Tetesi: Mwabukusi ni Pandikizi la CCM?, Ndiye mvurugaji mkuu wa Demokrasia!

Jaji Mfawidhi

JF-Expert Member
Feb 20, 2016
14,047
20,411

View: https://www.youtube.com/watch?v=rm8wI2pHQ4s

Nimemsikiliza Boniphace Mwabukusi, nimegundua yafuatayo kutoka kwake na namna akivyo

1. Ni Clip ndefu kiasi.
2. Nimeisikiliza yote
3. Alianza kuongea vizuri sana
4. Alitulia na kutoa hoja zenye nguvu. Anaamini Muda unatosha kuwa na katiba mpya kabla ya Uchaguzi.
5. Baadae alibadilika kutoka alichokuwa anaongea.
6. Aliegemea mno CHADEMA na anaona kama ndio chama pekee cha Upinzani.
7. Akabadilika tena na kunanga CCM waliomtuma akawa anawasilisha anayoyataka yeye
9. Ana uwezo mkubwa wa kujenga Hoja, ila hajui kusimamia hoja.
10. Mwishoni hajatoa nafasi kabisa (room) kuwa kuna watu wanaweza kuwa na mtazamo tofauti.
11. Anaamini Katiba ya Warioba na ile pendekezwa ni njia pekee ya kutoka.
12. Nadhani ni vzr akajua NA SISI TUPO N.A TUNA MAWAZO TOFAUTI
13. Pia si vzr kutoa vitisho kuwa ataua mtu akiibiwa kura anaweza kufa yeye maana kifo ni haki ya Mungu pekee.


Mbinu mojawapo inayotumiwa na vyama vilivyo madarakani kushinda uchaguzi unaofuata ni kuandaa watu wao kwa kuwavisha joho la upinzani. Miaka kabla ya uchaguzi, watatiwa misukosuko mingi ili waonekane kweli ni wapinzani. Wataonekana kupingana na serikali na hata kushtakiwa. Wakishaingia kwenye kinyanganyiro cha uchaguzi kupitia upinzani, basi lengo linakuwa limetimia.

Watavuruga mikutano na uchaguzi ndani kwa ndani . Hawa wapo kuanzia ngazi ya kata hadi ngazi za juu kabisa. Tumeyaona haya katika kila uchaguzi kuanzia kuhalalishwa sera ya vyama vingi.

Cha kushangaza na kusikitisha ni kwamba upinzani haujataka kujifunza. Turejee tu historia ya vyama vyote vya upinzani, tutaona vurugu zinazotokana na wafuasi wa chama tawala kuingia upinzani na kurejea kwenye chama chao baada ya uchaguzi.

Jambo hili linajirudia rudia kama mzunguko wa dunia kwenye jua. Msaliti hapashwi kukubalika hata mara moja. Kwa bahati mbaya vyama vya upinzani vimejaza watu wanaobeba bendera zao lakini kimsingi wako upande mwingine. Wataingia wengi kwenye uchaguzi kuwakilisha upinzani, lakini lengo lao ni kuhakikisha chama tawala kinashinda. Kwa mwenendo huu, upinzani hautaweza kutoboa
 
Wewe mwenyewe hueleweki, ukiulizwa utuoneshe ushahidi wa vipi Adv. Mwabukusi anatumiwa na CCM unaweza kufanya hivyo?

Kujenga hoja kweli namkubali jamaa yuko vizuri sana, nami nimemsikiliza nikamuelewa vizuri kabisa.

Hasa alipozungumzia wapi ile Rasimu ya Warioba ilipofia, akadai ilifia bungeni kwa kuletwa Katiba Pendekezwa, hivyo kama ni kujinasua na mkwamo, kujinasua huko sharti kuanzie bungeni kwasababu bungeni ndipo ulipofia, na sio kurudisha mpira kwa wananchi, kwasababu wananchi walishatoa maoni yao yaheshimiwe.

Sent from my SM-G900H using JamiiForums mobile app
 
Sasa ndugu upinzani gani kila siku, hauwezi kuitoa CCM kwenye urais. M nataka tu ubunge, ili mkapate pesa. Hamtaki katiba mpya. Huo ni ujinga. Tutafute katiba mpya tu. Achana na ubunge na ruzuku, hav itawasaidia watanzania. Huyu Mwabukusi yupo sahihi.
 
