Socio-Economic Intelligence na hatma ya Taifa

zitto junior

JF-Expert Member
Oct 7, 2013
19,039
28,689
UTANGULIZI
Tokea tumepata uhuru bara letu la Afrika tumekuwa na changamoto zinazofanana ambazo sio tu zimetuacha maskini bali tumerudi nyuma kimaendeleo kuliko hata kipindi cha ukoloni. Na matatizo haya yameshazoeleka kiasi kila mtu haoni kama yana ufumbuzi na wanabuni msemo "Miafrika ndivyo tulivyo".

Mara nyingi watanzania tukiwa na changamoto mfano za umaskini,ufisadi,ukame,magonjwa ilihali tuna rasilimali zote muhimu, huwa tunakimbilia kulaumu "mfumo" wa jamii kuwa Afrika nzima mambo kama demokrasia au utawala bora hatuuwezi sababu "ndio tulivyo" hivyo haiwezi kubadilika "mpaka kiama".

Hii excuse imetumika sana kutucheleweshea mabadiliko ya kiuchumi,kiutawala na kijamii lakini kwa nchi za wenzetu ambazo zilikuwa na matatizo ya kimfumo kama haya waliweza kuyabadilisha na leo hii jamii zao zimebadilika sana kwa sababu ya mbinu chache tu na ntatumia case ya nestle kutoka Quora kufikisha ujumbe.
images (4).jpg

NESTLE
Miaka ya 1970 kampuni ya kimarekani Nestle inayotengeneza snacks kama chocolate,kahawa,maziwa n.k ilitaka kupanua biashara zake na kuingia Japan. Kigumu ni kwamba jamii ya japan haikuwa imezoea kahawa bali chai hivyo ilibidi ufanyike utafiti namna gani wataweza teka soko.

Baada ya tafiti kadhaa wakagundua kuna watu wachache wamependa ladha ya kahawa hivyo wakajiridhisha wakianzisha migahawa ya kahawa italipa.

Baada ya miezi kadhaa ikaonekana Japan haikupenda kahawa maana imezoea chai hivyo kiufupi biashara ikawa imeingia hasara kubwa sana kuliko ilivyotarajiwa.

Ili kuokoa jahazi ikabidi nestle ije na mpango mkakati wa kuleta mabadiliko ya soko lake japan na sio tu walimuajiri mwanasaikolojia kama Mkuu wa Idara ya masoko bali waliamua kulenga soko tofauti kabisa kwa kuja na bidhaa tofauti.
images (6).jpg

Nestle walilenga watoto ili kuwaandaa kama soko lao la kesho. Walifanya hivyo wakiamini kama jamii ya sasa imegoma kubadilika kupenda kahawa basi tunaweza fanya jambo leo ili jamii ya kesho ibadilike.

Waliingiza sokoni pipi za kahawa za aina zote ili kuwazoeza kuhusu ladha ya kahawa, na miaka 10 baadae wakaanza ona matokeo chanya kwa ''jamii'' mpya kuanza kushambulia vikombe vya kahawa na biashara yao ikawa na faida kubwa kwa mauzo kupaa.

FUNZO
Hapa tunajifunza kwamba jamii inaweza kubadilishwa kabisa mtazamo,tabia,haiba na maamuzi maana makuzi ndio kila kitu.

Mfano tatizo la ufisadi kama tokea udogoni katuni zitengenezwe za kuonesha mafisadi ni maadui wa taifa. Hata nyimbo za watoto ziimbwe hivo kama ambavyo tunatumia nguvu kuwakaririsha kuhusu Allah ni mzuri na shetani ni mbaya huko sunday school na madrassa then trust me tungejikwamua hapa tulipo.

Hapa kati nikikatiza uswahilini nikakuta watoto wa miaka chini ya 7 wanaimba nyegezi.... Wengine wanajifanya wanapigana kung fu. Nikajua ni influence ya mambo wanayoyaona kwenye makuzi ndio yanatufikisha taifa letu hapa lilipo.

