Slaa tishio CCM Uchaguzi 2015

Slaa tishio CCM Uchaguzi 2015

Kweli hizi ni busara tosha,tunahitaji wazee wenye busara ndani ya Chadema kama Mtagazwa!Siyo kila mwenye mvi kichwan amejaa busara but Arcado you have something wise to say!Just spoke it out more!
 
Kama kweli Dr. Slaa ni mwanachama MTIIFU wa CCM (according to Nape) Mimi nawashauri CCM, 2015 wamsimamishe Dr. Slaa kugombea nafasi ya URAIS wa JMT. Kwasababu ndiye mwana CCM pekee anayekemea UFISADI NA RUSHWA kwa maneno na vitendo. Nafikiri CCM wakimsimamisha Dr. Slaa watapa USHINDI wa KIMBUNGA kuliko hata ule wa JMK 2005

NI WAZO LA LEO
 
CCM wamelogwa? watende mema ili watu wawaamini siasa za majitaka hazitawasaidia watabaki mavuvuzela tu
 
Well said mzee, wanahangaika na kadi ya Dr. Slaa wakati watu wanakufa hospitalini hakuna dawa na waadhirika wa HIV/AIDS wakipewa ARV feki za kuwamaliza zaidi. Habari yao kwisha they cant go any more.......

Ukweli mtupu.... Jana nilienda hospitali ya Wilaya kupata matibabu...maabara hazifanyi kazi, hakuna dawa na wauguzi wachache waliopo wamenuna ile mbaya. CCM shughulikieni huduma za jamii achaneni na Dr. Slaa
 
Ntagazwa kweli sikio a kufa, Ile kesi yake ya Kutapeli tishet imeyumbisha uwezo wake wa kutafakari, ajiulize misingi ya TANU iliruhusu julius Nyerere kumteua ndugu yake Joseph Butiku kuwa Katibu mkuu kiongozi ikulu, Sofia kawaw akateuliwa kuwa Mwenyekiti wa UWT, wakuu wote wa majeshi ukitoa Abdallah Twalipo walikuwa ndugu zake nani? Ajiulize Joseph Nyerere mdogo wake julius Nyerere alieuliwa na nani kwenye nyadhifa alizoshika mpaka anakufa?.asitudanganye Alihama CCM alipotoswa kwenye kinyang'anyiro cha ubunge Kigoma je alisubiri kura zisitoshe ndo ajue ubaya wa CCM bora ya mwenzie mpendazoe anaeleweka alitoka akiwa mbunge!
 
Hapa na wewe unataka kuwadanganya watu.

Sofia Kawawa, aliteuliwa au alichaguliwa? Kwa wakuu wa Majeshi, tukianzia Sarakikya, Kyaro, Musuguri unataka kusema walikuwa ndugu zake Mwalimu, ni uwongo mkubwa. Msuguri alikuwa akitoka kijiji kimoja na Mwalimu lakini siyo ndugu yake, Kyaro alikuwa anataoka Mkoa wa Mara lakini si ndugu wa Mwalimu, Sarakikya hakuwa ndugu wa Mwalimu. Butiku alikuwa mtu wa Karibu sana na Mwalimu lakini hakuwa ndugu yake. Joseph Nyerere alikuwa na wadhifa gani aliokuwa amepewa na Kaka yake? Aliwahi kuwa M/Kiti wa TANU Youth League lakini ni kwa kuchaguliwa. Unaandika vitu vya jumla jumla visivyokuwa na ukweli wowote. Hapa Ntagazwa haongelei kiongozi ndugu wa kuchaguliwa bali wa kuteuliwa na wewe ndugu yake. JK anaongozwa zaidi na undugu na uswahiba katika uteuzi wake, huo ni ukweli ambao utaendelea kubakia katika kumbukumbu za historia za uongozi wa Taifa letu kuwa, 'Aliwahi kutokea kiongozi aliyeitwa Jakaya ambaye mara nyingi katik uteuzi wa viongozi wa serikali aliongozwa zaidi na undugu, urafiki na uswahiba kuliko uwezo mtu, kitu ambacho kiliufanya uongozi wake ushindwe kutekeleza wajibu na kudharaulika sana na wananchi kiasi cha wananchi wengi kujilaumu kwa nini walimchagua'.