Huyu jamaa naye nimemuona hayupo serious anadhani upinzani ni vuguvugu na kelele tu. Yaani ni radicalist hapa anataka ajenge political capital ashinde ubunge tu sio kingine.

Sasa CCM hawataki, CHADEMA hawataki, mazungumzo hataki, ammendments hataki, yaani hana compromise wala dialogue ila ni kwamba lazima wote tufuate mawazo yake.

Hapana huo sio upinzani ajifunze kwa Odinga kwenye maandamano ataandamana, kwenye dialogue ataita dialogue na kwenye kuunga mkono serikali kwenye baadhi ya mambo hufanya hivyo.

Huyu ni immature mbaya zaidi Mdude ndio aina ya washauri wake!! What do you expect?
 
Wewe mwenyewe hueleweki, ukiulizwa utuoneshe ushahidi wa vipi Adv. Mwabukusi anatumiwa na CCM unaweza kufanya hivyo?

Sent from my SM-G900H using JamiiForums mobile app
Aliteka mjadala wa bandari ili ajijenge kisiasa ili by the time watu wote wakimuona kama mbadala wa Chadema/Mbowe ndio atumike kudiscredit upinzani.

Unfortunately amefeli kabla hajaanza, mtu huwezi pambana na taasisi ukashinda. Badala ya kuungana na wapinzani yuko busy kutukana wapinzani wenzake sasa hapo si kugawa kura tu.
 
Huyu jamaa naye nimemuona hayupo serious anadhani upinzani ni vuguvugu na kelele tu. Yaani ni radicalist hapa anataka ajenge political capital ashinde ubunge tu sio kingine.

Sasa CCM hawataki, CHADEMA hawataki, mazungumzo hataki, ammendments hataki, yaani hana compromise wala dialogue ila ni kwamba lazima wote tufuate mawazo yake.

Hapana huo sio upinzani ajifunze kwa Odinga kwenye maandamano ataandamana, kwenye dialogue ataita dialogue na kwenye kuunga mkono serikali kwenye baadhi ya mambo hufanya hivyo.

Huyu ni immature mbaya zaidi Mdude ndio aina ya washauri wake!! What do you expect?
Nyie watu hamueleweki mnataka kitu gani, mtu akiwa radical mfano wa Lissu mnamkubali, akiwa Adv. Mwabukusi, au Mdude mnawakataa!
 
Turejee tu historia ya vyama vyote vya upinzani, tutaona vurugu zinazotokana na wafuasi wa chama tawala kuingia upinzani na kurejea kwenye chama chao baada ya uchaguzi.
Walio wengi hurejea kwasabb ya vitisho na wachache huahidiwa vyeo na kwa uroho wao huvifuata vyeo.

Kwa kufanya hivyo ndiyo hujengeka dhana kuwa ccm imeweka mapandikizi upinzani.

Hakuna pandikizi na Mwabukusi ammejitia kwa dhati kuipambania haki.
 
Aliteka mjadala wa bandari ili ajijenge kisiasa ili by the time watu wote wakimuona kama mbadala wa Chadema/Mbowe ndio atumike kudiscredit upinzani.

Unfortunately amefeli kabla hajaanza, mtu huwezi pambana na taasisi ukashinda. Badala ya kuungana na wapinzani yuko busy kutukana wapinzani wenzake sasa hapo si kugawa kura tu.
Hapana. Haya ni mawazo yenu negative dhidi yake, msimhukumu mtu kwa hisia zenu negative.

- Unapodai aliteka mjadala wa bandari una maana gani, kwamba kuna yeyote aliyetaka kuzungumzia ile issue akanyimwa na Adv. Mwabukusi? Wale kina Nshalla, TEC na wengine waliozungumza hawakuwa watu?!

• Ok, kosa lake kwenu najua ni kule kuzungumza kwake bila kuchoka, ndio maana mkawa mnaamini anachofanya ni nguvu ya soda atachoka tu, seriously; mko na siasa za upinzani plastic sana.

Sijawahi kuona baya lolote toka kwa Adv. Mwabukusi, ubaya wake ni mazoea yenu ya kudhani ukiwa mpinzani basi unyamaze usiseme mabaya ya upinzani uliopo, hii mindset yenu ndio kosa lake, nothing else.

Jamaa ni mkweli, na anaisema kweli kama ilivyo, hapepesi wala kuyumbisha maneno, yupo tayari ku sacrifice his everything.

Namkubali sana kwa namna alivyo direct, ni vile tu amekosa support ya kuendana na kile anachoamini toka kwetu, bado tunaishi kwenye kivuli cha mazoea kuamini kwamba wapinzani ni malaika, kumbe uongo.

Sent from my SM-G900H using JamiiForums mobile app
 
Mbowe kahaidiwa ubunge na biashara ya Chadema imeisha dadeki

Nusu mkate ni Hai tu kwingine kote CCM wamekataa 🐼
 
Nyie watu hamueleweki mnataka kitu gani, mtu akiwa radical mfano wa Lissu mnamkubali, akiwa Adv. Mwabukusi, au Mdude mnawakataa!

Sent from my SM-G900H using JamiiForums mobile app
Sijawahi kuunga mkono "radicalism" ya Lissu na mara nyingi nimeongelea hilo kama weakness yake maana ataweza kuwa dikteta kuliko JPM!! Ila mtu kama Heche yuko balanced anajua wapi awe radical, wapi dialogue muhimu na wapi kuunga mkono serikali kama swala ni reasonable.
 
Sijawahi kuunga mkono "radicalism" ya Lissu na mara nyingi nimeongelea hilo kama weakness yake maana ataweza kuwa dikteta kuliko JPM!! Ila mtu kama Heche yuko balanced anajua wapi awe radical, wapi dialogue muhimu na wapi kuunga mkono serikali kama swala ni reasonable.
Hapana tena, lazima ujifunze kuwakubali wanasiasa na namna zao za kuifanya siasa, usitake wote wafanane kama maembe sokoni, hilo haliwezekani.

Kusema Lissu anaweza kuja kuwa dikteta mbaya zaidi ya Magufuli, ni muendelezo tu wa hisia zako negative, hawa watu wa aina ya Lissu, Mdude, na Mwabukusi ni wazuri kwa namna kwamba nyeusi wataita nyeusi, nyeupe itaitwa nyeupe kama ilivyo.

Kuwa na siasa za kubembelezana unazotaka mbele ya CCM inayojiita chama dola ni kupoteza muda, yale maridhiano yaliishia wapi? ukitaka kwenda na siasa za namna hiyo huoni tayari tumeshafeli?

Sent from my SM-G900H using JamiiForums mobile app
 
Unapodai aliteka mjadala wa bandari una maana gani, kwamba kuna yeyote aliyetaka kuzungumzia ile issue akanyimwa na Adv. Mwabukusi? Wale kina Nshalla, TEC na wengine waliozungumza hawakuwa watu?!
Chadema walipokua na operation okoa bandari alikataa kusiriki akitaka naye afanye yake "parallel" na kwamba chadema ndio waache ziara ya kanda ya ziwa ili waende kwenye mikutano yake kwa kutumia resources za chadema kama magari, majukwaa, chopper!! What the hell?
Ok, kosa lake kwenu ni kule kuzungumza kwake bila kuchoka, ndio maana mkawa mnaamini anachofanya ni nguvu ya soda atachoka tu, seriously; mko na siasa za upinzani plastic sana.
Speak when necessary ndio unatunza value yako kwamba ukiongea una material. Sasa agenda ya bandari wabongo wameshaisahau yeye anageukia kutukana kina Mbowe kisa kupokea michango ya Rais kanisani as if Mbowe ni kiongozi wa KKKT?? Hatuwezi jenga upinzani kwa kubomoana tutakuwa na utitiri wa vyama huku CCM ikinawili tu.
Jamaa ni mkweli, na anaisema kweli kama ilivyo, hapepesi wala kuyumbisha maneno, yupo tayari ku sacrifice his everything.
Ukweli upi mnafiki huyu, kipindi yupo NCCR chadema walisusia vikao vya TCD ila yeye akiwa wakili wa chama alikua anaenda na Mbatia huku wakitusi chadema kwa kususa!! Baada ya mgogoro akawa hana chama baadaya kutimuliwa na kina Selasini sasa kwenye kutapatapa ndio mnahisi ni mzalendo sijui anaongea ukweli? If that's the case tuambie kabla ya kutimuliwa NCCR uliwahi msikia akimpinga JPM, kupinga uchaguzi wa 2020 au manyanyaso ya wapinzani 2016-2020?
Namkubali sana kwa namna alivyo direct, ni vile tu amekosa support ya kuendana na kile anachoamini toka kwetu, bado tunaishi kwenye kivuli cha mazoea kuamini kwamba wapinzani ni malaika, kumbe uongo.
Wewe unakubaligi kila mzalendo uchwara wanaofoka baada ya kukosa uongozi!!, si hadi Mpina ulikua unampamba ni mzalendo sahivi kahaaidiwa cheo kimyaaaaa haropoki tena. Huyu akiteuliwa na Samia hutoamini atakavyokana katiba mpya.
 
Chadema walipokua na operation okoa bandari alikataa kusiriki akitaka naye afanye yake "parallel" na kwamba chadema ndio waache ziara ya kanda ya ziwa ili waende kwenye mikutano yake kwa kutumia resources za chadema kama magari, majukwaa, chopper!! What the hell?

Speak when necessary ndio unatunza value yako kwamba ukiongea una material. Sasa agenda ya bandari wabongo wameshaisahau yeye anageukia kutukana kina Mbowe kisa kupokea michango ya Rais kanisani as if Mbowe ni kiongozi wa KKKT?? Hatuwezi jenga upinzani kwa kubomoana tutakuwa na utitiri wa vyama huku CCM ikinawili tu.

Ukweli upi mnafiki huyu, kipindi yupo NCCR chadema walisusia vikao vya TCD ila yeye akiwa wakili wa chama alikua anaenda na Mbatia huku wakitusi chadema kwa kususa!! Baada ya mgogoro akawa hana chama baadaya kutimuliwa na kina Selasini sasa kwenye kutapatapa ndio mnahisi ni mzalendo sijui anaongea ukweli? If that's the case tuambie kabla ya kutimuliwa NCCR uliwahi msikia akimpinga JPM, kupinga uchaguzi wa 2020 au manyanyaso ya wapinzani 2016-2020?
Wewe unakubaligi kila mzalendo uchwara wanaofoka baada ya kukosa uongozi!!, si hadi Mpina ulikua unampamba ni mzalendo sahivi kahaaidiwa cheo kimyaaaaa haropoki tena. Huyu akiteuliwa na Samia hutoamini atakavyokana katiba mpya.
- Hoja yako ya kwanza alikataa kushiriki inahitaji ushahidi, usiishie kuandika tu hivyo inakuwa rahisi unaweza kuandika chochote dhidi yake, tuambie aliwahi kusema wapi alikataa kushiriki, au nani wa Chadema aliwahi kusema hivyo.

- Issue ya bandari alikuwa anaizungumzia kwasababu ndio iliyopo mezani, na ushahidi alikuwa nao, wewe ukawa kimya wakati ule nilipokuuliza ukadai huwezi kuzungumzia jambo la hisia, nilipokwambia IGA ile pale, ukapotea kimya, ndio maana nahisi una chuki binafsi na Adv. Mwabukusi.

- Suala la Chadema kususia vikao ni maamuzi yao, nao kina Adv. Mwabukusi na Mbatia kwenda yalikuwa maamuzi yao pia, usilete udikteta wa kuwapangia watu nini cha kufanya hata kama hawapo kwenye chama chenu, lazima mkomae mjue kuna wakati mtatofautiana kwenye jambo moja, kisha mnaweza kuungana kwenye jambo lingine, sio kimnunia mtu forever hata kama akifanya jambo la msingi, utoto.

