SIYO Jukumu la CHADEMA kuikosoa CCM ili ijisahihishe na kutawala Vizuri

Mzee MM,

Heshima kwako!
Ni jana tu nilikuwa najadiliana na mwenza wangu kuhusu hatma ya nchi yetu na vizazi vyetu.
Nimekuwa na wasiwasi sana, na inaniuma sana kwamba chama kilichopo madarakani kanafanya kitakavyo na sisi wenye nchi tunawaangalia tuu, helpless!
Tunahitaji vyama mbadala, vyama vyenye nguvu, vyama vitakavyo fanana na mahitaji yetu.
Chama cha siasa ni nyenzo tuu, sio MUNGU,
Tunaweza kubadili wakati wowote tunopoona inafaa,
Nasema tena, chama cha siasa ni kama kisu, kijiko, kikombe (sio cha babu), jembe nk
Nyenzo ikichoka, ikivunjika, ikipiga kutu, ikipitwa na wakati, ikikengeuka inabadilishwa tuu,
Tusiogope watanzania,
Hivi vyama vya siasa ni kutusaidia kupata maendeleo,
Havitakiwi viwe mizigo, kansa au miungu,

Tuamke na tulete mabadiliko kwa faida yetu na vizazi vyetu1
 
NDUGU MWANAKIJIJI nakusifu kwa kuandika a very longer article.Lakini kwenye articles yako kuna dosari nyingi sana za kimantiki, maana and kifalsafa.Pegine I will just cite a few of such flaws.Kwanza ni vizuri ukawa na knowlege ya political science based on contemporary studies, particularly about Politics, at global and local level.
Role of opposition parties
Kazi kuu za opposition parties, include, watchdog role (kukosoa serikali iliyoko madarakani), giving alternative viewpoints.The Opposition’s main role is to question the government of the day and hold them accountable to the public.Thus the opposition represents an alternative government, and is responsible for challenging the policies of the government and producing different policies where appropriate. Kwa hivyo CHADEMA wanapoonyesha udhaifu wa serikali such as corruption, mismanagement of the national resources, na faulty policies, mimi naona wako sahihi kabisa kwa vile hatutarajii, kwa mfano, serikali iliyoko madarakani ijikosoe yenyewe. Kwa maana nyingine ni kwamba chadema wanapoonyesha madhaifu ya CCM ni dhahiri kwamba wanaidhoofisha serikali in public eyes, (people loose confidence to their government).Kazi kubwa iliyofanywa na CDM ni pamoja na kuelimisha au kuwafumbua macho milions of Tanzanians ambao walikuwa hawajui jinsi ufisadi ulivyokuwa ukifanywa cladenstinely na madhara yake kwenye jamii yetu.
chadema iCOPY KUTOKA CCM?.
Kwenye article yako umetanabaisha kuwa "CHADEMA kama kweli kinataka kuja kushika madaraka ni lazima kitambue na kianze kufikiri nakutenda kama chama kinachotaka kutawala. Viongozi na wanachama wake, mashabiki na wapenzi wake ni lazima wawe na fikra kama waliyonayo wana CCM na viongozi wao. CCM imejenga imani ndani ya wanachama wake kuwa kinataka kutawala na kitatumia mbinu zozote zile.Ushauri kama huo is absolutelly misleading and also defies the relaity on the ground.Hali halisi inaonyesha kwamba wanachama wengi hawaridhishwi na muelekeo wa chama chao, na kama unakumbuka vyema hata raisi Kikwete aliwahi kulalamika hadharani akikiri kuna mgawanyiko kwenye chama chake, na hata baadhi ya CCM members walipigia kura opposition parties during the 2010 general elections.So hiyo scenario si ya kuiga hata kidogo, na kwa kuiiga ccm hasa kwa this era is tantamount to putting yourself in a melting pot.
wabunge wengi:kuwa na wabunge wengi is a good strategy kwa kutasaidia chama husika kwenye bunge hasa pale to support jambo linalohitaji overwhelming majority.Hivi sasa ambao CCM ina wabunge wengi tumeshuhudia baadhi ya miswaada ya hovyo na isiyo na maslahi kwa taifa imepita kwa sababu tu chama tawala kina idadi kubwa ya MPs.Kwa hivyo kuwa na mkakati wa kuwa na wabunge wengi is a right, viable and pragmatic strategy.
Napenda kuhitimisha kwa kusema kwa kusema kwamba chadema wako on the right path, has few but competent people in all crucial fields.Na ndiyo maana hivi sasa kinaungwa mkono na idadi kubwa watanzania ukilinganisha na miaka ya hapo nyuma.
 
