Thinker96
JF-Expert Member
- Jan 15, 2011
- 347
- 135
"Intelligence Spinning"
Ni uwasilishaji wa taarifa za kiintelligensia kwa namna iliyopindishwa kwa maslahi ya umma au viongozi.
Yaani kuna taarifa ni kwa ajili ya kuubhagaza umma ili uamini kitu na pia kuna taarifa nyingine zinabhagaza viongozi ili waone wako sawa na salama.
Taarifa inayofanyiwa "spinning" inakuwa ya ukweli kabisa ila uwasilishaji wake ndo unakuwa wa uongo. Mfano "Tumepokea taarifa ya maandamano ya ..... ila kwa taarifa za kiintelligensia kutakuwa na uvunjifu wa amani", na viongozi pia huwanyiwa spinning kwa kupindishiwa taarifa hasa ikiwa parallel state ndo kabisa anaweza akatishwa kwa taarifa za kawaida na kuonekana kubwa ili akae kwa tahadhari na vitu vingine vya kimkakati asifanye kwa ukaribu.
Ila kuna mambo ambayo mara nyingi wengi wetu hudhania ni spinning kumbe sivyo ila malengo yake hutarget umma au uongozi na hitimisho la mlengo ni kama spinning inavyohitimisha mambo hayo ni kama:-
1. Diversionary politics (Siasa za mkwepo)
Kutengeneza issue nyingine ili kuutoa umma au utawala kwenye issue iliyokuwepo awali huenda ilikuwa nzuri au mbaya. Mfano kunakuwa na habari za kuhusu masuala ya uchaguzi watu wamewaka moto kweli kweli wanaweza kuhatarisha usalama inaletwa issue ya udini inapewa promo watu wanahama na wasipo hama wanagawanyika basi issue ya awali inakuwa imepunguziwa nguvu au imeondolewa hatari iliyodhaniwa.
2. Distraction tactics (Mkakati haribifu)
Hii ni ile hali ya kuondoa mtazamo wa umma kwa nguvu bila kuwa na hoja mbadala mfano umma unataka taarifa fulani ambayo itajenga sifa mbaya kwa nchi viongozi wanagoma kutoa hiyo taarifa kwa kutoa sababu isiyo na mashiko kwa umma.
3. Agenda setting/Agenda manipulation(Kuibalaghaza agenda)
Hii ni ile hali ya kuongoza yale ambayo umma unaongea kwa sana kwa kuyapindisha au kuyatengenezea tafsiri ngumu kwa umma kwa mfano " Umma unadai haki moja wapo ni haki ya kuishi ila wataalamu wa kumanipulate wanaishi kwenye hiyo hiyo ajenda wanakuambia unapodai haki hakikisha umetimiza wajibu kumbuka haki inayodaiwa na umma ni haki ya kuishi ila unaambiwa utimize wajibu"
4. Smoke and Mirrors(Moshi na Kioo)
Yaani moshi ukionekana kwenye kioo ni jitu kubwa sana ni kama linashikika hii imekaa hivi kuanzisha mambo madogo ambayo yanachukua nafasi ya mambo makubwa ili kutoa watu kwenye ufuatiliaji wa mambo makubwa. Mfano mambo ya wasanii na michezo yanaweza kupewa nafasi kubwa ilhali kuna mambo ya nchi yanatokota na ni makubwa hayana nafasi, inch fulani deni lipo Trillions za Shilling za kwao 12 ila wao mameshika masuala ya ukabila na upendeleo kwenye vyeo.
5. Red herring (Sill nyekundu)
Hii ni ile hali ya kuiondoa jamii kwenye hoja za kipaumbele kwa kuanzisha hoja mbadala ambazo zitaitoa jamii katika kelele za hoja zao za msingi mfano Goldberg Scandal kwenye nchi hiyo walisema kuna watu wanatengeza taarifa ili kujinufaisha kisiasa na kulichafua kabila fulani, Cashgate scandal kwanini watu mnatengeza hoja za uongo kwa ajili ya minajili ya kisiasa, kuna Scandal ilikuwepo babu wa Loliondo alichukua front page.
Sababu ya kufanya hivyo huenda ikawa:-
1. Kuhalalisha maamuzi ya serikali.
Mfano: kuhalalisha vita, operesheni ya usalama, au sheria mpya.
2. Kuepusha hofu kwa wananchi.
Wakati mwingine ukweli hufichwa au hupunguzwa ili watu wasipate hofu.
3. Kushawishi maoni ya umma.
Kufanya tishio lionekane kubwa au dogo ili watu waunge mkono hatua fulani.
4. Kulinda vyanzo vya taarifa.
Kuepusha kufichua majina ya watoa taarifa au mbinu za kijasusi.
5. Propaganda / taswira ya kisiasa
Kuifanya taasisi au upande fulani uonekane sahihi zaidi ilhali wamefanya sawa au si sawa lakini hulazimishwa kuonekana ni sawa hata kama ni ufisadi wizi ubadhilifu na mengineyo mabaya kwa maslahi ya umma.
Kama kuna lolote unaliona linaendelea kwa pamoja tunaweza kusaidiana kulichambua na kuliweka katika kundi lake kuwa hilo lipo mlengo gani kama ni kweli au ni mbinu za kuingizana maboya
Nipo tayari kurekebishwa na kueleweshwa zaidi karibuni kwa maoni na kila linalotokea tutaarifiane na kulichambua
Ni uwasilishaji wa taarifa za kiintelligensia kwa namna iliyopindishwa kwa maslahi ya umma au viongozi.