Ntagazwa kweli sikio a kufa, Ile kesi yake ya Kutapeli tishet imeyumbisha uwezo wake wa kutafakari, ajiulize misingi ya TANU iliruhusu julius Nyerere kumteua ndugu yake Joseph Butiku kuwa Katibu mkuu kiongozi ikulu, Sofia kawaw akateuliwa kuwa Mwenyekiti wa UWT, wakuu wote wa majeshi ukitoa Abdallah Twalipo walikuwa ndugu zake nani? Ajiulize Joseph Nyerere mdogo wake julius Nyerere alieuliwa na nani kwenye nyadhifa alizoshika mpaka anakufa?.asitudanganye Alihama CCM alipotoswa kwenye kinyang'anyiro cha ubunge Kigoma je alisubiri kura zisitoshe ndo ajue ubaya wa CCM bora ya mwenzie mpendazoe anaeleweka alitoka akiwa mbunge!
 
Hapa na wewe unataka kuwadanganya watu.

Sofia Kawawa, aliteuliwa au alichaguliwa? Kwa wakuu wa Majeshi, tukianzia Sarakikya, Kyaro, Musuguri unataka kusema walikuwa ndugu zake Mwalimu, ni uwongo mkubwa. Msuguri alikuwa akitoka kijiji kimoja na Mwalimu lakini siyo ndugu yake, Kyaro alikuwa anataoka Mkoa wa Mara lakini si ndugu wa Mwalimu, Sarakikya hakuwa ndugu wa Mwalimu. Butiku alikuwa mtu wa Karibu sana na Mwalimu lakini hakuwa ndugu yake. Joseph Nyerere alikuwa na wadhifa gani aliokuwa amepewa na Kaka yake? Aliwahi kuwa M/Kiti wa TANU Youth League lakini ni kwa kuchaguliwa. Unaandika vitu vya jumla jumla visivyokuwa na ukweli wowote. Hapa Ntagazwa haongelei kiongozi ndugu wa kuchaguliwa bali wa kuteuliwa na wewe ndugu yake. JK anaongozwa zaidi na undugu na uswahiba katika uteuzi wake, huo ni ukweli ambao utaendelea kubakia katika kumbukumbu za historia za uongozi wa Taifa letu kuwa, 'Aliwahi kutokea kiongozi aliyeitwa Jakaya ambaye mara nyingi katik uteuzi wa viongozi wa serikali aliongozwa zaidi na undugu, urafiki na uswahiba kuliko uwezo mtu, kitu ambacho kiliufanya uongozi wake ushindwe kutekeleza wajibu na kudharaulika sana na wananchi kiasi cha wananchi wengi kujilaumu kwa nini walimchagua'.

Wewe usie mnafiki na usie muongo tutajie Ushemeji wa Kikwete kwa Mwema, Tutajie Dadake au ndugu yake JK alieolewa na Mwema au ndugu wa mwema alieolewa na JK, Usifanywe kokoro la kubeba Propaganda bila kushirikisha Bongo yako, Unasema Sofia kawawa hakuteuliwa alichaguliwa hivi unajua wakati huo watu walikuwa wanachaguliwa vipi? unajua Kamati kuu ya kuwapitisha Joseph Nyerere na Sofia Kawawa Nyerere na Kawawa HAWAKUWA WAKITOKA ukumbini ili kuonesha uadilifu, Imarisheni uwezo wa Viongozi wenu kwa kuwahoji wanapoleta Madai ili muwajengee uwezo wa kuzungumza vitu vyenye Uhalisia, imekuaje wataje udugu wa Mwema na JK miaka saba tangu ateuliwe???.
Unamtuhumu JK kwa ujamaa na udugu halafu unakiri kuwa hao niliowataja hawakuwa ndugu wa Nyerere bali wametoka Kijiji kimoja. Mnamtetea Nyerere kwa kuruhusu Mdogo wake kuteuliwa kuwa Mwenyekiti wa UV CCM Taifa Halafu mnamshambulia Jakaya kwa Mwanae kuwa Mjumbe wa NEC kutokea Bagamoyo. Tulimchukia sana JK kipindi kile mnampenda sana, sasa tunampenda sana kwa kuwa nyie mnamchukia sana!
 