So tutapiga kelele sana kuwa tabia ni chafu,vibaka wengi,magaidi kuongezeka,ufisadi,madikteta n.k huku Afrika lakini hatujui kiini ni sisi wenyewe tunataka tubane huku juu kwa kuweka sheria kali,kukamata mashoga,kuchoma moto wezi huku tunasahau mizizi ndio iliyooza sio tunda.

MASHIRIKA YA INTELLIGENTSIA
Nchi zetu za Afrika ziache kutumia mashirika ya intelijensia kumaliza wanasiasa au kufanya ''umbea'' tu nchi jirani kuna nini kinaendelea bali watumie muda huo kupandikiza mbegu njema kwenye jamii yetu na hata wanaweza kwenda mbali zaidi na kupandikiza bidhaa zetu kama korosho au mbaazi kupendwa nchi jirani kwa kutumia mbinu za kijasusi ili miaka ijayo tupate soko la uhakika la mazao yetu. Tukifanya haya jamii na uchumi wetu utapaa kuliko kutumia nguvu kudhoofisha wapinzani wako kisiasa.
images (5).jpg

Kama wanataka sera zao zifanikiwe iwe Tanzania ya viwanda, kupunguza mimba mashuleni,UKIMWI, kuongeza ufaulu masomo ya sayansi n.k kitengo waanze kubuni mikakati ya kuwapatia "pipi za kahawa" watoto wetu ili baadae wakue wakiwa kama ambavyo kitengo wanataka na tutaona mabadiliko kwenye jamii yetu na Afrika nzima.

Naomba kuwasilisha tafadhali
 

Attachments

  • Screenshot_2019-06-04-19-43-11.png
    Screenshot_2019-06-04-19-43-11.png
    53.6 KB · Views: 41
Unaishi Tanzania haiwwezi kua asa huu uahari nasaha utawafikiaje hao wawezeshi maana hoja hii bila kufika kule hakuna kitakachofanyika
 
mkuu asante sana kwa wazo zuri la namna hiyo na hii inaonesha kabisa kuwa katika nchi hii kuna watu wana mawazo chanya kabisa kuhusu mustakabali wa taifa letu 'but mind you mkuu you're not the one with the only positive idea...wapo wengi mno but nikueleze ukweli kabisa toka moyoni....we are destroyed by others ... not us.....mataifa makubwa yanapandikiza ujinga mkubwa sana kwetu sisi kisha kuanza kunufaika na ujinga huo ....

Nitakweleza kwa namna ya pekee.....mfumo wa vyama vingi katika nchi za Africa uliletwa na wazungu hao hao( Indirectly) ambao kwao haupo sasa hivi...wanajua mkiweka mfumo wa vyamavingi kelele zitakuwepo za kugombea madaraka hence watu wataingiza mambo yao binafsi na kusahau Tanzania kwanza....

( education skolaship -then wanarudi kwenye nchi zao kuhimiza yale ambayo wametoka wamesaini mikataba kuja kutekeleza kama kutoa shukrani kwa elimu ya huko juu kwani ada ya Kumudu masomo katika nchi za wenzetu ni kubwa sana ndo mana waliosomea nje ya nchi huwa hawakatwi kabisa make ni pesa mbayo hata ustaafu huwezi ilipa labda uibe pesa BOT,it's direct Grant fee)

Kila msaada unaoupata toka kwa wale watu una madhara makubwa sana kwa baadae japo ni ngumu kulijua hilo.....

Ni kwamba ,nchi ambazo zina offer skolaship ya elimu ya juu kwa waafrica ndo hizo hizo zinaingia mikataba na serikali kuwa tunawasomesha watu wenu ili badae waje wawatumikia na hao hao watu wenu hupitisha mikataba mibovu kwenye nchi zao kisha utafata mfumo nyemelezi wa kinyonyaji toka kwa wenzetu.....