Maoni ya Dk Lwaitama:

Hapa chini nawaletea maoni ya Dk Lwaitama kuhusu makala ya MM kama nilivyoyachote kutoka kwa wanabidii-yeye nafikri hana account hapa. Someni kwa furaha wenye kufurahi:
*************************************************************************************************
Kwa heshima na taadhima naomba tuwe makini katika tafakuri zetu...Mimi nadhani nimakosa ya kimaadili , kimkakati na kimantiki kusema kuwa kazi ya chama cha siasa (kiwe tawala au cha upinzania) nikukidhoofisha chama mshindani wake... Vyama vya
kisiasa vinavyokumbatia dhana hii ni vyama vya kimamuluki...CCM sasa hivi kimesheheni viongozi wengi na wanachama wachache wenye mawazo ya kimamuluki kama haya tangu kilipotekwa nyara na mafisadi kuanzia miaka ya 1995...na hasa tangu Mwalimu Nyerere alipofariki mwaka 1999....Na wameitumia dhana hii kikamilifu

...Ndio maana kinathamini sana ushauri na kazi za kimamuluki za wanachama wake waliokiama hapo nyuma na kwenda upinzani halafu wakarudi kwa kishindo kwa kulubuniwa na ahadi za vyeo na masilahi binafsi mengine ...Nadhani hawa ni kama vile Mh Guninita , Mh. Wasira, na Mh. Tamwe Hiza....Lengo la chama kisichokuwa madarakani ni kugundua na kungamua nini sera bora mbadala za nyakati husika, matumaini na hasira zilizo kwenye vichwa vya wananchi walio wengi ili kuyajumuisha haya yote pamoja na kuyatafsiri katika sera na kauli mbiu za chama hicho mbadala wa sera na kauli mbiu za chama tawala...

Chama adilifu cha upinzani kazi yake ni kuchota mawazo na busara za wananchi walio wengi ambao wamechoka sera na matendo ya watendaji wa chama tawala ...Ni kuelekeza hasira halali za wananchi dhidi ya vitendo vibaya vya chama tawala kwenye kupiga

kura ya kukiondoa chama kilicho madarakani na kukiweka chama chenye kuelewa vizuri zaidi nini umma sasa unatarajia kutoka kwa watawala...Chama cha CCM sasa hivi kimeshindwa kuyangamua matumaini na matakwa ya Watanzania walio wengi...ndiyo maana asili mia kubwa ya Watanzania hawakukichagua chama cha CCM uchanguzi uliopita...au walivipigia kura vyama vya upinzani au hawakwenda kupiga kura kabisa.....

Watanzania wanataka elimu bure, afya bure na ruzuku kwenye vifaa vya ujenzi wa makazi... CCM ya sasa ni chama kisicho madhubuti na ndiyo maana kweli nchi inayumba...Wananchi wanatafuta CCM mpya maana ya zamani ni mfu....

Watanzania wanataka serikari sikivu na yenye mawaziri wasio zidi 15 na mikoa hisiozidi kumi...Wanatamani chama cha CCM kipumzishwe kutawala kwani watendaji wake wamekuwa na kiburi na dharau itokanayo na kutawala kwa muda mrefu.... Watanzania sasa hivi wanakifurahia chama cha Chadema vile wanakiona ndicho chenye walau walau nidhamu ya kutosha ndani kwa ndani kuweza kutumikia wananchi kwa unyenyekevu.....Chonde chonde Chadema kisiige dhana ya siasa za umamuluki za

kudhoofishana kwa kueneza uongo kuficha udhaifu wake....

