Soko la Kariakoo: Moja ya Ngome za TANU 1955

Mohamed Said

JF-Expert Member
Nov 2, 2008
20,916
30,259
Ndugu yangu Kheri katufanyia hisani kubwa sana.

Kaniletea picha hizi za Kariakoo Market na aliyepiga picha hizi kaweka na tarehe mwaka wa 1955.

Huu ndiyo mwaka TANU ilimsafirisha Mwalimu Nyerere kwenda UNO kuidai Tanganyika.

Angalia hizi picha za soko lenyewe kama jengo kisha inamisha macho yako uwaangalie wafanyabiashara ndani ya soko pamoja na wanunuzi.

Kisha geuza macho yako nje ya soko uangalie maduka jirani ya soko.

Ukimaliza haya yote utakuwa umepata picha kamili ya hali za Watanganyika.

Nje ya soko utakuwa umewaona watu wanatembea miguu peku peku, hawana viatu.

Watu hawa uliokutananao ndani na nje ya soko ndiyo waliokuwa wanachama wa mwanzo wa TANU na wengine bila shaka walinunua kadi zao pale sokoni kwenye himaya ya Market Master Abdulwahid Kleist Sykes na wasaidizi wake wawili, Shariff Abdallah Omar Attas na Mshume Kiyate.

Screenshot_20211019-180109_Facebook.jpg
 
Nimeangalia wengi ni waislam, Hakuna mkristo hapo sokoni kabisa

Naona barakashia tu hapo sokoni

Mkoloni hakuwa mtu mzuri kabisa hasa mwingereza, Aliamua kuwatenga waislam kabisa na kuwapa soko Lao la kariakoo.

Kingine nilichoona, ni watu hawana viatu, Ishara ya Umaskini uliotopea kabisa yaani kwisha habari kabisa watu weusi

Nina maswali kadhaa:
Je, Kama Dar es Salaam kulikuwa na waislam tu mbona kanisa la St Joseph la katoliki hapo mjini Posta baharini lilianza kujengwa mwaka 1898 na kumalizika mwaka 1908 huku watu wakisali weusi. Hao watu wanaosali walitokea wapi mwaka huo?

Je, Unataka kusema Posta waliishi wakristo weusi na Gavana wao, Halafu kariakoo na magomeni waliishi waislam weusi tu

Je, Gavana wa Tanzania mwaka huo na wakristo soko Lao lilikuwa sehemu gani. Wasaidizi wengi wa Gavana walikuwa wakristo hapo Dar es Salaam na wao walitokea wapi?

Je, kama waislam walikuwa wengi hapo kariakoo hivyo mbona Dar es Salaam hakuna shule yeyote kubwa na maarufu inayofanya vizuri ya kiislam.

Je, Imekuaje soko la kariakoo sasa linamilikiwa na kabila dogo kabisa la wakinga. Wakinga ndio wanaendesha biashara kariakoo sasa, Kila duka unakutana na vijana toka Makete huko wakinga, Na wakinga hawavai barakashia.

Sent from my INE-LX2 using JamiiForums mobile app
 
Nimeangalia wengi ni waislam, Hakuna mkristo hapo sokoni kabisa

Naona barakashia tu hapo sokoni...

Sent from my INE-LX2 using JamiiForums mobile app
Gussie,
Mswali haya ungewauliza Waingereza.

Ukawauliza, ''Ilikuwaje Waislam ndiyo waliokupingeni sana hadi kukutoeni Tanganyika mliwaudhi kitu gani?''

Naamini wanayo majibu.
Kuelekeza maswali hayo kwangu si mahali pake.

Ukipenda unaweza pia kuwauliza CCM vipi mliandika historia ya TANU mkawasahau wazalendo wenyewe akina Sykes, Mwapachu, Sheikh Hassan bin Ameir, Sheikh Mohamed Yusuf Badi, Ali Migeyo, Sheikh Suleiman Takadir, Sheikh Abdallah Rashid Sembe kwa kuwataja wachache.

Unaweza pia kuwauliza Wajerumani, ''Ilikuwaje mliwanyonga majemadari zaidi ya 60 Waislam, akina Abdulrauf Songea Mbano, Khadija Mkomanile kuwataja wachache walioongoza Vita Vya Maji Maji.

Ugomvi wenu ulikuwa nini?''

Maswali yako mengi lakini hebu anza na hayo kwanza.

Hili la shule kubwa na hakuna shule inayofanya vizuri nitakupa rejea usome kwani si swali jepesi:

(1989)

Utakutana na mambo muhimu sana katika historia ya Waislam wa Tanganyika:

First Muslim Congress 1962.
Second Muslim Congress 1963.

Agenda ya Congress hizi zote mbili ilikuwa ELIMU.

Ugomvi ndani ya Halmashauri Kuu ya TANU kati ya Julius Nyerere na Bi. Titi Mohamed kuhusu EAMWS 1963.

Nasaa za Bilal Rehani Waikela kwa Nyerere uso na macho kwenye mkutano wa mwaka wa EAMWS 1963.

