Kumbukumbu Katika Ofisi ya TANU ya Miaka ya 1960

Mohamed Said

JF-Expert Member
Nov 2, 2008
20,925
30,273
OFISI YA TANU ILIVYOKUWA MIAKA YA 1960

Kuna mtu kaniletea picha hii ya ofisi ya TANU kama ilivyokuwa katika miaka ya 1960.
Pamoja na picha hiki kaniandikia ujumbe ananambia kuwa picha hii itanikumbusha mengi.

Kweli na hakika picha hii imenirudisha nyuma sana na imenikumbusha mbali katika historia ya TANU na uhuru wa Tanganyika.

Hii nyumba ya kushoto ndiyo ilikuwa ofisi ya African Association na ilijengwa na wanachama wenyewe kwa kujitolea kati ya mwaka wa 1929 na 1933.

Ofisi hii ilikuwa kwenye kona ya Mtaa wa Kariakoo na New Street.

Nyuma ya nyumba hii ilikuwa nyumba ya Bi. Mwamtoro bint Chuma ikipakana ua na ofisi ya TANU.
Nyumba hii ya Bi. Mwamtoro ipo hadi hivi sasa.

Wakati wa kupigania uhuru TANU ilipokuwa inataka kufanya mkutano wa ndani Bi. Mwamtoro alikuwa akivunja ua wake wa makuti kuunganisha ua wa nyumba yake na ua wa TANU ili ipatikane nafasi kubwa.

Ofisi hii ikaja kuwa ofisi ya TAA na ndipo ilipoundwa TANU mwaka wa 1954.

Ilivunjwa ofisi ile ya zamani na ikajengwa ofisi hii kwenye picha kabla ya uhuru mwaka wa 1961.
TANU ilipokea uhuru wa Tanganyika ikiwa kwenye ofisi hii.

Mbali na historia hii ya nyumba ya Bi. Mwamtoro picha hii inanikumbusha wanachama wawili shupavu wa TANU waliokuwa wakiishi jirani sana na ofisi ya TANU - Mzee bin Sudi na Iddi Tosiri.

Mzee bin Sudi ni muasisi wa African Association na alipatakuwa President wake.

Mzee bin Sudi alifariki miezi michache baada ya kutoa risala ya kumkaribisha Rais Nimiery wa Sudan alipotembelea ofisi ya TANU akiwa na Mwalimu Nyerere mwaka wa 1972.

Iddi Tosiri kadi yake ya TANU ni No. 25 na alihudhuria mkutano wa kwanza wa TANU mwezi August 1954 uliofanyika Ukumbi wa Arnautoglo.

Mkutano huu ulihudhuriwa na wanachama wasiozidi 20.

Iddi Tosiri na Iddi Faiz ni ndugu na ni binamu kwa Sheikh Mohamed Ramiyya wa Bagamoyo.
Ndugu hawa ndiyo waliomchukua Nyerere hadi Bagamoyo kumtambulisha kwa Sheikh Ramiyya.

Lakini kumbukumbu yangu kubwa nikitazama nyimba hii kuwa ndani ya nyumba hii mwaka wa 1962 TANU walikaa watu wawili, Abdul Sykes na Dr. Klerruu kuandika historia ya TANU.

TANU iliamua kuandika historia yake kutokana na mazungumzo kati ya Julius Nyerere, Abdul Sykes, Dossa Aziz na Mwalimu Kihere.

Kazi ya kuandika historia ya TANU ilianza lakini haikukamilika kama ilivyokusudiwa kuwa itakuwa ni mswada ulioandikwa na watu wawili mmoja, Abdul akiwa anaijua vyema historia hiyo.

Abdul Sykes alijitoa kabla ya mswada kukamilika mswada ukakamilishwa na Dr. Klerruu peke yake.
Mswada haukuchapwa kitabu.

Mswada huu wa Dr. Klerruu hakuna ajuaye ulipo wala hakuna ajuaye kabla ya kujitoa Abdul Sykes na Dr. Klerruu walifika wapi katika kuiandika historia ya TANU.

Picha:
Mzee bin Sudi.
Iddi Tosiri na Mwalimu Nyerere na viongozi wa Tanganyika African Parents Association (TAPA).
Iddi Faiz Mafongo kwa kwanza kushoto, Sheikh Mohamed Ramiyya, Julius Nyerere, Saadani Abdu Kandoro, Haruna Taratibu, Dodoma Railway Station.











All reactions:
8Alick Barack Khameecy, Beberu La Mbegu and 6 others
 
Mzee inatakiwa utambue kuwa kwenye mafanikio yoyote ni lazima Kuna watu wataumia , watateseka na kupambana .
Lakini ni kawaida miongoni mwa hao akatokea Mtu mmoja kuwa shujaa Na kubeba nembo ya utambuzi ya safari ya mafanikio yao .

Mfano halisi tu kwenye timu ya mpira inaposhinda wote hushangilia ushindi bila kujali nani aliupiga mwingi miongoni mwao wachezaji . Tena sisi mashabiki humsifia zaidi mfungaji wa goli la ushindi kuliko aliyetoa assist ya goli Hilo . Nenda pale Simba anaimbwa mfungaji BALEKE lakini Kuna mtu anaitwa KIUNGO PUNDA Wala hatajwi na hanung'uniki . Nenda YANGA alikuwa anaimbwa MAYELE lakini Kuna mtu anaitwa AUCHO Wala haimbwi . Hiyo ni Kwa sababu timu inacheza Ili ISHINDE na ushindi huletwa Kwa MAGOLI so si ajabu kumsifia mfungaji .
Kwa kipindi kile nchi ilikuwa inahitaki kuwa HURU watanganyika na raia wote walikuwa wamechoka kuwa watumwa kuanzia wakati wa MUARABU Hadi MZUNGU . Kwa hiyo Kuna watu iliwabidi waumie . Wateseke na wajitoe Ili lengo lifikiwe . Sasa si ajabu miongoni mwa watu hao mmoja wao kuonekana shujaa .
Ifike hatua mjadara wa Nyerere na wapigania uhuru waliobaki uufunge Mzee wetu.
 
Mzee inatakiwa utambue kuwa kwenye mafanikio yoyote ni lazima Kuna watu wataumia , watateseka na kupambana .
Lakini ni kawaida miongoni mwa hao akatokea Mtu mmoja kuwa shujaa Na kubeba nembo ya utambuzi ya safari ya mafanikio yao .

Mfano halisi tu kwenye timu ya mpira inaposhinda wote hushangilia ushindi bila kujali nani aliupiga mwingi miongoni mwao wachezaji . Tena sisi mashabiki humsifia zaidi mfungaji wa goli la ushindi kuliko aliyetoa assist ya goli Hilo . Nenda pale Simba anaimbwa mfungaji BALEKE lakini Kuna mtu anaitwa KIUNGO PUNDA Wala hatajwi na hanung'uniki . Nenda YANGA alikuwa anaimbwa MAYELE lakini Kuna mtu anaitwa AUCHO Wala haimbwi . Hiyo ni Kwa sababu timu inacheza Ili ISHINDE na ushindi huletwa Kwa MAGOLI so si ajabu kumsifia mfungaji .
Kwa kipindi kile nchi ilikuwa inahitaki kuwa HURU watanganyika na raia wote walikuwa wamechoka kuwa watumwa kuanzia wakati wa MUARABU Hadi MZUNGU . Kwa hiyo Kuna watu iliwabidi waumie . Wateseke na wajitoe Ili lengo lifikiwe . Sasa si ajabu miongoni mwa watu hao mmoja wao kuonekana shujaa .
Ifike hatua mjadara wa Nyerere na wapigania uhuru waliobaki uufunge Mzee wetu.
F9T,
Silalamiki.

Wala huu si mjadala wewe unaita, "mjadara."

Nimeandika historia hii kama njia mojawapo ya kuhifadhi historia ya baba na babu zangu waliopigania uhuru wa Tanganyika.

Historia hii haikupata kuwepo kabisa na laiti kama nisingeiandika ingepotea.

Wala historia hii si ya Julius Nyerere.

Mwalimu Nyerere anaingia na unamsoma pamoja na wazee wangu kwa kuwa ni sehemu ya historia ya wazee wangu.

Mzee bin Sudi alikuwa Rais wa African Association mwaka wa 1934.

Julius Nyerere alikuwa Rais wa TAA 1953.

Ikiwa labda historia hii huipendi njia nyepesi ni kuacha kuisoma lakini usinikataze mimi kuisomesha.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom