October 2020, mliwafundisha wizi wa kura,sasa wamehamia kwenye uchumi
 
Back
Top Bottom