Slaa tishio CCM Uchaguzi 2015

Slaa tishio CCM Uchaguzi 2015

Kweli Dr.Slaa ni mfano wa kuigwa kwa ccm wala wasione aibu na kuanza kumchafua. Mwaka 2010 ccm wamemkashifu Dr.Slaa wakisema elimu bure haiwezekani,leo wanasemaje? Dr.Slaa ndani ya CHADEMA imara kwa sera zinazotekelezeka alisema inabidi vifaa vya ujenzi vishuke bei ili kumwinua mwananchi masikini kimakazi lakini ccm gambaz wakasema haiwezekani,leo kina Prof.Tibaijuka wanasemaje? Au tusubirie nyumba za walalahoi za NHC zinazouzwa 200mln tsh? Acheni siasa za kipuuzi enyi wanaccm,mnapomchafua mtu ambaye watu masikini na wanyonge wanamwamini mnajipunguzia credit wenyewe.Mbona mnakosa shukrani,Dr.Slaa aliwambia msione haya kutekeleza ilani ya CHADEMA (kama ambavyo JK anatekeleza ilani ya katiba mpya ambayo ccm hamkuwa nayo) maana mkitekeleza mnabarikiwa vile wananchi wanapata unafuu!
 
Juzi Jumapili nimezika jirani yangu aliyefariki baada ya kujifungua mtoto wake, mwezi wa kumi na moja nimezika mke wa shemeji yangu aliyebakia na uchafu tumboni kwa muda wa wiki mbili toka ajifungue, mwezi huo huo nilizika rafiki wa mke wa mdogo wa jamaa tuliyeoa familia moja mtoto na mama walifariki at pa, jana mtoto wa marehemu tuliyemzika jumapili nae kafariki wote hawa hapa hapa dar es salaam.

Katikati ya vifo vyote hivi vya kizembe kabisa anajitokeza mtu mwenye mamlaka katika uendeshaji wa serikali yetu anatutangazia kwamba fulani ana kadi ya CCM na anailipia. what the ****!!!!

Hayatuhusu
 
Hii inanipa mashaka sana kumbe hata kama si kushinda uchaguzi wa 2010,kura za dr slaa zilichakachuliwa sana.Ni kwanini aandamwe kila siku na ccm?kwanini ccm wanataka kummaliza kisiasa?watapata faida gani dr slaa akifa kisiasa?ni kwanini ccm wasipambane nae kwa hoja wanapambana kwa mbinu chafu?kwanini wanunue mamluki kama kweli wanajiamini?kwanini hizo nguvu wasizitumie kuwatumikia wananchi?

Nionavyo mimi kuchafuliwa kwa dr slaa kunazidi kumjenga na kumpa umaarufu mara dufu
 
Hii inanipa mashaka sana kumbe hata kama si kushinda uchaguzi wa 2010,kura za dr slaa zilichakachuliwa sana.Ni kwanini aandamwe kila siku na ccm?kwanini ccm wanataka kummaliza kisiasa?watapata faida gani dr slaa akifa kisiasa?ni kwanini ccm wasipambane nae kwa hoja wanapambana kwa mbinu chafu?kwanini wanunue mamluki kama kweli wanajiamini?kwanini hizo nguvu wasizitumie kuwatumikia wananchi?

Nionavyo mimi kuchafuliwa kwa dr slaa kunazidi kumjenga na kumpa umaarufu mara dufu
MKUU umeshaambiwa kuwa "mti wenye matunda bora na yaloiva ndio unaotupiwa mawe na vigingi" nao ni Dr Slaa.
 
Wanazo data sahihi jinsi alivyowachachafya 2010. Sasa wanatafuta njia ya kutokea 2015.
 
Hii inanipa mashaka sana kumbe hata kama si kushinda uchaguzi wa 2010,kura za dr slaa zilichakachuliwa sana.Ni kwanini aandamwe kila siku na ccm?kwanini ccm wanataka kummaliza kisiasa?watapata faida gani dr slaa akifa kisiasa?ni kwanini ccm wasipambane nae kwa hoja wanapambana kwa mbinu chafu?kwanini wanunue mamluki kama kweli wanajiamini?kwanini hizo nguvu wasizitumie kuwatumikia wananchi?

Nionavyo mimi kuchafuliwa kwa dr slaa kunazidi kumjenga na kumpa umaarufu mara dufu

watapata faida kubwa sana kuendelea kula mali za watanzania bila kuwepo mtu wa kuwasumbua
 
mawazo ya chooni.
Labda kama unaongelea kule uchagani na kule karatu

Kumbe chooni nako kuna mawazo? Punguza Munkari Ngwendu. Lakini Mkuu hukusema kama mawazo ya chooni ni mabaya au mazuri
 
Hata uchaguzi mkuu mwaka jana 2010 Dr. Slaa alishinda hivyo hivyo na alimshinda JK ila walichakachua kama kawaida yao magamba!
Huu utafiti unatia wasiwasi, Maana siamini kama Dk Slaa alishindwa.
 
Ni ukweli usopingika kuwa ccm wanahofu kubwa kwa watz kurejeshema mali zao zilizofichwa na wezi dr slaa akiwa rais.
 
Wanafanya JUHUDI ili kupOTEeza uhai wake.ila wajue mungu ametupilia mbali utawala wa ccm kwa jinsi walivo mtenda dhambi.
 
Habari wanajf, haya ni mawazo na fikra zangu tu. Binafsi naona Dr. Slaa nafaa kabisa kuwa mgombea wa urais mwaka huu kupitia Ukawa tofauti na Prof. Lipumba. Nina sababu zifuatazo.

1. Dr. Slaa anamvuto na kupendwa na wengi katika mambo ya siasa
2. Nchi yetu haina upendeleo katika mambo ya dini, hivyo sasa ni zamu ya rais mkristo kuongoza nchi kama ambavyo nchi yetu imejiwekea utaratibu huu.
3. Watu waliosoma sana na wenye elimu ya juu kabisa mara nyingi hawafai kupewa nafasi nyeti kama hii, hawa ni watendaji wazuri wanatakiwa watumie muda mwingi kufanya research na kuandaa policy mbalimbali kwa ajili ya manufaa ya nchi. Elimu kama ya Dr. Slaa ndiyo inafaa zaidi hivyo Lipumba angalau apewe uwaziri mkuu sio mbaya sana.

Hayo ni maoni yangu kama unacho cha kuongezea karibu
 
Kama kuna utaratibu wa kubadilisha Rais kwa dini zao basi safari hii awekwe Mlutheri....kwa vile ukawa tunawaombea wachukuwe nchi..hebu tuambie ni Mlutheri gani yuko ukawa anaefaa
 
Kama kuna utaratibu wa kubadilisha Rais kwa dini zao basi safari hii awekwe Mlutheri....kwa vile ukawa tunawaombea wachukuwe nchi..hebu tuambie ni Mlutheri gani yuko ukawa anaefaa
Mkuu wanaagalia dini sio dhehebu
 
Kama kuna utaratibu wa kubadilisha Rais kwa dini zao basi safari hii awekwe Mlutheri....kwa vile ukawa tunawaombea wachukuwe nchi..hebu tuambie ni Mlutheri gani yuko ukawa anaefaa

Ni kweli mkuu maana Waislamu wawili tayari, RC wawili sasa ni zamu ya dhehebu jingine, tumechoka kunyanyasika.
 
Back
Top Bottom