Kazi ya chama kiadilifu cha upinzani ni kuwa karibu na wananchi na kujua hasira za wananchi za ukweli ni kuhusu matendo yepi ya chama kilicho madarakani kwa miaka 50 hadi leo hii...na CCM kimejidhoofisha na kinazidi kujidhoofisha chenyewe kwa ubaradhuri na jeuri ya kijinga ya viongozi wake wenye kulemewa na mawazo ya kujilimbikizia mali yakichanganywa na ulevi wa madaraka yasiyo na ukomo ...... Chama cha siasa makini daima kikumbuke kuwa wananchi walio wengi si wanachama wa chama chochote cha siasa...Mara nyingi wananchi , hasa vijana, hawakiamini chama chochote kinachokaa madarakani kwa muda mrefu huku maisha ya walio wengi yakizidi kuwa ya matatizo matatizo....Chonde chonde Chadema kisiige dhana za siasa za maji taka zinazotawala CCM ya mafisadi waliowaengua viongozi wa CCM makini kama Dr. Salim Ahmed Salim katika mchakato wa uteunzi wa ugombea wa urais mwaka 2005 kwa dhana kuwa urais ni ulaji na ilikuwa ni zamu ya fulani badala ya fulani kula....

Tutafakari kwa kina juu ya tofauti kati ya nini maana ya upinzani adilifu na upinzani wa umamuluki...

Mwl. Azaveli Lwaitama
 


Haya ndio mawazo ambayo nataka tuachane nayo; upinzani unapokosoa serikali au viongozi wake una lengo la kudhoofisha serikali hiyo ili ianguke kwenye uchaguzi ili wao wapinzani waje kusimamia sera zao za maendeleo na kuwaongoza wananchi kuelekea mafanikio. Lengo la upinzani siyo kuwa upinzani wa kudumu bali kuja kushika dola na kutekeleza sera zake. JIulize kama wapinzani watatoa sera mbadala na sera hizo nzuri za upinzani zikichukuliwa na chama tawala na kufanyiwa kazi upinzani utahitaji kushika dola kwa ajili gani? Wananchi watataka kuwapa dola wapinzani kwa sababu gani wakati sera zao zinatekelezwa na serikali iliyoko madarakani.?

Napendekeza wananchi wetu waanze kujua kuwa CHADEMA ni chama kinachotaka kutawala. CUF kilijua hili na kikahakikisha kinaidhohofisha serikali ya Zanzibar kiasi kwamba CCM walikuwa hawana jinsi isipokuwa kukubali kuwamegea kidogo keki ya kutawala kule Zanzibar.

Kwenye kauli yako ya mwisho ni kuwa ni jukumu la chama tawala kujikosoa na wanachama wake kuikosoa ijisahihishe isije ikakosolewa na chama cha upinzani na kuondolewa madarakani. Mpinzani wa kweli anataka kuona serikali inaboronga inafanya vibaya ili kumulilka udhaifu wa serikali hiyo na kuwafanya wananchi waangalie nje ya chama tawala na kutafuta chama kingine ambacho kitakidhi mahitaji yao.
 
Reactions: Ame
Safi kabisa, CCM jamani basi tu, Tanzania ingekua nchi ya ukweli kabisa kabisa, CCM si chama cha kututawala hata kidogo. Na watanzania tungekuwa wananchi wakweli tusingeweza kiruhusu hiki chama kiendelee kuwa madarakani hata siku moja...
 

Inasikitisha Lwaitama ameweka maneno ambayo mimi sikuyatumia. Kudhoofisha chama tawala haiitaji uongo au majitaka inahitaji mbinu za kisayansi ambazo zinazingatia ukweli. Utaona kwenye makala yangu haihusiani na kuwadanganya umma au kuwafanya wananchi waamini kitu kisicho cha kweli. Huwezi kujenga nchi kwa kusimamia kwenye uongo kwani kutawala kwa kutegemea ulaghai na maneno matamu ndiko kumefanywa na CCM kwa miaka 50.
 
Reactions: Ame

Nilidhani unapinga ninachosema naona unakithibitisha. Kama umesoma vizuri nimeelezea kwa kudokezea kuwa kuna jukumu la kisiasa la wapinzani kuishauri na hata kuisimamia serikali. Lakini at the end siyo maslahi ya upinzani kuona serikali inafanya vizuri kwa kutekeleza sera za serikali mbadala. Lengo la upinzani ni kuiondoa serikali iliyoko madarakani. Huwezi kujitahidi kuiondoa serikali ambayo ina nguvu au inayokubalika.

