Mkesha wa Maulid na Ujio wa Julius Nyerere Kilwa Pande 1955

Mohamed Said

JF-Expert Member
Nov 2, 2008
20,918
30,259
John Iliffe amepata kusema kuwa historia ya TANU nyingi iko katika mikono ya watu.

Hakika maneno haya ni ya kweli wala hayana shaka.

Nimepokea nyaraka nyingi na picha kutoka kwa watu zinazohusu historia ya TANU na historia ya Mwalimu Nyerere kutoka kwa watu na sehemu ambazo sikutegemea kabisa.

Nimepokea simu kutoka kwa rafiki yangu yuko Kilwa Pande ananiambia kakutana na kijana amekaa anaaangalia video yangu moja nazungumzia historia ya uhuru wa Tanganyika.

Huyu ndugu yangu akamfahamisha yule kijana kuwa anamfahamu huyo anaemtazama kwenye hiyo video.

Hivi ndivyo nilivyokutana na huyu kijana akanipa kipande cha historia ya nyumba ya Bi. Mgumba, nyumba ambayo Mwalimu Nyerere alilala mwaka wa 1955 wakati wa kueneza TANU kupigania uhuru wa Tanganyika.

Yule kijana akanirushia picha ya nyumba hiyo na akanipa na simu za mtu ambae yeye alikuwa kijana mdogo kiasi cha miaka 10 wakati Nyerere alipokwenda Kilwa Pande.

Huyu bwana Sheikh Suleiman Mwandu nilimpata na tukafanya mazungimzo.
Nilistarehe na nafsi yangu.

‘’Mimi nilikuwa na umri kiasi cha miaka 10 wakati Nyerere alipokuja Pande wakati wa kupigania uhuru akapokelewa na Bwana Abdul Manafi, baba yake Bi. Mgumba.

Hawa vijana wa leo wanapoieleza ile nyumba aliyolala Mwalimu Nyerere wanasema kalala nyumba ya Bi. Mgumba.

Huyu Bi. Mgumba wakati ule yeye alikuwa mtoto lakini hiki kizazi cha leo wamekuta nyumba ile anakaa Bi. Mgumba kwa kuwa baba yake Abdul Manafi alikuwa keshafariki na Bi. Mgumba ambae jina lake khasa ni Halima bint Abdi Manafi ndiye akiishi nyumba ile.

Aliyempokea Mwalimu Nyerere ni Bwana Abdul Manafi na yeye alikuwa mtu akijiweza akifanya biashara ya duka hapo nyumbani kwake.

Pamoja na yeye walikuwa Khamisi Mamboya, Bakari Suleiman Mtondoo na Suleiman Shaweji ambao baadae walikuja kuwa viongozi wa tawi la TANU hapa Kilwa Pande.

Hii nyumba ambayo unayopicha yake ndiyo khasa nyumba aliyofikia Mwalimu Nyerere lakini ile ilikuwa nyumba ya makuti hii nyumba hivi sasa imeezekwa bati.

Mwalimu Nyerere aliingia na mguu wa kulia Kilwa Pande akitokea Kilwa Masoko na alikuja na boti inayoitwa, ‘’Makunganya.’’

Mtandula ndipo kilipo kivuko kuja Pande.

Hapa ilibidi nimkatishe kauli mpashaji habari wangu Sheikh Suleiman Mwandu kutaka uhakika kama nimesikia vizuri kuwa Mwalimu Nyerere kenda Kilwa Pande na boti inaitwa Makunganya.

Hassan Omari Makunganya alipigana na Wajerumani na walipomkamata walimnyonga na mnara wa kumbukumbu yake na wazalendo wengine upo Kilwa.

Hapakuwa na tawi la TANU lakini Pande kulikuwa na wanachama wa TANU waliokuwa na kadi zikiuzwa senti hamsini lakini wakizificha kuogopa serikali.
Mwalimu Nyerere aliingia Pande kwa mguu wa kulia kwa kuwa siku ile usiku wake kulikuwa na mkesha wa Maulidi, kulikuwa na Ziara ya kila mwaka ya Tariqa Qadiriyya tarehe 14 kuamkia 15 Rajab.

