Spika Job Ndugai: Matatizo yetu na Prof. Mussa Assad ni kutuita dhaifu, alitakiwa ajiuzulu. Hatuna tatizo na ripoti yake, tutaifanyia kazi

Spika wa Bunge Job Ndugai, leo Aprili 14 atazungumza na waandishi wa habari jambo muhimu kuhusu bunge.

Mazungumzo hayo yatafanyika katika ofisi ndogo ya bunge jijini Dar es salaam majira ya saa sita na nusu mchana.


=====

UPDATES:

View attachment 1071319

=> Spika Ndugai: CAG anaposema mbele ya umma kuwa ataendelea kutuita 'dhaifu' wakati ni jina ambalo hatulipendi na tumelikataa, tunashindwa kumuelewa kama analipenda sana ajiite yeye. Sasa kusema unaendelea kutumia endelea na nitakuita tena na safari hii itakuwa mbaya zaidi"

=> Spika Ndugai: "Namwambia ndugu yangu Prof. Assad hilo neno aliache, sisi taarifa tumeipata na tutaifanyia kazi. Msisitizo wetu ni mmoja, kwakuwa bunge lilishapitisha uamuzi wa kutofanya kazi na Prof. Assad ni uamuzi halali"


=> Spika Ndugai: "Sina chuki binafsi na Prof. Assad, yule ni ndugu yangu na ni mtanzania mwenzangu tatizo ni lugha anayoitumia na nisinhependa itufikishe hapa kama taifa."

=> Spika Ndugai: "Tunataka tumuoneshe Prof. Assad kuwa Bunge halichezewi, simuelekezi kazi ila anatakiwa ajiongeze kama ni kujiuzulu au laaa!. Maana tushamwambia hatumtaki, anavyoendelea kubaki ofisini ni kumpa tu wakati mgumu Rais

=> Spika Ndugai: Zipo njia za kumaliza mambo kama haya, mojawapo aende kwa Rais akajieleze kwamba mimi nimepima nimeona nimekosea hapa na pale. Maana Rais ni sehemu yetu sisi (Bunge) hatuwezi kupitisha sheria bila yeye kupitisha mkono wake,

=> Spika wa Bunge Mh. Job Ndugai amewahakikishia watanzania kuwa bunge linaendelea vizuri na kazi yake ya kutunga sheria, uwakilishi, kuisimamia Serikali pamoja na mipango ya nchi ikiwemo suala la bajeti ambalo linaendelea bungeni.

=> Spika Ndugai:“Sasa kumekuwa na ufafanuzi usiokuwa sawa sawa, kilichowekwa mezani ni ‘Audit Queries’ …kilichowekwa mezani sio ukweli wenyewe kwamba aliyetajwa mule sasa huyo mwizi… ‘Audit queries’ zile zikishawekwa mezani kazi yetu ni kuwaita mezani na kuwasikiliza

=> Spika Ndugai:Tunataka tumuoneshe Prof. Assad kuwa Bunge halichezewi, simuelekezi kazi ila anatakiwa ajiongeze kama ni kujiuzulu au la! maana tushamwambia hatumtaki, anavyoendelea kubaki ofisini ni kumpa tu wakati mgumu Rais

=> Spika Ndugai:Hatuna tatizo na ripoti ya CAG…tatizo letu ni maneno ambayo Profesa Mussa Juma Assad ameyatoa akiwa Marekani, na alipoita waandishi akarudia tena, maneno yale sie tumeyakataa sio ya kistaarabu.

=> Spika Ndugai:Sisi kama Bunge hatutaki hilo neno dhaifu, kwa sababu Bunge kama Bunge halifanyiwi tathmini na ofisi ya CAG ila wanaofanyiwa tathmini ni watendaji wa Ofisi hiyo hivyo hawakupaswa kudhihakiwa na lugha hiyo inayotajwa kuwa ya kihasibu.

=> Spika Ndugai: “Hata katika maisha ya kawaida, we unamuita mtu jina flani, anakwambia bwana tafadhali jina hili silipendi, lakini unaendelea kumuita na kuahidi utaendelea kulitumia, ni ustaarabu duniani?”