Lakini inashangaza ati unasema hutarajii "serikali ijikosoe yenyewe" kwanini? Serikali au chama tawala kinatakiwa kijikose chenyewe ili kiwe mbele ya chama cha upinzani. Kisipojikosoea kitaanguka.
Kazi kubwa iliyofanywa na CDM ni pamoja na kuelimisha au kuwafumbua macho milions of Tanzanians ambao walikuwa hawajui jinsi ufisadi ulivyokuwa ukifanywa cladenstinely na madhara yake kwenye jamii yetu.
Hii ni sehemu ya kudhoofisha chama tawala.


You really really missed the point. Kufikiri chama kinachotaka na kujiandaa kutawala siyo kuiiga CCM ni kuwa a true opposition party.

Napenda kuhitimisha kwa kusema kwa kusema kwamba chadema wako on the right path, has few but competent people in all crucial fields.Na ndiyo maana hivi sasa kinaungwa mkono na idadi kubwa watanzania ukilinganisha na miaka ya hapo nyuma.
Wamefanikiwa hivyo kwa sababu wameweza kuidhoofisha serikali na chama kilichoko madarakani.
 

Hicho kinaitwa precision
 
Good message.ni muhimu tuifanyie kazi.nakupongeza kwa kutumia mda wako mwingi kupigana vita hii ya kutufunza na kutuhabarisha.
 

Hapa Mzee MKJJ hutakiwi kusikitika kwa maana hukueleza mbinu hizo za kisayansi ni zipi. ingependeza kidogo kama ungetoka nje ya Rhetoric na kuivisha nyama kidogo kidogo hoja yako ili tuone unasimamia nini katika hii mada.
Je ni mbinu gani hizo za kisayansi unazoziona!, je Propaganda siyo mojawapo?.
Msingi wa hoja hii ni nini?, kwa sababu binafsi ninaona Chadema toka ianzishwe imefanya na inaendelea kufanya juhudi za kuing'oa CCM madarakani, na uchaguzi wa 2010 ni ushahidi tosha kuonyesha ni jinsi gani Chadema ilikuja CLOSE. na kwa mantiki hiyo basi juhudi za kuidhoofisha CCM zimekuwepo tangia awali na hivi sasa ndiyo zimepamba kasi. Kujaribu kuimply kwamba CHADEMA haiidhoofishi CCM ni kutokuzingatia picha pana ya harakati zake. isipokuwa ninakubaliana na wewe kwamba ni lazima juhudi hizo ziongezeke na ziwe za kisayansi zaidi zenye kuzingatia ukweli. siyo kuidhoofisha CCM for the case ya kuidhoofisha, kwa sababu ukidhoofisha na ilhali huna uwezo wa kudeliver so what?.
Kwa maoni yangu ni dhahiri, Kuimarika kwa Upinzani ndo kudhoofika kwa CCM yenyewe
 

Propaganda siyo uongo wala kupaka watu matope. Propaganda ni mwamvuli mkubwa ambapo chini yake kuna mbinu nyingi zenye kujengwa kutoka katika ukweli na zinaweza kutumika.

 
Kwa mtazamo wangu ni kwamba CHADEMA hawaikosoi CCM bali wanaanika UOZO wa baadhi ya watu wa CCM. Mbinu ambayo imewapatia kura si haba mwaka jana. Ukimsoma vizuri Dr Slaa na wenzake wao hawadili na CCM, wanahangaika na watu ndani ya CCM.