Maisha haya yapo katika flux condition...ili uendelee ni lazima awepo ndezi wa kunyonywa....ukilijua hilo ndo utajua kwanini nchi za huko zimeendelea kwa kasi bila sisi kujua......but the truth ni kwamba these people prepared ways to harvest .......

usidhani serikali za Africa ni wajinga kiasi hicho kiasi cha kukosa mawazo mbadala kama yako ,but regularities na conditions ambazo wanakuwa washakubaliana miaka ya nyuma ndo zinawafunga mkuu...kwa mfano mikataba ambayo inatiwa saini sasa hivi madhara yake yataathiri miaka ya 2050 huko...yani ni long plan effects mkuu......tazama Nchi ya China sasa hivi ndo inongoza kwa kutoa maskolaship fasta kwa wasomi wa elimu za juu...badae ndo utakuja kuelewa madhara ya kuwa offered kule....when you're back utatakiwa kuipliment sera za kufeva uwekezaji wa China zaidi..na Nchi haitaepuka hilo janga.....

Mandela mwenyewe na jeuri yake aliiuza nchi ya South Africa ila awe huru na watu wapate kuwa huru ila watu hawajui why that happened ...but in reality yule jamaa alikubali masharti mazito sana kwenye ile Nchi ili maisha yawe sare and one of the agreement ilikuwa ni kuruhusu HIV innoculation kwenye jamii ili nchi za magharibi ziwekeze kwenye madawa ya kurefusha maisha....na hiyo ni long plan n
ndo mana mpaka sasa 37% ya watu wote South Africa ni seropositive( sero converted) the matter is not being a leader,but who stands behind you while others being blind.....kuna mambo serikali inamua kunyamaza kwa sababu ishatiwa msumari kwa nyuma huna jinsi mkuu....

Kingine unatakiwa ujiulize Nyerere aliofa nini kwa hawa jamaa kwanini umaskini umekithiri Tz despite of having a lot of resources...? kuna nini nyuma ya pazia....?? kila anaeingia madarakani kwa hasira ya kubadilisha maisha ya watanzania anakuta kitu chenye ncha kali kinamwambia acha mambo yaende in this way.....

Nikuombe tu mkuu jaribu kusoma baadhi ya Nyaraka za siri ambazo zinaelezea kwanini serikali za Africa zilipewa chance ya kupeleka watoto wakasome njee ili waje kuwa viongozi wa huku na ndo hao hao wanakuja kuwa viongozi wakuu wa idara nyeti....we fuatilia tu utajua kwanini mambo wanayoyafanya ni kinyume na utashi wa taifa hili...Mwenye uchungu na nchi hii sio wewe pekee but we are many broo ila namna ya kuwezesha mawazo haya into changes ndo mtihani .....but..........something driving our mind ...
 
mkuu asante sana kwa wazo zuri la namna hiyona hii inaonesha kabisa kuwa katika nchi hii kuna watu wana mawazo chanya kabisa kuhusu mustakabali wa taifa letu 'but mind you mkuu you're not the one with the only positive idea...wapo wengi mno but nikweleze ukweli kabisa toka moyoni....we are destroyed by others ... not us.....mataifa makubwa yanapandikiza ujinga mkubwa sana kwetu sisi kisha kuanza kunufaika na ujinga huo ....

Nitakweleza kwa namna ya pekee.....mfumo wa vyama vingi katika nchi za Africa uliletwa na wazungu hao hao ambao kwao haupo sasa hivi...

( education skolaship -then wanarudi kwenye nchi zao kuhimiza yale ambayo wametoka wamesaini mikataba kuja kutekeleza kama kutoa shukrani kwa elimu ya huko juu kwani ada ya Kumudu masomo katika nchi za wenzetu ni kubwa sana ndo mana waliosomea nje ya nchi huwa hawakatwi kabisa make ni pesa mbayo hata ustaafu huwezi ilipa labda uibe pesa BOT,it's direct Grant fee)

Kila msaada unaoupata toka kwa wale watu una madhara makubwa sana kwa baadae japo ni ngumu kulijua hilo.....

