Hili nilitaka kulisema. Kuna mawili aidha ni hujuma iliyofanywa ili wafanyabiashara wakubali kuhamia maeneo maalumu ambako watakuwa wakilipa kodi, au kuna watu wachache wamewasha moto ili kutafuta sympathy kwa sita na ccm. Na kwa vile ccm ina wakti mgumu, watakuwa blackmailed kufanya jambo lolote jema kwa wafanyabiashara na kw aajili ya unafiki wa sita, watakubaliana ili wakubalike. Mtasikia.
Poleni waathrika wote. Kikubwa jipangeni katika uongozi wenu wa soko, mshinikize ccm iwalipe fidia kwa sababu ni jukumu la seriakli kuandaa mazingira sahihi na salama kwa watu wake. Walitakiwa wawe wameona hizi hatari mapema na kuchukua maamuzi sahihi ya kiuongozi badala ya kuacha hadi mnapotelewa mali zenu zote na kwa unafiki waje kuwapa pole za maneno. Walitakiwa wawe wameshaandaa mipango ya bima za biashara ndogo ndogo kwa nchi nzima. Lakini wao wamekaa kuratibu mauaji ya wapinzani tu.
La pili, mshinikizeni sita awajengee soko la kisasa sehemu safi ya biashara ili muongoze tija katika biashara zenu. Msikubali ahadi za maneno kwa sababu, kipita 2015 hamjafanyiwa, mtaona matusi na dharau mtakazofanyiwa.