Haijapatapo kutokea katika historia ya nchi yetu hadi leo.
Ilikuwa kidole na jicho.

Kuzuiwa kwa EAMWS kujenga shule na Chuo Kikuu na kuvunjwa kwa EAMWS na serikali kuunda BAKWATA na ugomvi kati ya Julius Nyerere upande wa serikali na Bi. Titi Mohamed na Tewa Said Tewa upande wa EAMWS mwaka wa 1968.

Kufukuzwa TanganyIka Mufti Sheikh Hassan bin Ameir nk. nk.

Usifanye haraka ya kurejea kwangu kwa mjadala.
Soma kwanza uelewa historia ya Waislam ya kupigania uhuru na baada ya uhuru kupatikana 1961.

Umesoma kitabu cha Abdul Sykes?
Hayo yote nimeyaandika katika kitabu hicho hapo chini.

Kipo sokoni mwaka wa 23 sasa wewe leo unanirejesha nyuma nieleze yale niliyoeleza zaidi ya niaka 30 iliyopita.

Sikulaumu labda hukuwepo au ulikuwa bado mdogo.

Ukisoma kitabu hiki hutamuuliza mtu yeyote kwa nini Waislam wako nyuma ilhali Wengine wanazidi kusonga mbele?

1634661529981.png
 
Gussie,
Mswali haya ungewauliza Waingereza.

Ukawauliza, ''Ilikuwaje Waislam ndiyo waliokupingeni sana hadi kukutoeni Tanganyika mliwaudhi kitu gani?''

Naamini wanayo majibu.
Kuelekeza maswali hayo kwangu si mahali pake.

Ukipenda unaweza pia kuwauliza CCM vipi mliandika historia ya TANU mkawasahau wazalendo wenyewe akina Sykes, Mwapachu, Sheikh Hassan bin Ameir, Sheikh Mohamed Yusuf Badi, Ali Migeyo, Sheikh Suleiman Takadir, Sheikh Abdallah Rashid Sembe kwa kuwataja wachache.

Unaweza pia kuwauliza Wajerumani, ''Ilikuwaje mliwanyonga majemadari zaidi ya 60 Waislam, akina Abdulrauf Songea Mbano, Khadija Mkomanile kuwataja wachache walioongoza Vita Vya Maji Maji.

Ugomvi wenu ulikuwa nini?''

Maswali yako mengi lakini hebu anza na hayo kwanza.

Hili la shule kubwa na hakuna shule inayofanya vizuri nitakupa rejea usome kwani si swali jepesi:

(1989)

Utakutana na mambo muhimu sana katika historia ya Waislam wa Tanganyika:

First Muslim Congress 1962.
Second Muslim Congress 1963.

Agenda ya Congress hizi zote mbili ilikuwa ELIMU.

Ugomvi ndani ya Halmashauri Kuu ya TANU kati ya Julius Nyerere na Bi. Titi Mohamed kuhusu EAMWS 1963.

Nasaa za Bilal Rehani Waikela kwa Nyerere uso na macho kwenye mkutano wa mwaka wa EAMWS 1963.

Haijapatapo kutokea katika historia ya nchi yetu hadi leo.
Ilikuwa kidole na jicho.

Kuzuiwa kwa EAMWS kujenga shule na Chuo Kikuu na kuvunjwa kwa EAMWS na serikali kuunda BAKWATA na ugomvi kati ya Julius Nyerere upande wa serikali na Bi. Titi Mohamed na Tewa Said Tewa upande wa EAMWS mwaka wa 1968.

Kufukuzwa TanganyIka Mufti Sheikh Hassan bin Ameir nk. nk.

Usifanye haraka ya kurejea kwangu kwa mjadala.
Soma kwanza uelewa historia ya Waislam ya kupigania uhuru na baada ya uhuru kupatikana 1961.

Umesoma kitabu cha Abdul Sykes?
Hayo yote nimeyaandika katika kitabu hicho hapo chini.

Kipo sokoni mwaka wa 23 sasa wewe leo unanirejesha nyuma nieleze yale niliyoeleza zaidi ya niaka 30 iliyopita.

Sikulaumu labda hukuwepo au ulikuwa bado mdogo.

Ukisoma kitabu hiki hutamuuliza mtu yeyote kwa nini Waislam wako nyuma ilhali Wengine wanazidi kusonga mbele?

View attachment 1979897
Mzee M.Said hoja zako huwa zimeshiba...tatizo pekee ni lawama kwa Nyerere kuona aliwaonea Sana waislamu na kuufifisha.Si kweli wenyewe mlifitiniana na kujidhoofisha
 
Mzee M.Said hoja zako huwa zimeshiba...tatizo pekee ni lawama kwa Nyerere kuona aliwaonea Sana waislamu na kuufifisha.Si kweli wenyewe mlifitiniana na kujidhoofisha
Blue...
Umesema kweli na hayo nimeeleza yote na jinsi nguvu nyingine ilivyotumika.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom