GODZILLA
JF-Expert Member
- Dec 26, 2014
- 5,902
- 10,503
Muda unaenda kasi sana.CCM wanajua fika kwamba kinachowabakisha madarakani ni mfumo wa ovyo wa kisiasa na sio utashi wa wananchi. Katika hali ya kawaida, na kwa kuzingatia kwamba wana namba bungeni, watahakikisha katiba yeyote ijayo haiharibu mazingira yao kisiasa. Mimi binafsi nipo cynical and skeptical na zoezi zima la katiba mpya kusimamiwa na CCM. Mswada huu uliopo ni ushahidi mdogo tu kwamba inawezekana tutakapata katiba mpya lakini itakuwa ni mbovu kuliko hii iliyopo.
Mimi ninaamini kabisa kuwa pakiwepo juhudi zaidi, mshikamano zaidi na akili zaidi, CCM inashindika hata kwa mazingira haya tuliyo nayo. Mazingira ya kuishinda CCM ni mazuri kuliko yaliyokuwepo Kenya kuiondoa KANU. Lakini bado kuna kitu kinakosekana. Vyama vyetu vya upinzani bado vinategemea makosa ya CCM ili viweze kufanya siasa na kupata umaarufu. Ndio kusema CCM wangekuwa smart wakafanikiwa kuweka mambo yao sawa na kupata watu smart katika safu yao ya uongozi, upinzani ungeweza kupwaya ghafla.
Tunahitaji twende mbele zaidi. Ifike mahala watu waone kwamba CDM, kwa mfano, ni zaidi ya chama cha upinzani. Waone kwamba ni chama kinachosubiri kuunda serikali. Inabidi tuwafikishe wananchi mahala ambapo watakosa imani na CCM in totatilty kiasi kwamba hata wamuweke nani na hata waje na sera gani, bado wananchi washindwe kurudisha imani nao. Hatujawafikisha hapo bado. Ukiona watu wanaongelea kwa kusifia kwamba upinzani mzuri unaona wanavyochachafya CCM ujue bado. Lengo la upinzani sio kuichachafya CCM; ni kuiondoa madarakani ili upinzani wapate fursa ya kutekeleza dira, falsafa na sera zao. We are on the right track, but we need to work a bit harder especially in shaping and redirecting our people's attitudes!