Usiwe na shaka, tuko wengi!!
Hivi watu wanapata wapi muda wa kuzingusha macho mitandao yote...Yaani umalizane na MMU, halafu uchungulie Siasa, Chit chat na JF photos, then ukimbilie FB, twitter and kwingine...Huo muda utapata wapi?? Kazi zingine je? Na muda wa kupiga story na wapenzi wetu je??
Mie nitabaki hapa hapa JF na huko kwingine watanisamehe!!
Babu DC!!
Wengi walioko JF wanadai kama wewe kuwa hawako Facebook wala Twitter. Pitia threads zote zinazolinganisha JF na Facebook utakuta wengine mpaka wanauliza facebook ndio nini. Ina maana kweli watu kama hawa hawaijui Facebook? Kuna mtu ambaye anaitumia JF lakini hajawahi kusikia mtandao unaoitwa Facebook?
Je, kwa upande wako Unajiepusha vipi au, ...nini msimamo wako unapokumbana na comments za ajabu ajabu kwenye profile page ya mwenza wako, iwe ni kwenye wall, picha (incl tags), 'Questionable' friends au hata likes na private mails anazotoa na yeye anazopokea? how far can you tolerate each other,...au 'unakufa' na tai yako shingoni?
Kwanza kabisa inabidi tukubali kuwa wa kulaumiwa hapa sio hiyo mitandao bali watumiaji wake. Hili ni muhimu sana. Kuna watu wanatengeza pesa nzuri sana Facebook na ukiwaambia kuwa huo mtandao unaharibu mahusiano ya kimapenzi sijui kama watakuelewa. Pia wapo wengine watakuambia kuwa Facebook imewasadia kupata wachumba, mume/mke, nk.
Kwa hiyo, madhara ya Facebook yanategemea na mtumiaji mwenyewe. Nina uhakika wakati teknologia ya simu za mikononi ilipoingia, watu pia walikuwa wanalalamika kuwa mobile phones zinaharibu mahusiano. The same was wakati teknologia ya barua pepe ilivyoingia. Kama Facebook, Twitter, nk, isingekuwepo bado watu wangeendelea kulalamikia mobile phones kwa kuharibu mahusiano.
Kama Facebook inavyoweza kuharibu mahusiano kati ya wanasiasa na wananchi, pia inaweza kuharibu mahusiano ya kimapenzi. It all go down kwa mtumiaji mwenyewe. In deed, wanasheria wa nchi zilizoendelea siku hizi wana-rely sana kwenye ushahidi kutoka Facebook kwenye kesi za divorce. Lakini kwa upande wa Tanzania, ni watu wangapi wanatumia Facebook, let alone internet mpaka zivunje mahusiano? Last time I checked number ilikuwa ndogo sana. Na wengi wanaotumia hiyo mitandao hawako kwenye mahusiano.
Watu tunaweza kuilamu Fecebook kwa kuvunja mahusiano, lakini tuwe wakweli. Is Facebook really the root cause of relationship breakdown? Sio kwamba, tunajaribu kuyakimbia matatizo badala ya kuya-face na ku-deal nayo? Bado naamini Facebook ni means of communication whether you're breaking up or just getting together. Naamini Facebook ni njia tuu ya mawasiliano kama ilivyokuwa barua, na sasa ilivyo simu and emails. If you face (not facebook) and treat (not tweet) your problems, sidhani kama Facebook or Twitter will be a threat to your relationship.
Face your problems don't Facebook them.
Treat your issues don't Tweet them.
Your social network may be online, but your troubles don't have to be!