Sera ya ushuru sifuri ya China yafungua fursa kwa sekta ya kahawa ya nchini Kenya

Sera ya ushuru sifuri ya China yafungua fursa kwa sekta ya kahawa ya nchini Kenya

ldleo

JF-Expert Member
Joined
Jan 9, 2010
Posts
1,276
Reaction score
1,246
VCG31N1243615785.jpg


Kuanzia Mei Mosi, 2026, China itaanza kutekeleza sera ya ushuru sifuri kwa bidhaa zinazotoka nchi 53 za Afrika zenye uhusiano wa kidiplomasia na China. Sera hii inachukuliwa kama fursa muhimu kwa nchi za Afrika kuingia katika soko kubwa la China kwa kuleta bidhaa zao za kipekee na za ubora wa juu. Moja ya nchi zitakazonufaika na sera hiyo ni Kenya.

Ndani ya kiwanda cha kuchakata kahawa pembezoni mwa mji mkuu wa Kenya, Nairobi, wafanyakazi wanakagua na kufungasha mbegu za kahawa aina ya Arabica ambazo zimechakatwa kwa ajili ya kusafirishwa nje ya nchi, huku sehemu ya mbegu hizo za kijani ikiwa njiani kuelekea China.

Kwa Mbula Musau, mwanzilishi wa Utake Coffee, China imeibuka kuwa kituo muhimu kwa kahawa ya ubora wa juu ya Kenya. Muungano wake na soko la China ulianza karibu muongo mmoja uliopita. Muda mfupi baada ya kuanzisha kampuni yake mwaka 2016, Musau alitembelea mkoa wa Yunnan, kusini magharibi mwa China mwaka 2018 na kushiriki kwenye shindano la kahawa. Safari hiyo ilifungua mlango kwa ushirikiano zaidi.

Musau anasema, wateja wa China wanathamini sana kahawa yenye ubora wa juu, na kwamba mauzo mengi ya Utake Coffee nchini China ni mbegu za kijani zenye ubora wa juu zinazopata alama zaidi ya 90, na kuchukua karibu asilimia 40 ya mauzo ya jumla ya kampuni hiyo. Anasema wanunuzi wa China wanaweka umuhimu mkubwa sana katika ufuatiliaji, kwani wanataka kujua ni wapi hasa kahawa inatoka, nani amelima, na jinsi gani imechakatwa. Musau anasema, China sio tu ni soko kubwa la kahawa, bali pia ni mzalishaji anayeibuka wa kahawa, na hii inaonyesha kuwa soko linaweza kutambua na kukumbatia kahawa ya ubora wa juu, na mwelekeo kama huu unatarajiwa kuunga mkono mauzo ya nje ya kahawa ya Kenya kwa muda mrefu ujao.

Sekta ya kahawa ya nchini Kenya, msingi wa muda mrefu wa mauzo ya nje ya kilimo ya nchi hiyo, inapata kasi mpya wakati matumizi ya kahawa nchini China yanapoongezeka. Kasi hii nzuri iko tayari kupokea umaarufu mkubwa kutokana na sera ya China ya ushuru sifuri. Kwa kampuni ndogo na za ukubwa wa kati kama Utake Coffee, hatua hiyo inatarajiwa kupunguza kwa kiasi kikubwa gharama za kuingia kwenye soko.

Musau anasema, kwa kuondolewa kabisa kwa ushuru, bei ya ushindani itaongezeka kwa dhahiri, na anaongeza kuwa kampuni yake inatarajia kupokea maagizo zaidi na inapanga kupanua operesheni zake. Kufuatia maonyesho ya karibuni, tayari amesafirisha sampuli kwa wateja wa China na wanaunda uhusiano mpya.

Kwa mujibu wa Musau, faida inatarajiwa kwenda mbali zaidi ya thamani ya mauzo. Kadiri wateja wa China wanavyokuwa na mahitaji anuai, kutoka kahawa ya jadi hadi vidonge na vinywaji baridi, kuongezeka kwa mahitaji kunaweza kujenga athari chanya katika mnyororo wa thamani, na hatimaye kunufaisha wakulima wadogo.

Utake Coffee inalenga kwenda mbali zaidi ya uuzaji wa mbegu za kijani za kahawa kwa kutoa kahawa zilizobanwa kwenye soko la China, hatua ambayo Musau anasema itatoa nafasi zaidi za ajira kwa vijana wa huko na kuongeza thamani katika chanzo.
 
Back
Top Bottom