Ni kwamba ,nchi ambazo zina offer skolaship ya elimu ya juu kwa waafrica ndo hizo hizo zinaingia mikataba na serikali kuwa tunawasomesha watu wenu ili badae waje wawatumikia na hao hao watu wenu hupitisha mikataba mibovu kwenye nchi zao kisha utafata mfumo nyemelezi wa kinyonyaji toka kwa wenzetu.....

Maisha haya yapo katika flux condition...ili uendelee ni lazima awepo ndezi wa kunyonywa....ukilijua hilo ndo utajua kwanini nchi za huko zimeendelea kwa kasi bila sisi kujua......but the truth ni kwamba these people prepared ways to harvest .......

usidhani serikali za Africa ni wajinga kiasi hicho kiasi cha kukosa mawazo mbadala kama yako ,but regularities na conditions ambazo wanakuwa washakubaliana miaka ya nyuma ndo zinawafunga mkuu...kwa mfano mikataba ambayo inatiwa saini sasa hivi madhara yake yataathiri miaka ya 2050 huko...yani ni long plan effects mkuu......tazama Nchi ya China sasa hivi ndo inongoza kwa kutoa maskolaship fasta kwa wasomi wa elimu za juu...badae ndo utakuja kuelewa madhara ya kuwa offered kule....when you're back utatakiwa kuipliment sera za kufeva uwekezaji wa China zaidi..na Nchi haitaepuka hilo janga.....

Mandela mwenyewe na jeuri yake aliiuza nchi ya South Africa ila awe huru na watu wapate kuwa huru ila watu hawajui why that happened ...but in reality yule jamaa alikubali masharti mazito sana kwenye ile Nchi ili maisha yawe sare and one of the agreement ilikuwa ni kuruhusu HIV innoculation kwenye jamii ili nchi za magharibi ziwekeze kwenye madawa ya kurefusha maisha....na hiyo ni long plan n
ndo mana mpaka sasa 37% ya watu wote South Africa ni seropositive( sero converted) the matter is not being a leader. but who stands behind you while others being blind.....kuna mambo serikali inamua kunyamaza kwa sababu ishatiwa msumari kwa nyuma huna jinsi mkuu....

Kingine unatakiwa ujiulize Nyerere aliofa nini kwa hawa jamaa kwanini umaskini umekithiri Tz despite of having a lot of resources...? kuna nini nyuma ya pazia....?? kila anaeingia madarakani kwa hasira ya kubadilisha maisha ya watanzania anakuta kitu chenye ncha kali kinamwambia acha mambo yaende in this way.....

Nikuombe tu mkuu jaribu kusoma baadhi ya Nyaraka za siri ambazo zinaelezea kwanini serikali za Africa zilipewa chance ya kupeleka watoto wakasome njee ili waje kuwa viongozi wa huku na ndo hao hao wanakuja kuwa viongozi wakuu wa idara nyeti....we fuatilia tu utajua kwanini mambo wanayoyafanya ni kinyume na utashi wa taifa hili...Mwenye uchungu na nchi hii sio wewe peke yako.....but..........something driving our mind ...
Nimekuelewa sana mkuu, ndio maana mtu kama 'uncle' unamuona kabisa ana nia ya dhati kuivushaTZ ila kuna mahali ananasa. Hadi najiuliza shida ni nini? Kama tatizo ni mifumo yetu anashindwaje kufanya reformation ili mambo yaende kama anavyotaka, kumbe kuna mengi nyuma yake ambayo ni kikwazo kikubwa na yapo nje ya uwezo wake.
 
mkuu asante sana kwa wazo zuri la namna hiyo na hii inaonesha kabisa kuwa katika nchi hii kuna watu wana mawazo chanya kabisa kuhusu mustakabali wa taifa letu 'but mind you mkuu you're not the one with the only positive idea...wapo wengi mno but nikueleze ukweli kabisa toka moyoni....we are destroyed by others ... not us.....mataifa makubwa yanapandikiza ujinga mkubwa sana kwetu sisi kisha kuanza kunufaika na ujinga huo ....

Nitakweleza kwa namna ya pekee.....mfumo wa vyama vingi katika nchi za Africa uliletwa na wazungu hao hao( Indirectly) ambao kwao haupo sasa hivi...

( education skolaship -then wanarudi kwenye nchi zao kuhimiza yale ambayo wametoka wamesaini mikataba kuja kutekeleza kama kutoa shukrani kwa elimu ya huko juu kwani ada ya Kumudu masomo katika nchi za wenzetu ni kubwa sana ndo mana waliosomea nje ya nchi huwa hawakatwi kabisa make ni pesa mbayo hata ustaafu huwezi ilipa labda uibe pesa BOT,it's direct Grant fee)

Kila msaada unaoupata toka kwa wale watu una madhara makubwa sana kwa baadae japo ni ngumu kulijua hilo.....

Ni kwamba ,nchi ambazo zina offer skolaship ya elimu ya juu kwa waafrica ndo hizo hizo zinaingia mikataba na serikali kuwa tunawasomesha watu wenu ili badae waje wawatumikia na hao hao watu wenu hupitisha mikataba mibovu kwenye nchi zao kisha utafata mfumo nyemelezi wa kinyonyaji toka kwa wenzetu.....

Maisha haya yapo katika flux condition...ili uendelee ni lazima awepo ndezi wa kunyonywa....ukilijua hilo ndo utajua kwanini nchi za huko zimeendelea kwa kasi bila sisi kujua......but the truth ni kwamba these people prepared ways to harvest .......

usidhani serikali za Africa ni wajinga kiasi hicho kiasi cha kukosa mawazo mbadala kama yako ,but regularities na conditions ambazo wanakuwa washakubaliana miaka ya nyuma ndo zinawafunga mkuu...kwa mfano mikataba ambayo inatiwa saini sasa hivi madhara yake yataathiri miaka ya 2050 huko...yani ni long plan effects mkuu......tazama Nchi ya China sasa hivi ndo inongoza kwa kutoa maskolaship fasta kwa wasomi wa elimu za juu...badae ndo utakuja kuelewa madhara ya kuwa offered kule....when you're back utatakiwa kuipliment sera za kufeva uwekezaji wa China zaidi..na Nchi haitaepuka hilo janga.....

Mandela mwenyewe na jeuri yake aliiuza nchi ya South Africa ila awe huru na watu wapate kuwa huru ila watu hawajui why that happened ...but in reality yule jamaa alikubali masharti mazito sana kwenye ile Nchi ili maisha yawe sare and one of the agreement ilikuwa ni kuruhusu HIV innoculation kwenye jamii ili nchi za magharibi ziwekeze kwenye madawa ya kurefusha maisha....na hiyo ni long plan n
ndo mana mpaka sasa 37% ya watu wote South Africa ni seropositive( sero converted) the matter is not being a leader,but who stands behind you while others being blind.....kuna mambo serikali inamua kunyamaza kwa sababu ishatiwa msumari kwa nyuma huna jinsi mkuu....

Kingine unatakiwa ujiulize Nyerere aliofa nini kwa hawa jamaa kwanini umaskini umekithiri Tz despite of having a lot of resources...? kuna nini nyuma ya pazia....?? kila anaeingia madarakani kwa hasira ya kubadilisha maisha ya watanzania anakuta kitu chenye ncha kali kinamwambia acha mambo yaende in this way.....

Nikuombe tu mkuu jaribu kusoma baadhi ya Nyaraka za siri ambazo zinaelezea kwanini serikali za Africa zilipewa chance ya kupeleka watoto wakasome njee ili waje kuwa viongozi wa huku na ndo hao hao wanakuja kuwa viongozi wakuu wa idara nyeti....we fuatilia tu utajua kwanini mambo wanayoyafanya ni kinyume na utashi wa taifa hili...Mwenye uchungu na nchi hii sio wewe peke yako.....but..........something driving our mind ...
Tatizo ndiyo hili sasa badala ya kuboresha wazo unashambulia kiitikadi, hili ni wazo zuri. Watu huandaliwa kama mambo hayaendi, siku hizi mtu anajiandaa kutawala mikele siyo kuwaendeleza watu.
 
huwezi ukaanza kusolve tatizo bila kujua chanzo ni kipi.....problem solving technique ina protocol zake.....hili tatizo la umaskini ni pana sana...wala sijacritisize mbona nimeongelea mambo bayana mkuu.....the problem ya sisi tunataka kusolve tatizo bila kujua source...watu wanaumiza akili sana but mambo yapo nje ya uwezo wao.....

