Somo la Hisabati bado ni changamoto

zandrano

JF-Expert Member
Jan 24, 2017
7,136
7,711
Pamoja na matokeo ya kidato cha 4 kuongezeka ufaulu, kidato cha 2 na darasa la 4 kwa mujibu wa taarifa/ripoti ya Baraza la Elimu Tanzania limesema kuwa bado ufaulu wa Somo la Hisabati uko chini sana.

Nimekuwa nikijiuliza sana tatizo ni nini lkn majibu yamekuwa yalitolewa na wadau wa elimu ni yaleyale kila mwaka eti;

1. Mtazamo wa wanafunzi kudhani kuwa somo lenyewe la Hisabati ni gumu.

2. Ukosefu wa walimu weledi n.k

Sababu hizo zimekuwa zikitolewa miaka nenda miaka rudi, nadhani tangu tumepata uhuru sababu ni hizohizo!

Kwanini NECTA isifanye utafiti ikaja na majibu sahihi ya tatizo hili? kuliko kila mwaka wanatuambia ufaulu wa somo la Hisabati uko chini!!

Wataalamu wamejazana Wizarani/Idara ya Elimu.

Inawezekana ikawa sababu sio hizo inawezekana ikawa mitihani inayo tungwa ni migumu sana, au siyo standard, hayo yote tutayajua tu endapo tutafanya utafiti na tukaja na ufumbuzi.

Tuanze kwenye Shule za Msingi, maana hapo ndipo tatizo linapo anzia.
Msingi mbovu.

Kwa maoni yangu Somo la Hisabati sio Gumu.
 
Hisabati sio ngumu ila walimu wa hisabati wengi ni wa kuunga unga. Yaani nao ni wa kukariri na wametoka kwenye mfumo huu wenye uzalishaji mbovu wa wanahisabati
 
Unakuta wale wabobezi waliosoma hisabati hadi vyuo vikuu hata wakafanikiwa kupata Pihechidii zao, mwishowe wanakimbilia SIASANI. ^Tar-tea-zo^ linaanzia hapo!
 
ukijua hisabu, +-*/, inatosha

hisabati haina application in real life, zaidi ya kuumizana vichwa tu uko utopoloni
 
Tanzania hatuna Baraza la Elimu, kwa hiyo umepewa taarifa feki, maana hakuna baraza kama hilo. Umeingizwa chaka kijana!
 
Hisabati sio ngumu ila walimu wa hisabati wengi ni wa kuunga unga. Yaani nao ni wa kukariri na wametoka kwenye mfumo huu wenye uzalishaji mbovu wa wanahisabati
Kwa nini walimu wawe wa kuunga unga kwa hisabati tu na isiwe masomo mengine. Hii inadhihirisha kuwa hisabati ni ngumu!
 
Walimu wenyewe wanatandika huko shule za kata Kama wanapiga wanyama bana,nilikuta vijana wanatandikwa kwa mstari Yani kila mwalimu hata wa kiswahili anapita na fimbo mbilimbili za miguuni kwa kila mwanafunz aliyepata "F" testi ya math.
 
asilimia 89% ya wanafunzi wa Darasa la 7 wafeli HISABATI katika mitihani yao ya Taifa 2021

1.Kuna tatizo la ukosefu wa wataalamu walio bobea ktk somo la Hisabati.

2. Baraza la mitihani linatunga mitihani ya kuwafelisha wanafunzi?
maana haiwezekani watoto wafundishwe halafu wafeli somo la Hisabati kisha masomo mengine wafaulu.
NECTA wanapaswa wajitafakari.
 
asilimia 89% ya wanafunzi wa Darasa la 7 wafeli HISABATI katika mitihani yao ya Taifa 2021

1.Kuna tatizo la ukosefu wa wataalamu walio bobea ktk somo la Hisabati.

2. Baraza la mitihani linatunga mitihani ya kuwafelisha wanafunzi?
maana haiwezekani watoto wafundishwe halafu wafeli somo la Hisabati kisha masomo mengine wafaulu.
NECTA wanapaswa wajitafakari.
Duh. Hiyo ni karibia na asilimia 90 !
Wanafunzi waongeze jitihada zaidi.
Walezi pia wajitahidi.
 
Walimu wenyewe wanatandika huko shule za kata Kama wanapiga wanyama bana,nilikuta vijana wanatandikwa kwa mstari Yani kila mwalimu hata wa kiswahili anapita na fimbo mbilimbili za miguuni kwa kila mwanafunz aliyepata "F" testi ya math.
Wapi huko?
Kwani bado wanatumia fimbo wakati kuna uwezo wa kutumia mbinu tofautinza ufundishaji kusaidia wanafunzi waliopata F?
 
Hisabati sio ngumu ila walimu wa hisabati wengi ni wa kuunga unga. Yaani nao ni wa kukariri na wametoka kwenye mfumo huu wenye uzalishaji mbovu wa wanahisabati
Walimu wazuri wapo wengi.
Ila sio wote. Na hii ni kwa masomo yote.
Pia staili tofauti kwa watu tofauti kwenye ueleweshaji, na uelewa.
Kuna sehemu nyingi zinazotoa staili za ufundishaji tofauti.
 
Back
Top Bottom