=> Spika Ndugai: “Katika kutekeleza majukumu yake #CAG hakupaswa na hapaswi kulitukana #Bunge kwa lugha zile za rejareja. Bunge huangalia taratibu zake na kuendesha mambo yake kufuatana na kanuni za Bunge…lile Bunge lenyewe hawezi kulikagua”

=> Spika Ndugai: Hatuna tatizo na ripoti ya CAG…tatizo letu ni maneno ambayo Profesa Mussa Juma Assad ameyatoa akiwa Marekani, na alipoita waandishi akarudia tena, maneno yale sie tumeyakataa sio ya kistaarabu.

=> Spika Ndugai: “Sasa kumekuwa na ufafanuzi usiokuwa sawa sawa, kilichowekwa mezani ni ‘Audit Queries’ …kilichowekwa mezani sio ukweli wenyewe kwamba aliyetajwa mule sasa huyo mwizi… ‘Audit queries’ zile zikishawekwa mezani kazi yetu ni kuwaita mezani na kuwasikiliza”

"Nilipokuwa sipo kuna mambo mengi yamezungumzwa, na mengine yameandikwa kuhusu Ripoti ya CAG. Nitakapokuwa Dodoma nitaagiza ripoti ipelekwe kwenye kamati za PAC na LAC"




Zaidi soma.....

Dar es Salaam. Spika wa Bunge la Tanzania, Job Ndugai amemshauri Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), Profesa Mussa Assad akamwone Rais John Magufuli ili mzozo wake na Bunge uishe.

Kauli ya Spika inakuja wakati tayari Bunge limeshapitisha azimio la kutofanya kazi na Profesa Assad bali ofisi ya CAG.

Spika Ndugai aliyekuwa ziarani nchini Sweden wiki iliyopita ameyasema hayo leo Jumapili Aprili 14, 2019 akieleza kusikitishwa na hatua ya Profesa Assad kurudia neno udhaifu kwa Bunge alipotoa taarifa yake hivi karibuni.

"Zipo njia za kumaliza mambo kama haya, mojawapo aende kwa Rais akajieleze kwamba mimi nimepima nimeona nimekosea hapa na pale. Maana Rais ni sehemu yetu sisi (Bunge) hatuwezi kupitisha sheria bila yeye kupitisha mkono wake," alisema Ndugai.

Ameongeza kuwa hata bajeti inayojadiliwa na Bunge lazima ipitishwe na Rais. Amesema kwa kuwa Bunge limeshapitisha azimio la kutofanya kazi na Profesa Mussa Assad alitakiwa ajiuzulu.

"Kwa kuwa Bunge likishaaamua kuwa halifanyi kazi na mtu, ni uamuzi halali. Katika nchi zote Bunge likishakosa imani na wewe unajiuzulu," amesema.

Ameongeza, "Sasa hatumfundishi kazi Mussa Assad, anampa wakati mgumu Rais tu. Tutafanya kazi na ofisi ya wananchi."

Spika Ndugai amemsifu Profesa Assad kwa ujasiri wake huku akiufananisha na ujasiri wa mbwa kumtukana mtu anayemlisha.

"Unatukana hadi mkono unaokulisha, inahitaji ujasiri na jamaa ana ujasiri. Ila ni ujasiri ule wa mbwa anayemtukana anayemlisha," amesema.

Hata hivyo, Ndugai amesema hana chuki binafsi na Assad bali tatizo ni lugha tu aliyotumia ya kuliita Bunge dhaifu.
Therefore Professor is like a dog?Matusi kwa Professor ni sawa ila udhaifu wa Bunge Ni kosa la jinai.Hii imekaaje wadau?
 
Sidhani kama cheo cha Speaker ni kikubwa kama cheo cha CAG kiutendaji.

Speaker anasimamia mambo ya CCM, wakati CAG anasimamia mambo ya kitaifa.

Kama Speaker hawezi kufanya kazi na CAG basi ajiuzulu yeye na sio kumwelekeza CAG ajiuzulu.

Halafu, wafugaji (wala nyama kwa sana) ni watu wa ku react sana. Nadhani nyama zina element fulani za chemical reactions at confrontations hahahaha
 
Nimemsikiliza sana huyu Ndugai hajui anachokisema. Profesa ni profesa tu hata kama hataki ahitwe hivyo. Ni nani aliyemzuhia yeye hasisome?

