Snitch ndiye mtu hatari zaidi🙌

2017 Ilinitokea hii, sisahau maishayangu yote.

Jamaa alikuwa akifanya kazi sehemu flani sasa alikuwa akija kunitembelea kazini kwangu.

Tukazoeana, baada ya muda akawa rafikiangu sana sana asana.

Sikumoja akaniambia anaomba nimtafutie nafasi kwenye ninapo fanyia kazi mimi kwasababu kazi anayo fanya anapata ela ya kulatu hawezi fanya kitu kingine chochote.

Nikaona sio ishu nikamvuta nikamtambulisha kwa mkurugenzi nikamtafutia nafasi nzuri mambo yakawa fresh.

Siku zilivyo kwenda nikaamua kumfundisha kaziyangu kwa vitendo then nikamwambie aende akasome kidogo akapata cheti, alivyorudi
Nikamfanya kuwa msaidiziwangu,daah.

Kilicho fuata Mungu mwenyewe ndio anajua jamaa rohoile ya kunisnich aliipatia wapi.

Yani kunaishu nilimfundisha nikamuonyesha jinsi ya kupata pesa, tukawa tunafanya pamoja lakini jamaa alinirecodi na kupeleka kilakitu kwa mkurugenzi, aisee, sitaki hata kukumbuka.

Baada ya muda mflani nilipokwenda rotation kurudi nikakuta mambo yame haribika na kazi imeisha,.
Nilijiuliza sana what happened, sikupata jibu, alafu lijamaa linanipigisha stori tu na kuchekacheka lenyewe.

Mungu mkubwa baada ya kuondoka skumoja mkuu akanipigia sim akaniambia A To Z nilicho fanya na aliempelekea taarifa zote.

Nili huzunika sana, ila Mungu mwema this time na fanya mambo yangu mwenyewe na jamaa linajua nasonga mbele mara kumi ya linivyo kuwa pale.

Nikama Mngu alinifanyia njia kuondoka ili mambo yangu yazidi kunyooka.

Thanks God umefanya njia pasipo na njia.
 
2017 Ilinitokea hii, sisahau maishayangu yote.
Pole mkuu😢
Sina hata la kusema aiseee 🙌
Mungu mkubwa baada ya kuondoka skumoja mkuu akanipigia sim akaniambia A To Z nilicho fanya na aliempelekea taarifa zote.
Na elewa ulivyohisi maumivu 😭
Hongera sana mkuu
yaan watu wa aina hiyo wanasababisha hata wengine wenye uhitaji na wasiokua na roho mbaya wakose msaada

Kwa story yako sidhani kama unaweza kumshirikisha mtu mwingine issue zako muhimu
 
si wanasema jifanye mjinga

mda mwingine ukweli humuweka mtu huru

Aiseee hapo pengine mkiwa wote sasa anakusifia japo ukiwa makini utagundua ana fake

Wengine una kuta kakuzi ila tu hataki umfikie au upate na wewe msije kufanana
Marafiki waliokuzidi ndio marafiki sijui kwanini wengine huwageuza kuwa maadui!
 
80% Binafsi sijawah kuwa na mwana anaetaka tushindane! Siku yoyote ninayomjua tu namkatilia mbali siku hiyohiyo. Na sio rafiki tuhata ndugu

Na wale ambao naona kabisa mitikas yao na yangu haielewan nampunguza kabisa.
 
Bado mnaendekeza ushost na wanawake tu? Hamkomi

Mi wanawake wenzangu nishawakatia laini zamani Sana,wivu roho mbaya, husda, uchawi...wanini mimi aku!

Wanaume wako poa sana,hata michongo ya hela asee ndo wananivuta na kunipa ramani
 
80%
Binafsi sijawah kuwa na mwana anaetaka tushindane! Siku yoyote ninayomjua tu namkatilia mbali siku hiyohiyo. Na sio rafiki tuhata ndugu

Na wale ambao naona kabisa mitikas yao na yangu haielewan nampunguza kabisa.
Wewe hulembi mwandiko 😅
Longolongo nyingi kumaliza miti😅
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…