The best option is to ammend the reformation ya system..not only that bht also kuna ulazima wa kujua long term plan effects za kufanya negotiations na mataifa makubwa kabla ya yote....mind you aliyekuzidi akili kakutangulia maisha pia bado tunahitajikujitafakari zaidi
Tatizo ndiyo hili sasa badala ya kuboresha wazo unashambulia kiitikadi, hili ni wazo zuri. Watu huandaliwa kama mambo hayaendi, siku hizi mtu anajiandaa kutawala mikele siyo kuwaendeleza watu.
 
Mandela mwenyewe na jeuri yake aliiuza nchi ya South Africa ila awe huru na watu wapate kuwa huru ila watu hawajui why that happened ...
Huu ni ukweli mchungu ambao wengi hawapendi kuusikia na ndio maana mpaka leo wazungu wanamhusudu.

Back to mada: unaona suluhisho la kwanza ni lipi ili tuweze kufikia mabadiliko ya kijamii na kiuchumi kizazi kijacho?? (maana hiki kimeshaoza)
 
Hii kitu ni nzuri sana lkn nani wakuifanya? Mifumo yetu ya uendeshaji iko shaghala baghala , hatuna long plan, wala short plan
Mkuu za masiku.... Unadhani suluhisho ni lipi na sisi kufikia mabadiliko ya kifikra,kiuchumi na kijamii kama nchi za wenzetu refer meiji era japan ama age of renaissance huko ulaya karne ya 14.
 
Mkuu za masiku.... Unadhani suluhisho ni lipi na sisi kufikia mabadiliko ya kifikra,kiuchumi na kijamii kama nchi za wenzetu refer meiji era japan ama age of renaissance huko ulaya karne ya 14.
Salama kabisa Mkuu, kwa mtazamo wangu lzm ,Fikra zetu zibadilike ,zigeuze changamoto kuwa Fursa ,km hao Nestle walivyofanya bila hivyo tutakua bado tuko nyuma
 
The best option hapo nchi ikasomeshe watu nje ya nchi hasa nchi zenye technolojia kubwa kisha warudi wawe recruited na jeshi na watakuwa chini wa uangalizi wa jeshi huku wakitrasform knowledge walioipata kule kwa kuomba serikali yetu ihakikishe inapata raw material pamoja na mashine kwa ajili ya kuendeleza production ya creativity huku wakiwa chini ya jeshi la Nchi yetu....

Nitatolea mfano nchi ya China ..ilisomeshe watu Nchi za ulaya kisha ikapitisha sheria ya kwamba ukihitimu masomo yako unapitiliza kwenda jeshi na ukifika huko jeshi unakuwa recruited katika idara husika ya masomo yako kisha kuamriwa utrasform knowlege uliyotoka nayo huko kwa ajili ya kufanya cretivity na uzalishaji mali...kwa kufanya hivo serikali ilikuwa tayri ishacontrol maarifa ya watu wake na tayari access ya kuwa na mawasiliano ya mataifa walikosoma walikosa make wanakuwa chini ya uangalizi mkubwa. wa jeshi na kule ni kuobey command tu no argument na mijadara......

Ukiwa daktari utaulizwa enheee tueleze unataka serikali ilete nini ili uitumikie vizuri elimu yako kwenye mambo ya afya...??unasema mimi nataka mashine ya CT scan na Tomography tayari serikali inakusanya kodi kwa kila Raia njee ,pesa inapatikana hospital inajengwa na daktari unafanya kazi yako..