Nijualo ni kwamba taharifa aliyosema hawataipokea wameipokea.
 
Jobnduga amemwita CAG wetu "mbwa"
Je,Hii kauli ni kweli?
Yani Mtaalam msumi na Mtu mwadilifu kama Prof.Assad, bila aibu kabisa Jobnduga anamfananisha na Mbwa??

Sasa spika atuombe radhi watanzania wote waadilifu waislam na wakristo na wale wasio na dini kwa kumfananisha na mbwa CAG aliyeweka rekodi dunia nzima kwa uadilifu.

Spika alishakataa kufanya kazi na wananchi pale alipokubali Bunge lisionekane kwa wananchi hata hivyo hatukumtukana kama anavyomtukana CAG bila aibu.

Watanzania tusiwakubali kabisa wale wote wanaotumiwa na Wezi na mafisadi kuficha maovu kupitia bunge.
 
Mhe Ndugai kila unapojaribu kueleza maoni yako dhidi ya CAG Prof Assad ukiamini wewe ndiye mmiliki wa busara na ustaarabu hapa Tz, ndivyo unavyozidi kulidhalilisha bunge na kudhihirisha bila ya shaka UDHAIFU wako kama Job (that's your personality - kumbuka kisa cha fimbo ulizomtwanga mshindani wako huko jimboni) ambao unapelekea na taasisi unayoiongoza, Bunge, kuonekana DHAIFU. Wakati mwingine kukaa kimya yaweza kuwa busara kuliko kufokafoka!

 
Angejiuzuru yeye ili asifanye kazi na ASSAD
Spika wa Bunge Job Ndugai, leo Aprili 14 atazungumza na waandishi wa habari jambo muhimu kuhusu bunge.

Mazungumzo hayo yatafanyika katika ofisi ndogo ya bunge jijini Dar es salaam majira ya saa sita na nusu mchana.


=====

UPDATES:

View attachment 1071319

=> Spika Ndugai: CAG anaposema mbele ya umma kuwa ataendelea kutuita 'dhaifu' wakati ni jina ambalo hatulipendi na tumelikataa, tunashindwa kumuelewa kama analipenda sana ajiite yeye. Sasa kusema unaendelea kutumia endelea na nitakuita tena na safari hii itakuwa mbaya zaidi"

=> Spika Ndugai: "Namwambia ndugu yangu Prof. Assad hilo neno aliache, sisi taarifa tumeipata na tutaifanyia kazi. Msisitizo wetu ni mmoja, kwakuwa bunge lilishapitisha uamuzi wa kutofanya kazi na Prof. Assad ni uamuzi halali"


=> Spika Ndugai: "Sina chuki binafsi na Prof. Assad, yule ni ndugu yangu na ni mtanzania mwenzangu tatizo ni lugha anayoitumia na nisinhependa itufikishe hapa kama taifa."

=> Spika Ndugai: "Tunataka tumuoneshe Prof. Assad kuwa Bunge halichezewi, simuelekezi kazi ila anatakiwa ajiongeze kama ni kujiuzulu au laaa!. Maana tushamwambia hatumtaki, anavyoendelea kubaki ofisini ni kumpa tu wakati mgumu Rais

=> Spika Ndugai: Zipo njia za kumaliza mambo kama haya, mojawapo aende kwa Rais akajieleze kwamba mimi nimepima nimeona nimekosea hapa na pale. Maana Rais ni sehemu yetu sisi (Bunge) hatuwezi kupitisha sheria bila yeye kupitisha mkono wake,

=> Spika wa Bunge Mh. Job Ndugai amewahakikishia watanzania kuwa bunge linaendelea vizuri na kazi yake ya kutunga sheria, uwakilishi, kuisimamia Serikali pamoja na mipango ya nchi ikiwemo suala la bajeti ambalo linaendelea bungeni.

