Sizonje ndiye nani?Mpendwa Sizonje habari za siku.... natumaini u buheri wa afya kibaiolojia japokuwa kiroho u tofauti...
Rafiki yangu Sizonje nakumbuka enzi zile tukijadili mpira ulivyokua hodari kumlaumu kocha!! Kwamba kocha wa timu yetu hawezi... kocha mzembe na anafuga uvundo....
Kadiri tulipokutana kila baada ya sentensi tatu lazima umseme kocha kila siku ikawa hamkani si shwari!!
Sizonje utakumbuka kocha alikuvumilia sana japokuwa ulikua huwezi!! Mdomo na maneno mengi yalikubeba kwa mashabiki lakini wachezaji wenzio walikujua!! Ulikua bingwa wa kukariri tarakimu za mchezo bila ujuzi na weledi wa mchezo!! Hata kocha alipoonywa sana juu ya kiwango chako kibovu bado alikubeba ingawa ulimsogoa!!
Hayawi hayawi yakawa Sizonje!! Kauli zako zikalipa!! Kocha akastaafu na ukocha ukapewa wewe!! Kila mtu ndani ya timu akiduwaa mashabiki waliolewa kauli zako tamu ziso kifani walikubeba hatimaye ukawa kocha!!
Awali ulionesha uwezo wa kukonga mashabiki kwa sifa na vitimbi kemkem!! Siku zikasonga mashabiki wakaona timu inarejea nyuma kuliko ilikokuwa kwa kocha mzembe!!
Nakujua Sizonje!! Hupendi kukosolewa na wala hupendi kimya cha sifa!! Vigelegele vya mashabiki na vifijo vimekoma!! Mbinu zote za michezo ulizotumia zimebuma!! Timu inarudi nyuma kwa kasi na wachezaji wameshapoteza mori!! Kila ugusapo sasa hapagusiki!! Wachezaji wanaonesha ari machoni pako tu lakini uwanjani wamedorora!!
Sizonje usichanganyikiwe... mambo bado ndio kwanza safari inaanza!! Ishike ngao na kigao kuyahimili majira!!!
Kwa leo naishia hapa Sizonje nikija mjini ntakutembelea tule maboga ya enzi zetu.
-----------------------------------------------------------------
UPDATES:
----------------------------------------------- ---------------
Wakuu napenda kuwaarifu kuwa nimepata taarifa nyeti na rasmi kuwa kocha wetu mpendwa Sizonje ameusoma uzi huu na comments zenu zote. Shukrani kwa wote mliotoa ushauri kwa kocha wetu.
mwingine yupo anaitwa Le MutuzJamani mmeniacha Gizani.sizonje ndo nani
Pogba naye ni nani?SIZONJE sijui anapeleka wapi timu.....
Alafu mbona Sizonje amepewa majina mengi this time?.......
Mala Juma Ponda Mali ,Mala Nyampala,Tembo, Sasa nasikia anaitwa Trump ......
Kuna ukweli juu ya majina ya Shizonje?.......
Humjui Yohana Mvinyo, halfcast wa ki nyarwanda?Jamani mmeniacha Gizani.sizonje ndo nani
Jesca akikufinyia kwa ndani mdai risiti. Babake kasema.ukienda kwa mama ntilie,dai risiti..uwiiiiii,sizonje nikija mjini ntakuletea maboga na viazi..
Kwa ku kremu anatisha, anajua hata idadi ya nywele za kwapani za wote alowateua.Hata kamati za ufundi anazishauri yeye sio yeye ashauriwe nao!!
kama imesemwa na TRA hawaikanushi na mbaya zaidi wananchi hawasomewi tena mapato ya kila mwezi kwanini tusiamini ni kweli?Hivi hii ni kweli?
Kama kukaa ikulu ndo hivi bora akae dog nitam respect.Hata mkiimba nyimbo gani MTU wenu asahau kwenda Ikulu kabisaaaa!
Kweli hii kitu ya kusomewa mapato yetu sijui imeota mbawa...nakumbuka mtu mmoja alinimbia hii kusomewa mapato ni kiki ya kuvuta sapoti ya raia baada ya hapo itapotea.....kama imesemwa na TRA hawaikanushi na mbaya zaidi wananchi hawasomewi tena mapato ya kila mwezi kwanini tusiamini ni kweli?
mapato yameshuka wanaona serikali itaonekana imeshindwa kukusanya mapato hivyo haitangazwi tena.Kweli hii kitu ya kusomewa mapato yetu sijui imeota mbawa...nakumbuka mtu mmoja alinimbia hii kusomewa mapato ni kiki ya kuvuta sapoti ya raia baada ya hapo itapotea.....
Kuna maendeleo ya kuongezeka watu wasiojulikanaSasa hayo maendeleo si ndoto ya Alinacha
Sizonje alisema kuna wapiga dili walikuwa wanalipisha kiingilio mlangoni ila hela haionekani..mashabiki wanajaa uwanjani lakini hela hazionekani.....sa sijui kama ni kweli make kocha huyu ana tabia ya uwongo.Ukinunua dai risiti ...teh teh teh!! Sizonje atapata laana ya waathirika wa tetemeko