Hivi wakuu yule boss wa TISS na mkuu aliyedanganya umri, ili muda wa kula kasungura ka Taifa kaendelee ni ndugu?

I mean ni mtu na mdogo wake?
 
Nina hasira mno na hawa majambazi wakubwa wa uchumi wetu kutuona watanzania kama mazezeta. Ninasema hivi kwa sababu wao wanafikiri kwa kukichafua CHADEMA pamoja na viongozi wake wanatufanya watanzania tuamini uwongo wao wakiwa na fikra kuwa watanzania ni wajinga na hatuna uwezo wa kuchambua mambo. Ninawaombeni sana Ccm na serikali yenu kama wengi walivyokwisha kuwaasa, tatueni matatizo yanayowasibu wananchi na siyo kumtafuta Dr Slaa na CHADEMA.
 
Hapa na wewe unataka kuwadanganya watu.

Sofia Kawawa, aliteuliwa au alichaguliwa? Kwa wakuu wa Majeshi, tukianzia Sarakikya, Kyaro, Musuguri unataka kusema walikuwa ndugu zake Mwalimu, ni uwongo mkubwa. Msuguri alikuwa akitoka kijiji kimoja na Mwalimu lakini siyo ndugu yake, Kyaro alikuwa anataoka Mkoa wa Mara lakini si ndugu wa Mwalimu, Sarakikya hakuwa ndugu wa Mwalimu. Butiku alikuwa mtu wa Karibu sana na Mwalimu lakini hakuwa ndugu yake. Joseph Nyerere alikuwa na wadhifa gani aliokuwa amepewa na Kaka yake? Aliwahi kuwa M/Kiti wa TANU Youth League lakini ni kwa kuchaguliwa. Unaandika vitu vya jumla jumla visivyokuwa na ukweli wowote. Hapa Ntagazwa haongelei kiongozi ndugu wa kuchaguliwa bali wa kuteuliwa na wewe ndugu yake. JK anaongozwa zaidi na undugu na uswahiba katika uteuzi wake, huo ni ukweli ambao utaendelea kubakia katika kumbukumbu za historia za uongozi wa Taifa letu kuwa, 'Aliwahi kutokea kiongozi aliyeitwa Jakaya ambaye mara nyingi katik uteuzi wa viongozi wa serikali aliongozwa zaidi na undugu, urafiki na uswahiba kuliko uwezo mtu, kitu ambacho kiliufanya uongozi wake ushindwe kutekeleza wajibu na kudharaulika sana na wananchi kiasi cha wananchi wengi kujilaumu kwa nini walimchagua'.
Mkuu, nakupa BIG UP kwa ufafanuzi ulioenda shule, nadhani wengi watakubaliana na ukweli huu
 
Kweli Dr.Slaa kiboko maana yupo kwenye chati zaidi ya miaka 15, kila siku ni kupanda tu
 
Maneno mazuri kabisa yenye busara kutoka kwa Mh Ntagazwa,well said mzee.
 
JK kabakia kulipa fadhila kwa akina Ray C.

Nasikia aibu sana kwamba huyo ndio kiongozi wa nchi! yaani hivyo ndo vipaumbele vyake! Eee Mungu wasamehe wale wote waliopelekea kituko hiki kuingia katika kiti cha urais 2005!!! Pia naomba toba in advance kwa wale wote wenye mawazo ya kuiweka madarakani tena CCM 2015! Kamwe haitatokea!:israel:
 
Back
Top Bottom