Kwa kuruhusu wakuu wa idara zote kuwa chini ya jeshi la Nchi unakuwa umeshacontrol negative transformation toka nchi jirani pia inakuwa ngumu kuwa imposed na negative mind ideology ambazo zinakuwa zishapandikizwa kwa baadhi ya wasomi huko nje..


Hivyo basi mpango huo umefanya nchi nyingi duniani kuendelea kwa kasi sana kwani technolojia yote inakuwa chini ya jeshi la Nchi hence knowledge yote inakuwa ipo kwenye kambi za jeshi...

Angalia hata nchi ya Marekani ,taasisi zote zipo chini ya jeshi manake inakuwa ngumu mtu kutoka masomoni kisha kuwa mkuu wa kitengo na kuanza kujiamlia apitishe sheria hii aache hii ....ukiwa chini ya jeshi utakuwa na displine na watazuia transformation ya knowlege yako kwenda nchi zingine.....


Serikali yetu iliangalie hilo kwa umakini sana...fasta sana tunatusua....China kuna sheria kuwa, kwenda jeshi ni lazima kwa kila mtu mwenye umri wa miaka 18 ..ukifika jeshini tayari utakuwa recruited kwenye kitengo ambacho hobby yako inapendelea kulingana na saikolojia ambayo watakuwa washakustudy kuwa huyu mtu anafaa kusomea hiki na hapo utapelekwa idara husika..

Ndo mana inovations nyingi zinakuwa ni successfully coz zinakuwa chini ya uangalizi mkali...
Huu ni ukweli mchungu ambao wengi hawapendi kuusikia na ndio maana mpaka leo wazungu wanamhusudu.

Back to mada: unaona suluhisho la kwanza ni lipi ili tuweze kufikia mabadiliko ya kijamii na kiuchumi kizazi kijacho?? (maana hiki kimeshaoza)
 
Tangu kipindi hicho mpaka sasa tulishachelewa labda la kufacha hivyo vyombo tajwa hapo visafishwe na sisitimu ianze upya maana kwa sasa wameshaelenea upande mmoja wakati wenzetu wao hawako mrengo wowote umoja wao ni kusimamania kile walichoaminishiwa tangu enzi hizo
 
Humu kuna mawazo makubwa kabisa,,elimu ya kutosha.Kuna vitu huwa nikivisoma kwa namna nilivyovikubali.Huwa sitamani viishie kwenye maandishi,,ila huwa Natamani vibadilishwe viwe kwenye vitendo..

Leo marekani anamlalamikia china kwa suala la intellectual theft Unadhani ni jambo dogo lakini ni plan wachina waliiweka mda mrefu.Na imefanikiwa...Mmarekani akianzisha kiwanda China lazima awaachie wachina technology yote na inakuwa ni kwa manufaa ya china.
Kukitokea kampuni yoyote imetengeneza cyber tools mchina anainunua technology hio kwa pesa yoyote.Kwa nini?? Kwa sababu ameshawatambua wazungu walivyo.

Sisi tuna raslimali nyingi,,kabla ya kufikiria plan ya maendeleo yetu binafsi tuache kuingia mikataba, maana itafika siku hatuna pa kuanzia.
 
mko vizuri na hoja zenu zimetulia sana niwaulize mnaejalibu kumshauri (kumshawishi) ili atende ni nani....? Maada ni nzuri Je...itafikaje sehemu husika ili ifanyiwe kazi (au ndo nyie wale nguri mnajalbu kuwekana sawa na ndo watelelezaji wakuu. Fun)
 
mko vizuri na hoja zenu zimetulia sana niwaulize mnaejalibu kumshauri (kumshawishi) ili atende ni nani....? Maada ni nzuri Je...itafikaje sehemu husika ili ifanyiwe kazi (au ndo nyie wale nguri mnajalbu kuwekana sawa na ndo watelelezaji wakuu. Fun)
Mkuu haya mabadiliko yanaanza na watu coz hata hao viongozi walikuwa ni mtu kma ww na mimi hivyo wasomaji wa humu wanaweza pata mawazo na kuaanza kutekeleza at individual capacity sio kila kitu kisubiri serikali sababu mabadiliko ya kweli yanaanzia kwetu kama hatuwezi andaa watoto wetu kuwa viongozi wa kesho wenye kujituma/kuchukia ufisadi/kuwajibika basi hata serikali iweke mipango gani haitoweza kufanikiwa maana kutakua hakuna watu sahihi wa kutekeleza mipango yao.

