Mkuu Pasco,Edson Z. M, ni kweli huu ni ushindi kwa Watanzania wote na ndio umuhimu wa kuwa na upinzani wa kweli, ila pia upinzani wa kweli bila umoja wa wapinzani is nothing, kweli hili la huu muswada, vyama vyote vya upinzani vimepaza kauli moja, 'uondolewe' na serikali imepiga magoti, imeuondoa. Kama tangu uchaguzi wa 2010, vyama vyote vingekubaliana CCM iondoke, CCM, ingeondoka!.
unaweza kuwa sahihi kwenye hili la kuungana kwa vyama vya upinzani lakini unaungana kama kuna kukubaliana kwenye mambo ya msingi.Kama una mazingira ya vyama kama CUF,NCCR na TADEA unaungana na chama kipi? vyama vya upinzani kila kimoja kijiimarishe ili inapofika wakati wa uchaguzi wawe wana wafuasi na mashabiki wa uhakika wa kutosha badala ya kukimbilia kuungana na puppets! ni vyema kila unapozungumzia kuungana usilinganishe yaliyotokea Kenya na kwingineko bali angalia mazingira yanayokuzunguka. how can you form muungano na CUF au TADEA? Ni ngumu tusiongee kwasababu ni rahisi kutamka je is it practical?