Ninakuomba sana sana uwe mwangalifu na statements zinazoweza kuchukuliwa vibaya zikaonekena ni sera za nchi na kutusumbua mbele ya safari. Kumbuka hapa, kama ilivyotanzania kuna matabaka mengi sana ya watu. Wapo wanaoweza kuelewa makosa na udhaifu wa msemaji, lakini wapo ambao hawajui kuchambua wao kila kitu wakikisikai kinasemwa hata kama kinavunja katiba na kisheria hakiwezekani, wanashika bango kwamba uliwaambia!. Gharama ya kuwarudisha kwenye msingi, ni kubwa kuliko watu kuzuia ndimi zao.
Tanzania haina utaratibu wa kuchagua viongozi kwa mtindo wa kubadilishana dini.
Hatumchagui mtu kwa dini yake kwa sababu hatutegemei kupata miongozo inayohhusiana na dini za watu. Tunauhuru wa kuchagua dini moja mfululizo ili mradi tunapata kiongozi sahihi anayehitajika na mwenye maono na uwezo wa kukidhi haja za watanzania.
Ingelikuwa ni dini basi hata Wabung wangebadilishana, madiwani, wenyeviti wa mitaa n.k. Kama iingelikuwa ni kanuni ya nchi, mbona zanzibar hawajawahi kuwa na kiongozi wa dini nyingine zaidi ya Waislam?
Tanganyika vile vile haijawahi kuwa na raisi wa dini zingine zaidi ya Wakristo na Waislam? Nani alikuambia kuna kupokezana kidini? Acha kabisa hizo itikadi. Kama ilitokea ilitokea coincidentally tu lakini haipo na hatuwezi kuiweka kuwa ni utaratibu unless tunataka matatiz.
Vinginevyo, ukiondoa hilo la mambo ya dini, naunga mkono hoja.