Pia tuna wana JF wengi tu ni wabunge,watumishi wa umma,wakurugenzi wa idara/taasisi n.k nao kwa nafasi zao za ushawishi kwenye chama na serikali wanaona mada nyingi sana za humu JF na wengi tu wana ID feki ila wakipata idea mbili tatu basi wanaweza kuyafanyia kazi kwa mustakabali wa taifa.

Otherwise mlengwa ni ww na mmi tusisubiri serikali
 
mimi namshukuru Mungu atupae nguvu na uzima.

Mungu katuwekea majira na nyakati zilizo sawa, hakuna alie pewa saa 25 na sisi wengine tukapewa saa 24.

niliwahi kujiuliza sana nikitu gani kilitokea mpaka baadhi ya wenzetu kututangulia sana hali ya kuwa tumepewa muda mmoja?

nikagundua maisha ni kama mchezo na kila mmoja anacheza kwa ufanisi katika nafasi yake.
hoja uliotoa mkuu zitto junior inalenga huko huko kutumia mbinu ili kushinda mchezo wa maisha. mbinu hizo zinapatiakana kwa kutumia akili.

sasa kwa nini sisi tuna kosa mbinu? ni kwamba hatuna akili? naweza kusema ndio!
hoja alio toa ndugu lifecoded inaingia hapo kama wenzetu wametumia mbinu za kuturubuni kwa kutumia elimu yao na wakati huo sisi tukakubali kurubuniwa basi huu niukosefu mkubwa wa akili tulio nao ambao kwa kiasi kikubwa unasabaishwa na umaskini uliopelekea ukosefu wa chakula lishe ama wakati wa makuzi yetu ama wazazi wetu.

na hapo kwa sasa hatuna namna ya kuvuka hapo kwa wakati huu, wenzetu wametutangulia mbele sana lakini muda tulio nao ni mmoja, viongozi wetu wa serikali ama wa zama hizi ama zijazo bado sana kututoa hapa na hata viongozi wa dini sina hakika kama wanaweza kuwa sababu ya kututoa hapa

pendekezo alilotoa lifecoded kama suluhisho lina mantiki, lakini ninani kati ya viongozi wetu wa zama hizi ama zijazo atatuelekeza huko?

tufanye nini? ni mimi na wewe unaepata bahati ya kusoma mada kama hizi kuwaandaa watoto wetu namna ya kumkabili mtu aliemzidi kila kitu.
tuwalishe watoto wetu vyakula vinavyoleta afya ya ubongo.
tuwajulishe mbinu wanazotumia kuturubuni ili turudi nyuma,ili wao wajue wataanzia wapi ingawa bado wenzao watakuwa mbele.
tuwaambie wasiiamini sana elimu ya namna tulio nayo sasa kwamba inaweza kuwakomboa bali watumie akili zao binafsi kujikomboa.
tuwaambie wamuheshimu sana Mungu lakini wasiwagope na kuwanyenyekea viongozi wa dini maana na wao hawakutusaidia sana japo wanahubiri ukombozi kwa kiroho lakini wakatuweka kwenye utumwa wa fikra.
tuwaambie wasome sana vitabu lakini kwa akili maana sio kila kitabu kinalenga kukomboa vingine ni kudumaza akili.
pia tuwakumbushe kutunza asili na kuwaachia vizazi vitakaofuatia machapisho na nasaha kama hizo tulizo wapa.

kwa hayo angalao miaka mia moja ijayo watakua wana zungumza mengine.. .
 
Back
Top Bottom