=> Spika Ndugai:“Sasa kumekuwa na ufafanuzi usiokuwa sawa sawa, kilichowekwa mezani ni ‘Audit Queries’ …kilichowekwa mezani sio ukweli wenyewe kwamba aliyetajwa mule sasa huyo mwizi… ‘Audit queries’ zile zikishawekwa mezani kazi yetu ni kuwaita mezani na kuwasikiliza

=> Spika Ndugai:Tunataka tumuoneshe Prof. Assad kuwa Bunge halichezewi, simuelekezi kazi ila anatakiwa ajiongeze kama ni kujiuzulu au la! maana tushamwambia hatumtaki, anavyoendelea kubaki ofisini ni kumpa tu wakati mgumu Rais

=> Spika Ndugai:Hatuna tatizo na ripoti ya CAG…tatizo letu ni maneno ambayo Profesa Mussa Juma Assad ameyatoa akiwa Marekani, na alipoita waandishi akarudia tena, maneno yale sie tumeyakataa sio ya kistaarabu.

=> Spika Ndugai:Sisi kama Bunge hatutaki hilo neno dhaifu, kwa sababu Bunge kama Bunge halifanyiwi tathmini na ofisi ya CAG ila wanaofanyiwa tathmini ni watendaji wa Ofisi hiyo hivyo hawakupaswa kudhihakiwa na lugha hiyo inayotajwa kuwa ya kihasibu.

=> Spika Ndugai: “Hata katika maisha ya kawaida, we unamuita mtu jina flani, anakwambia bwana tafadhali jina hili silipendi, lakini unaendelea kumuita na kuahidi utaendelea kulitumia, ni ustaarabu duniani?”

=> Spika Ndugai: “Katika kutekeleza majukumu yake #CAG hakupaswa na hapaswi kulitukana #Bunge kwa lugha zile za rejareja. Bunge huangalia taratibu zake na kuendesha mambo yake kufuatana na kanuni za Bunge…lile Bunge lenyewe hawezi kulikagua”

=> Spika Ndugai: Hatuna tatizo na ripoti ya CAG…tatizo letu ni maneno ambayo Profesa Mussa Juma Assad ameyatoa akiwa Marekani, na alipoita waandishi akarudia tena, maneno yale sie tumeyakataa sio ya kistaarabu.

=> Spika Ndugai: “Sasa kumekuwa na ufafanuzi usiokuwa sawa sawa, kilichowekwa mezani ni ‘Audit Queries’ …kilichowekwa mezani sio ukweli wenyewe kwamba aliyetajwa mule sasa huyo mwizi… ‘Audit queries’ zile zikishawekwa mezani kazi yetu ni kuwaita mezani na kuwasikiliza”

"Nilipokuwa sipo kuna mambo mengi yamezungumzwa, na mengine yameandikwa kuhusu Ripoti ya CAG. Nitakapokuwa Dodoma nitaagiza ripoti ipelekwe kwenye kamati za PAC na LAC"




Zaidi soma.....

Dar es Salaam. Spika wa Bunge la Tanzania, Job Ndugai amemshauri Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), Profesa Mussa Assad akamwone Rais John Magufuli ili mzozo wake na Bunge uishe.

Kauli ya Spika inakuja wakati tayari Bunge limeshapitisha azimio la kutofanya kazi na Profesa Assad bali ofisi ya CAG.

Spika Ndugai aliyekuwa ziarani nchini Sweden wiki iliyopita ameyasema hayo leo Jumapili Aprili 14, 2019 akieleza kusikitishwa na hatua ya Profesa Assad kurudia neno udhaifu kwa Bunge alipotoa taarifa yake hivi karibuni.

"Zipo njia za kumaliza mambo kama haya, mojawapo aende kwa Rais akajieleze kwamba mimi nimepima nimeona nimekosea hapa na pale. Maana Rais ni sehemu yetu sisi (Bunge) hatuwezi kupitisha sheria bila yeye kupitisha mkono wake," alisema Ndugai.

Ameongeza kuwa hata bajeti inayojadiliwa na Bunge lazima ipitishwe na Rais. Amesema kwa kuwa Bunge limeshapitisha azimio la kutofanya kazi na Profesa Mussa Assad alitakiwa ajiuzulu.

"Kwa kuwa Bunge likishaaamua kuwa halifanyi kazi na mtu, ni uamuzi halali. Katika nchi zote Bunge likishakosa imani na wewe unajiuzulu," amesema.

Ameongeza, "Sasa hatumfundishi kazi Mussa Assad, anampa wakati mgumu Rais tu. Tutafanya kazi na ofisi ya wananchi."

