displayname
JF-Expert Member
- Feb 15, 2013
- 1,972
- 1,091
U.ji.nga ni mtu kujiwezea kuufanya usinilishe maneno vijana wa siku hizi viroba na shisha za kuiga zimewavuruga akili mtaita majina yoote mnayojisikia kuyaita lakini ukweli unasimama asiyefanya kazi na asile na ole wenu na hayo majina ya kebahi msije jutia baadae.Kaka mbona umekazania kwenye tafsiri? Unataka kuuaminisha umma kuwa Rais ndio Sizonje?
Na mtajipeleka tu huko kama ma.nyu.mbu nyie endeleeni muda utasemaHuyo anataka tufungwe kwa uchochezi!!
Mpendwa Sizonje habari za siku.... natumaini u buheri wa afya kibaiolojia japokuwa kiroho u tofauti...
Rafiki yangu Sizonje nakumbuka enzi zile tukijadili mpira ulivyokua hodari kumlaumu kocha!! Kwamba kocha wa timu yetu hawezi... kocha mzembe na anafuga uvundo....
Kadiri tulipokutana kila baada ya sentensi tatu lazima umseme kocha kila siku ikawa hamkani si shwari!!
Sizonje utakumbuka kocha alikuvumilia sana japokuwa ulikua huwezi!! Mdomo na maneno mengi yalikubeba kwa mashabiki lakini wachezaji wenzio walikujua!! Ulikua bingwa wa kukariri tarakimu za mchezo bila ujuzi na weledi wa mchezo!! Hata kocha alipoonywa sana juu ya kiwango chako kibovu bado alikubeba ingawa ulimsogoa!!
Hayawi hayawi yakawa Sizonje!! Kauli zako zikalipa!! Kocha akastaafu na ukocha ukapewa wewe!! Kila mtu ndani ya timu akiduwaa mashabiki waliolewa kauli zako tamu ziso kifani walikubeba hatimaye ukawa kocha!!
Awali ulionesha uwezo wa kukonga mashabiki kwa sifa na vitimbi kemkem!! Siku zikasonga mashabiki wakaona timu inarejea nyuma kuliko ilikokuwa kwa kocha mzembe!!
Nakujua Sizonje!! Hupendi kukosolewa na wala hupendi kimya cha sifa!! Vigelegele vya mashabiki na vifijo vimekoma!! Mbinu zote za michezo ulizotumia zimebuma!! Timu inarudi nyuma kwa kasi na wachezaji wameshapoteza mori!! Kila ugusapo sasa hapagusiki!! Wachezaji wanaonesha ari machoni pako tu lakini uwanjani wamedorora!!
Sizonje usichanganyikiwe... mambo bado ndio kwanza safari inaanza!! Ishike ngao na kigao kuyahimili majira!!!
Kwa leo naishia hapa Sizonje nikija mjini ntakutembelea tule maboga ya enzi zetu.
-----------------------------------------------------------------
UPDATES:
----------------------------------------------- ---------------
Wakuu napenda kuwaarifu kuwa nimepata taarifa nyeti na rasmi kuwa kocha wetu mpendwa Sizonje ameusoma uzi huu na comments zenu zote. Shukrani kwa wote mliotoa ushauri kwa kocha wetu.
Haha shukrani mkuu.Hongera sana kwa mashairi yaliyojaa ukweli, ingawa muanzilishi wa hili jina "sizonje" nae ametekwa na Sizonje na kuamua kumpaka mafuta kwa mgongo wa chupa. Muasisi wa "Sizonje" amesahau kwamba ni yeye aliyejijengea heshma kwa kutaka kwenda kumuona "mjomba" ili amueleze matatizo ya wachezaji na washangiliaji wa timu, lakini leo anaogopa kumueleza "Sizonje" kwani sizonje hataki "kujaribiwa." Tafadhali, naomba mashairi yako ili niingie nayo studio...
Unamtishia nani wewe? We ungekuwa unafanya kazi, usingekuwa maskini kama ulivyo sasa!!U.ji.nga ni mtu kujiwezea kuufanya usinilishe maneno vijana wa siku hizi viroba na shisha za kuiga zimewavuruga akili mtaita majina yoote mnayojisikia kuyaita lakini ukweli unasimama asiyefanya kazi na asile na ole wenu na hayo majina ya kebahi msije jutia baadae.
.....Kama nchi ni lazima ifike wakati tufanye maamuzi magumu,hata kama sio mtu kutoka chama kingine,2020 huyu bwana mkubwa hatufai miaka kumi itakuwa miaka mia
Wote mnaomchukia "Sizonje" ni majipu na wapiga "dili". Kama mnaendesha maisha yenu ya halali kabisa hamwezi kumchukia Sizonje.hshhaaaaaaaaaa hlf ndani kuna giza mlango hauonekani.duuuu
Hanalo hilooo.....Sizonje kashamtibua kila mtu,kabaki peke yake
ooooooooohHata mkiimba nyimbo gani MTU wenu asahau kwenda Ikulu kabisaaaa!