econonist
JF-Expert Member
- Jul 11, 2015
- 23,985
- 37,371
EAC ilikuwa ile ya nchi tatu,huu kwa sasa ni utopolo.
Kweli. Imekuwa kokoro linabeba kila uchafu.
EAC ilikuwa ile ya nchi tatu,huu kwa sasa ni utopolo.
Wanazidi kuyakaribisha magaidi sebuleni!!
Mkutano wa Wakuu wa Nchi Wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) uliofanyika Jijini Arusha nchini Tanzania, umeridhia Nchi ya Somalia kujiunga na EAC na sasa inakuwa Mwanachama wa nane wa Jumuiya hiyo.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki January Makamba ni miongoni mwa Viongozi waliotoa pongezi za awali kabisa kwa Somalia kuridhiwa kuwa Mwanachama mpya wa EAC ambapo ameitakia kheri Somalia katika kuielewa na kuiishi pamoja na kuitekeleza misingi ya EAC na itifaki zake katika kukuza na kuendeleza Jumuiya hiyo.
Katika hatua nyingine mkutano huo pia umemtangaza Rais wa Sudan, Salva Kiir Mayardit kuwa Mwenyekiti mpya wa Jumuiya ya Afrika Mashariki.
Itakumbukwa katika mkutano kama huo mwaka jana aliyekuwa Rais wa Kenya na Mwenyekiti wa Jumuiya hiyo wakati huo, Uhuru Kenyatta alitangaza rasmi Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) kujiunga na EAC.
Waliweka kigezo/sharti la ajabu sana, eti nchi yoyote ilipakana na mwanachama wa EAC anaruhusiwa kuomba uanachama. Nionavyo mimi ipo siku hata Ghana utakuta ni mwanachama wa EAC.
Kuna watu wana uzuzu wa kuzaliwa, hata usishangaeKwamba yeye ndo kaamua somalia ijiunge na EAC,njaa mbaya,muwe mnakul kabla ya kukoment
Hata sielewagi malengo ya hii jumuia, lol
Wewe ndo mpumbavu tena sana. Unajua kama Somalia ilikuwa mpatanishi wa mgogoro wa Tanzania na Uganda chini ya Rais Siad Barre? Kabla ya vita ya Kagera nchi ya Somalia ilipambana kupatanisha ili kuepusha vita. Somalia kinachowagharimu ni koo zao kutoelewana.Ujinga na upumbavu tu kuingiza Somalia EAC
Sisi Wananchi wa kawaida tuanze kuingiliana kuzoeana na kuoana viongozi wao wako bize na Chaguzi.Shida ya hii jumuiya imejifungia kwa Viongozi pekee. Wananchi hawahusishwi ipasavyo.
Kwani malengo ya EAC ni yepi?
Sidhani mkuuHofu yangu ni Majahazi yaliyojaa Wasomali na Bunduki likatie nanga Zanzibar😂 kabla ya Uchaguzi ujao chuki iliyopo Zanzibar inahitaji Spark ndogo tu Kisiwa kinarudi kwa wenyewe🫡
Tukishakuwa na soko la pamoja na sarafu moja Kwa jumuia za kikanda kama EAC tutakuwa tumefika mahali pazuri,jumuia kama umoja wa ulaya Wana sarafu Yao,inayokubalika nchi zote katika jumuia,ukija hapa kwetu Kila mtu ana sarafu yake,Hali hii inadhoofisha biashara miongoni mwa nchi wanachana.
Sent using Jamii Forums mobile app
Kweli kabisa. Maana hata Sudan ya akina Burhani inataka kuomba uanachama. Ila ndio integration inayopiga kazi.
Hio sarafu sijui itaitwaje? Pendekezeni majina.Nadhani walikubaliana mwaka 2024 ndio ipatikane sarafu ya pamoja. Ila naona wamesogeza mbele upatikanaji wa hiyo sarafu ya pamoja.
Mkuu mbona Wasomali zamani walikuwa wakivaa mavazi ya Kiafrika lakini siku hizi Makanzu kanzu na Mabaibui kama Waarabu ni kwanini au wameshindwa kupambana na Arabization of African Peoples?Wasomali wanauwana
Somalia inapakana na Kenya na hivyo kuwa na maingiliano ya moja kwa moja na EAC.... DRC vivyo hivyo.Kijiografia Somalia na Kongo DRC ziko Afrika ya Mashariki kweli?
Mkuu naona ni dini na kujistiri nakumbuka nilienda huko miaka ya nyuma nilikuta wanavaa hivyo ila sasa maisha yako tofauti na wanawake pia walikuwa wanavaa kama half naked ila wengi wanajistiri sasa na sio mbaya kuficha mwili kwa mwanamkeMkuu mbona Wasomali zamani walikuwa wakivaa mavazi ya Kiafrika lakini siku hizi Makanzu kanzu na Mabaibui kama Waarabu ni kwanini au wameshindwa kupambana na Arabization?
View attachment 2823803
Mimi nitakujibu kwa mtizamo wangu, na siyo lazima iwe hivyo:Kwani malengo ya EAC ni yepi?