Mkuu katika * za mwanakijiji ninahisi na hii ni moja wapo. Nyoka kichwa, identify the stregths of your competitor, identify the weaknesses of your competitor, develop a startegy to weaken the strengths while you are building your strength on the weaknesses of your competitor. Don't waste time to counter any action taken to strengthen your competitor(SWOT Analysis). CCM is now betting on reducing the coverage of all negatives against it while trying to magnify the negatives against CHADEMA. Bacause of desperate, CCM now have started to use fear tactic by action not by words, like planting fire arms to oposition and arrest them and force them to confess or seduce them to do so by bribing(Diwani wa CDM). this trend moves them into planting explosives to torrorise the public and blame CHADEMA
 

Hoping you will be RIP by the time taka zote zikiwa haziko kama huu ndiyo mtazamo wako, wakati watu wakitaka kuona CCM inakuwa chama cha upinzani kabla hawaja rest in peace wewe unataka hilo litokee wakati mjukuu wako akiwa anagombea urais!
 
Mimi nawashukuru sana kwanza Mzee Mwanakijiji sasa taswira yako ni wazi zaidi; pili sheba umetoa ufasaha wa jambo lile lile kwa kuongeza wigo wa maelezo wala si issue ya kukubaliana au kutokubaliana. Kwa sababu watu wote tungekuwa na fikra sawa hakungekuwa na hii kitu inaiwa democrasia. Huku kwetu mimi huiita domocrasia kwa sababu ni kweli kuwa ni maneno maneno. Hili ndilo linatufanya wengine tuwe na msimamo kuwa elimu ya siasa na uraia inahitajika kwa wote watawala, viongozi mbalimbali, watawaliwa na waongozwa.

Hapa kwetu kinachokosekana ni hiyo elimu ya siasa na uraia kama ambavyo mmechangia hapo juu. Ni mbinu ya chama tawala watu wasipate hiyo elimu kwa sababu kwanza mtaji wao mkubwa ni ujinga wa wananchi hasa wapiga kura. Halafu ni mbinu ya kijinga ya watawala kuwa na vyama vya ipinzani walivyovianzisha na kuvigharimia ingawaje kutekeleza hilo mlilolisema la kukosoa serikali ili ijirekebishe. Nadhani wananchi wameliona hilo (ila bado wananchi wanayumba kwa sababu hawapigii sera au agenda ya utekelezaji bali wanapigia mtu (ujinga mwingine))

Neno upinzani ni very negative na limekuwa instituted lakini kuna opportunity ndani yake kwa maana ya uelewa wa wananchi. Kwa sababu
upinzani wanapopinga mategemeo ya sisi wengine huja na mbadala uwe wa utendaji au hoja. Nina maana mawazo yakiwa contaminated huchukui panga kuyakwangua bali unatumia fursa iliyopo ndani ya contamination na kuonyesha mbadala lazima upo.

Kuhusu role za vyama nakubaliana na nyinyi sana lakini si CCM au CDM wanauelewa sawa kuwa uongozi wa nchi ni kuijenga kifikra, kiuchumi, kijamii na kuishindanisha nchi na jitihada za nchi zingine na kuibuka na benefits.

Nashauri tuendelea kuwa chinbuko la fikira lakini tuzifikishe kwa wadhirika(wananchi na baadhi yetu) nje na ndani kwani wengine tunao humuhumu kwa kutoelewa kwao au kutumikia kundi fulani kwa maslahi ya muda tu.
 
Maana ya chama cha siasa ni umoja wa watu wenye itikadi zinazofanana wakiwa na lengo la kuchukua madaraka ya nchi/dola.Chama cha upinzani ni kile kisichohodhi mamlaka ya serikali.

Hivyo basi,chama cha upinzani kitafanya njia yoyote ile ili kuchukua madaraka,ikiwezekana hata nguvu.Ndio maana sometimes kunakuwa na maandamano regardless kama yameruhusiwa au la.Hii inatokana na imani ambayo inatakiwa iwepo ndani ya mioyo ya wanachama kuwa chama chao kinawakilisha interests za umma au at least asilimia kubwa ya umma.

Kuhusu role ya chama cha upinzani kama ilivyoelezwa na dr.fulani kwenye post zilizopita,mie sikubaliani nae hata kidogo,na siamini kama yeye ni mtaalamu wasiasa hata kidogo!Chama cha upinzani au chama chochote cha siasa hakipaswi (not neccessary) kuzunguka na kuchukua maoni ya wananchi.Kiongozi bora sio mtu anayechukua maoni ya wananchi na kuyatekeleza bali ni kutumia hekima,akili na busara zake kama mwananchi kuongoza umma.