Mji ulikuwa umefurika watu kutoka vijiji vya jirani kuitika mwito wa Khalifa wao Sheikh Athmani Ahmed aliyechukua uongozi wa kutoka kwa Sheikh Khamis Abdallah ambae alikuwa kafariki mwaka wa 1952.

Usiku ule katika Maulid yale uwanjani kwa Sheikh Ahmed Athmani Waislam wakatangaziwa kuwa kesho Julius Nyerere anakuja Pande watu watoke kumpokea Mtandula na kutakuwa mkutano wa hadhara uwanjani kwa Abdul Manafi na Julius Nyerere atawahutubia wananchi wa Tanganyika.
Hivi ndivyo TANU ilivyobisha hodi Pande na wananchi sasa wakapata nguvu ya kuitangaza TANU.

Ikawa makarani wa kununua mbata na korosho katika kazi zao wakiwahimiza wale wanaokuja kuuza mazao yao kuwa watoe senti hamsini wakate kadi ya TANU.

Kama wanavyopenda kusema Waingereza, ‘’The Rest is history,’’ yaani yaliyobakia ni historia.

Hakika historia ya uhuru wa Tanganyika iko katika vichwa vya watu kama alivyosema John Iliffe.

Picha: Nyumba ya Mzee Mwinyimkuu Manafi aliyofika Baba wa Taifa Kilwa Pande mwaka wa 1955, wa katikati ni Hassan Omari Makunganya alipokamatwa na Wajerumani.

1697573814119.png

1697573902395.png

1697573939171.png
 

Attachments

  • 1697573877806.png
    1697573877806.png
    77.7 KB · Views: 14
Kumbukizi adimu na muhimu, hongera sana. Hizi kumbukumbu zilitakiwa kutambuliwa na kutunzwa iwe sehemu ya utalii na pia kujifunza kwa vizazi vijavyo. Ile sherehe ya tarehe 14 Oktoba kila mwaka ilitakiwa kwenda sambamba na kuhuisha kumbukumbu kama hizi kila mwaka ili baada hata ya miaka 10 ijayo kutakuwa na mwendelezo mkubwa na mzuri badala ya inavyofanyika sasa kwa kuuzima mwenge pekee. Inabidi Mamlaka zinazohusika kuwatafuta na kukaa na Wadau wa kihistoria kwa lengo la kuongeza ubunifu wa kutunza historia ya nchi yetu.

Hoja ya pili ni kama swali, ukiwa unatoka Morogoro kuelekea Dodoma kama kilomita takribani 20 hivi kuna sehemu inaitwa Kwa Makunganya, Je hili eneo lina uhusiano na huyo Makunganya aliyenyongwa na Wajerumani?
 
John Iliffe amepata kusema kuwa historia ya TANU nyingi iko katika mikono ya watu.

Hakika maneno haya ni ya kweli wala hayana shaka.

Nimepokea nyaraka nyingi na picha kutoka kwa watu zinazohusu historia ya TANU na historia ya Mwalimu Nyerere kutoka kwa watu na sehemu ambazo sikutegemea kabisa.

Nimepokea simu kutoka kwa rafiki yangu yuko Kilwa Pande ananiambia kakutana na kijana amekaa anaaangalia video yangu moja nazungumzia historia ya uhuru wa Tanganyika.

Huyu ndugu yangu akamfahamisha yule kijana kuwa anamfahamu huyo anaemtazama kwenye hiyo video.

Hivi ndivyo nilivyokutana na huyu kijana akanipa kipande cha historia ya nyumba ya Bi. Mgumba, nyumba ambayo Mwalimu Nyerere alilala mwaka wa 1955 wakati wa kueneza TANU kupigania uhuru wa Tanganyika.

Yule kijana akanirushia picha ya nyumba hiyo na akanipa na simu za mtu ambae yeye alikuwa kijana mdogo kiasi cha miaka 10 wakati Nyerere alipokwenda Kilwa Pande.

Huyu bwana Sheikh Suleiman Mwandu nilimpata na tukafanya mazungimzo.
Nilistarehe na nafsi yangu.

