Soko la SIDO (Mwanjelwa - MBEYA) linateketea kwa moto sasa hivi

kuna mama mmoja alikuwa anataka kuokoa pesa kwenye kiduka chake, kwa bahati mbaya akaangusha mtoto na huyo mtoto akafa.
 
Watanzania tujifunze kuwa wasafi na kujenga kwa mpangilio. Ukisikia soko siyo maana yake uchafu, lakini ndivyo ilivyo na hasa soko la Mbeya.
 
mkuu hii ni mara ya 15 masoko yanaungua mbeya katika kipindi cha miaka kama 10 hivi, soko la mwanjelwa hii ni mara ya tatu linaungua, soko kuu uhindini limewahi kuungua zaidi ya mara 4, soko matola limewahi kuungua zaidi ya mara 2, wakati soko la mbalizi limewahi kuungua mara 2 ndani ya mwezi mmoja miaka ya mwanzoni mwa 2000, kuna soko la ipinda pia liliwahi kuungua.

Mbaya zaidi matukio yote haya inasemekana yanasababishwa na hitilafu za umeme. Mimi nina mashaka sana na sababu kama hizi, naomba mamlaka husika zifanye uchunguzi wa kina juu ya sababu ya masoko ya mbeya kuungua moto.

Kwa taarifa yenu wana jf, hili soko la sido linaloungua hizi sasa ni soko lililoanzishwa mwaka juzi baada ya soko la mwanjelwa kuungua na hivyo manispaa kuamua kulijenga upya. Kwa hivyo kwa sasa hapa mbeya masoko makubwa mawili yamefungwa na yako kwenye matengenezo makubwa baada ya kuungua kwa moto.

Nawaonea huruma wafanyabiashara ambao kila mwaka wanapata hasara. Uwezi amini kinachotokea hapa sokoni sasa hivi....

nini matokeo ya uchungunzi? Haiwezekani kila mwaka likiungua inaundwa kamati halafu mapendokezo yake yanaonekana kama yanachochea moto mwingine.
 
Ikiwa ni takiribani miezi 9 sasa tangu soko la Uhindini liungue kwa moto leo tena majira ya saa 3 asubuhi soko ambalo wafanya biashara walio unguliwa na soko la Mwanjelwa walihamishiwa nalo limeteketea kwa moto kama kawaida ya masoko ya Mbeya. Hili ni soko la tatu kuungua kwa moto hapa Mbeya
 
Soko la SIDO liliko Mwanjelwa limeteketea kwa moto leo majira ya saa 3 asubuhi hili ni soko walikopelekwa wahanga walio unguliwa na soko la Mwanjelwa. Ikumbukwe kuwa soko hili lina ungua ikiwa ni takribani miezi 9 tu tangu soko la uhindini nalo liteketee kwa moto

hadi sasa hili ni soko la tatu kuungua kwa moto na wafanyabiashara wazidi kuwa maskini !!!!!
 
Siwezi kushangaa kuwa kila siku watu walikuwa wanapita na kusema "unajua hapa pakija kushika moto!" halafu wanacheka kwa kusema "temea mate pembeni". Watu bila ya shaka walikuwa wanaombea moto usije kuunga hilo soko. Na sasa hivi wapo wengine ambao wanaamini kabisa kuwa ni "kazi ya Mungu". Alimradi mduara wa faraja za uongo unazidi kuwa na wachezaji wengi.
 
Back
Top Bottom