Yaani kuna taarifa ni kwa ajili ya kuubhagaza umma ili uamini kitu na pia kuna taarifa nyingine zinabhagaza viongozi ili waone wako sawa na salama.
Taarifa inayofanyiwa "spinning" inakuwa ya ukweli kabisa ila uwasilishaji wake ndo unakuwa wa uongo. Mfano "Tumepokea taarifa ya maandamano ya ..... ila kwa taarifa za kiintelligensia kutakuwa na uvunjifu wa amani", na viongozi pia huwanyiwa spinning kwa kupindishiwa taarifa hasa ikiwa parallel state ndo kabisa anaweza akatishwa kwa taarifa za kawaida na kuonekana kubwa ili akae kwa tahadhari na vitu vingine vya kimkakati asifanye kwa ukaribu.
Ila kuna mambo ambayo mara nyingi wengi wetu hudhania ni spinning kumbe sivyo ila malengo yake hutarget umma au uongozi na hitimisho la mlengo ni kama spinning inavyohitimisha mambo hayo ni kama:-
1. Diversionary politics (Siasa za mkwepo)
Kutengeneza issue nyingine ili kuutoa umma au utawala kwenye issue iliyokuwepo awali huenda ilikuwa nzuri au mbaya. Mfano kunakuwa na habari za kuhusu masuala ya uchaguzi watu wamewaka moto kweli kweli wanaweza kuhatarisha usalama inaletwa issue ya udini inapewa promo watu wanahama na wasipo hama wanagawanyika basi issue ya awali inakuwa imepunguziwa nguvu au imeondolewa hatari iliyodhaniwa.
2. Distraction tactics (Mkakati haribifu)
Hii ni ile hali ya kuondoa mtazamo wa umma kwa nguvu bila kuwa na hoja mbadala mfano umma unataka taarifa fulani ambayo itajenga sifa mbaya kwa nchi viongozi wanagoma kutoa hiyo taarifa kwa kutoa sababu isiyo na mashiko kwa umma.
3. Agenda setting/Agenda manipulation(Kuibalaghaza agenda)
Hii ni ile hali ya kuongoza yale ambayo umma unaongea kwa sana kwa kuyapindisha au kuyatengenezea tafsiri ngumu kwa umma kwa mfano " Umma unadai haki moja wapo ni haki ya kuishi ila wataalamu wa kumanipulate wanaishi kwenye hiyo hiyo ajenda wanakuambia unapodai haki hakikisha umetimiza wajibu kumbuka haki inayodaiwa na umma ni haki ya kuishi ila unaambiwa utimize wajibu"
4. Smoke and Mirrors(Moshi na Kioo)
Yaani moshi ukionekana kwenye kioo ni jitu kubwa sana ni kama linashikika hii imekaa hivi kuanzisha mambo madogo ambayo yanachukua nafasi ya mambo makubwa ili kutoa watu kwenye ufuatiliaji wa mambo makubwa. Mfano mambo ya wasanii na michezo yanaweza kupewa nafasi kubwa ilhali kuna mambo ya nchi yanatokota na ni makubwa hayana nafasi, inch fulani deni lipo Trillions za Shilling za kwao 12 ila wao mameshika masuala ya ukabila na upendeleo kwenye vyeo.
5. Red herring (Sill nyekundu)
Hii ni ile hali ya kuiondoa jamii kwenye hoja za kipaumbele kwa kuanzisha hoja mbadala ambazo zitaitoa jamii katika kelele za hoja zao za msingi mfano Goldberg Scandal kwenye nchi hiyo walisema kuna watu wanatengeza taarifa ili kujinufaisha kisiasa na kulichafua kabila fulani, Cashgate scandal kwanini watu mnatengeza hoja za uongo kwa ajili ya minajili ya kisiasa, kuna Scandal ilikuwepo babu wa Loliondo alichukua front page.
Sababu ya kufanya hivyo huenda ikawa:-
1. Kuhalalisha maamuzi ya serikali.
Mfano: kuhalalisha vita, operesheni ya usalama, au sheria mpya.
2. Kuepusha hofu kwa wananchi.
Wakati mwingine ukweli hufichwa au hupunguzwa ili watu wasipate hofu.
3. Kushawishi maoni ya umma.
Kufanya tishio lionekane kubwa au dogo ili watu waunge mkono hatua fulani.
4. Kulinda vyanzo vya taarifa.
Kuepusha kufichua majina ya watoa taarifa au mbinu za kijasusi.
5. Propaganda / taswira ya kisiasa
Kuifanya taasisi au upande fulani uonekane sahihi zaidi ilhali wamefanya sawa au si sawa lakini hulazimishwa kuonekana ni sawa hata kama ni ufisadi wizi ubadhilifu na mengineyo mabaya kwa maslahi ya umma.
Kama kuna lolote unaliona linaendelea kwa pamoja tunaweza kusaidiana kulichambua na kuliweka katika kundi lake kuwa hilo lipo mlengo gani kama ni kweli au ni mbinu za kuingizana maboya
Nipo tayari kurekebishwa na kueleweshwa zaidi karibuni kwa maoni na kila linalotokea tutaarifiane na kulichambua