‘’Mimi nilikuwa na umri kiasi cha miaka 10 wakati Nyerere alipokuja Pande wakati wa kupigania uhuru akapokelewa na Bwana Abdul Manafi, baba yake Bi. Mgumba.

Hawa vijana wa leo wanapoieleza ile nyumba aliyolala Mwalimu Nyerere wanasema kalala nyumba ya Bi. Mgumba.

Huyu Bi. Mgumba wakati ule yeye alikuwa mtoto lakini hiki kizazi cha leo wamekuta nyumba ile anakaa Bi. Mgumba kwa kuwa baba yake Abdul Manafi alikuwa keshafariki na Bi. Mgumba ambae jina lake khasa ni Halima bint Abdi Manafi ndiye akiishi nyumba ile.

Aliyempokea Mwalimu Nyerere ni Bwana Abdul Manafi na yeye alikuwa mtu akijiweza akifanya biashara ya duka hapo nyumbani kwake.

Pamoja na yeye walikuwa Khamisi Mamboya, Bakari Suleiman Mtondoo na Suleiman Shaweji ambao baadae walikuja kuwa viongozi wa tawi la TANU hapa Kilwa Pande.

Hii nyumba ambayo unayopicha yake ndiyo khasa nyumba aliyofikia Mwalimu Nyerere lakini ile ilikuwa nyumba ya makuti hii nyumba hivi sasa imeezekwa bati.

Mwalimu Nyerere aliingia na mguu wa kulia Kilwa Pande akitokea Kilwa Masoko na alikuja na boti inayoitwa, ‘’Makunganya.’’

Mtandula ndipo kilipo kivuko kuja Pande.

Hapa ilibidi nimkatishe kauli mpashaji habari wangu Sheikh Suleiman Mwandu kutaka uhakika kama nimesikia vizuri kuwa Mwalimu Nyerere kenda Kilwa Pande na boti inaitwa Makunganya.

Hassan Omari Makunganya alipigana na Wajerumani na walipomkamata walimnyonga na mnara wa kumbukumbu yake na wazalendo wengine upo Kilwa.

Hapakuwa na tawi la TANU lakini Pande kulikuwa na wanachama wa TANU waliokuwa na kadi zikiuzwa senti hamsini lakini wakizificha kuogopa serikali.
Mwalimu Nyerere aliingia Pande kwa mguu wa kulia kwa kuwa siku ile usiku wake kulikuwa na mkesha wa Maulidi, kulikuwa na Ziara ya kila mwaka ya Tariqa Qadiriyya tarehe 14 kuamkia 15 Rajab.

Mji ulikuwa umefurika watu kutoka vijiji vya jirani kuitika mwito wa Khalifa wao Sheikh Athmani Ahmed aliyechukua uongozi wa kutoka kwa Sheikh Khamis Abdallah ambae alikuwa kafariki mwaka wa 1952.

Usiku ule katika Maulid yale uwanjani kwa Sheikh Ahmed Athmani Waislam wakatangaziwa kuwa kesho Julius Nyerere anakuja Pande watu watoke kumpokea Mtandula na kutakuwa mkutano wa hadhara uwanjani kwa Abdul Manafi na Julius Nyerere atawahutubia wananchi wa Tanganyika.
Hivi ndivyo TANU ilivyobisha hodi Pande na wananchi sasa wakapata nguvu ya kuitangaza TANU.

Ikawa makarani wa kununua mbata na korosho katika kazi zao wakiwahimiza wale wanaokuja kuuza mazao yao kuwa watoe senti hamsini wakate kadi ya TANU.

Kama wanavyopenda kusema Waingereza, ‘’The Rest is history,’’ yaani yaliyobakia ni historia.

Hakika historia ya uhuru wa Tanganyika iko katika vichwa vya watu kama alivyosema John Iliffe.

Picha: Nyumba ya Mzee Mwinyimkuu Manafi aliyofika Baba wa Taifa Kilwa Pande mwaka wa 1955, wa katikati ni Hassan Omari Makunganya alipokamatwa na Wajerumani.

Asante sana mzee Mohamed Said kwa historia hii adhimu... Ni wakati sasa kuweka picha zote na captions kwenye kitabu ili ziwafae vizazi vijavyo.
 
Back
Top Bottom