CDM ni chama ambacho kina kigeugeu when it comes to philosophy. Ni chama ambacho falsafa yake wakati kinaanzishwa ilikuwa ni kupinga siasa ya ujamaa na kuruhusu wawekezaji binafsi zaidi. Globally,that was a movement in the 90s,but now with the emergence of neo marxism especially in South America brought about by the spirit of the Bolivar Socialist revolution, wananchi wengi wa Africa south of sahara,wanageuza mawazo yao na kugundua kuwa privatisation will not take us nowhere instead ina expand gap kati ya masikini na tajiri.

Dr, Slaa, Zitto ni wanasiasa ambao deep in their hearts wana support government ownership of major means of production, against the "Mtei philosophy" na all of a sudden the whole party including Mbowe (who was viciously defeated in prior presidential race) wanaact like they are socialist. Ndio maana kunakuwa na idea ya mlengo wa kati,something that most political scientists can't really figure out what it means.

Lastly, Chama cha siasa ni lazima kipiganie falsafa yake, na kiweke bayana itikadi yake kwa umma i.e kama ni nguvu ya umma, then you are socialist. Kama ni nguvu ya binafsi,then you are capitalist.Na sio kusubiri kuona bei ya sukari imepanda then kuanza kupiga kelele.

NB: I would really love to see CDM's version of 2011/2012 budget, written as if they are in power i.e their alternative speech.
 

Vyama ni kama organism haviwezi kubakia vimefungwa na fikra za zamani. Kutokana na mahitaji ya nyakati na watu katika zama zao vyama vinaweza kubadilisha. Vinginevyo, wakati wa kuanzishwa CCM ilikuwa ni chama c ha Kijamaa. Leo hii kimekuwa chama kikuu cha kibepari nchini japo mfumo na muundo wake ni wa kijamaa. Think about it. CCM inafuata itikadi gani?
 
WildCard,

Umetusoma vizuri sana. Kudhoofisha CCM ni pamoja na kuanika uozo wao. Mbinu zetu kwa kiwango fulani tayari zimewanufaisha wananchi, km kitendo cha kushasha bei ya sukari baada ya kumpa kikwete siku 9. Kuitaka CCM kutekeleza ajenda za CCM ni mkakati mahususi wa kuidhoofisha.

Watanzania hadi vijijini ambako leo nimekuwa kijiji cha Mambali (wilaya ya Nzega), Bukene na hatimaye Nzega jioni hii imethibitisha Watanzania wanaelewa vizuri tunachofanya, na wakati tumekuwa watetezi wa wanyonge kwa kuanika maovu ya watawala wanaona kabisa kuwa siyo tu tunaidhoofisha CCM, bali tunaifuta kabisa katika uso wa ardhi ya Tanzania. Hata hivyo ushauri wa MMKJ tunaupokea kwa moyo mkunjufu kama tulivyofanya siku zote.

Kikubwa ni dhamira ya kumkomboa Mtanzania na Taifa, mbinu zinaweza kutofautiana kwa kuwa katika mambo haya hakuna formula mmoja kama ilivyo kwa 2+2=4
 


Sijui nchi itakuwa ya namna gani kwani kila baada ya siku 30 aliye kwenye upinzani ataiangusha Serikali na mtawala mtarajiwa nae ataangushwa baada ya siku 120. ( Iwapo nadharia yako itafanya kazi)
 
Mh. Dr Slaa nikupengeze sana kwa kazi nzuri unayofanya. Nakunaliana na MM na kwa kuongezea naomba CDM muengeze efforts kwenye kuweka CCM UNDER THE SPOT-LIGHT kwa ahadi zake. Nimeomba hili kwenye post yangu nyingine naomba nirudie tena hapa kwamba CDM iweke BANGO kwenye office makao makuu -DSM na huko mikoani ya count down to 90 days tangu kujivua gamba. Hii itahamasisha wananchi wengi zaidi kufuatilia kwa karibu ahadi au propaganda za CCM.
 

Dr. poleni kwa kazi ngumu mnayoifanya all in all tuko pamoja and please I do appreciate your commitment katika kuwasaidia wanyonge; may God reward you accordingly.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…