Spika Ndugai amemsifu Profesa Assad kwa ujasiri wake huku akiufananisha na ujasiri wa mbwa kumtukana mtu anayemlisha.

"Unatukana hadi mkono unaokulisha, inahitaji ujasiri na jamaa ana ujasiri. Ila ni ujasiri ule wa mbwa anayemtukana anayemlisha," amesema.

Hata hivyo, Ndugai amesema hana chuki binafsi na Assad bali tatizo ni lugha tu aliyotumia ya kuliita Bunge dhaifu.
 
  1. Profesa aliapa kutimiza majukumu yake kwa kufuata katiba ya nchi siyo kwa kufuata Ndugai au mtu yeyote anataka nini
  2. Profesa akikubali kujiuzulu kwa kushinikizwa maana yake ameshindwa kutimiza kiapo chake.
  3. Profesa lazima atambue kuwa hakutakiwa kujiuzulu kwa sababu kalidharau bunge, bali wanataka ajiuzulu kwa sababu anafanya kazi yake vizuri na wanachukia hilo.
  4. Profesa lazima ajue kuwa ana dhima ya kulinda uhuru wa ofisi ya CAG kwa ajili ya kizazi hiki na kijacho, Akikubali kuwapa wanachotaka basi ataweka precedence ya kudhoofisha ofisi ya CAG, Profesa asikubali kuweka precendence ya ofisi ya CAG kukanyagwakanyagwa. Asikubali kujiuzulu
  5. Namshauri Profesa awe Makini na Masheikh na Wazee wazito wazto watakaotumwa kumlainisha, asikubali katakata kwa sababu alipoapa kulinda Katiba pengine haohao ndo walimsomea dua, Leo asikubali maneno ya kumlainisha eti aachie, aachie kwa nini?
  6. Profesa lazima ajue, Cheo cha CAG kilitungiwa sheria maalum ya kukilinda kwenye katiba kwa sababu watu wenye busara walijua kuwa ipo siku mgongano kama huu utatokea pindi CAG akifanya kazi yake kwelikweli, Sasa ni Jukumu la CAG kulinda tunu hii ya hadhi ya ofisi yake kwa ajili ya faida ya nchi yetu leo, kesho na keshokutwa.
  7. Nimalizie kwa kumkumbusha CAG aya ya Qur'an inayosema kuwa usiwatii wanaopinga ukweli na wanafiki bali Mtegemee Mwenyezi Mungu peke yake!
  8. CAG akikubali kujiuzulu maana yake ni kwamba anakiri kuwa kalitukana bunge wakati hajalitukana na hivyo anajutia ndo maana akajiuzulu hii inaweza kutafsiriwa kuwa kavunja sheria ya maadili ya umma na inaweza kumletea shida mbele kwa sababu hawa watu wana visasi.
  9. TAFADHALI CAG ULIAPA KULINDA KATIBA, NA UKAOMBA MWENYEZI MUNGU AKUSAIDIE, USIKUBALI KUVUNJA KIAPO CHAKO KWA SABABU YA WATU WENYE HILA, SIMAMIA UKWELI NA USIKUBALI WAZEE WATAKAOTUMWA KWAKO KUKULAINISHA!.
 
Wasitupotezee muda hapa yaonekana Hon Speaker anataka kuwasha moto wala si kutikisha kiberiti.
Nyuma yake ana wafuasi wa kijani wanaotaka CAG ajiuzuru au afukuzwe.
Kulikuwa kuna umuhimu gani wa kuvihutubia vyombo vya habari kama mmeishaamua kumsusia sisi tutawasaidia nini?
Wakumuuliza ni Jaji Mkui,Mwanasheria Mkuu,Waziri Mkuu,Makamu wa Raisi,na Raisi Mwenyewe.Kwani nyote mpo chama tawala.
Ikishindikana raisi avunje bunge tuanze upya.
 
Press conference ya Leo imethibitisha pasi na shaka udhaifu wa Bunge

Leo Ndugai katumia muda Mwingi kuibeza report ya CAG badala ya kutumia report hiyo kuihoji Serikali

Anaposema zile ni audit query tu na sio kuwa kuna ubadhirfu maana yake ameanza kufanya kazi ya kujibu hoja za serikali badala ya kuachia watu wa Serikali kufanya kazi hiyo

Yaani DPP unaletewa mashtaka na Polisi na wewe unaanza kutetea mtuhumiwa badala ya kuacha mtuhumiwa kujitetea mwenyewe

Prof Assad to the extent ninavyomfahamu yupo radhi kutokuwa CAG kwa namna yoyote ile kuliko kukanusha Ukweli anaouamini
Hata mimi nimeshangaa sana yule DHAIFU kuwa upande wa ku.Defence as if yeye ni serikali.

