Strategist7
JF-Expert Member
- Sep 9, 2024
- 315
- 531
Siyo kwamba wanawake wa hivyo wote wana roho mabaya. Kujisahau, mazoea mabaya kama kuweka simu silence, kukaa mbali na simu etc ni baadhi ya sababu common zinazo wafanya some women wawe useless pale wanapohitajika na waume zao halafu wakawa hawapatikani. Halafu sasa hapohapo ndo unakuta mtu kama mchepuko yupo available kukusaidia.Wewe na rafiki yako mmeoa wanawake wenye roho mbaya. Jirani tu nikisikia amepata ajali huwa nakimbia chaap nikajue kulikoni sembuse mume ambaye ni baba wa wanangu ndio nichukue masaa yote hayo na pesa ipo?
Wanaume wengi mmeoa mashetani bila kujijua. Kuna mahali macho yaliwadanganya mkafanya maamuzi ya maisha na watu wasio sahihi.
Yes unapaswa kukataa kupokea msaada kutoka kwa mtu anayeweza kukuharibia ndoa unayoithamini. But kuna mazingira huwezi. Mfano: ajali. Upo mahututi, unasaidiwa. Unakuja kuzinduka unakuta aliyekuokoa ni ex mcheps tena yupo hapoo pembeni yako bado anafuatilia hali yako. Mke wako hayupo. Kisa kapigiwa simuu wee hapokei.
Mtoa mada katoa mfano halisi wa kuumwa, kukamatwa na police. Sasa imagine ghafla umeswekwa jela. Anakuja askari ndani anakuambia jiandae kutoka umewekewa dhamana. Unatoka nje unakutana na mchepuko ndo kakuwekea dhamana. Hapo ni hakuna ubishi, ni kwamba ni umesaidiwa na mchepuko. Kwamba kwanini una mchepuko ni suala jingine kabisaa.