Soko kuu Urambo lawaka moto

Soko kuu Urambo lawaka moto

mimi_wewe

Member
Joined
Jul 27, 2014
Posts
70
Reaction score
17
Ikiwa katika hali ya kustajabisha na kuwaacha watu midomo wazi usiku huu soko kuu Urambo linawaka moto na cha kusikitisha hakuna gari la zima moto wala kikosi cha kuzima moto. Moto ni mkali na unateketeza mali nyingi sana.

------------------

Soko kuu la Urambo Mkoani Tabora linazidi kuteketea kwa moto muda huu,chanzo cha moto huo ni shoti ya umeme ambayo imetokea katika soko hili, mpaka sasa hakuna kikosi cha zima moto wala askari polisi aliyefika katika eneo la tukio, japo wananchi wanajaribu kuuzima moto pasipo na mafanikio.

12th October 2014 23:29


1413145744129.jpg
Pia soma: Soko la Kariakoo lateketea kwa moto
 
mleta mada soko hilo ni la urambo tabora au! tupe habari zaidi
 
Uchunguzi ufanyike mapema. Isijekuwa UKAWA wamelipiza kisasi.

Poleni sana waathirika.
 
Soko kuu la Urambo Mkoani Tabora linazidi kuteketea kwa moto muda huu,chanzo cha moto huo ni shoti ya umeme ambayo imetokea katika soko hili, mpaka sasa hakuna kikosi cha zima moto wala askari polisi aliyefika katika eneo la tukio, japo wananchi wanajaribu kuuzima moto pasipo na mafanikio.
 
Poleni sana, tujuze mkuu hasahasa upande gani linaungua muda huu!
 
Soko kuu la Urambo Mkoani Tabora linazidi kuteketea kwa moto muda huu,chanzo cha moto huo ni shoti ya umeme ambayo imetokea katika soko hili, mpaka sasa hakuna kikosi cha zima moto wala askari polisi aliyefika katika eneo la tukio, japo wananchi wanajaribu kuuzima moto pasipo na mafanikio.

kesho mtasema wafuasi wa chadema wamechoma soko. vipi umepiga picha wakatoi shoti inatokea?
 
hiyo ni laana inawatafuna wapuuzi ccm, kwa kuwa watu wa maeneo hayo wanawapenda hawa wapuuzi..


Sisiemu ni wapuuzi, chama kinanuka rushwa na chadema ni maarufu.. By kinana. Ova
 
nilikuwa eneo la tukio kunajamaa anaongea kwa hisia sana ila anasema hii ajari imepangwa kwani soko kuu la urambo halilipi ushuru halmashauri kwa mgongo wa sitta, hivyo limechomwa ili halimashauri ilijenge upya na lianze kulipa ushuru. Jamaa anaonesha ni km anauhakika na maneno yake kwani anasema hata TANESCO wamehusika kwani kabla ya moto umeme ulizima mjimzima na baada ya soko kuwaka umeme ulirudi km kawaida.
 
nilikuwa eneo la tukio kunajamaa anaongea kwa hisia sana ila anasema hii ajari imepangwa kwani soko kuu la urambo halilipi ushuru halmashauri kwa mgongo wa sitta, hivyo limechomwa ili halimashauri ilijenge upya na lianze kulipa ushuru. Jamaa anaonesha ni km anauhakika na maneno yake kwani anasema hata TANESCO wamehusika kwani kabla ya moto umeme ulizima mjimzima na baada ya soko kuwaka umeme ulirudi km kawaida.

duu hii kali . hebu jaribu kumrekodi
 
Back
Top Bottom