Kweli leo ule udhaifu wake amejipambanua vizuri sana,press ya leo amethibitisha udhaifu wake kabisa.

Siku za nyuma,viongozi kibao walitimuliwa nafasi zao kwa hizo hizo ambazo anaziita "audit queries",lakini leo haona umuhimu wa govt kuwajibika due to shortcoming that raised in CAG report,huyu jamaa ni waajabu sana.

Huyu ******* anaongea as if hajui jinsi CAG anavyofanya kazi zake, hajui kama CAG anawapata nafasi ya kujibu hoja wakaguliwa wote ndani ya muda husika then ndio report inaandikwa according to majibu waliyotoa,lakini huyu ******* anatoa reasoning ya kitoto. Huyu jamaa ni DHAIFU SANA SANA. Kwakweli MAGU ametuletea SPIKA kituko mwaka huu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ni kwamba ,hii ligi inachezwa kwa ustadi sana,report ya cag rais ni dhaifu,unategemea nini?

Lilikua suala dogo sana ,excuse me,maisha yanaendelea ,sasa wapambe ndio wanaoendesha mkote,wakati uhanga wao uko kwa mbali sana


Sent using Jamii Forums mobile app

Naomba kuuliza, nj wapi CAG alisema rais ni dhaifu. Kwa kumbukumbu zangu huyu mdhibiti jibu lake kwa bunge ni dhaifu ni kwa mantiki kwamba, anaibua madudu, anatoa mapendekezo ambayo bunge kama bunge (i mean parliament) hapo rais hawi sehemu ya bunge, na siyo (general assembly) hawayafanyii kazi na kila mwaka yanajirudia na kuongezeka. So bunge linakuwa halitimizi wajibu wake wa kuisimamia serikali na kuhakikisha fedha za walipa kodi zinatumilka km ilivyokusudiwa, huu automatically ni udhaifu katika utendaji wa kazi, ndo maana ufisaidi hauishi. Bunge lingekuwa imara na lingesimama kama lenyewe basi leo tusingekuwa tunajadili haya. Wabadilike, wawatumikie wanainchi kama walivyoomba ridhaaa na si kutumikia matumbo yao au kumfurahisha bwana mkubwa.

CAG hajasema popote kuwa rais ni dhaifu, wasitafute pa kutokea wajadili ripoti waifanyie kazi. Tunataka maisha bora.
 
Leo naona amethibitisha kuwa Raisi ni sehemu yao na ndio maana anawacontrol, Kikatiba Raisi ni kitengo kinajitegemea hakina ushoga na Bunge zaidi ya kuletewa sheria na kuona kama ziko vibaya rudisha huko sita sign hizi wakarekebishe.
NCHI WAMEPEWA WASHAMBA KAZI TUNAYO.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Yaani CAG akijiuzulu tu imekula kwake mazimaaaaa. Ashikilie hapo hapo watatuliza boli tu, kinachowauma hawawezi kumtumbua kwa jinsi wanavyotaka wao. Serikali imefanya matumizi mangapi kinyume na bajeti iliyopitishwa na Bunge? Sijasikia hata siku moja Bunge likiikemea serikali alafu wanagoma kuitwa dhaifu wakati ni sifa yao

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hili ni fumbo kubwa sana katika sakata hili la Spika vs Assad.
Kilichobaki ni moja kati ya mawili.

yaani Assad aombe radhi au ajiuzulu ili kudiffuse mgogoro huu ambao naweza kusema aliuanzisha.
 
Kwani kila siku ukiangalia live kuapishwa watu na ziara mbalimbali inakuongezea nini ktk familia yako?
Hakuniongezei kitu. Vipi we kunakuongezea nn?

We think too small, like the frog at the bottom of the well. He thinks the sky is only as big as the top of the well. If he surfaced, he would have an entirely different view.
 
Back
Top Bottom