- Kumuunga mkono Mpina niko sahihi, na nitaendelea kufanya hivyo mpaka mwisho ikiwa ataendelea kupigania maslahi ya taifa, wewe unayesubiri mpaka kina Mbowe ndio waseme endelea kufanya hivyo, kwangu Mpina ni mzalendo halisi anayepigania maslahi ya taifa, kumuita uchwara ni ubinafsi wako tu.

Sent from my SM-G900H using JamiiForums mobile app
 
Hapana tena, lazima ujifunze kuwakubali wanasiasa na namna zao za kuifanya siasa, usitake wote wafanane kama maembe sokoni, hilo haliwezekani.

Kusema Lissu anaweza kuja kuwa dikteta mbaya zaidi ya Magufuli, ni muendelezo tu wa hisia zako negative, hawa watu wa aina ya Lissu, Mdude, na Mwabukusi ni wazuri kwa namna kwamba nyeusi wataita nyeusi, nyeupe itaitwa nyeupe kama ilivyo.

Kuwa na siasa za kubembelezana unazotaka mbele ya CCM inayojiita chama dola ni kupoteza muda, yale maridhiano yaliishia wapi? ukitaka kwenda na siasa za namna hiyo huoni tayari tumeshafeli?

Sent from my SM-G900H using JamiiForums mobile app
Sio kubembelezana ila ni vizuri kusikiliza maoni ya wengine. Mfano Mnyika anampinga sana Mbowe tokea Akiwa naibu mpaka amekua katibu ila huwezi sikia anamkosoa Mbowe au wapinzani in public. Hata suala la Lowassa alipinga kabisa ila alifoka kwenye vikao na akasusa kabisa ofisi ila kwenye public hakuwahi "ropoka" makosa ya Mbowe.

Mfano kumchafua Mbowe ni obvious unagawa kura za chadema, na sababu Mwabukusi hana watu wa kutosha ina maana CCM ndio inabaki kama alternative pekee sasa hapo unamfaidisha nani?

Kuhusu lissu nimesema hapa ni mzuri sana na mie nilimpigia kura 2020 na nitampigia kura 2025!! Ila nimeshaweka hadi uzi humu kuwa awe "rebranded" ili apunguze radicalism na nashukuru hilo linafanyika. Namuona kwenye charity anachangia, namuona kwenye matukio ya kidini yaani kujichanganya na vyama vyote ni political capital kubwa kuliko kutegemea kura za hard-core conservatives pekee.
 
Sio kubembelezana ila ni vizuri kusikiliza maoni ya wengine. Mfano Mnyika anampinga sana Mbowe tokea Akiwa naibu mpaka amekua katibu ila huwezi sikia anamkosoa Mbowe au wapinzani in public. Hata suala la Lowassa alipinga kabisa ila alifoka kwenye vikao na akasusa kabisa ofisi ila kwenye public hakuwahi "ropoka" makosa ya Mbowe.

Mfano kumchafua Mbowe ni obvious unagawa kura za chadema, na sababu Mwabukusi hana watu wa kutosha ina maana CCM ndio inabaki kama alternative pekee sasa hapo unamfaidisha nani?

Kuhusu lissu nimesema hapa ni mzuri sana na mie nilimpigia kura 2020 na nitampigia kura 2025!! Ila nimeshaweka hadi uzi humu kuwa awe "rebranded" ili apunguze radicalism na nashukuru hilo linafanyika. Namuona kwenye charity anachangia, namuona kwenye matukio ya kidini yaani kujichanganya na vyama vyote ni political capital kubwa kuliko kutegemea kura za hard-core conservatives pekee.
Kumbuka Mnyika na Mbowe wako chama kimoja, hawa wana namna yao ya kumaliza mambo yao, unataka Adv. Mwabukusi akaombe ruhusa ya kuhudhuria vikao vya Chadema ili ayasemee huko?

- What is kugawa kura za Chadema? Uoga tu usiokuwa na maana, mawazo ya zamani.

Halafu hivi unajua hiki unachopigania, kufichiana maovu ya upinzani ni utoto, uchanga kabisa kwenye siasa, mkiwa na tabia hiyo mkaingia madarakani mtaweza kumsikiliza anayewakosoa?

Hujui unachoandika hapa. Adv. Mwabukusi is the best kwa wakati huu.

Sent from my SM-G900H using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom